Monday, September 3, 2007

Hii ndiyo moja ya hotuba mbaya za P. W. Botha

HII ni hotuba ya aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini, marehemu P. W. Botha alipolihutubia Baraza lake la Mawaziri wakati wa utawala wa ubaguzi wa rangi nchini humo. Katika hotuba hiyo iliyochapishwa katika gazeti la Sunday Times la nchini humo toleo la Agosti 18, 1985, Botha anajigamba eti ardhi hiyo ni mali yao na hawapaswi kuingiliwa. Ikumbukwe kuwa katika utawala huo, mtu Mweusi aliteswa na kunyimwa haki zake za msingi na alifanywa kuwa kiumbe kisichostahili kuishi kwa raha katika ardhi hiyo.

Pretoria imetengenezwa na watu Weupe kwa ajili ya watu Weupe na hatuna haja ya kuuthibitisha umma au mtu Mweusi kuwa sisi ni watu bora, tumekuwa tukiwaambia watu Weusi jambo hili kwa njia elfu.

Afrika Kusini ya leo haikutengenezwa katika mawazo ya kawaida, tumeitengeneza kwa kutumia akili nyingi, jasho na damu. Mnaposema kuwa tunawabagua Weusi sielewi. Hivi ni Afrikaners ndio waliojaribu kusitisha kizazi cha Aborigines wa Australia? Je, ni Afrikaners waliotenga na kuwanyanyasa watu Weusi Marekani Kaskazini kwa kuwaita niggaz?

Je, ni Afrikaners ndio waliowatenga na kuwanyanyasa watu Weusi huko England kwa kuwatungia sheria ya kuwakandamiza? Canada, Ufaransa, Russia na Japan nao wana njia zao za kibaguzi. Hivi kwa nini hasa kuna kelele nyingi dhidi yetu? Huu ni uendawazimu! Kwanini wanatukaba koo kiasi hiki? Hawatutendei haki hata kidogo.

Nataka kuwaeleza kuwa hakuna kibaya tunachokitenda hapa ambacho hao wanaojiita wako katika dunia ya ustaarabu wameacha kukifanya. Sisi ni watu wema tusio na hatia na ambao tumeweka wazi mfumo wa maisha ya tunayotaka tuishi kama watu Weupe.

Sisi sio wanafiki kama Wazungu wenzetu wafanyavyo kwamba wanawapenda watu weusi. Ukweli kuwa Weusi wanaofanana na binadamu na kutenda mambo kama binadamu hayawahalalishi wao kuwa watu wenye akili timamu au binadamu aliyetimia. Kanunguyeye si nungunungu na mijusi hawawezi kuwa mamba eti kwa sababu tu wanafanana.

Kama Mungu alitaka tufanane na Weusi angetufanya sote tuwe na rangi moja na fikra sawa. Lakini alituumba tofauti; Weupe, Weusi, Wanjano, watawala na watawaliwa. Katika upeo sisi ni bora kuliko Weusi na hilo halina ubishi kwani limejihidhirisha kwa miaka mingi iliyopita.

Naamini kuwa Afrikaner ni mtu safi, mwenye hofu na Mungu. Ni mtu ambaye ameonyesha kwa vitendo njia sahihi ya utu. Hata hivyo, inafurahisha kuona kuwa Ulaya, America, Canada, Australia na wengine wengi wako nyuma yetu achilia mbali maneno yao. Kuhusu uhusiano wa kidiplomasia, sote tunafahamu lugha inavyotakiwa kutumika. Na kwa ushahidi ulio wazi hivi kuna mtu hapa asiyejua kuwa nchi nyingi za Ulaya zinatamani kuja kuwekeza Afrika Kusini?

Nani anayenunua dhahabu yetu, nani anayenunua almasi yetu? Nani anafanya biashara nasi? Nani anatusaidia katika kuendesha silaha za nuklia? Ukweli ni kwamba sisi ni watu wao na wao ni watu wetu. Hii ni siri kubwa. Nguvu ya uchumi wetu inajengwa kwa kiasi kikubwa na America, Britain na Ujerumani. Ni jambo kubwa sana hili na kwa maana hiyo, Mweusi ni malighafi kwa Mweupe.

Hivyo basi, kaka na dada zangu hebu tuungane kumpiga vita huyu shetani Mweusi. Napiga mbiu kwa kwa Afrikaners wote kujitokeza kwa hali na mali kupigana vita hii. Kwa hakika Mungu hawezi kuwatupa watu wake ambao ni sisi. Hadi sasa imeonekana kwa vitendo kuwa Weusi hawawezi kujitawala. Wape bunduki kama hawataanza kuuana.

Hawana lolote jema isipokuwa mashujaa wa kupiga kelele, kucheza ngoma, kuoa wanawake wengi na kupenda sana ngono. Hebu sasa tukubali kuwa mtu Mweusi ni alama ya umasikini, udumavu wa akili, uvivu na aliyekosa ushindani. Hivi hapo je, si kweli kwamba mtu Mweupe aliumbwa ili kumtawala mtu Mweusi? Hivi utajisikiaje unaamka asubuhi unakuta Kaff*ir amekalia kiti cha utawala? Hivi unajua kitakachotokea kwa wanawake wetu? Hivi kuna mtu anawaza kwamba Mweusi ataitawala nchi hii.

Kwa hiyo tuna sababu nzuri ya kuwapeleka akina Mandela jela waozee huko na katika hili nadhani upo umuhimu wa kupewa pongezi kwani tungekuwa na uwezo wa kuwaangamiza lakini sasa wanaishi. Napenda kuwatangazia mikakati mipya ya kuwaangamiza hawa Weusi. Tutumie sumu kuwamaliza.

Kamwe tusiruhusu idadi ya watu hawa iendelee kukua vinginevyo tutakwisha. Tayari nimeshawaleta wanasayansi ambao wamekuja na sehemu kubwa ya mzigo wa sumu na ninawasaka watafiti wengine zaidi waangalie sehemu murua za kuitumia sumu hiyo kwa lengo la kuwaangamiza Weusi.

Sehemu nzuri za kuwaangamiza kwa sumu ni hospitali na pia katika usambazaji wa chakula inaweza kutumika. Tumetengeneza sumu inayoua taratibu na kupunguza uwezo wa uzazi. Lakini hofu yetu ni kwamba itakuwaje kama sumu hiyo itaangukia kwenye mikono yao.

Hata hivyo, tunafanya kila tuwezalo kuhakikisha kuwa sumu hiyo inabaki katika himaya yetu. Pili, watu Weusi wanapenda sana pesa kwa hiyo tunaweza kuwatenga kwa njia hiyo. Wataalamu wetu wanalifanyia kazi suala hilo ili mtu Mweusi amchukie Mweusi mwenzake. Hawana upeo wa kufikiri na huyo ndiye kiumbe dhaifu kisicho na akili ya kuona mbali.

Kuna umuhimu mkubwa wa kupanga mambo hayo yaendelee kwa muda mrefu ili wasibaini kinachoendelea. Kwa kawaida mtu mweusi hapangi mikakati inayozidi kipindi cha mwaka mmoja. Na hapa napenda niwaombe kina mama wote wa ki Afrikaner wazae kwa fujo kuongeza idadi.

Litakuwa jambo la maana pia kama kutatengwa vituo maalumu ambako vijana wa kike na kiume watakaa na Serikali kuwawezesha ili wazae kwa idadi kubwa iwezekanavyo ili kuongeza idadi yetu. Wakati hilo likiendelea, lazima tuwabane watu Weusi waachane na wake zao.

Ninayo kamati inayoratibu na kuangalia njia nzuri ya kuwafanya watu hawa wachukiane na wauane wenyewe kwa wenyewe. Adhabu kwa Mweusi aliyemuua Mweusi iwe ndogo ili kuwapa hamasa ya kuendelea na mauaji.

Wanasayansi wangu wameshauri pia kuna ulazima wa kuwawekea sumu kwenye pombe, sumu ambayo itakuwa inawaua taratibu na kumaliza uwezo wa kuzaa pia. Njia kama hii na nyingine zifananazo na hii itawarahisha kuwapunguza idadi.

Rekodi zinaonyesha pia kuwa mtu Mweusi anapenda sana mwanamke Mweupe. Hii ni nafasi nzuri kwetu. Wanawake wetu warembo wanaotumika katika mbinu za kuwaangamiza wapinzani wetu watatumika kuwaua hao wanaopinga ubaguzi wa rangi.

Hili jeshi letu la mwituni la mapenzi huku tukiwa na jeshi kama hilo kwa upande wa wanaume ambao watawafuata wanawake Weusi. Pia Serikali imeagiza malaya kutoka Marekani na Ulaya kwa ajili ya kukidhi haja hiyo.

Ombi langu la mwisho ni kwamba wajawazito wanapozaa hospitalini, watoto lazima wauae pindi tu wanapotoka tumboni. Hatuwalipi wale wauguzi kwa ajili ya kutuletea watoto Weusi katika hii dunia bali kuwaangamiza.

Serikali yangu imetenga fungu maalumu la pesa kwa ajili ya kujenga hospitali na kliniki kwa ajili ya kufanikisha mpango huo. Pesa inafanya lolote na kwa vile tunazo tuzitumie ipasavyo.

Kwa muda huu ndugu zangu Weupe, msiyaweke moyoni yanayosemwa dhidi yenu na wala msione aibu kuitwa wabaguzi na wala sijali kuitwa mhandisi na Mfalme wa Ubaguzi. Siwezi kugeuka nyani eti kwa sababu mtu kaniita nyani. Nitabaki kuwa nyota inayong’aa…mtukufu Botha.

Leo naondoa mawingu; kesho nitajaribu milima!

"Maisha yetu huanza kukoma siku ambayo tunaanza kuwa kimya juu ya mambo muhimu." Dk. Martin Luther King Jr.

"Ni vema kufa kwa ajili ya imani itayoishi kuliko kuishi kwa jambo litakalokufa.” Steven Bantu Biko.

No comments: