na innocent munyuku
SIKU za maumivu zimeanza. Pilika zimezidi, watu wanakuna vichwa wakihaha kusaka neema ya matumbo na viwalo vya sikukuu.
Mzee wa Busati ni miongoni mwao. Kaya yake imemkodolea macho. Hana namna ya kukwepa kwani husemwa kwamba tembo hawezi kuona uzito wa mkonga wake. Kikombe hiki kitanywewa!
Kila mmoja kwa nafasi yake anajipanga ili mambo yasiende upogo. Nidhamu ya matumizi ya fedha imekuwa juu. Bajeti imeshapangwa na kinachosubiriwa ni siku zifike watu watafune vipapatio vya kuku kama si kwato za mbuzi.
Vibaka nao wanakwenda na wakati, mbinu zimekuwa za kisasa zaidi katika wizi wanaoufanya. Kwao hiyo ni ajira ingawa si halali. Lakini wafanyeje? Ndio staili yao ya maisha. Watakimbilia wapi? acha waendelee hadi siku wakikumbana na harufu ya moto wa petroli.
Hayo ndiyo mambo ya kila siku ukianza kuyafuatilia unaweza kuongeza uchizi, la maana ni kuyaacha yapite.
Huo ulikuwa utangulizi wa Mwandika Busati ambaye wiki hii katua kwenye safu yake ya kujidai akiwa na nguvu mpya. Mola kamwongezea misuli.
Lililo kuu juma hili ni suala la usukaji wa vipaji vya sanaa nchini. Wakati mwingine inashangaza kuona kwamba wapo watu kwa makusudi wameamua kupotosha vichwa vya sanaa.
Hao ni hodari wa kubuni mambo na kwa vile wako kwenye ardhi ya Wadanganyika, wanachokibuni na kukisema huonekana kuwa ni bora na chenye mwelekeo.
Mzee wa Busati angali akishangaa programu iliyoitwa ya kusaka vipaji vya muziki Tanzania. Hivi kweli nyota wa muziki anasakwa kwa staili hiyo? Huko ni kupotoka kwa kiwango cha hali ya juu.
Nyota wa muziki anapatikana kwa kumwangalia usoni? Ni lini mwanamuziki nyota akapimwa kwa umbo lake?
Ni lini nyota njema ya muziki ilipimwa kwa majaji ambao baadhi yao hawaujui huo muziki? Hivi ni vichekesho ambavyo kwa hakika vinaleta kichefuchefu cha kufungia mwaka.
Leo mwataka kuwa na kizazi kitakachowika kwenye anga ya muziki ndani na nje ya Tanzania. kwa mtindo huo wa kuangaliana usoni kama mpo kwenye gwaride la utambuzi wa wahalifu.
Wajuzi wa Kiswahili husema kwamba panya wengi hawachimbi shimo. Wanachomaanisha ni kuwa uwingi si hoja katika utekelezaji wa mambo muhimu.
Hao wanaojipanga kwa wingi wakinadi kusaka vipaji vya muziki nchini bila shaka ni wapotoshaji kutokana na ukweli kwamba staili inayotumika kuwasaka nyota wa muziki inakwenda isivyo.
Matokeo yake ni kwamba taifa lazidi kupoteza vipaji vya muziki kila uchao. Waandaaji wa shughuli kama hizo wengi wao wamekaa kwa ajili ya neema binafsi na si kweli kwamba wana mema kwa muziki wa Tanzania.
Matatizo ya aina hiyo ni mengi na ndio maana asilimia kubwa ya Wabongo wamesusa mema ya kwao.
Anachosema Mzee wa Busati ni kuwa wasanii wetu hasa wa muziki hawasaidiwi katika kuendesha maisha yao kwa thamani halisi ya kazi zao.
Leo hii Mwandika Busati angetaraji kuona mashabiki wa muziki wamevaa fulana zenye nembo za wanamuziki kama Msafiri Zawose au Vitali Maembe.
Hazipo mtaani kwani hata chache zinazochapwa zinasuswa na maelfu kukimbilia fulana na kofia za 50 Cent.
Hayo yote yanakuja kutokana na namna jamii ilivyojengwa kuanzia huko nyuma. Na ndio maana Mzee wa Busati anasema staili ya kusaka vipaji vya muziki iangaliwe upya.
Hizi kelele zinazopigwa na kuchezwa na wengi wakiamini kwamba kuna vipaji vinasakwa ni kudanganyana na ni kupotosha sanaa.
Huu ni ukomo wa Mzee wa Busati kwa wiki hii. Panapo majaliwa tukutane wiki ijayo kwenye Noeli. Kila lililo jema liwakute na fanaka tele.
Wasalaam,
Monday, December 17, 2007
Sunday, December 9, 2007
Hili la Dewji na mustakabali wa soka yetu
na innocent munyuku
NI jambo la kawaida katika mkusanyiko wa binadamu kuwa na mawazo tofauti.
Hii maana yake ni kwamba kama itatokea siku binadamu wote duniani wakafanana mawazo katika kila jambo basi si ajabu dunia ikasambaratika zaidi.
Mzee wa Busati wiki iliyopita alisikia habari kwamba kuna wapenda michezo wametangaza kuipa Kilimanjaro Stars zawadi nono katika mfumo wa fedha kama wataibuka na Kombe la Chalenji.
Alianza Mohamed Dewji kuwatangazia Wabongo kwamba yeye binafsi atawazadia wachezaji donge nono la Sh milioni 35 na Sh milioni 24 kama watashika nafasi ya pili.
Baada ya Dewji kutangaza hilo, mfanyabiashara maarufu nchini Alex Massawe naye akasema atawapa wachezaji Sh milioni 10 kama watafanikiwa kutwaa Kombe la Chalenji.
Wenye busara wakaanza kunong’ona kwamba wawili hao hawakuwa na nia njema ya kuifanya Kilimanjaro Stars kufikia kilele cha mafanikio.
Kwamba kama wamelenga kuifanya Tanzania iwike katika medani ya soka hawakuwa na haja ya kuibuka leo na ahadi kama hizo za danganya toto.
Mzee wa Busati anaamini kuwa kuendekeza ahadi kama hizo ni sawa na kuua medani ya soka nchini. Ni wazi kwamba Shirikisho la Soka Tanzania lina uhaba wa fedha. Dewji analifahamu hilo hali kadhalika Massawe.
Mwandika Busati alitarajia kuwasikia watu hao wakitoa fedha kwa ajili ya maandalizi kabambe na si kuiacha timu dhaifu iingie mashindanoni.
Anachokiona Mzee wa Busati hapa ni porojo na hadaa kwa Watanzania na katika hili wanasoka wamedhihakiwa. Haiingii akili kwa mtu makini na mwenye nia ya dhati ya kuinua soka asubiri timu iingie uwanjani ndipo atoe ahadi ya fedha nono.
Dewji na Massawe walikuwa wapi wakati Kilimanjaro Stars inahitaji fedha za maandalizi? Hivi ni kweli hawakujua kwamba kambi inahitaji fedha kwa ajili ya maandalizi?
Ukweli wa mambo ni kwamba huo ni mfano kwamba Watanzania walio wengi mbali na kuwa na uwezo wa kukuza michezo wanajificha kwa makusudi.
Ahadi kama hizo hazina maana nyingine zaidi ya kudidimiza michezo nchini. Vijana wanatakiwa waandaliwe na kama wamepata maandalizi ya kutosha hawana haja ya kuahidiwa mema kwani watakuwa tayari wana ubavu wa kufanya vema mashindanoni.
Tangu mwanzo Mzee wa Busati ameweka wazi kwamba binadamu lazima watofautiane katika mtazamo. Ndicho anachofanya hapa. Kuna waliokaa na kukenua wakifurahia ahadi hiyo ya fedha. Hiyo ni haki yao ya msingi na wana uhuru wa kufanya hivyo.
Lakini kwa mtazamo wa Mwandika Busati kinachofaa kufanywa kama kweli bongo inahitaji kuvuma katika soka basi ni maandalizi na si kupiga soga.
Kama wana nia ya dhati ya kuinua soka ni heri wajitokeze mapema wakati wa maandalizi kwa timu za taifa. Kutoa ahadi pekee si dawa ya Tanzania kuwa kichwa cha mwendawazimu.
Hii ni sawa na kwenda kwa jirani yako mwenye njaa halafu unamwambia akimbie mbio za nyika na kwamba akishamaliza atazawadia fedha za kujaza mifuko yake.
Hiyo ni hadaa kwani mwenye njaa hawezi kumudu mbio hizo. Ataanguka na kupoteza maisha kwani hana ubavu wa kumaliza mbio hizo.
Kama una mapenzi na jirani huyo basi ni vema ukampa lishe bora na hapo umweleze aanze mbio za nyika. Huo ndio uungwana!
Hizo ngwenje mnazoahidi fanyeni mpango wa kuwaweka wachezaji kambini. Walishwe vema wawe na stamina, wafundwe njia za kisasa katika soka ili wakitinga dimbani waonyeshe makali.
Kukaa mezani na kusema juu ya ahadi si njia mbadala ya kuendeleza soka. Muda wa kubembelezana kwa peremende bila shaka umepitwa na wakati. Badilikeni!
Mzee wa Busati ameona awe tofauti na hao wanaokenua wakichekelea ahadi ya fedha. Kwani naye anao uhuru wa kuwa na msimamo wa tofauti.
Vinginevyo busati kwa sasa halikaliki. Mzee wa Busati yu katika pilika za kila aina ili kulinda heshima ya kaya yake kwa majuma ya raha na karaha yajayo.
Wasalaam,
NI jambo la kawaida katika mkusanyiko wa binadamu kuwa na mawazo tofauti.
Hii maana yake ni kwamba kama itatokea siku binadamu wote duniani wakafanana mawazo katika kila jambo basi si ajabu dunia ikasambaratika zaidi.
Mzee wa Busati wiki iliyopita alisikia habari kwamba kuna wapenda michezo wametangaza kuipa Kilimanjaro Stars zawadi nono katika mfumo wa fedha kama wataibuka na Kombe la Chalenji.
Alianza Mohamed Dewji kuwatangazia Wabongo kwamba yeye binafsi atawazadia wachezaji donge nono la Sh milioni 35 na Sh milioni 24 kama watashika nafasi ya pili.
Baada ya Dewji kutangaza hilo, mfanyabiashara maarufu nchini Alex Massawe naye akasema atawapa wachezaji Sh milioni 10 kama watafanikiwa kutwaa Kombe la Chalenji.
Wenye busara wakaanza kunong’ona kwamba wawili hao hawakuwa na nia njema ya kuifanya Kilimanjaro Stars kufikia kilele cha mafanikio.
Kwamba kama wamelenga kuifanya Tanzania iwike katika medani ya soka hawakuwa na haja ya kuibuka leo na ahadi kama hizo za danganya toto.
Mzee wa Busati anaamini kuwa kuendekeza ahadi kama hizo ni sawa na kuua medani ya soka nchini. Ni wazi kwamba Shirikisho la Soka Tanzania lina uhaba wa fedha. Dewji analifahamu hilo hali kadhalika Massawe.
Mwandika Busati alitarajia kuwasikia watu hao wakitoa fedha kwa ajili ya maandalizi kabambe na si kuiacha timu dhaifu iingie mashindanoni.
Anachokiona Mzee wa Busati hapa ni porojo na hadaa kwa Watanzania na katika hili wanasoka wamedhihakiwa. Haiingii akili kwa mtu makini na mwenye nia ya dhati ya kuinua soka asubiri timu iingie uwanjani ndipo atoe ahadi ya fedha nono.
Dewji na Massawe walikuwa wapi wakati Kilimanjaro Stars inahitaji fedha za maandalizi? Hivi ni kweli hawakujua kwamba kambi inahitaji fedha kwa ajili ya maandalizi?
Ukweli wa mambo ni kwamba huo ni mfano kwamba Watanzania walio wengi mbali na kuwa na uwezo wa kukuza michezo wanajificha kwa makusudi.
Ahadi kama hizo hazina maana nyingine zaidi ya kudidimiza michezo nchini. Vijana wanatakiwa waandaliwe na kama wamepata maandalizi ya kutosha hawana haja ya kuahidiwa mema kwani watakuwa tayari wana ubavu wa kufanya vema mashindanoni.
Tangu mwanzo Mzee wa Busati ameweka wazi kwamba binadamu lazima watofautiane katika mtazamo. Ndicho anachofanya hapa. Kuna waliokaa na kukenua wakifurahia ahadi hiyo ya fedha. Hiyo ni haki yao ya msingi na wana uhuru wa kufanya hivyo.
Lakini kwa mtazamo wa Mwandika Busati kinachofaa kufanywa kama kweli bongo inahitaji kuvuma katika soka basi ni maandalizi na si kupiga soga.
Kama wana nia ya dhati ya kuinua soka ni heri wajitokeze mapema wakati wa maandalizi kwa timu za taifa. Kutoa ahadi pekee si dawa ya Tanzania kuwa kichwa cha mwendawazimu.
Hii ni sawa na kwenda kwa jirani yako mwenye njaa halafu unamwambia akimbie mbio za nyika na kwamba akishamaliza atazawadia fedha za kujaza mifuko yake.
Hiyo ni hadaa kwani mwenye njaa hawezi kumudu mbio hizo. Ataanguka na kupoteza maisha kwani hana ubavu wa kumaliza mbio hizo.
Kama una mapenzi na jirani huyo basi ni vema ukampa lishe bora na hapo umweleze aanze mbio za nyika. Huo ndio uungwana!
Hizo ngwenje mnazoahidi fanyeni mpango wa kuwaweka wachezaji kambini. Walishwe vema wawe na stamina, wafundwe njia za kisasa katika soka ili wakitinga dimbani waonyeshe makali.
Kukaa mezani na kusema juu ya ahadi si njia mbadala ya kuendeleza soka. Muda wa kubembelezana kwa peremende bila shaka umepitwa na wakati. Badilikeni!
Mzee wa Busati ameona awe tofauti na hao wanaokenua wakichekelea ahadi ya fedha. Kwani naye anao uhuru wa kuwa na msimamo wa tofauti.
Vinginevyo busati kwa sasa halikaliki. Mzee wa Busati yu katika pilika za kila aina ili kulinda heshima ya kaya yake kwa majuma ya raha na karaha yajayo.
Wasalaam,
Miaka 46 ya uhuru twajivunia nini?
Na Innocent Munyuku
NIPATAPO nafasi ya kuketi vijiweni na Watanzania wenzangu hasa vijana nanasa mambo mengi ambayo natamani mtawala wa nchi pia angepata wasaa wa kuyasikia.
Bila shaka anayapata lakini kwa vile sina uhakika ni heri nitumie nafasi hii kuyasema baadhi ya masuala yanayojadiliwa kila wakati huko mitaani.
Leo hii Watanzania wanatimiza miaka 46 tangu wapate uhuru kutoka mikononi mwa Waingereza mwaka 1961. Ni sherehe kubwa na yenye simulizi nyingi; mbaya na njema.
Miaka 46 ya uhuru si lele mama. Hii maana yake ni kwamba kama ni maisha ya binadamu Tanzania tayari ni mtu mzima anayejitegemea kwa mambo mengi.
Lakini kwa bahati mbaya sana miaka hii ya uhuru ni dhahiri kwamba hakuna jema la kujivunia ukilinganisha na mataifa mengine yaliyopata uhuru baada ya Tanzania.
Kinachosemwa mitaani ni kwamba Tanzania licha ya kuwa taifa huru, maisha ya Watanzania yameendelea kuwa magumu kila uchao.
Watu wanalalama juu ya kupanda kwa bei ya bidhaa hasa zile zinazohitajika katika maisha ya kila siku. Hicho ndicho wanacholalamikia.
Lakini pia wanasema juu ya uwajibikaji mdogo wa watendaji wa Serikali. Wanazungumzia ubovu wa baadhi ya mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya.
Ingawa wengi wao hawana ubavu wa kupaza sauti, wanasema kwa kadiri wawezavyo kwamba hata watendaji katika ngazi ya vijiji ni waovu wasiopaswa kukalia viti hivyo.
Hawaishii hapo, wanakerwa juu ya ubovu wa huduma za afya. Kina mama na watoto, wazee na wahitaji wengine wa huduma hiyo wanakwazwa na utendaji wa wauguzi na madaktari.
Hili pengine halihitaji mjadala mrefu kwani hospitali na zahanati nyingi mambo si shwari kwa wagonjwa. Ni jambo la kawaida kwa wagonjwa kulala wanne kitanda kimoja. Hili si la ajabu.
Si jambo geni pia kuwakuta wagonjwa wamerundikana chini wakilalia mkeka. Watanzania wamezoea. Si kama wameridhika bali mfumo umewaweka hapo.
Muhuri wa Mtendaji wa Serikali za Mitaa nao siku hizi umekuwa mradi mkubwa kwa hao wenye dhamana ya kuushika. Karatasi haigongwi pasipo rupia mkononi.
Wananchi wamezoea kulipa fedha hata kwa yale ambayo wanapaswa wahudumiwe bure. Yanaonekana kama vile yameshakuwa sugu na yasiyoweza kufutwa.
Hayo ndiyo yanayojiri katika miaka hii 46 ya uhuru wa Tanganyika. Rushwa imeendelea na inazidi kushika kasi ya ajabu kutokana na ukweli kwamba mbinu za utoaji na upokeaji rushwa zinabadilika.
Watu wanakwenda kwa mtindo wa kisasa na kutokana na hali hiyo si rahisi leo hii kuwanasa wala rushwa kama ilivyokuwa miaka 10 iliyopita. Mbinu zinabadilika.
Pamoja na ukweli kwamba wananchi wana mchango mkubwa katika kukabiliana na rushwa, wanacholalamikia wao ni kwamba walio juu ndio viongozi wa jambo hilo.
Wanasema kama katibu mkuu wa wizara anadaka rushwa mwananchi wa kawaida afanyeje? Tule wote kwani huo ndio utaratibu uliopo.
Wengine wananong’ona kwamba kama mbunge fulani katinga bungeni kwa njia ya hongo diwani naye ataachaje kutetea nafasi yake kwa rushwa?
Haya si mambo ya siri yanasemwa lakini kwa bahati mbaya sana si rahisi kuyapatia ushahidi. Lakini ukweli wa mambo ni huo rushwa inanuka nchini.
Hii maana yake ni kwamba walio wengi hawapati huduma kwa kiwango kinachostahili. Kama ni ajira, matibabu na mengine hayapatikani mpaka utoe rushwa.
Ukikanyaga polisi utaambiwa hawana karatasi ya kuandikia maelezo ya mlalamikaji. Lakini kabla ya hilo kama utakuwa unahitaji kuwapeleka mahala alipo mtuhumiwa utaelezwa kwamba hawana gari na kama lipo watasema halina mafuta. Kodi tunazolipa zinatumikaje?
Hizo zote ni njia za kukufanya uwe mstari wa mbele kufungua pochi na kuwapa ulichonacho ili mambo yaende.
Hii ndiyo miaka 46 ya uhuru wa Tanganyika tunayoishi. Kwa uwazi ni kwamba maisha ya rushwa hayana maana nyingine zaidi ya kuendelea kukandamizana na kwa njia hiyo kuliangamiza taifa.
Kuna waliodiriki kusaini mikataba hafifu ya kimataifa ambayo leo hii taifa linaangamia kwa kukosa maarifa. Waliopewa dhamana wamekula cha kwao na hawana hofu ya maisha.
Anayepata taabu ni mlalahoi ambaye hajui aanzie wapi ili afikie kilele cha maisha bora. Amekwazwa na mfumo ambao hautaki mabadiliko.
Hayo ndiyo yanayosemwa vijiweni lakini hakuna shaka kwamba ndiyo hali halisi kwa maisha ya kila siku.
Je, katika miaka 46 ya uhuru Watanzania tunajivunia nini? Imani na utulivu wa kutoona mabomu yakilipuka mitaani? Pengine yapaswa kuwapo na tafakuri ya kina kwani kwa mtazamo wangu amani kamili maana yake ni kuwa na utulivu wa akili pia.
Kama matumbo hayana shibe sidhani kama mtu anaweza kutembea kwa matao akisema kuwa yu na amani ya kweli. Tusibweteke na miaka 46 ya uhuru tusake njia ya kujikwamua uwezo tunao.
NIPATAPO nafasi ya kuketi vijiweni na Watanzania wenzangu hasa vijana nanasa mambo mengi ambayo natamani mtawala wa nchi pia angepata wasaa wa kuyasikia.
Bila shaka anayapata lakini kwa vile sina uhakika ni heri nitumie nafasi hii kuyasema baadhi ya masuala yanayojadiliwa kila wakati huko mitaani.
Leo hii Watanzania wanatimiza miaka 46 tangu wapate uhuru kutoka mikononi mwa Waingereza mwaka 1961. Ni sherehe kubwa na yenye simulizi nyingi; mbaya na njema.
Miaka 46 ya uhuru si lele mama. Hii maana yake ni kwamba kama ni maisha ya binadamu Tanzania tayari ni mtu mzima anayejitegemea kwa mambo mengi.
Lakini kwa bahati mbaya sana miaka hii ya uhuru ni dhahiri kwamba hakuna jema la kujivunia ukilinganisha na mataifa mengine yaliyopata uhuru baada ya Tanzania.
Kinachosemwa mitaani ni kwamba Tanzania licha ya kuwa taifa huru, maisha ya Watanzania yameendelea kuwa magumu kila uchao.
Watu wanalalama juu ya kupanda kwa bei ya bidhaa hasa zile zinazohitajika katika maisha ya kila siku. Hicho ndicho wanacholalamikia.
Lakini pia wanasema juu ya uwajibikaji mdogo wa watendaji wa Serikali. Wanazungumzia ubovu wa baadhi ya mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya.
Ingawa wengi wao hawana ubavu wa kupaza sauti, wanasema kwa kadiri wawezavyo kwamba hata watendaji katika ngazi ya vijiji ni waovu wasiopaswa kukalia viti hivyo.
Hawaishii hapo, wanakerwa juu ya ubovu wa huduma za afya. Kina mama na watoto, wazee na wahitaji wengine wa huduma hiyo wanakwazwa na utendaji wa wauguzi na madaktari.
Hili pengine halihitaji mjadala mrefu kwani hospitali na zahanati nyingi mambo si shwari kwa wagonjwa. Ni jambo la kawaida kwa wagonjwa kulala wanne kitanda kimoja. Hili si la ajabu.
Si jambo geni pia kuwakuta wagonjwa wamerundikana chini wakilalia mkeka. Watanzania wamezoea. Si kama wameridhika bali mfumo umewaweka hapo.
Muhuri wa Mtendaji wa Serikali za Mitaa nao siku hizi umekuwa mradi mkubwa kwa hao wenye dhamana ya kuushika. Karatasi haigongwi pasipo rupia mkononi.
Wananchi wamezoea kulipa fedha hata kwa yale ambayo wanapaswa wahudumiwe bure. Yanaonekana kama vile yameshakuwa sugu na yasiyoweza kufutwa.
Hayo ndiyo yanayojiri katika miaka hii 46 ya uhuru wa Tanganyika. Rushwa imeendelea na inazidi kushika kasi ya ajabu kutokana na ukweli kwamba mbinu za utoaji na upokeaji rushwa zinabadilika.
Watu wanakwenda kwa mtindo wa kisasa na kutokana na hali hiyo si rahisi leo hii kuwanasa wala rushwa kama ilivyokuwa miaka 10 iliyopita. Mbinu zinabadilika.
Pamoja na ukweli kwamba wananchi wana mchango mkubwa katika kukabiliana na rushwa, wanacholalamikia wao ni kwamba walio juu ndio viongozi wa jambo hilo.
Wanasema kama katibu mkuu wa wizara anadaka rushwa mwananchi wa kawaida afanyeje? Tule wote kwani huo ndio utaratibu uliopo.
Wengine wananong’ona kwamba kama mbunge fulani katinga bungeni kwa njia ya hongo diwani naye ataachaje kutetea nafasi yake kwa rushwa?
Haya si mambo ya siri yanasemwa lakini kwa bahati mbaya sana si rahisi kuyapatia ushahidi. Lakini ukweli wa mambo ni huo rushwa inanuka nchini.
Hii maana yake ni kwamba walio wengi hawapati huduma kwa kiwango kinachostahili. Kama ni ajira, matibabu na mengine hayapatikani mpaka utoe rushwa.
Ukikanyaga polisi utaambiwa hawana karatasi ya kuandikia maelezo ya mlalamikaji. Lakini kabla ya hilo kama utakuwa unahitaji kuwapeleka mahala alipo mtuhumiwa utaelezwa kwamba hawana gari na kama lipo watasema halina mafuta. Kodi tunazolipa zinatumikaje?
Hizo zote ni njia za kukufanya uwe mstari wa mbele kufungua pochi na kuwapa ulichonacho ili mambo yaende.
Hii ndiyo miaka 46 ya uhuru wa Tanganyika tunayoishi. Kwa uwazi ni kwamba maisha ya rushwa hayana maana nyingine zaidi ya kuendelea kukandamizana na kwa njia hiyo kuliangamiza taifa.
Kuna waliodiriki kusaini mikataba hafifu ya kimataifa ambayo leo hii taifa linaangamia kwa kukosa maarifa. Waliopewa dhamana wamekula cha kwao na hawana hofu ya maisha.
Anayepata taabu ni mlalahoi ambaye hajui aanzie wapi ili afikie kilele cha maisha bora. Amekwazwa na mfumo ambao hautaki mabadiliko.
Hayo ndiyo yanayosemwa vijiweni lakini hakuna shaka kwamba ndiyo hali halisi kwa maisha ya kila siku.
Je, katika miaka 46 ya uhuru Watanzania tunajivunia nini? Imani na utulivu wa kutoona mabomu yakilipuka mitaani? Pengine yapaswa kuwapo na tafakuri ya kina kwani kwa mtazamo wangu amani kamili maana yake ni kuwa na utulivu wa akili pia.
Kama matumbo hayana shibe sidhani kama mtu anaweza kutembea kwa matao akisema kuwa yu na amani ya kweli. Tusibweteke na miaka 46 ya uhuru tusake njia ya kujikwamua uwezo tunao.
Tuesday, December 4, 2007
Tusisubiri wawe watu wazima wa mitaani
Na Innocent Munyuku
HUSEMWA kwamba usipoziba ufa utajenga ukuta. Lakini wajuzi wengine wa lugha wakaja na msemo mwingine kwamba samaki mkunje angali mbichi.
Wapo wengine waliosema pia kuwa tohara ya Ijumaa huanza Alhamisi. Hii yote ni misemo ya hadhari kwa binadamu awe na hulka ya maandalizi.
Kwamba kama wahusika wa jambo wanafanya mambo pasipo maandalizi ni wazi kuwa suala walifanyalo halitakwenda sawia. Watavurunda na hivyo kuonekana waliokosa umakini.
Jamii yetu leo hii inahaha kufuta wimbi la watoto wa mitaani. Semina na warsha mbalimbali zinajadili suala hilo.
Sehemu za mijini watoto hao ni wengi. Tunapishana nao na la kusikitisha ni kwamba haieleweki ni nani anawajali watoto hao kwa dhati.
Wataambulia Sh 100 au Sh 500 ambazo kwa mtazamo wa kawaida haziwasaidii kuishi kwa uhakika.
Hii ni kusema kwamba maisha ya watoto hawa ni ya shibe ya leo. Wakiumwa na washindwe kujipanga mitaani kusaka fedha kutoka kwa raia wenye huruma basi hakuna shaka kwamba siku hiyo ni kama kiama kwao.
Zipo asasi zilizojiandikisha kuwa mstari wa mbele kuwatumikia watoto hao. Vipo vituo vinavyolea watoto hao wa mitaani lakini ukweli wa mambo ni kwamba mahitaji hayatoshelezi.
Hii ni kusema kuwa watoto waliopo vituoni ni wachache ukilinganisha na ujumla wa waliobaki kuzurura mitaani.
Lakini hoja yangu ni kwamba mtima wangu umejaa shaka juu ya mustakabali wa watoto hao ambao wengi wao ni wenye umri wa miaka kati ya miwili hadi 15.
Hawa wanaendelea kuomba lakini wakishavuka umri huo ‘wanajiajiri’ katika kazi nyingine. Katika miji mbalimbali nchini watoto hao wakishakomaa hujihusisha na kuosha magari ili wapate kuishi.
Wakati mwingine watoto wa aina hiyo hugeuka kuwa ‘walinzi’ wa muda wa magari hayo ingawa uzoefu unaonyesha ni hao hao wanaokwapua vioo vya magari au vipuri.
Kwa mtazamo wangu, hatua ya aina hiyo ni mbaya kwani wakishaanza kukwapua vipuri wataenda mbali zaidi kwa kujifunza uhalifu uliokomaa.
Hawana nafasi kwa elimu ambayo kwa hali ya kawaida ingewasaidia kusaka namna nyingine ya kuishi.
Kwa maana hiyo wataelekeza akili zao kutenda uhalifu zaidi kuliko wema ndani ya jamii.
Watafanya hivyo kutokana na ukweli kwamba hawana namna nyingine ya kujiingizia kipato. Wataosha magari na mwishowe watachoka.
Na ukizingatia kuwa watoto hao wako mjini ni wazi kuwa wanaishi katika mazingira ya kujifunza mbinu mbalimbali za kuyasukuma maisha.
Hawa sasa ndio hao ambao kwa mtazamo wangu sisiti kuwaita watu wazima wa mitaani.
Kwamba athari zake ni kubwa kuliko pengine sehemu kubwa ya jamii inavyofikiria. Madhara yake ni makubwa na hii maana yake ni kuwa tutakuwa na jamii yenye shaka daima.
Nani ataweza kuwadhibiti watu wazima hao wa mitaani ambao katika maisha yao ya awali wamekuwa katika dhiki na kukata tamaa?
Mamlaka gani inaweza kusimama na kujigamba kwamba inayo ubavu wa kuwadhibiti watu wazima hao wa mitaani?
Ukweli wa mambo ni kwamba tusitarajie kuwaona wakiwa na mema katika maisha kwani tayari wameshaathirika na mfumo wa maisha.
Mtu aliyeishi kwa mashaka katika miaka mingi si ajabu akawa na uamuzi wa kubomoa zaidi kuliko kuijenga jamii. Hebu fikiria tangu akiwa na umri wa miaka miwili anaishi mtaani unadhani akiendelea hivyo hadi miaka 25 atakuwa katika hali gani?
Hakuna shaka kwamba atajifunza njia mbadala ya kujikwamua na ugumu wa maisha na katika hili hatasita kujifunza njia yoyote atakayoona inafaa. Atafanya hivyo kwa sababu hana cha kupoteza.
Tusifikishane huko kwani jamii ya Watanzania inao uwezo wa kuwanusuru watoto wa mitaani. Tusisubiri waitwe watu wazima wa mitaani.
HUSEMWA kwamba usipoziba ufa utajenga ukuta. Lakini wajuzi wengine wa lugha wakaja na msemo mwingine kwamba samaki mkunje angali mbichi.
Wapo wengine waliosema pia kuwa tohara ya Ijumaa huanza Alhamisi. Hii yote ni misemo ya hadhari kwa binadamu awe na hulka ya maandalizi.
Kwamba kama wahusika wa jambo wanafanya mambo pasipo maandalizi ni wazi kuwa suala walifanyalo halitakwenda sawia. Watavurunda na hivyo kuonekana waliokosa umakini.
Jamii yetu leo hii inahaha kufuta wimbi la watoto wa mitaani. Semina na warsha mbalimbali zinajadili suala hilo.
Sehemu za mijini watoto hao ni wengi. Tunapishana nao na la kusikitisha ni kwamba haieleweki ni nani anawajali watoto hao kwa dhati.
Wataambulia Sh 100 au Sh 500 ambazo kwa mtazamo wa kawaida haziwasaidii kuishi kwa uhakika.
Hii ni kusema kwamba maisha ya watoto hawa ni ya shibe ya leo. Wakiumwa na washindwe kujipanga mitaani kusaka fedha kutoka kwa raia wenye huruma basi hakuna shaka kwamba siku hiyo ni kama kiama kwao.
Zipo asasi zilizojiandikisha kuwa mstari wa mbele kuwatumikia watoto hao. Vipo vituo vinavyolea watoto hao wa mitaani lakini ukweli wa mambo ni kwamba mahitaji hayatoshelezi.
Hii ni kusema kuwa watoto waliopo vituoni ni wachache ukilinganisha na ujumla wa waliobaki kuzurura mitaani.
Lakini hoja yangu ni kwamba mtima wangu umejaa shaka juu ya mustakabali wa watoto hao ambao wengi wao ni wenye umri wa miaka kati ya miwili hadi 15.
Hawa wanaendelea kuomba lakini wakishavuka umri huo ‘wanajiajiri’ katika kazi nyingine. Katika miji mbalimbali nchini watoto hao wakishakomaa hujihusisha na kuosha magari ili wapate kuishi.
Wakati mwingine watoto wa aina hiyo hugeuka kuwa ‘walinzi’ wa muda wa magari hayo ingawa uzoefu unaonyesha ni hao hao wanaokwapua vioo vya magari au vipuri.
Kwa mtazamo wangu, hatua ya aina hiyo ni mbaya kwani wakishaanza kukwapua vipuri wataenda mbali zaidi kwa kujifunza uhalifu uliokomaa.
Hawana nafasi kwa elimu ambayo kwa hali ya kawaida ingewasaidia kusaka namna nyingine ya kuishi.
Kwa maana hiyo wataelekeza akili zao kutenda uhalifu zaidi kuliko wema ndani ya jamii.
Watafanya hivyo kutokana na ukweli kwamba hawana namna nyingine ya kujiingizia kipato. Wataosha magari na mwishowe watachoka.
Na ukizingatia kuwa watoto hao wako mjini ni wazi kuwa wanaishi katika mazingira ya kujifunza mbinu mbalimbali za kuyasukuma maisha.
Hawa sasa ndio hao ambao kwa mtazamo wangu sisiti kuwaita watu wazima wa mitaani.
Kwamba athari zake ni kubwa kuliko pengine sehemu kubwa ya jamii inavyofikiria. Madhara yake ni makubwa na hii maana yake ni kuwa tutakuwa na jamii yenye shaka daima.
Nani ataweza kuwadhibiti watu wazima hao wa mitaani ambao katika maisha yao ya awali wamekuwa katika dhiki na kukata tamaa?
Mamlaka gani inaweza kusimama na kujigamba kwamba inayo ubavu wa kuwadhibiti watu wazima hao wa mitaani?
Ukweli wa mambo ni kwamba tusitarajie kuwaona wakiwa na mema katika maisha kwani tayari wameshaathirika na mfumo wa maisha.
Mtu aliyeishi kwa mashaka katika miaka mingi si ajabu akawa na uamuzi wa kubomoa zaidi kuliko kuijenga jamii. Hebu fikiria tangu akiwa na umri wa miaka miwili anaishi mtaani unadhani akiendelea hivyo hadi miaka 25 atakuwa katika hali gani?
Hakuna shaka kwamba atajifunza njia mbadala ya kujikwamua na ugumu wa maisha na katika hili hatasita kujifunza njia yoyote atakayoona inafaa. Atafanya hivyo kwa sababu hana cha kupoteza.
Tusifikishane huko kwani jamii ya Watanzania inao uwezo wa kuwanusuru watoto wa mitaani. Tusisubiri waitwe watu wazima wa mitaani.
Safari hii jaribuni Miss Bantu
na innocent munyuku
YAMETIMIA! Hadithi imekuwa ile ile kwa Tanzania kuangukia pua kwenye mashindano ya urembo ya dunia.
Binti aliyelalamikiwa hadi koo kuwaka moto, Richa Adhia aliyeiwakilisha Tanzania katika Miss World amevurunda na wala hakupata nafasi ya kufurukuta.
Kilichosemwa na mrembo huyo ambaye rangi yake ilimweka mbali na mashabiki wengi wa urembo akasema kuwa Kamati ya Miss Tanzania imechangia yeye kuboronga.
Kimwana huyo akaweka wazi kwamba Kamati ya Miss Tanzania ilishindwa kuwahisha DVD yenye shughuli alizozifanya baada ya kuwa mrembo wa Tanzania katika Kamati ya Miss World.
Anacholalama Richa ni kwamba kama DVD yake ingewahi angekuwa na nafasi ya kushinda katika kipengele cha Urembo wa Malengo.
Hii ni bahati mbaya kwa mlimbwende huyo na wadau wa urembo nchini. Lakini yaweza semwa pia kuwa bado kuna kikwazo katika mchakato mzima wa kumsaka Miss Tanzania.
Mzee wa Busati alikuwa mmoja wa walionyesha shaka juu ya uwezo wa kimwana huyo katika uwakilishi wake katika mashindano hayo ya dunia.
Alichosema Mwandika Busati wakati huo ni kwamba ushindi wake ulijaa shaka na hata ndimi za mashabiki zimeendelea kuwa hivyo. Wengine wakasema pia kuwa kwani kulikuwa na ulazima gani wa kumvisha taji na kimwana huyo mwenye damu ya Kihindi?
Wanaojiita wanaharakati na watetezi wa haki za binadamu wakasema kuwa huo ni ubaguzi wa rangi. Lakini hoja ikabaki ile ile kwamba je, mrembo huyo anaujua vema utamaduni wa Kitanzania?
Pengine hoja hizo hazina nguvu tena kwani mambo yamekwenda na yamesikika sasa kilichobaki ni wenye mamlaka na urembo wajipange upya.
Lakini wakati wanajipanga upya Mzee wa Busati anawaza jambo moja ambalo laweza kuijengea heshima na Tanzania kwa ujumla wake.
Kwanini basi tusisitize kuwapo kwa Miss Bantu? Mashindano ambayo kwa hakika yanalenga moja kwa moja asili ya kina dada wengi hapa Bongo.
Kuwa Miss Bantu si jambo gumu kwa sababu kwa baadhi ya vigezo ambavyo Mwandika Busati anavielewa ni kwamba binti hahitaji kuwa mwembamba ili kupata sifa ya kupanda jukwaani.
Hiyo ndiyo burudani ya Miss Bantu. Kimwana na ‘minyama’ yake anakuwa huru kupanda jukwaani kusaka ushindi mbele ya majaji.
Hii maana yake ni kwamba mabinti washiriki hawabanwi kula na kunyaza miili yao. Inasemwa pia kuwa hata lugha si kikwazo, unanena Kiswahili utakavyo na wala hakuna haja ya kwenda inglishi kozi.
Mtazamo wa Mzee wa Busati ni kwamba kama mashindano ya Miss Bantu yatawekewa mkazo basi nasi siku moja tutaungana na Wakongo, Warundi, Waganda na Wakenya na kuanzisha mashindano ya kanda.
Wakifikia hatua hiyo ni wazi kuwa Afrika itakuwa na kitu chake manake matarajio ni kwamba yatapanuka hadi kwingineko.
Ndoto ya Mzee wa Busati ni kwamba ifike siku hata Wazungu na Wahindi vibonge nao waje washiriki mashindano hayo. Hata kama wao si Wabantu waruhusiwe kwa sifa yao ya ubonge.
Kwanini yatuwia vigumu kuamini mambo mema ya kwetu? Kwani lazima tufuate kila kitu kilichoanzishwa Ulaya? Bila shaka hakuna haja hiyo. Yawezekana mengine yakaanzia Afrika na kuwashangaza walioko nje ya Afrika.
Huo ni mtazamo tu na si lazima wote mkubaliane na Mwandika Busati leteni hoja zenu kwa mjadala na lengo liwe kufikia mwafaka.
Huenda ikasemwa kuwa Mzee wa Busati ni mwepesi wa kukata tamaa la hasha! Mwelekeo wetu katika mashindano hayo ya Wazungu si mwema na siasa za Miss World katu hatuziwezi.
Si mmesikia wiki iliyopita warembo kutoka Afrika walivyokuwa wakilalama? Walikuwa wakilalamikia ubaguzi. Walichosema wala si uzushi ni ukweli na wazi wa mambo.
Basi himizeni mashindano yenye kufanana na utamaduni wetu. Waacheni warembo wetu wa Kiafrika wawe na pahala pa kujitanua.
Msiwashindishe njaa eti ili waonekane warembo wenye sifa za kupanda jukwaani kuwania taji la Miss World. Waacheni wale matoke na maharagwe.
Vinginevyo kung’ang’ania hayo ya ughaibuni ni kuzidi kujaza nafasi na ghasia kwenye ardhi ya Wadanganyika.
Huu ndio ukomo wa Mwandika Busati kwa juma hili. Mwendo mdundo kwa kasi ya ajabu manake ujio wa Masiha unayumbisha fikra.
Ngwenje zinasakwa kwa kila mtindo, kihalali na kiharamu ili mradi mifuko yao ijazwe fedhwa kwa ajili ya Noeli na mwaka mpya.
Wasalaam,
YAMETIMIA! Hadithi imekuwa ile ile kwa Tanzania kuangukia pua kwenye mashindano ya urembo ya dunia.
Binti aliyelalamikiwa hadi koo kuwaka moto, Richa Adhia aliyeiwakilisha Tanzania katika Miss World amevurunda na wala hakupata nafasi ya kufurukuta.
Kilichosemwa na mrembo huyo ambaye rangi yake ilimweka mbali na mashabiki wengi wa urembo akasema kuwa Kamati ya Miss Tanzania imechangia yeye kuboronga.
Kimwana huyo akaweka wazi kwamba Kamati ya Miss Tanzania ilishindwa kuwahisha DVD yenye shughuli alizozifanya baada ya kuwa mrembo wa Tanzania katika Kamati ya Miss World.
Anacholalama Richa ni kwamba kama DVD yake ingewahi angekuwa na nafasi ya kushinda katika kipengele cha Urembo wa Malengo.
Hii ni bahati mbaya kwa mlimbwende huyo na wadau wa urembo nchini. Lakini yaweza semwa pia kuwa bado kuna kikwazo katika mchakato mzima wa kumsaka Miss Tanzania.
Mzee wa Busati alikuwa mmoja wa walionyesha shaka juu ya uwezo wa kimwana huyo katika uwakilishi wake katika mashindano hayo ya dunia.
Alichosema Mwandika Busati wakati huo ni kwamba ushindi wake ulijaa shaka na hata ndimi za mashabiki zimeendelea kuwa hivyo. Wengine wakasema pia kuwa kwani kulikuwa na ulazima gani wa kumvisha taji na kimwana huyo mwenye damu ya Kihindi?
Wanaojiita wanaharakati na watetezi wa haki za binadamu wakasema kuwa huo ni ubaguzi wa rangi. Lakini hoja ikabaki ile ile kwamba je, mrembo huyo anaujua vema utamaduni wa Kitanzania?
Pengine hoja hizo hazina nguvu tena kwani mambo yamekwenda na yamesikika sasa kilichobaki ni wenye mamlaka na urembo wajipange upya.
Lakini wakati wanajipanga upya Mzee wa Busati anawaza jambo moja ambalo laweza kuijengea heshima na Tanzania kwa ujumla wake.
Kwanini basi tusisitize kuwapo kwa Miss Bantu? Mashindano ambayo kwa hakika yanalenga moja kwa moja asili ya kina dada wengi hapa Bongo.
Kuwa Miss Bantu si jambo gumu kwa sababu kwa baadhi ya vigezo ambavyo Mwandika Busati anavielewa ni kwamba binti hahitaji kuwa mwembamba ili kupata sifa ya kupanda jukwaani.
Hiyo ndiyo burudani ya Miss Bantu. Kimwana na ‘minyama’ yake anakuwa huru kupanda jukwaani kusaka ushindi mbele ya majaji.
Hii maana yake ni kwamba mabinti washiriki hawabanwi kula na kunyaza miili yao. Inasemwa pia kuwa hata lugha si kikwazo, unanena Kiswahili utakavyo na wala hakuna haja ya kwenda inglishi kozi.
Mtazamo wa Mzee wa Busati ni kwamba kama mashindano ya Miss Bantu yatawekewa mkazo basi nasi siku moja tutaungana na Wakongo, Warundi, Waganda na Wakenya na kuanzisha mashindano ya kanda.
Wakifikia hatua hiyo ni wazi kuwa Afrika itakuwa na kitu chake manake matarajio ni kwamba yatapanuka hadi kwingineko.
Ndoto ya Mzee wa Busati ni kwamba ifike siku hata Wazungu na Wahindi vibonge nao waje washiriki mashindano hayo. Hata kama wao si Wabantu waruhusiwe kwa sifa yao ya ubonge.
Kwanini yatuwia vigumu kuamini mambo mema ya kwetu? Kwani lazima tufuate kila kitu kilichoanzishwa Ulaya? Bila shaka hakuna haja hiyo. Yawezekana mengine yakaanzia Afrika na kuwashangaza walioko nje ya Afrika.
Huo ni mtazamo tu na si lazima wote mkubaliane na Mwandika Busati leteni hoja zenu kwa mjadala na lengo liwe kufikia mwafaka.
Huenda ikasemwa kuwa Mzee wa Busati ni mwepesi wa kukata tamaa la hasha! Mwelekeo wetu katika mashindano hayo ya Wazungu si mwema na siasa za Miss World katu hatuziwezi.
Si mmesikia wiki iliyopita warembo kutoka Afrika walivyokuwa wakilalama? Walikuwa wakilalamikia ubaguzi. Walichosema wala si uzushi ni ukweli na wazi wa mambo.
Basi himizeni mashindano yenye kufanana na utamaduni wetu. Waacheni warembo wetu wa Kiafrika wawe na pahala pa kujitanua.
Msiwashindishe njaa eti ili waonekane warembo wenye sifa za kupanda jukwaani kuwania taji la Miss World. Waacheni wale matoke na maharagwe.
Vinginevyo kung’ang’ania hayo ya ughaibuni ni kuzidi kujaza nafasi na ghasia kwenye ardhi ya Wadanganyika.
Huu ndio ukomo wa Mwandika Busati kwa juma hili. Mwendo mdundo kwa kasi ya ajabu manake ujio wa Masiha unayumbisha fikra.
Ngwenje zinasakwa kwa kila mtindo, kihalali na kiharamu ili mradi mifuko yao ijazwe fedhwa kwa ajili ya Noeli na mwaka mpya.
Wasalaam,
Sunday, November 25, 2007
Tohara ya Ijumaa huanza Alhamisi
na innocent munyuku
KATIKA jamii nyingi za Kiafrika tohara ni mpango maalumu unaowalenga vijana wa kiume.
Mpango huo huwakusanya wahusika na kuwekwa jando ambako ni sehemu ya kufanyiwa tohara na kisha kupewa mafundisho kwa ajili ya maisha yao ya siku zijazo.
Hapa watafundwa juu ya ujasiri, uzalishaji mali na malezi kwa familia zao. Yaweza semwa kwamba jando ni pahala penye kutoa elimu kwa vijana.
Lakini kabla ya kuwekwa jando, huja maandalizi kwa ajili ya shughuli hiyo. Jando haliji kwa pupa kama kifanyavyo kimbunga. Mambo hupangwa yakanyooka.
Kutokana na umakini wa maandalizi hayo, ndio maana Waswahili wakaja na msemo kwamba tohara ya Ijumaa huanza Alhamisi. Kwamba kila jambo lafaa liwe na maandalizi badala ya papara.
Mzee wa Busati juma hili ameona anene juu ya hulka ya wadau wa soka nchini ambao kila uchao wamekuwa na ndoto ya kufika Kombe la Dunia lakini wanakwama kutokana na sababu mbalimbali.
Si mara moja au mbili washika kalamu na wenye uwezo wa kujenga hoja wameshasema juu ya vikwazo vilivyoko katika soka nchini.
Wameshahubiri juu ya nidhamu, programu endelevu, miradi na kubwa ni umuhimu wa kutambua kuwa soka nchini haiwezi kukua kama hakuna vitalu vya soka.
Mbaya zaidi ni kwamba wenye mamlaka katika uendeshaji wa mpira wa miguu nchini hawana jipya kwenye bongo zao.
Wamebaki kupiga porojo na kusahau kuwa pasipo vitalu vya soka mambo yatakwenda upogo.
Hao wamekaa kwenye viti wakisubiri kufika paradiso bila kuonja mauti. Wanahubiri na kuamini hadithi za Alfu Lela U Lela.
Wanaishi maisha ya kufikirika zaidi kuliko uhalisi wa mambo. Matokeo yake ni kwamba soka badala ya kupanda chati inageuka kuwa konokono kwenye sakafu iliyojaa chumvi. Vipaji vya soka vinapukutika.
Wamebakia kuamini ulozi kwenye viwanja vya soka na suala la maandalizi kwa miaka 50 ijayo hawanalo kwenye mipango yao. Wanawaza ya leo na si kesho.
Huko kwenye kusaka uchawi wameenea na idadi yao inaridhisha. Wamejaa tele kiasi kwamba hawaoni tena mwanga. Wamebaki gizani na wako radhi kuomba fedha kwa wafadhili eti kwa ajili ya kamati za ufundi.
Kamati ambazo wachezaji na viongozi waandamizi watalishwa madudu kama si kulala makaburi siku chache kabla ya mechi muhimu. Huo ndio mpira wetu!
Mzee wa Busati hasemi kwa ubaya bali kauli yake imetokana na kukerwa na haya magugu na mbigili kwenye soka.
Walau hivi karibuni wadau walipewa vidonge vya kule Bwagamoyo kwenye kile kilichoitwa semina elekezi ya wiki moja kwa klabu 14 za Ligi Kuu Bara.
Wakati wa kufunga semina hiyo, huku Mkurugenzi wa Maendeleo ya Soka wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), Ashford Mamelodi akizitaka klabu kuachana na ndumba.
Alichosema Mamelodi siku hiyo ni kwamba makocha na viongozi wa soka nchini wanao wajibu wa kujifunza masuala ya ufundi na uongozi.
Mamelodi ambaye ni Mkurugenzi wa Maendeleo wa FIFA Kanda ya Afrika, aliwataka washiriki wa semina kuyafanyia kazi yote waliyojifunza kwa maslahi ya timu zao na soka kwa ujumla, huku wakiweka kando masuala ya imani za kishirikina au ndumba katika mpira wa miguu.
Akasema semina hiyo haitakuwa ya maana kama waliyojifunza hawatayafanyia kazi.
“…matarajio ni kubadilika kuanzia sasa, kuanzia masuala ya utawala hadi ufundi huku mambo ya kishirikina yakiwekwa kando,” alisema Mamelodi.
Hakuishia hapo, kiongozi huyo akaweka wazi kwamba klabu kongwe kama Simba na Yanga zafaa ziwe mfano wa kuigwa.
Kwamba timu hizo sharti zionyeshe dira ya mabadiliko na kuachana kabisa na mambo ya kishirikina dimbani. Huo ndio mtazamo wake ambao bila kigugumizi unaungwa mkono na Mwandika Busati.
Hii maana yake ni kwamba kama klabu za Ligi Kuu zitakuwa na mwelekeo sahihi hakuna shaka timu nyingine zitaiga ufundi huo.
Mpira wa miguu haupelekwi kwa ndumba bali ufundi na kupanga dira ya maendeleo. Huo ndio ukweli kuhusu soka.
Tanzania imejaa vijana wenye vipaji vya hali ya juu katika soka. Hata hivyo, vipaji hivyo vitaibuka kama viongozi wa soka watafuata utawala bora.
Vipaji hivyo vitavuma na kutamba kimataifa kama kutakuwa na mpango mzuri katika maandalizi ya mashindano na mgawanyo wa kazi na pia kuachana na migogoro.
Kuendelea na mtazamo wa kizamani ni ni kuifukia soka kaburini. Yafaa basi samaki akunjwe angali mbichi.
Mzee wa Busati anaamini kwamba kama maandalizi yatakuwa makini hakuna shaka kwamba Tanzania itatoa wachezaji wengi wazuri watakaotamba kimataifa.
Hilo linawezekana kama tutakubali na kutambua kuwa tohara ya Ijumaa huanza Alhamisi. Acheni papara kuweni na mipango ya maandalizi.
Wasalaam,
KATIKA jamii nyingi za Kiafrika tohara ni mpango maalumu unaowalenga vijana wa kiume.
Mpango huo huwakusanya wahusika na kuwekwa jando ambako ni sehemu ya kufanyiwa tohara na kisha kupewa mafundisho kwa ajili ya maisha yao ya siku zijazo.
Hapa watafundwa juu ya ujasiri, uzalishaji mali na malezi kwa familia zao. Yaweza semwa kwamba jando ni pahala penye kutoa elimu kwa vijana.
Lakini kabla ya kuwekwa jando, huja maandalizi kwa ajili ya shughuli hiyo. Jando haliji kwa pupa kama kifanyavyo kimbunga. Mambo hupangwa yakanyooka.
Kutokana na umakini wa maandalizi hayo, ndio maana Waswahili wakaja na msemo kwamba tohara ya Ijumaa huanza Alhamisi. Kwamba kila jambo lafaa liwe na maandalizi badala ya papara.
Mzee wa Busati juma hili ameona anene juu ya hulka ya wadau wa soka nchini ambao kila uchao wamekuwa na ndoto ya kufika Kombe la Dunia lakini wanakwama kutokana na sababu mbalimbali.
Si mara moja au mbili washika kalamu na wenye uwezo wa kujenga hoja wameshasema juu ya vikwazo vilivyoko katika soka nchini.
Wameshahubiri juu ya nidhamu, programu endelevu, miradi na kubwa ni umuhimu wa kutambua kuwa soka nchini haiwezi kukua kama hakuna vitalu vya soka.
Mbaya zaidi ni kwamba wenye mamlaka katika uendeshaji wa mpira wa miguu nchini hawana jipya kwenye bongo zao.
Wamebaki kupiga porojo na kusahau kuwa pasipo vitalu vya soka mambo yatakwenda upogo.
Hao wamekaa kwenye viti wakisubiri kufika paradiso bila kuonja mauti. Wanahubiri na kuamini hadithi za Alfu Lela U Lela.
Wanaishi maisha ya kufikirika zaidi kuliko uhalisi wa mambo. Matokeo yake ni kwamba soka badala ya kupanda chati inageuka kuwa konokono kwenye sakafu iliyojaa chumvi. Vipaji vya soka vinapukutika.
Wamebakia kuamini ulozi kwenye viwanja vya soka na suala la maandalizi kwa miaka 50 ijayo hawanalo kwenye mipango yao. Wanawaza ya leo na si kesho.
Huko kwenye kusaka uchawi wameenea na idadi yao inaridhisha. Wamejaa tele kiasi kwamba hawaoni tena mwanga. Wamebaki gizani na wako radhi kuomba fedha kwa wafadhili eti kwa ajili ya kamati za ufundi.
Kamati ambazo wachezaji na viongozi waandamizi watalishwa madudu kama si kulala makaburi siku chache kabla ya mechi muhimu. Huo ndio mpira wetu!
Mzee wa Busati hasemi kwa ubaya bali kauli yake imetokana na kukerwa na haya magugu na mbigili kwenye soka.
Walau hivi karibuni wadau walipewa vidonge vya kule Bwagamoyo kwenye kile kilichoitwa semina elekezi ya wiki moja kwa klabu 14 za Ligi Kuu Bara.
Wakati wa kufunga semina hiyo, huku Mkurugenzi wa Maendeleo ya Soka wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), Ashford Mamelodi akizitaka klabu kuachana na ndumba.
Alichosema Mamelodi siku hiyo ni kwamba makocha na viongozi wa soka nchini wanao wajibu wa kujifunza masuala ya ufundi na uongozi.
Mamelodi ambaye ni Mkurugenzi wa Maendeleo wa FIFA Kanda ya Afrika, aliwataka washiriki wa semina kuyafanyia kazi yote waliyojifunza kwa maslahi ya timu zao na soka kwa ujumla, huku wakiweka kando masuala ya imani za kishirikina au ndumba katika mpira wa miguu.
Akasema semina hiyo haitakuwa ya maana kama waliyojifunza hawatayafanyia kazi.
“…matarajio ni kubadilika kuanzia sasa, kuanzia masuala ya utawala hadi ufundi huku mambo ya kishirikina yakiwekwa kando,” alisema Mamelodi.
Hakuishia hapo, kiongozi huyo akaweka wazi kwamba klabu kongwe kama Simba na Yanga zafaa ziwe mfano wa kuigwa.
Kwamba timu hizo sharti zionyeshe dira ya mabadiliko na kuachana kabisa na mambo ya kishirikina dimbani. Huo ndio mtazamo wake ambao bila kigugumizi unaungwa mkono na Mwandika Busati.
Hii maana yake ni kwamba kama klabu za Ligi Kuu zitakuwa na mwelekeo sahihi hakuna shaka timu nyingine zitaiga ufundi huo.
Mpira wa miguu haupelekwi kwa ndumba bali ufundi na kupanga dira ya maendeleo. Huo ndio ukweli kuhusu soka.
Tanzania imejaa vijana wenye vipaji vya hali ya juu katika soka. Hata hivyo, vipaji hivyo vitaibuka kama viongozi wa soka watafuata utawala bora.
Vipaji hivyo vitavuma na kutamba kimataifa kama kutakuwa na mpango mzuri katika maandalizi ya mashindano na mgawanyo wa kazi na pia kuachana na migogoro.
Kuendelea na mtazamo wa kizamani ni ni kuifukia soka kaburini. Yafaa basi samaki akunjwe angali mbichi.
Mzee wa Busati anaamini kwamba kama maandalizi yatakuwa makini hakuna shaka kwamba Tanzania itatoa wachezaji wengi wazuri watakaotamba kimataifa.
Hilo linawezekana kama tutakubali na kutambua kuwa tohara ya Ijumaa huanza Alhamisi. Acheni papara kuweni na mipango ya maandalizi.
Wasalaam,
Sunday, November 18, 2007
Isikieni ndoto ya Msagasoli
na innocent munyuku
NI heri uchoke viungo vyote vya mwili kuliko uchovu wa ubongo. Hii ni hatari kubwa inayoweza kukufanya uonekane hamnazo kwenye kaya.
Bila shaka umeshawahi kukumbana na hali hiyo japo mara moja kila mwezi, iwe mwanzo wa mwezi au katikati yake. Ndo yalomkuta Mzee wa Busati juzi.
Mwandika Busati katoka kwenye mihangaiko yake huko mjini kati. Kasaka nyoka hadi soli za viatu zikaimba tungo za maombolezo.
Si mchezo mwanawane kusaga mguu kutoka Posta Mpya hadi Magomeni. Kisa? Kupunguza ukali wa bajeti ili mambo yasizidi kwenda upogo! Si ndo waambiwa mjini shule. Usione watu wana vitambi ukadhani maisha yao supa la hasha. Wengine wameshiba mihogo ilo chacha.
Mambo ya mjini ndivyo yalivyo. Usimwone jirani yako ananukia bia kila siku ukadhani anazo ngwenje za kutosha. Anachofanya ni kupitia kwa Mama Ubaya anaonja glasi zake tatu za machozi ya simba af baada ya hapo anapitia kwa Massawe anameza safari lager mbili kazi imekishwa.
Basi Mzee wa Busati baada ya kufika Magomeni na Sh 200 yake kibindoni akakwea daladala kuelekea maskani. Kutokana na uchovu wa kusaga mguu kutwa nzima mara baada ya kupata kigoda akautandika usingizi.
Yaliko maskani yake ni mbali na ukichanganya na foleni za Darisalama ni wazi kwamba alipata muda wa kuota ndoto pia na yaliyojiri kwenye ndoto ni haya yafuatayo.
Mzee wa Busati kaota eti yu katika kilele cha Mlima Kilimanjaro, kajiviringisha blanketi kuinusuru ngozi yake na baridi kali. Huko kileleni akaziona klabu za soka nchini zikiishi kwa upendo.
Akawaona wanachama wa Simba na Yanga wakipanga foleni ndefu kuwania hisa kwenye klabu zao baada ya kukubaliana kuwa sasa ziendeshwe kibiashara zaidi.
Akaiona pia Ashanti United, Moro United na Mtibwa Sugar zikifuata nyayo za Simba na Yanga. Hakuna tena uzandiki ndani ya klabu.
Wale wanachama waliokuwa wakitoleana maneno ya kejeli na matusi ya nguoni wakawa wameketi pamoja wakinywa kahawa na kupeana mawazo ya kuiinua soka nchini.
Ndoto ya Mzee wa Busati ikakatishwa na kelele za kijana muuza maji kwenye foleni. Hata hivyo, baada ya muda akaendelea kuuchapa usingizi.
Safari hii usingizi ukaja na ndoto mpya. Ndoto ikahamia kwenye filamu Tanzania. Mwandika Busati akawaona wasanii wakisaka elimu ya filamu kwa umakini.
Ile hali aliyozoea siku zote ya mtu mmoja kuamka tu asubuhi na kujiita prodyuza ikatoweka. Sasa hawa wakawa nguli wenye ustadi na kazi zao.
Akaziona filamu zilizopikwa zikapikika na si tena mpango wa kwenda dukani na kukuta video zilizotayarishwa kwa siku 28 eti nazo zikaitwa sinema kali.
Ndoto ikawa tamu kweli kweli manake hata wale wanamuziki ambao Mzee wa Busati alizoea kuwasikia wakiimba mapenzi tu na kusifia mavazi wakatoweka.
Kwenye ndoto yake akawasikia wakikemea ufisadi na wala rushwa waliovimba matumbo kwa sababu ya kula visivyo vyao.
Akasikia tungo zilizojaa uzalendo na kuwakemea wachache wanaouza nchi kwa njaa ya teni pasenti. Hao ambao hawajali kwamba milima ya Uluguru yafaa ilindwe kwa vizazi vijavyo.
Hao ambao wanajifanya hamnazo wasijue kuwa madini yetu ni mali ya kulijenga taifa kwa vitegemezi vyetu ambavyo baadhi yao havijui hata urithi wao.
Ndoto ikawa tamu zaidi manake akajikuta anazuru mitaa mbalimbali na kukutana na Watanzania wakijivunia utaifa wao. Wanateta Kiswahili kwa ufasaha.
Mzee wa Busati akawaona raia wengi wakiwania kuingia kwenye kumbi kuangalia ngoma na michezo ya asili. Wengi sasa wakawa wameyapa kisogo mambo ya Kimagharibi. Hakuna aliyejali tena ya kigeni.
Kina dada wakaachana na nywele za bandia. Sasa wengi wakawa wanalilia nywele zao za asili zenye kipilipili. Midomo ya wanawali hao ikapendeza kwa mdaha huku kucha ziking’aa kwa hina ya mwituni.
Honi ya lori kubwa ndiyo iliyomwamsha Mzee wa Busati usingizini akiwa ndani ya daladala. Anageuka kushoto anajikuta yu kituo kimoja kabla ya kufika anapoteremkia.
Anapangusa uso lakini moyo wake umejaa kero baada ya kubaini kuwa kumbe ilikuwa ndoto na dada aliyekuwa kulia kwake alikuwa na nywele bandia na rangi ya mdomo kutoka dukani.
Wimbo uliokuwa ukitoka kwenye spika za daladala ulikuwa ukimsifia jamaa aliyevaa mavazi ya kifahari kutoka ughaibuni.
Heri angesikia ngoma za Morris Nyunyusa au Mzee Mwinamila. Mzee wa Busati akanywea asipate raha ya ndoto yake.
Lakini je, hatuwezi kuishi kwa ndoto hiyo? Kweli Wabongo hawawezi kuendeleza utamaduni wao na kuacha kukumbatia yanayoonekana kwenye vioo vya luninga?
Hivi ni kweli klabu za soka haziwezi kujiendesha kibiashara na kuacha hii staili ya kushikiana bakora?
Mzee wa Busati amefikia ukomo akiamini kuwa kila mwenye ubongo uliotulia anao uwezo wa kuleta tafakuri na kuweka mwafaka kwenye bakuli.
Wasalaam,
NI heri uchoke viungo vyote vya mwili kuliko uchovu wa ubongo. Hii ni hatari kubwa inayoweza kukufanya uonekane hamnazo kwenye kaya.
Bila shaka umeshawahi kukumbana na hali hiyo japo mara moja kila mwezi, iwe mwanzo wa mwezi au katikati yake. Ndo yalomkuta Mzee wa Busati juzi.
Mwandika Busati katoka kwenye mihangaiko yake huko mjini kati. Kasaka nyoka hadi soli za viatu zikaimba tungo za maombolezo.
Si mchezo mwanawane kusaga mguu kutoka Posta Mpya hadi Magomeni. Kisa? Kupunguza ukali wa bajeti ili mambo yasizidi kwenda upogo! Si ndo waambiwa mjini shule. Usione watu wana vitambi ukadhani maisha yao supa la hasha. Wengine wameshiba mihogo ilo chacha.
Mambo ya mjini ndivyo yalivyo. Usimwone jirani yako ananukia bia kila siku ukadhani anazo ngwenje za kutosha. Anachofanya ni kupitia kwa Mama Ubaya anaonja glasi zake tatu za machozi ya simba af baada ya hapo anapitia kwa Massawe anameza safari lager mbili kazi imekishwa.
Basi Mzee wa Busati baada ya kufika Magomeni na Sh 200 yake kibindoni akakwea daladala kuelekea maskani. Kutokana na uchovu wa kusaga mguu kutwa nzima mara baada ya kupata kigoda akautandika usingizi.
Yaliko maskani yake ni mbali na ukichanganya na foleni za Darisalama ni wazi kwamba alipata muda wa kuota ndoto pia na yaliyojiri kwenye ndoto ni haya yafuatayo.
Mzee wa Busati kaota eti yu katika kilele cha Mlima Kilimanjaro, kajiviringisha blanketi kuinusuru ngozi yake na baridi kali. Huko kileleni akaziona klabu za soka nchini zikiishi kwa upendo.
Akawaona wanachama wa Simba na Yanga wakipanga foleni ndefu kuwania hisa kwenye klabu zao baada ya kukubaliana kuwa sasa ziendeshwe kibiashara zaidi.
Akaiona pia Ashanti United, Moro United na Mtibwa Sugar zikifuata nyayo za Simba na Yanga. Hakuna tena uzandiki ndani ya klabu.
Wale wanachama waliokuwa wakitoleana maneno ya kejeli na matusi ya nguoni wakawa wameketi pamoja wakinywa kahawa na kupeana mawazo ya kuiinua soka nchini.
Ndoto ya Mzee wa Busati ikakatishwa na kelele za kijana muuza maji kwenye foleni. Hata hivyo, baada ya muda akaendelea kuuchapa usingizi.
Safari hii usingizi ukaja na ndoto mpya. Ndoto ikahamia kwenye filamu Tanzania. Mwandika Busati akawaona wasanii wakisaka elimu ya filamu kwa umakini.
Ile hali aliyozoea siku zote ya mtu mmoja kuamka tu asubuhi na kujiita prodyuza ikatoweka. Sasa hawa wakawa nguli wenye ustadi na kazi zao.
Akaziona filamu zilizopikwa zikapikika na si tena mpango wa kwenda dukani na kukuta video zilizotayarishwa kwa siku 28 eti nazo zikaitwa sinema kali.
Ndoto ikawa tamu kweli kweli manake hata wale wanamuziki ambao Mzee wa Busati alizoea kuwasikia wakiimba mapenzi tu na kusifia mavazi wakatoweka.
Kwenye ndoto yake akawasikia wakikemea ufisadi na wala rushwa waliovimba matumbo kwa sababu ya kula visivyo vyao.
Akasikia tungo zilizojaa uzalendo na kuwakemea wachache wanaouza nchi kwa njaa ya teni pasenti. Hao ambao hawajali kwamba milima ya Uluguru yafaa ilindwe kwa vizazi vijavyo.
Hao ambao wanajifanya hamnazo wasijue kuwa madini yetu ni mali ya kulijenga taifa kwa vitegemezi vyetu ambavyo baadhi yao havijui hata urithi wao.
Ndoto ikawa tamu zaidi manake akajikuta anazuru mitaa mbalimbali na kukutana na Watanzania wakijivunia utaifa wao. Wanateta Kiswahili kwa ufasaha.
Mzee wa Busati akawaona raia wengi wakiwania kuingia kwenye kumbi kuangalia ngoma na michezo ya asili. Wengi sasa wakawa wameyapa kisogo mambo ya Kimagharibi. Hakuna aliyejali tena ya kigeni.
Kina dada wakaachana na nywele za bandia. Sasa wengi wakawa wanalilia nywele zao za asili zenye kipilipili. Midomo ya wanawali hao ikapendeza kwa mdaha huku kucha ziking’aa kwa hina ya mwituni.
Honi ya lori kubwa ndiyo iliyomwamsha Mzee wa Busati usingizini akiwa ndani ya daladala. Anageuka kushoto anajikuta yu kituo kimoja kabla ya kufika anapoteremkia.
Anapangusa uso lakini moyo wake umejaa kero baada ya kubaini kuwa kumbe ilikuwa ndoto na dada aliyekuwa kulia kwake alikuwa na nywele bandia na rangi ya mdomo kutoka dukani.
Wimbo uliokuwa ukitoka kwenye spika za daladala ulikuwa ukimsifia jamaa aliyevaa mavazi ya kifahari kutoka ughaibuni.
Heri angesikia ngoma za Morris Nyunyusa au Mzee Mwinamila. Mzee wa Busati akanywea asipate raha ya ndoto yake.
Lakini je, hatuwezi kuishi kwa ndoto hiyo? Kweli Wabongo hawawezi kuendeleza utamaduni wao na kuacha kukumbatia yanayoonekana kwenye vioo vya luninga?
Hivi ni kweli klabu za soka haziwezi kujiendesha kibiashara na kuacha hii staili ya kushikiana bakora?
Mzee wa Busati amefikia ukomo akiamini kuwa kila mwenye ubongo uliotulia anao uwezo wa kuleta tafakuri na kuweka mwafaka kwenye bakuli.
Wasalaam,
Jihadharini na wafadhili wa siri katika siasa
Na Innocent Munyuku
HAKUNA jambo jema katika jamii kama uwazi na ukweli. Kwamba ili mambo yasiende upogo sharti mojawapo ni kuwa wazi na mkweli daima.
Kaya au jamii isiyo wazi mara zote itakuwa katika migogoro ya aina mbalimbali kwa sababu tu mambo mengi yamefichwa.
Kipato cha baba au mama kwa familia kikiwa siri basi hakuna shaka kwamba familia hiyo itakuwa kwenye mikwaruzo ya hapa na pale.
Wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa rais na wabunge mwaka 2005 kulikuwa na hoja kutoka kwa vyama vya Upinzani kwamba Chama Cha Mapinduzi kiliendesha kampeni zake kwa fedha ‘haramu’.
Watoa hoja hawakunyamaza bali wameendelea kulisema hilo hata baada ya uchaguzi kwamba sehemu kubwa ya fedha za kampeni kwa CCM hazikufahamika zimetoka wapi.
Wananchi wanaounga mkono upande wa Upinzani nao wanalijadili hilo vijiweni kila wanapopata muda wa kufanya hivyo.
Baada ya Rais wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jakaya Kikwete kufunga Mkuu wa Nane wa chama hicho, mjini Dodoma siku chache zilizopita akiwa jijini Dar es Salaam alitoa kauli iliyonivuta kuandika waraka huu mfupi.
Rais Kikwete aliwahutubia wananchi waliomlaki Ofisi Ndogo ya CCM Lumumba jijini Dar es Salaam ambako pamoja na mambo mengine alisisitiza umuhimu wa chama kuwa na vitega uchumi.
Alichosema Rais Kikwete siku ile ni kwamba CCM ijipange kutafuta namna ya kuwa na vipato mbadala ili wakati wa kampeni kusiwe na minong’ono kuhusu vyanzo vya fedha.
Bila shaka kauli ya Rais imekuja baada ya kuzuka minong’ono kuhusu mapato ya CCM wakati wa kampeni kwenye uchaguzi uliopita.
Rais kanena umuhimu wa kuwa na vyanzo vya fedha vilivyo wazi kwa chama chake lakini kwa mtazamo wangu zumari alilopiga mkuu wa nchi ni vema likasikilizwa na vyama vingine pia.
Kwamba vyama vyote vya siasa nchini viwe wazi kuhusu mapato yake. Wawaeleze wananchi wanakopata fedha za kuzunguka nchi nzima kumwaga sera zao kwa ajili ya kujiongezea uhai wa chama na wanachama.
Leo hii ni jambo lisilohitaji mjadala mrefu kwani vyama vingi sasa vinaangalia namna ya kupata ushindi katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2010.
Kama inavyofahamika, kampeni zozote za uchaguzi kote duniani zinahitaji fedha za kutosha ili kuwafikia wapigakura. Hii maana yake ni kwamba vyama vinajipanga sasa kuangalia ni namna gani wanatunisha mifuko yao.
Lakini kwa bahati mbaya sana hapa kwetu hakuna utamaduni wa kuweka bayana juu ya vyanzo vya mapato kwa vyama vya siasa badala yake utasikia minong’ono kwamba mfanyabiashara fulani katoa kiasi fulani cha fedha.
Ingawa wapo wafanyabiashara wanaojitangaza wazi kwamba wametoa kiasi fulani cha fedha kwa chama fulani, bado ni haki ya wananchi kujua fedha nyingine zimetokana na nini.
Nasisitiza uwazi wa vyanzo vya fedha kutokana na ukweli kwamba yawezekana ikaja siku, fedha za kampeni zikatokana na mauzo ya dawa za kulevya au njia nyingine haramu hatarishi kwa taifa lililo huru.
Tuelezwe pasipo kificho kwamba mabilioni haya yametokana na michango ya aina hii au msaada kutoka taasisi fulani iwe ya ndani ya nje ya nchi.
Kama ni fedha za wafadhili pia tuelezwe ni wa aina gani na zimetolewa kwa masharti gani.
Kukaa kimya hakuna maana nyingine zaidi ya kuendelea kuzua minong’ono ambayo ingeweza kufutwa kama kila kitu kingewekwa hadharani.
Nalisema hili kwa sababu mwaka 2010 si mbali kutoka hivi sasa na bila shaka baadhi ya vyama vya siasa vimeshaanza kukusanya fedha kwa ajili ya uchaguzi ujao.
Hivyo basi, wakati ukifika ni busara kuwaeleza wananchi nani kafanya kipi kufanikisha mizunguko ya kampeni.
Vinginevyo ipo siku tutashuhudia wafadhili wa siri wakidai kulipwa fadhila kwa mtindo wa kuliangamiza taifa. Tusifikishane huko.
HAKUNA jambo jema katika jamii kama uwazi na ukweli. Kwamba ili mambo yasiende upogo sharti mojawapo ni kuwa wazi na mkweli daima.
Kaya au jamii isiyo wazi mara zote itakuwa katika migogoro ya aina mbalimbali kwa sababu tu mambo mengi yamefichwa.
Kipato cha baba au mama kwa familia kikiwa siri basi hakuna shaka kwamba familia hiyo itakuwa kwenye mikwaruzo ya hapa na pale.
Wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa rais na wabunge mwaka 2005 kulikuwa na hoja kutoka kwa vyama vya Upinzani kwamba Chama Cha Mapinduzi kiliendesha kampeni zake kwa fedha ‘haramu’.
Watoa hoja hawakunyamaza bali wameendelea kulisema hilo hata baada ya uchaguzi kwamba sehemu kubwa ya fedha za kampeni kwa CCM hazikufahamika zimetoka wapi.
Wananchi wanaounga mkono upande wa Upinzani nao wanalijadili hilo vijiweni kila wanapopata muda wa kufanya hivyo.
Baada ya Rais wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jakaya Kikwete kufunga Mkuu wa Nane wa chama hicho, mjini Dodoma siku chache zilizopita akiwa jijini Dar es Salaam alitoa kauli iliyonivuta kuandika waraka huu mfupi.
Rais Kikwete aliwahutubia wananchi waliomlaki Ofisi Ndogo ya CCM Lumumba jijini Dar es Salaam ambako pamoja na mambo mengine alisisitiza umuhimu wa chama kuwa na vitega uchumi.
Alichosema Rais Kikwete siku ile ni kwamba CCM ijipange kutafuta namna ya kuwa na vipato mbadala ili wakati wa kampeni kusiwe na minong’ono kuhusu vyanzo vya fedha.
Bila shaka kauli ya Rais imekuja baada ya kuzuka minong’ono kuhusu mapato ya CCM wakati wa kampeni kwenye uchaguzi uliopita.
Rais kanena umuhimu wa kuwa na vyanzo vya fedha vilivyo wazi kwa chama chake lakini kwa mtazamo wangu zumari alilopiga mkuu wa nchi ni vema likasikilizwa na vyama vingine pia.
Kwamba vyama vyote vya siasa nchini viwe wazi kuhusu mapato yake. Wawaeleze wananchi wanakopata fedha za kuzunguka nchi nzima kumwaga sera zao kwa ajili ya kujiongezea uhai wa chama na wanachama.
Leo hii ni jambo lisilohitaji mjadala mrefu kwani vyama vingi sasa vinaangalia namna ya kupata ushindi katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2010.
Kama inavyofahamika, kampeni zozote za uchaguzi kote duniani zinahitaji fedha za kutosha ili kuwafikia wapigakura. Hii maana yake ni kwamba vyama vinajipanga sasa kuangalia ni namna gani wanatunisha mifuko yao.
Lakini kwa bahati mbaya sana hapa kwetu hakuna utamaduni wa kuweka bayana juu ya vyanzo vya mapato kwa vyama vya siasa badala yake utasikia minong’ono kwamba mfanyabiashara fulani katoa kiasi fulani cha fedha.
Ingawa wapo wafanyabiashara wanaojitangaza wazi kwamba wametoa kiasi fulani cha fedha kwa chama fulani, bado ni haki ya wananchi kujua fedha nyingine zimetokana na nini.
Nasisitiza uwazi wa vyanzo vya fedha kutokana na ukweli kwamba yawezekana ikaja siku, fedha za kampeni zikatokana na mauzo ya dawa za kulevya au njia nyingine haramu hatarishi kwa taifa lililo huru.
Tuelezwe pasipo kificho kwamba mabilioni haya yametokana na michango ya aina hii au msaada kutoka taasisi fulani iwe ya ndani ya nje ya nchi.
Kama ni fedha za wafadhili pia tuelezwe ni wa aina gani na zimetolewa kwa masharti gani.
Kukaa kimya hakuna maana nyingine zaidi ya kuendelea kuzua minong’ono ambayo ingeweza kufutwa kama kila kitu kingewekwa hadharani.
Nalisema hili kwa sababu mwaka 2010 si mbali kutoka hivi sasa na bila shaka baadhi ya vyama vya siasa vimeshaanza kukusanya fedha kwa ajili ya uchaguzi ujao.
Hivyo basi, wakati ukifika ni busara kuwaeleza wananchi nani kafanya kipi kufanikisha mizunguko ya kampeni.
Vinginevyo ipo siku tutashuhudia wafadhili wa siri wakidai kulipwa fadhila kwa mtindo wa kuliangamiza taifa. Tusifikishane huko.
Monday, November 12, 2007
Mkiitwa majinuni msirushe ngumi
na innocent munyuku
IKITOKEA binadamu akatoa maneno ya vichekesho na yasiyo na maana basi huyo ataitwa majinuni. Huyu hupachikwa kofia hiyo kwa sababu hana akili sawa sawa.
Pahala pengine mtu wa aina hiyo hutajwa kuwa ni punguani, mwendawazimu, kichaa ama wakati mwingine huitwa bahau.
Yawezekana mtu wa aina hiyo asifikie hatua ya kuvua nguo hadharani na kusomba kila akionacho lakini ukweli ni kwamba wapo binadamu ambao katika utendaji wao wa kazi hawana tofauti na vichaa wanaozagaa mitaani.
Ukiona dereva anayevunja sheria za usalama barabarani kwa kupenda mwendo kasi katika eneo lililokatazwa basi huyo ni punguani.
Hali kadhalika kwa muuguzi na daktari kutenda yasiyotarajiwa katika fani yao hapo watakuwa wamejihalalishia kuitwa vichaa au wendawazimu.
Mzee wa Busati leo wiki hii ameona ni vema kuwekana sawa katika majukumu ya kila siku kwenye klabu za soka.
Usiposikia moto wawaka Yanga basi ni Simba au kwenye vyama vya soka ndani ya Tanzania. Huko ni vurugu mtindo mmoja.
Huko utakutana na mahuluti kwa maana ya mchanganyiko wa watu wenye mawazo tofauti. Huyu anawaza begi mwingine anafikiria sanduku.
Kwa maana hiyo hata wanapoketi kwenye mikutano na kuleta mjadala, hakuna linalokwenda sawia. Hayaendi sawa kwa sababu kila mmoja la lwake.
Kuna msemo maarufu kwenye klabu hizo za soka. Kwamba uongozi umepinduliwa. Hii ni staili ya miaka mingi nchini. Kundi fulani la kihuni linajikusanya na kutangaza maasi.
Hilo si kwa Simba pekee bali hata Yanga. Kwa maneno mengine jambo hilo lipo kwenye ndimi za wanachama wa klabu hizo kama ilivyo sala ya ‘Baba Yetu’ kwa Wakristo.
Ni heri kwao wanaojiita wanamapinduzi wakaja na fikra pevu za kujenga klabu na soka kwa ujumla. Wangeleta mageuzi chanya na si hasi kama wafanyavyo sasa.
Kwa mtazamo wa Mzee wa Busati kinachofanywa kwenye klabu hizi ni uhuni usiokuwa na mfanowe. Ubabaishaji uliojaa simulizi za lege lege.
Mwenye Busati pengine aulize, kwa mfano hili fukuto la Simba kati ya kina Rubeya na Dalali nani ananufaika nalo? Kelele kibao na ghasia ambazo zingeweza kuzuilika.
Leo twaimba wimbo wa kuijenga Tanzania katika medani ya soka. Miezi michache nyuma sifa ziliwaelemea wachezaji wa timu ya taifa waliokuwa wakisaka tiketi ya kwenda fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika nchini Ghana.
Bendera na fulana zikachapishwa kwa wingi, wenye bahati zao msimu huo ukawa wa mavuno. Wakajaza pochi zao kwa ngwenje kwa kuuza sura za kina Mapunda na Henry Joseph.
Ingawa safari ya Ghana imeota mbaya ukweli wa mambo ni kwamba mshikamano ule wa mashabiki wa soka haukuwa na maana nyingine zaidi ya mapenzi kwa timu yao ya taifa.
Wabongo wamezoea kuzililia Simba na Yanga lakini siku ile Msumbiji ilipomaliza ndoto ya Stars kwenda Ghana, waliungana kwa kilio na majonzi. Huo ni mshikamano wa dhati.
Taswira hapo ni kwamba walio wengi wanapenda soka lakini wanakwamishwa na utawala hasa katika ngazi za klabu. Huko kuna mbigili na magugu sugu.
Anachosema Mzee wa Busati ni kwamba wahuni waliojaa kwenye klabu za soka nchini ndio wanaosababisha kukwama kwa uundaji wa timu ya taifa makini.
Hivi mwatarajia kuwe na timu ya taifa yenye ubora wakati huko chini ni vurugu tupu? Nani kawafunda hayo?
Uhuni na uzandiki unaoendelea katika soka hivi sasa hauna lolote la maana zaidi ya kuua mwelekeo mwema wa soka.
Soga na porojo zinazoendelea katika klabu za soka hazina budi kukomeshwa kwa maslahi ya taifa. Vinginevyo tukubali kuendelea kuwashabikia wenzetu wa ng’ambo.
Endeleeni kuvuruga ili mbaki kuvaa fulana za wachezaji wa ughaibuni huku wa kwenu wakikaa vijiweni kusubiri mia mbili ya kahawa.
Lakini Mzee wa Busati kabla hajafikia ukingoni pengine aweke mambo hadharani kwamba kwenu nyie mnaovuruga mambo ya soka msije kurusha ngumi siku mtakapoitwa majinuni.
Msihamaki wala kushika panga kwani hiyo ni halali kwenu. Kuitwa wehu ni zawadi mwafaka kwenu na wahuni wenzenu wanaowarubuni kuharibu mambo.
Mwandika Busati katoa mwanga. Wapo wengine wenye uwezo wa kuasa ni heri wakafanya hayo ili taifa lisiwe la mabahau.
Wasalaam,
IKITOKEA binadamu akatoa maneno ya vichekesho na yasiyo na maana basi huyo ataitwa majinuni. Huyu hupachikwa kofia hiyo kwa sababu hana akili sawa sawa.
Pahala pengine mtu wa aina hiyo hutajwa kuwa ni punguani, mwendawazimu, kichaa ama wakati mwingine huitwa bahau.
Yawezekana mtu wa aina hiyo asifikie hatua ya kuvua nguo hadharani na kusomba kila akionacho lakini ukweli ni kwamba wapo binadamu ambao katika utendaji wao wa kazi hawana tofauti na vichaa wanaozagaa mitaani.
Ukiona dereva anayevunja sheria za usalama barabarani kwa kupenda mwendo kasi katika eneo lililokatazwa basi huyo ni punguani.
Hali kadhalika kwa muuguzi na daktari kutenda yasiyotarajiwa katika fani yao hapo watakuwa wamejihalalishia kuitwa vichaa au wendawazimu.
Mzee wa Busati leo wiki hii ameona ni vema kuwekana sawa katika majukumu ya kila siku kwenye klabu za soka.
Usiposikia moto wawaka Yanga basi ni Simba au kwenye vyama vya soka ndani ya Tanzania. Huko ni vurugu mtindo mmoja.
Huko utakutana na mahuluti kwa maana ya mchanganyiko wa watu wenye mawazo tofauti. Huyu anawaza begi mwingine anafikiria sanduku.
Kwa maana hiyo hata wanapoketi kwenye mikutano na kuleta mjadala, hakuna linalokwenda sawia. Hayaendi sawa kwa sababu kila mmoja la lwake.
Kuna msemo maarufu kwenye klabu hizo za soka. Kwamba uongozi umepinduliwa. Hii ni staili ya miaka mingi nchini. Kundi fulani la kihuni linajikusanya na kutangaza maasi.
Hilo si kwa Simba pekee bali hata Yanga. Kwa maneno mengine jambo hilo lipo kwenye ndimi za wanachama wa klabu hizo kama ilivyo sala ya ‘Baba Yetu’ kwa Wakristo.
Ni heri kwao wanaojiita wanamapinduzi wakaja na fikra pevu za kujenga klabu na soka kwa ujumla. Wangeleta mageuzi chanya na si hasi kama wafanyavyo sasa.
Kwa mtazamo wa Mzee wa Busati kinachofanywa kwenye klabu hizi ni uhuni usiokuwa na mfanowe. Ubabaishaji uliojaa simulizi za lege lege.
Mwenye Busati pengine aulize, kwa mfano hili fukuto la Simba kati ya kina Rubeya na Dalali nani ananufaika nalo? Kelele kibao na ghasia ambazo zingeweza kuzuilika.
Leo twaimba wimbo wa kuijenga Tanzania katika medani ya soka. Miezi michache nyuma sifa ziliwaelemea wachezaji wa timu ya taifa waliokuwa wakisaka tiketi ya kwenda fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika nchini Ghana.
Bendera na fulana zikachapishwa kwa wingi, wenye bahati zao msimu huo ukawa wa mavuno. Wakajaza pochi zao kwa ngwenje kwa kuuza sura za kina Mapunda na Henry Joseph.
Ingawa safari ya Ghana imeota mbaya ukweli wa mambo ni kwamba mshikamano ule wa mashabiki wa soka haukuwa na maana nyingine zaidi ya mapenzi kwa timu yao ya taifa.
Wabongo wamezoea kuzililia Simba na Yanga lakini siku ile Msumbiji ilipomaliza ndoto ya Stars kwenda Ghana, waliungana kwa kilio na majonzi. Huo ni mshikamano wa dhati.
Taswira hapo ni kwamba walio wengi wanapenda soka lakini wanakwamishwa na utawala hasa katika ngazi za klabu. Huko kuna mbigili na magugu sugu.
Anachosema Mzee wa Busati ni kwamba wahuni waliojaa kwenye klabu za soka nchini ndio wanaosababisha kukwama kwa uundaji wa timu ya taifa makini.
Hivi mwatarajia kuwe na timu ya taifa yenye ubora wakati huko chini ni vurugu tupu? Nani kawafunda hayo?
Uhuni na uzandiki unaoendelea katika soka hivi sasa hauna lolote la maana zaidi ya kuua mwelekeo mwema wa soka.
Soga na porojo zinazoendelea katika klabu za soka hazina budi kukomeshwa kwa maslahi ya taifa. Vinginevyo tukubali kuendelea kuwashabikia wenzetu wa ng’ambo.
Endeleeni kuvuruga ili mbaki kuvaa fulana za wachezaji wa ughaibuni huku wa kwenu wakikaa vijiweni kusubiri mia mbili ya kahawa.
Lakini Mzee wa Busati kabla hajafikia ukingoni pengine aweke mambo hadharani kwamba kwenu nyie mnaovuruga mambo ya soka msije kurusha ngumi siku mtakapoitwa majinuni.
Msihamaki wala kushika panga kwani hiyo ni halali kwenu. Kuitwa wehu ni zawadi mwafaka kwenu na wahuni wenzenu wanaowarubuni kuharibu mambo.
Mwandika Busati katoa mwanga. Wapo wengine wenye uwezo wa kuasa ni heri wakafanya hayo ili taifa lisiwe la mabahau.
Wasalaam,
Wednesday, November 7, 2007
Ranking Boy: Reggae ilete mijadala yenye suluhu
na innocent munyuku
KAMA ningetakiwa kuwataja wanamuziki wa reggae wenye dira njema ya maelekeo nchini basi nisingesita kumweka Ranking Boy kundini.
Hivi karibuni mwanamuziki huyo amefanya mahojiano na Mtanzania na kuweka wazi mikakati yake na vikwazo katika muziki huo nchini.
Ranking Boy ambaye si mzungumzaji lakini mahiri jukwaani ashikapo maikrofoni upole na ‘ububu’ wake hauonekani. Anatema cheche za ajabu akitoa elimu na burudani.
Ana mambo mengi anayoyaandaa mojawapo ni kuipua albamu yake mpya mapema mwezi ujao. Albamu hiyo ameipachika jina la More Than Dread.
“Natarajia albamu yangu ya More Than Dread itakuwa sokoni mapema Desemba na itatoka pamoja na video yake,” anaeleza Ranking Boy.
Mwanamuziki huyo mbali na kuimba reggae anamudu pia raga na midundo dance hall huku akiwa na uwezo wa kutumia ala mbalimbali.
Alianza kujikita katika fani ya muziki mwaka 1998 na baada ya siku chache akahamishia makazi yake nchini Kenya na Uganda akifanya kazi zake za muziki kwa miaka minne nje ya Tanzania.
Ni katika kipindi hicho, Ranking Boy alifanikiwa kufyatua single nne ambazo ni Medicine, Matatizo, Fiesta na Ghetto.
“Nyimbo zangu kwa kweli zinajieleza kwa mfano wimbo wa Matatizo nimesema ukweli juu ya hali halisi ya maisha ya kila siku,” anasema na kisha kuongeza:
“Kila kukicha nchi inaendelea kuwa masikini na watu kwa hakika wanataabika…kwa hiyo nimejaribu kuelezea hali hiyo katika wimbo wangu huo.”
Anasema baada ya kuishi nje ya Tanzania kwa takribani miaka minne aliamua kurejea nchini kuendelea na shughuli zake za muziki wa reggae.
“Mwaka jana nikatua nchini kwa lengo la kuendeleza muziki wa reggae. Nikaja na wimbo wa Fire Ban Dem Head. Nashukuru kwamba single hii ilifanya vizuri na redio nyingi wameendelea kuupiga.
“Kufanya vizuri kwa wimbo huo kukanipa nguvu sana na ndio maana si rahisi kusema kuwa naweza kukata tamaa,” anasema mwanamuziki huyo ambaye tayari ana albamu nyingine ya Dad Fred.
Ranking Boy kwa sasa anaandaa kuzindua mradi maalumu wa muziki wa reggae aliouita Reggae Search utakaodumu kwa mwaka mmoja.
“Lengo la mradi huu ni kuwakusanya wasanii wachanga wa muziki wa reggae na kuwapa dira mpya.
“Muziki wa reggae lazima tukubali pia unahitaji fikra mpya. Hatuwezi kuishi kama walivyoishi wanamuziki wa kale mambo yamebadilika,” anasema na kuongeza:
“Lakini hii haina maana kwamba tunakwepa misingi ya muziki wa reggae hapana. Ninachosema ni kwamba tuwe tayari kwa mabadiliko.”
Anasema anaamini kuwa kuwa na vijana wadogo katika reggae kutawezesha muziki huo kuwa na uhai hasa katika Afrika.
“Mpango wa kuwasaka vijana umeshaanza na hii naweza kusema kuwa ni project ya Afrika Mashariki nzima.
“Kwanza tutawafundisha hao wachanga na baadaye kuwapa muda wa kutunga nyimbo na hapo tutaangalia wimbo gani bora. Lengo hapa ni kuleta ushindani,” anasema.
Anaeleza kuwa anafarijika kuona kuwa wadau wake kutoka Uganda na Kenya wanatoa ushirikiano mzuri na hivyo anaamini kuwa mradi huo wa reggae utazaa matunda mema.
“Ushirikiano unatia moyo kwa kiasi kikubwa, watu wana mwamko sana. Naweza kusema kuwa sasa reggae inakwenda katika neema zaidi kuliko miaka ya nyuma.”
Lakini anasisitiza kuwa kuna haja ya wanamuziki wa reggae kwenda mbele na kuacha imani kwamba lazima kuiga kila jambo la waliopita.
“Kila kizazi kina mambo yake. Ya kale ni kama mwongozo kwamba wenzetu walifanya nini na sisi kazi yetu ni kuboresha.
“Nitatoa mfano kwamba enzi za kina Kalikawe si za sasa na kama mimi sasa nakuja na mtindo wa Bongo Jamaica.
“Bongo Jamaica ni mtindo mpya ambao ni mchanganyiko wa vionjo kutoka Jamaica na ukanda wa Afrika Mashariki. Nami muda wangu ukimalizika watakuja wengine na vionjo vyao,” anasema Ranking Boy.
Hata hivyo, bado anasisitiza kuwa kazi kubwa ya muziki wa reggae ni kuleta mapinduzi ya fikra.
“Huu si muziki wa porojo, muziki wa reggae lazima ulenge mabadiliko katika jamii na si malumbano au hoja ambazo hazina kichwa wala miguu.
“Reggae ilete mijadala yenye ufumbuzi na si kujadili mambo ambayo hayana suluhisho,” anasema Ranking Boy.
Pamoja na hilo, Ranking Boy anasema kuwa katika muziki wa reggae nchini kuna kikwazo ambacho hakina budi kuondolewa.
Anasema tatizo kubwa miongoni mwa wanamuziki hao ni kukosa ushirikiano wa dhati.
“Inashangaza sana na binafsi jambo hili linanikera kwamba hatuna ushirikiano wa kweli. Huo ni uwazi kwamba hatuna umoja.
“Kila mmoja yuko kivyake na hii maana yake ni kwamba mipango mingi itavurugika na tutabaki kulalama.”
Pamoja na yote hayo, msanii huyo ana faraja kuona kuwa muziki wa reggae kwa kiasi kikubwa unakubalika nchini.
“Zamani ilionekana kama kuimba reggae ni kuhamasisha uvutaji bangi lakini sasa mambo yamegeuka hata watu wazima wanapenda reggae,” anaeleza Ranking Boy.
KAMA ningetakiwa kuwataja wanamuziki wa reggae wenye dira njema ya maelekeo nchini basi nisingesita kumweka Ranking Boy kundini.
Hivi karibuni mwanamuziki huyo amefanya mahojiano na Mtanzania na kuweka wazi mikakati yake na vikwazo katika muziki huo nchini.
Ranking Boy ambaye si mzungumzaji lakini mahiri jukwaani ashikapo maikrofoni upole na ‘ububu’ wake hauonekani. Anatema cheche za ajabu akitoa elimu na burudani.
Ana mambo mengi anayoyaandaa mojawapo ni kuipua albamu yake mpya mapema mwezi ujao. Albamu hiyo ameipachika jina la More Than Dread.
“Natarajia albamu yangu ya More Than Dread itakuwa sokoni mapema Desemba na itatoka pamoja na video yake,” anaeleza Ranking Boy.
Mwanamuziki huyo mbali na kuimba reggae anamudu pia raga na midundo dance hall huku akiwa na uwezo wa kutumia ala mbalimbali.
Alianza kujikita katika fani ya muziki mwaka 1998 na baada ya siku chache akahamishia makazi yake nchini Kenya na Uganda akifanya kazi zake za muziki kwa miaka minne nje ya Tanzania.
Ni katika kipindi hicho, Ranking Boy alifanikiwa kufyatua single nne ambazo ni Medicine, Matatizo, Fiesta na Ghetto.
“Nyimbo zangu kwa kweli zinajieleza kwa mfano wimbo wa Matatizo nimesema ukweli juu ya hali halisi ya maisha ya kila siku,” anasema na kisha kuongeza:
“Kila kukicha nchi inaendelea kuwa masikini na watu kwa hakika wanataabika…kwa hiyo nimejaribu kuelezea hali hiyo katika wimbo wangu huo.”
Anasema baada ya kuishi nje ya Tanzania kwa takribani miaka minne aliamua kurejea nchini kuendelea na shughuli zake za muziki wa reggae.
“Mwaka jana nikatua nchini kwa lengo la kuendeleza muziki wa reggae. Nikaja na wimbo wa Fire Ban Dem Head. Nashukuru kwamba single hii ilifanya vizuri na redio nyingi wameendelea kuupiga.
“Kufanya vizuri kwa wimbo huo kukanipa nguvu sana na ndio maana si rahisi kusema kuwa naweza kukata tamaa,” anasema mwanamuziki huyo ambaye tayari ana albamu nyingine ya Dad Fred.
Ranking Boy kwa sasa anaandaa kuzindua mradi maalumu wa muziki wa reggae aliouita Reggae Search utakaodumu kwa mwaka mmoja.
“Lengo la mradi huu ni kuwakusanya wasanii wachanga wa muziki wa reggae na kuwapa dira mpya.
“Muziki wa reggae lazima tukubali pia unahitaji fikra mpya. Hatuwezi kuishi kama walivyoishi wanamuziki wa kale mambo yamebadilika,” anasema na kuongeza:
“Lakini hii haina maana kwamba tunakwepa misingi ya muziki wa reggae hapana. Ninachosema ni kwamba tuwe tayari kwa mabadiliko.”
Anasema anaamini kuwa kuwa na vijana wadogo katika reggae kutawezesha muziki huo kuwa na uhai hasa katika Afrika.
“Mpango wa kuwasaka vijana umeshaanza na hii naweza kusema kuwa ni project ya Afrika Mashariki nzima.
“Kwanza tutawafundisha hao wachanga na baadaye kuwapa muda wa kutunga nyimbo na hapo tutaangalia wimbo gani bora. Lengo hapa ni kuleta ushindani,” anasema.
Anaeleza kuwa anafarijika kuona kuwa wadau wake kutoka Uganda na Kenya wanatoa ushirikiano mzuri na hivyo anaamini kuwa mradi huo wa reggae utazaa matunda mema.
“Ushirikiano unatia moyo kwa kiasi kikubwa, watu wana mwamko sana. Naweza kusema kuwa sasa reggae inakwenda katika neema zaidi kuliko miaka ya nyuma.”
Lakini anasisitiza kuwa kuna haja ya wanamuziki wa reggae kwenda mbele na kuacha imani kwamba lazima kuiga kila jambo la waliopita.
“Kila kizazi kina mambo yake. Ya kale ni kama mwongozo kwamba wenzetu walifanya nini na sisi kazi yetu ni kuboresha.
“Nitatoa mfano kwamba enzi za kina Kalikawe si za sasa na kama mimi sasa nakuja na mtindo wa Bongo Jamaica.
“Bongo Jamaica ni mtindo mpya ambao ni mchanganyiko wa vionjo kutoka Jamaica na ukanda wa Afrika Mashariki. Nami muda wangu ukimalizika watakuja wengine na vionjo vyao,” anasema Ranking Boy.
Hata hivyo, bado anasisitiza kuwa kazi kubwa ya muziki wa reggae ni kuleta mapinduzi ya fikra.
“Huu si muziki wa porojo, muziki wa reggae lazima ulenge mabadiliko katika jamii na si malumbano au hoja ambazo hazina kichwa wala miguu.
“Reggae ilete mijadala yenye ufumbuzi na si kujadili mambo ambayo hayana suluhisho,” anasema Ranking Boy.
Pamoja na hilo, Ranking Boy anasema kuwa katika muziki wa reggae nchini kuna kikwazo ambacho hakina budi kuondolewa.
Anasema tatizo kubwa miongoni mwa wanamuziki hao ni kukosa ushirikiano wa dhati.
“Inashangaza sana na binafsi jambo hili linanikera kwamba hatuna ushirikiano wa kweli. Huo ni uwazi kwamba hatuna umoja.
“Kila mmoja yuko kivyake na hii maana yake ni kwamba mipango mingi itavurugika na tutabaki kulalama.”
Pamoja na yote hayo, msanii huyo ana faraja kuona kuwa muziki wa reggae kwa kiasi kikubwa unakubalika nchini.
“Zamani ilionekana kama kuimba reggae ni kuhamasisha uvutaji bangi lakini sasa mambo yamegeuka hata watu wazima wanapenda reggae,” anaeleza Ranking Boy.
Monday, November 5, 2007
Wasanii mtapakwa tope hadi lini?
na innocent munyuku
SIKU zinasonga mbele na kinachohesabiwa sasa ni namna ya kuhitimisha mwaka kwa nguvu za Mola.
Hakuna mwenye uhakika wa moja kwa moja kama ataiona Januari Mosi ya mwaka 2008. Badala yake wengi wanaendelea kupiga dua, waendelee ndani ya dimba wasikalishwe benchi.
Mwandika Busati naye yu katika sala akiomba kwa nguvu zote ili auone mwaka mpya kwani kapanga mengi ya neema kwa mwaka ujao.
Tukiachana na dua za mwaka mpya, Mzee wa Busati juma hili anakuja na dukuduku lake ambalo kadri siku zinavyoyoma ndivyo anavyoumia kwenye mtima.
Limekuwa jambo la mazoea sasa kwa mtu fisadi, mshenzi au tapeli kuitwa ‘msanii’. Hilo ndilo jina la ubatizo kwa watu wa jamii hiyo.
Kwamba watu waongo wenye upande hasi katika kaya zetu huitwa ‘wasanii’. Hili jambo kwa hakika linakera nafsi hasa ya Mzee wa Busati.
Linakera kwa sababu hakuna njia nyepesi ya kuliezea hili zaidi ya ukweli kwamba wasanii nchini wanadhalilishwa na kupakwa matope.
Ajuavyo Mzee wa Busati ni kwamba tafsiri rahisi ya msanii ni mtu mwenye ustadi wa kuchora, kuchonga, au kutia nakshi.
Lakini pia pahala pengine, msanii hutajwa kuwa ni mtu mwenye ufundi wa kutunga na kutoa mawazo yake kama vile kwa kutoa shairi, hadithi au tamthiliya.
Leo hii sifa hizo nzuri zimetoweka na wajuzi wameamua kuwapaka matope wasanii kwa kuwahusisha na yasiyofaa.
Tapeli na wasio makini katika jamii huitwa wasanii. Wahuni na wababaishaji leo hii wamepewa jina la usanii. Hii maana yake nini?
Huku ni kudhalilishwa, wasanii wamevuliwa nguo na hakuna anayeonekana kujali. Wamepakwa matope nao kwa unyonge wao ni kama waliokubali hali hiyo.
Hivi kwanini basi waongo na matapeli wasiitwe wahandisi, madaktari, wauguzi, walimu au marubani. Iweje msanii ndiye apakwe tope? Huku ni kudhalilishana.
Mzee wa Busati analia na hili kutokana na ukweli kwamba kuna upotoshaji wa makusudi katika hadhi ya wasanii nchini na pengine duniani kote.
Twawafunda nini vijana wetu wanaochipukia? Tunawalea kwa mtindo gani? Makuzi yao twayapotosha kwani kuna hatari jinsi wanavyokua wakakosa hamu ya kujiingiza katika sanaa.
Hawatakubali kwa sababu tayari wameshanasa vichwani mwao kwamba wasanii ni watu wa hovyo wasio na mwelekeo mwema katika jamii.
Watakimbia kwa vile wamefundishwa kwamba msanii si lolote. Watabaki kufifisha vipaji vyao na hii maana yake ni kwamba jamii itakosa wabunifu na waburudishaji.
Lakini pengine kuna haja ya wasanii kutoa tamko la kulaani hali hii ambayo sasa imezoeleka ndani ya kaya zetu. Amkeni mseme kwamba wasiendelee kugusa mboni za macho yenu.
Msikae kimya manake kimya chenu kitachukuliwa kuwa tayari mmeridhia kuchafuliwa kwa kiwango cha hali ya juu. Itasemwa kwamba ndivyo mlivyo kwani hakuna pahala mmewahi kukemea jambo hilo.
Vinginevyo Mzee wa Busati anaelekea ukingoni akiangalia namna Wanamsimbazi wanavyoendelea kuvutana kwa kile kinachosemwa kwamba kusafisha uongozi.
Simba wa Yuda na Mwenyekiti wake na wengine wanne wamepigwa chini kwa madai ya ‘kutafuna’ fedha za chama na ulegevu wa timu katika Ligi Kuu Tanzania Bara.
Hao wamesomewa tuhuma 10 na hivyo wanachama 271 kuridhia kupigwa chini kwa Simba wa Yuda na bosi wake. Wamesimamishwa lakini je, hiyo ni suluhu ya mambo ndani ya Simba?
Hofu ya Mzee wa Busati ni kwamba isije ikaja kesi ambayo itaendelea kuvuruga klabu hiyo yenye mashabiki tele ndani ya Tanzania.
Msije mkajikuta mmekwamba sehemu kwenye mto wenye mamba wenye njaa kwani huko hakuna salama hata kidogo. Huo utakuwa mwisho wenu wa kila kitu.
Mnachokifanya sasa ni kuanza kutafunana. Mtawatafuna sita baadaye saba hadi 10 mwishowe mtajitafuna na kumalizana na huo utakuwa mwisho wenu.
Kwamba moto huu uliowashwa Msimbazi usije unguza kila kitu na kuyaacha mahame.
Wasalaam,
SIKU zinasonga mbele na kinachohesabiwa sasa ni namna ya kuhitimisha mwaka kwa nguvu za Mola.
Hakuna mwenye uhakika wa moja kwa moja kama ataiona Januari Mosi ya mwaka 2008. Badala yake wengi wanaendelea kupiga dua, waendelee ndani ya dimba wasikalishwe benchi.
Mwandika Busati naye yu katika sala akiomba kwa nguvu zote ili auone mwaka mpya kwani kapanga mengi ya neema kwa mwaka ujao.
Tukiachana na dua za mwaka mpya, Mzee wa Busati juma hili anakuja na dukuduku lake ambalo kadri siku zinavyoyoma ndivyo anavyoumia kwenye mtima.
Limekuwa jambo la mazoea sasa kwa mtu fisadi, mshenzi au tapeli kuitwa ‘msanii’. Hilo ndilo jina la ubatizo kwa watu wa jamii hiyo.
Kwamba watu waongo wenye upande hasi katika kaya zetu huitwa ‘wasanii’. Hili jambo kwa hakika linakera nafsi hasa ya Mzee wa Busati.
Linakera kwa sababu hakuna njia nyepesi ya kuliezea hili zaidi ya ukweli kwamba wasanii nchini wanadhalilishwa na kupakwa matope.
Ajuavyo Mzee wa Busati ni kwamba tafsiri rahisi ya msanii ni mtu mwenye ustadi wa kuchora, kuchonga, au kutia nakshi.
Lakini pia pahala pengine, msanii hutajwa kuwa ni mtu mwenye ufundi wa kutunga na kutoa mawazo yake kama vile kwa kutoa shairi, hadithi au tamthiliya.
Leo hii sifa hizo nzuri zimetoweka na wajuzi wameamua kuwapaka matope wasanii kwa kuwahusisha na yasiyofaa.
Tapeli na wasio makini katika jamii huitwa wasanii. Wahuni na wababaishaji leo hii wamepewa jina la usanii. Hii maana yake nini?
Huku ni kudhalilishwa, wasanii wamevuliwa nguo na hakuna anayeonekana kujali. Wamepakwa matope nao kwa unyonge wao ni kama waliokubali hali hiyo.
Hivi kwanini basi waongo na matapeli wasiitwe wahandisi, madaktari, wauguzi, walimu au marubani. Iweje msanii ndiye apakwe tope? Huku ni kudhalilishana.
Mzee wa Busati analia na hili kutokana na ukweli kwamba kuna upotoshaji wa makusudi katika hadhi ya wasanii nchini na pengine duniani kote.
Twawafunda nini vijana wetu wanaochipukia? Tunawalea kwa mtindo gani? Makuzi yao twayapotosha kwani kuna hatari jinsi wanavyokua wakakosa hamu ya kujiingiza katika sanaa.
Hawatakubali kwa sababu tayari wameshanasa vichwani mwao kwamba wasanii ni watu wa hovyo wasio na mwelekeo mwema katika jamii.
Watakimbia kwa vile wamefundishwa kwamba msanii si lolote. Watabaki kufifisha vipaji vyao na hii maana yake ni kwamba jamii itakosa wabunifu na waburudishaji.
Lakini pengine kuna haja ya wasanii kutoa tamko la kulaani hali hii ambayo sasa imezoeleka ndani ya kaya zetu. Amkeni mseme kwamba wasiendelee kugusa mboni za macho yenu.
Msikae kimya manake kimya chenu kitachukuliwa kuwa tayari mmeridhia kuchafuliwa kwa kiwango cha hali ya juu. Itasemwa kwamba ndivyo mlivyo kwani hakuna pahala mmewahi kukemea jambo hilo.
Vinginevyo Mzee wa Busati anaelekea ukingoni akiangalia namna Wanamsimbazi wanavyoendelea kuvutana kwa kile kinachosemwa kwamba kusafisha uongozi.
Simba wa Yuda na Mwenyekiti wake na wengine wanne wamepigwa chini kwa madai ya ‘kutafuna’ fedha za chama na ulegevu wa timu katika Ligi Kuu Tanzania Bara.
Hao wamesomewa tuhuma 10 na hivyo wanachama 271 kuridhia kupigwa chini kwa Simba wa Yuda na bosi wake. Wamesimamishwa lakini je, hiyo ni suluhu ya mambo ndani ya Simba?
Hofu ya Mzee wa Busati ni kwamba isije ikaja kesi ambayo itaendelea kuvuruga klabu hiyo yenye mashabiki tele ndani ya Tanzania.
Msije mkajikuta mmekwamba sehemu kwenye mto wenye mamba wenye njaa kwani huko hakuna salama hata kidogo. Huo utakuwa mwisho wenu wa kila kitu.
Mnachokifanya sasa ni kuanza kutafunana. Mtawatafuna sita baadaye saba hadi 10 mwishowe mtajitafuna na kumalizana na huo utakuwa mwisho wenu.
Kwamba moto huu uliowashwa Msimbazi usije unguza kila kitu na kuyaacha mahame.
Wasalaam,
Friday, November 2, 2007
Yarab epusha hasira zao zisivuke mpaka
Na Innocent Munyuku
KWA zaidi ya miezi 12 sasa, Watanzania wengi wamekuwa wakitupa lawama kwa Serikali kwamba imeshindwa kutekeleza ahadi zake kwa maslahi ya umma.
Wanacholalamikia ni hali duni ya maisha waliyonayo. Wengi wao hawana ajira na hivyo kuwawia vigumu kupata mahitaji yao ya kila siku kama inavyostahili.
Wanacholilia ni maisha bora na ajira zitakazowawezesha kuwa na vipato vya uhakika vya kutoshelezesha mahitaji ya msingi katika ustawi wa jamii.
Vilio ni kila mahala, kwani ukweli wa mambo ni kwamba, ukali wa maisha ungali ukiendelea kutokana na hali halisi ya upandaji bei katika bidhaa mbalimbali.
Sehemu kubwa ya Tanzania kinachoimbwa na wananchi ni ugumu wa maisha. Wengi sasa hudiriki kusema ya kuwa, maisha ya leo nafuu ya jana, wakimaanisha kwamba kila uchao mambo yamekuwa ya kukatisha tamaa.
Na ndio maana, hivi karibuni baadhi ya mawaziri walipozuru mikoani kuelezea ‘uzuri’ wa bajeti ya mwaka huu wa fedha 2007/08 walizomewa na wananchi.
Binafsi, habari kwamba baadhi ya mawaziri walizomewa huko mikoani na hivyo kuwa shubiri kwao ilinishangaza kidogo, lakini pia ikanifunza jambo moja kwamba sasa watu wamechoka!
Kwamba kama imefikia mahala wananchi badala ya kusikiliza hotuba za mawaziri wanawatolea maneno ya kejeli na kuwazomea, hili jambo si la kupuuzia au kuliacha hivi hivi.
Sauti zile zina maana yake na kama sitakwenda mbali na ukweli, ni kwamba watu sasa wamekata tamaa na ndio maana mazungumzo katika kila kona ya nchi ni mjadala kuhusu maisha bora.
Mwaka 2005, bei ya mkate wa kawaida kabisa ilikuwa kati ya Sh 200 hadi Sh 300. Leo hii mkate huo unaliwa kwa Sh 500 hadi Sh 700. Si mkate pekee bali karibu kila bidhaa imepanda bei.
Ndicho wanacholalamikia raia wa nchi hii kwamba sasa mambo ni magumu na kwa hakika hawaoni pa kutokea labda kwa nguvu za Muumba.
Sasa hivi kuna hili wimbi la kile kinachoitwa ‘orodha ya mafisadi’. Wananchi wengi wanaendelea na mijadala kila wapatapo nafasi ya kusema juu ya jambo hilo. Wanajadili hoja hizo za wapinzani na kwa vile Serikali imeamua kutulia, nao wanajawa na maswali tele kwenye vichwa vyao.
Wanasema juu ya mfumo mzima wa mikataba ya wawekezaji wa madini nchini. Na ndio maana huko North Mara mwezi uliopita, wananchi waliishambulia kwa jiwe helikopta ya wawekezaji.
Katika shambulizi hilo, kioo cha helikopta hiyo kilitobolewa na rubani wake kuumizwa jicho. Hii maana yake ni kwamba, kama wananchi hao wangekuwa na silaha ya kisasa wangeleta madhara makubwa.
Hawa wana hasira na wawekezaji ambao wanaendelea kuchimba madini yetu na kutuachia mahandaki. Mwananchi wa kawaida haelewi manufaa katika miradi hiyo ya madini, anachojua ni kwamba kuna hitilafu.
Anaamini kuna hitilafu, kwa sababu bado maisha yake yameendelea kuwa ya dhiki. Anachoamini ndicho hicho kwamba nchi inaliwa na wachache.
Hapa kuna ulazima wa kuyaweka haya mambo bayana. Kwamba hakuna maana njema kuendelea kushabikia misaada ya wawekezaji hao kama hakutakuwa na uwiano unaoeleweka juu ya wanachokipata na wanachokiacha kwa wananchi.
Hatuwezi kuchekelea miundombinu kwenye migodi hiyo kwa sababu ni wazi kwamba imewekwa kwa ajili ya kurahisisha utendaji wao wa kila siku.
Pengine nirejee mfano wa kombeo lililotumika kurusha jiwe lililoharibu kioo cha helikopta North Mara. Aliyerusha ni wazi alikuwa amejaa hasira akiamini kwamba nchi yake inafilisiwa. Akashindwa kujizuia akafanya alichofanya.
Leo hii wametumia kombeo, kesho watakamata chupa na jambia mkono mwingine. Wakiona mambo bado hayaendi, si ajabu wakaamua kuingia mitaani wakiwa na kila kinachofaa kubebeka.
Hili halitashangaza, kwani tayari wameshaanza kuvamia vituo vya polisi na wala hakuna mwenye hofu ya kutwangwa risasi za moto. Wananchi wanaonyesha wazi hasira zao kwa dola.
Hawatajali, kwa sababu maisha yao tayari yamekwenda upogo na hawana tena imani ya kufika nchi ya ahadi yenye maziwa na asali ya mwitu. Wataona heri wafe wakidai wanachoamini kuwa ni haki yao.
Wamechoka kwa sababu wanaona kila kitu hakiendi katika mstari unaofaa. Misaada ya nchi za nje inatumikaje? Ndivyo wanavyojiuliza.
Kuna watu leo hii wana vitambi vya ukimwi, magorofa ya ukimwi na hata magari ya kifahari ya ukimwi. Hawa wametafuna fedha za wahisani zilizolenga kuwasaidia waathirika wa ukimwi. Wakageuka wajanja wakaziweka kwenye mifuko yao.
Wajanja hawapo kwenye miradi ya ukimwi pekee, wapo kila mahala wakiwa mahiri wa kuandika ‘proposals’ za kuombea fedha za wafadhili katika miradi mbalimbali. Mingi kati ya hiyo ni yao binafsi wakila na kusaza pasipo woga.
Leo hii, hawa ndio wafalme wanaotembea kwa kujiamini wakikanyaga ardhi ya Tanzania kama ya kwao pekee. Hawa ni wateule ambao wamesimama sawia na si rahisi wakapigwa mwereka.
Lakini, hoja ya msingi hapa ni kwamba dhana ya uwiano wa maisha kwa raia wa taifa hili lazima ijadiliwe kwa mapana kwani uwezo wa kuwawezesha wananchi upo kutokana na ukweli kwamba bado tunazo rasilimali za kutosha.
Nionavyo mimi ni kwamba, kuna haja basi kukawa na jukwaa huru ambalo wananchi wa kawaida watapata mwanya wa kuwaeleza watawala wao kero na dhiki zao.
Watawala wasikae kimya au kupangua hoja kwa msimamo wa kisiasa kwani ni ukweli usiopingika kuwa maisha sasa ni magumu na yanaendelea kuwa magumu.
Wananchi wanahoji mengi na wana shaka kama wasaidizi wakuu wa watawala wanayafikisha kama yalivyo au wanaondoa ukakasi kabla ya Mkuu wa Kaya hajasoma ripoti zao.
Sidhani kama anaelezwa kero kwenye vituo vya polisi, mahakama, hospitalini au katika ofisi nyingine za Serikali ambako usumbufu wa kupewa huduma umerejea kama miaka ya nyuma.
Kama haya yataendelea, basi ni wazi kuwa wananchi watachoka na kitakachofuata ni vigumu kusema kwamba kitakuwa cha heri. Basi na tumwombe Muumba tusiione siku hiyo.
0754 471 920
KWA zaidi ya miezi 12 sasa, Watanzania wengi wamekuwa wakitupa lawama kwa Serikali kwamba imeshindwa kutekeleza ahadi zake kwa maslahi ya umma.
Wanacholalamikia ni hali duni ya maisha waliyonayo. Wengi wao hawana ajira na hivyo kuwawia vigumu kupata mahitaji yao ya kila siku kama inavyostahili.
Wanacholilia ni maisha bora na ajira zitakazowawezesha kuwa na vipato vya uhakika vya kutoshelezesha mahitaji ya msingi katika ustawi wa jamii.
Vilio ni kila mahala, kwani ukweli wa mambo ni kwamba, ukali wa maisha ungali ukiendelea kutokana na hali halisi ya upandaji bei katika bidhaa mbalimbali.
Sehemu kubwa ya Tanzania kinachoimbwa na wananchi ni ugumu wa maisha. Wengi sasa hudiriki kusema ya kuwa, maisha ya leo nafuu ya jana, wakimaanisha kwamba kila uchao mambo yamekuwa ya kukatisha tamaa.
Na ndio maana, hivi karibuni baadhi ya mawaziri walipozuru mikoani kuelezea ‘uzuri’ wa bajeti ya mwaka huu wa fedha 2007/08 walizomewa na wananchi.
Binafsi, habari kwamba baadhi ya mawaziri walizomewa huko mikoani na hivyo kuwa shubiri kwao ilinishangaza kidogo, lakini pia ikanifunza jambo moja kwamba sasa watu wamechoka!
Kwamba kama imefikia mahala wananchi badala ya kusikiliza hotuba za mawaziri wanawatolea maneno ya kejeli na kuwazomea, hili jambo si la kupuuzia au kuliacha hivi hivi.
Sauti zile zina maana yake na kama sitakwenda mbali na ukweli, ni kwamba watu sasa wamekata tamaa na ndio maana mazungumzo katika kila kona ya nchi ni mjadala kuhusu maisha bora.
Mwaka 2005, bei ya mkate wa kawaida kabisa ilikuwa kati ya Sh 200 hadi Sh 300. Leo hii mkate huo unaliwa kwa Sh 500 hadi Sh 700. Si mkate pekee bali karibu kila bidhaa imepanda bei.
Ndicho wanacholalamikia raia wa nchi hii kwamba sasa mambo ni magumu na kwa hakika hawaoni pa kutokea labda kwa nguvu za Muumba.
Sasa hivi kuna hili wimbi la kile kinachoitwa ‘orodha ya mafisadi’. Wananchi wengi wanaendelea na mijadala kila wapatapo nafasi ya kusema juu ya jambo hilo. Wanajadili hoja hizo za wapinzani na kwa vile Serikali imeamua kutulia, nao wanajawa na maswali tele kwenye vichwa vyao.
Wanasema juu ya mfumo mzima wa mikataba ya wawekezaji wa madini nchini. Na ndio maana huko North Mara mwezi uliopita, wananchi waliishambulia kwa jiwe helikopta ya wawekezaji.
Katika shambulizi hilo, kioo cha helikopta hiyo kilitobolewa na rubani wake kuumizwa jicho. Hii maana yake ni kwamba, kama wananchi hao wangekuwa na silaha ya kisasa wangeleta madhara makubwa.
Hawa wana hasira na wawekezaji ambao wanaendelea kuchimba madini yetu na kutuachia mahandaki. Mwananchi wa kawaida haelewi manufaa katika miradi hiyo ya madini, anachojua ni kwamba kuna hitilafu.
Anaamini kuna hitilafu, kwa sababu bado maisha yake yameendelea kuwa ya dhiki. Anachoamini ndicho hicho kwamba nchi inaliwa na wachache.
Hapa kuna ulazima wa kuyaweka haya mambo bayana. Kwamba hakuna maana njema kuendelea kushabikia misaada ya wawekezaji hao kama hakutakuwa na uwiano unaoeleweka juu ya wanachokipata na wanachokiacha kwa wananchi.
Hatuwezi kuchekelea miundombinu kwenye migodi hiyo kwa sababu ni wazi kwamba imewekwa kwa ajili ya kurahisisha utendaji wao wa kila siku.
Pengine nirejee mfano wa kombeo lililotumika kurusha jiwe lililoharibu kioo cha helikopta North Mara. Aliyerusha ni wazi alikuwa amejaa hasira akiamini kwamba nchi yake inafilisiwa. Akashindwa kujizuia akafanya alichofanya.
Leo hii wametumia kombeo, kesho watakamata chupa na jambia mkono mwingine. Wakiona mambo bado hayaendi, si ajabu wakaamua kuingia mitaani wakiwa na kila kinachofaa kubebeka.
Hili halitashangaza, kwani tayari wameshaanza kuvamia vituo vya polisi na wala hakuna mwenye hofu ya kutwangwa risasi za moto. Wananchi wanaonyesha wazi hasira zao kwa dola.
Hawatajali, kwa sababu maisha yao tayari yamekwenda upogo na hawana tena imani ya kufika nchi ya ahadi yenye maziwa na asali ya mwitu. Wataona heri wafe wakidai wanachoamini kuwa ni haki yao.
Wamechoka kwa sababu wanaona kila kitu hakiendi katika mstari unaofaa. Misaada ya nchi za nje inatumikaje? Ndivyo wanavyojiuliza.
Kuna watu leo hii wana vitambi vya ukimwi, magorofa ya ukimwi na hata magari ya kifahari ya ukimwi. Hawa wametafuna fedha za wahisani zilizolenga kuwasaidia waathirika wa ukimwi. Wakageuka wajanja wakaziweka kwenye mifuko yao.
Wajanja hawapo kwenye miradi ya ukimwi pekee, wapo kila mahala wakiwa mahiri wa kuandika ‘proposals’ za kuombea fedha za wafadhili katika miradi mbalimbali. Mingi kati ya hiyo ni yao binafsi wakila na kusaza pasipo woga.
Leo hii, hawa ndio wafalme wanaotembea kwa kujiamini wakikanyaga ardhi ya Tanzania kama ya kwao pekee. Hawa ni wateule ambao wamesimama sawia na si rahisi wakapigwa mwereka.
Lakini, hoja ya msingi hapa ni kwamba dhana ya uwiano wa maisha kwa raia wa taifa hili lazima ijadiliwe kwa mapana kwani uwezo wa kuwawezesha wananchi upo kutokana na ukweli kwamba bado tunazo rasilimali za kutosha.
Nionavyo mimi ni kwamba, kuna haja basi kukawa na jukwaa huru ambalo wananchi wa kawaida watapata mwanya wa kuwaeleza watawala wao kero na dhiki zao.
Watawala wasikae kimya au kupangua hoja kwa msimamo wa kisiasa kwani ni ukweli usiopingika kuwa maisha sasa ni magumu na yanaendelea kuwa magumu.
Wananchi wanahoji mengi na wana shaka kama wasaidizi wakuu wa watawala wanayafikisha kama yalivyo au wanaondoa ukakasi kabla ya Mkuu wa Kaya hajasoma ripoti zao.
Sidhani kama anaelezwa kero kwenye vituo vya polisi, mahakama, hospitalini au katika ofisi nyingine za Serikali ambako usumbufu wa kupewa huduma umerejea kama miaka ya nyuma.
Kama haya yataendelea, basi ni wazi kuwa wananchi watachoka na kitakachofuata ni vigumu kusema kwamba kitakuwa cha heri. Basi na tumwombe Muumba tusiione siku hiyo.
0754 471 920
Monday, October 29, 2007
Ole wao wanaoikana michezo ya jadi
na innocent munyuku
BARAKA ziko mlangoni na shari kisogoni. Nyakati za kulalama kwamba maharagwe yanakaribia kuota tumboni zimekwenda likizo. Kilichopo ni tungo na vibwagizo vyenye utamu kwenye ndimi.
Siku kama hizi Mzee wa Busati huwa makini sana katika mikusanyiko. Iwe kwenye daladala au kwenye kilauri. Manake walio wengi wanatembea kwa matao wakijivunia ujazo kwenye mifuko yao.
Tarehe kama hizi, ubabe wa kila aina hutokea na anayekufanyia ubabe hudiriki kutamba kwamba anaweza kukupoteza mjini. Kisa? Anazo za kupandia taksi kwa siku mbili hizi.
Dada zetu ndo usiseme wameshasahu nywele zao za kipilipili. Siku hizi wanapanga foleni kwenye saluni kuzibadili nywele zao zifanane za kina Victoria Beckham au Jennifer Lopez. Si vibaya kwani ndivyo dunia inavyokwenda.
Tulidai uhuru wa kujitawala tukapewa lakini waliotupa uhuru huo wakaongeza mbinu kuhakikisha kuwa wanaziteka bongo zetu. Ndio maana Mzee wa Busati amekuwa akikemea utumwa wa akili ambao ni mbaya kuliko utumwa wa aina nyingine.
Tumefunzwa kuamini kuwa kila litokalo majuu ni jema na halina kasoro. Pita mitaa ya bongo utashangaa kuona kuwa hadi hii leo mitaa hupachikwa majina ya kigeni. Twakimbilia wapi?
Hoja ya Mwandika Busati juma hili ni kwamba jamii ya Kitanzania inapaswa kuthamini utamaduni wake na katika hili michezo ya jadi isisahauliwe.
Husemwa kwamba nchi haiwezi kutambulika kama taifa huru pasipo kuwa na utamaduni wake kama vile michezo na mengine yafananayo na hayo.
Ni kutokana na hilo, mwaka 1967 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha Sheria Na. 12 iliyobariki kuanzishwa kwa Baraza la Michezo la Taifa (BMT).
Lakini kwa bahati mbaya michezo mingi ya jadi imekuwa ikiachwa kando na kuendeleza michezo mingine.
Ipo haja ya kuunda mkakati wa kuendeleza michezo mbalimbali ya jadi na kuifanyia utafiti kama ilivyopata kutamkwa katika sera ya maendeleo ya michezo.
Leo hii twaifumbia macho lakini ukweli wa mambo ni kwamba siku chache zijazo taifa litalia na kusaga meno.
Kuidharau michezo yetu ya jadi ni kujikana na kulisaliti taifa. Huku ni kupotoka na kwenda katika barabara ya giza.
Mzee wa Busati mara kadhaa ameshashuhudia katika matamasha mbalimbali namna Wabongo walivyosahau mema ya kwao. Watapenda kushabikia nyimbo za ng’ambo na kuzifumbia macho ngoma za kwao.
Wasanii wa ngoma za jadi huangaliwa kama wasiostaarabika. Hawapewi nafasi inayostahili kwa ufundi na ubunifu wao. Wamebaki kuwa mawe ya pembeni.
Leo hata vitegemezi vyetu havitaki kusikia mdundiko wala mdumange. Watakwambia wao wanakwenda na wakati kwa kusikiza muziki kutoka Ulaya na Marekani.
Mzee wa Busati hasemi kwamba nyimbo za ng’ambo zibezwe la hasha! Anachosema ni kwamba mkazo uwekwe kujali na kuthamini mema ya kwetu na hakika inawezekana.
Hivi kweli tutaendelea kujikana namna hii hadi lini? Akili zetu zimewekwa nini? au hizi peremende tunazopewa kutoka ughaibuni? Tatizo li wapi?
Leo hii Mmakonde ukikutana naye mjini hataki umsalimie kwa lugha yake. Yu radhi kusema kwa Kiingereza kuliko lugha yake ya nyumbani. Hata Kiswahili nacho huwa shida kwake. Mtasemaje juu ya hilo? Kama si uzumbukuku ni nini?
Basi na tukae tujipange upya katika hili. Watawala wetu waungane na walio chini yao ili kuendeleza utamaduni wetu.
Wasimame na waseme kwamba tujiweke katika mstari wa kufufua akili zilizodumaa na kusahau mambo ya kijadi. Yakipotea tutakuja kuangamia miaka michache ijayo.
Basi na tuhubiri hayo na wala kusiwe na sababu ya kukwepa majukumu. Twauchimbia kaburi utamaduni wetu kwa kile tunachosema kwenda na wakati. Huu ni ulimbukeni.
Mwaona fahari gani kuwaona watoto wa kiume wakisuka nywele na kuvaa hereni masikioni? Hao wanasema wanakwenda na wakati lakini ukweli wa mambo ni kwamba wamekosa bahati.
Kila walionalo kwenye kioo cha luninga basi ni jema tena jema sana. Hivi ni kweli haya hayaepukiki? Hivi ni kweli kwamba twaona sawia tu vijana kuyumba katika ardhi yao?
Mzee wa Busati anafikia ukomo akiamini kuwa mdumange au sindimba zingali na nafasi nchini Tanzania.
Mwandika Busati atakuwa mwenye faraja kusikia kuwa ngoma za kina Vital Maembe au Zemkala zinagombewa huko Marekani na Ulaya. Hilo litafanikiwa kama tutaweka mkakati maalumu wa kufufua akili zilizolala.
Akili hizo zikifufuka ni wazi kuwa hata michezo ya jadi kama pia, tufe, mieleka na mingi ifananayo na hiyo itanguruma na kupendwa na jamii.
Wasalaam
BARAKA ziko mlangoni na shari kisogoni. Nyakati za kulalama kwamba maharagwe yanakaribia kuota tumboni zimekwenda likizo. Kilichopo ni tungo na vibwagizo vyenye utamu kwenye ndimi.
Siku kama hizi Mzee wa Busati huwa makini sana katika mikusanyiko. Iwe kwenye daladala au kwenye kilauri. Manake walio wengi wanatembea kwa matao wakijivunia ujazo kwenye mifuko yao.
Tarehe kama hizi, ubabe wa kila aina hutokea na anayekufanyia ubabe hudiriki kutamba kwamba anaweza kukupoteza mjini. Kisa? Anazo za kupandia taksi kwa siku mbili hizi.
Dada zetu ndo usiseme wameshasahu nywele zao za kipilipili. Siku hizi wanapanga foleni kwenye saluni kuzibadili nywele zao zifanane za kina Victoria Beckham au Jennifer Lopez. Si vibaya kwani ndivyo dunia inavyokwenda.
Tulidai uhuru wa kujitawala tukapewa lakini waliotupa uhuru huo wakaongeza mbinu kuhakikisha kuwa wanaziteka bongo zetu. Ndio maana Mzee wa Busati amekuwa akikemea utumwa wa akili ambao ni mbaya kuliko utumwa wa aina nyingine.
Tumefunzwa kuamini kuwa kila litokalo majuu ni jema na halina kasoro. Pita mitaa ya bongo utashangaa kuona kuwa hadi hii leo mitaa hupachikwa majina ya kigeni. Twakimbilia wapi?
Hoja ya Mwandika Busati juma hili ni kwamba jamii ya Kitanzania inapaswa kuthamini utamaduni wake na katika hili michezo ya jadi isisahauliwe.
Husemwa kwamba nchi haiwezi kutambulika kama taifa huru pasipo kuwa na utamaduni wake kama vile michezo na mengine yafananayo na hayo.
Ni kutokana na hilo, mwaka 1967 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha Sheria Na. 12 iliyobariki kuanzishwa kwa Baraza la Michezo la Taifa (BMT).
Lakini kwa bahati mbaya michezo mingi ya jadi imekuwa ikiachwa kando na kuendeleza michezo mingine.
Ipo haja ya kuunda mkakati wa kuendeleza michezo mbalimbali ya jadi na kuifanyia utafiti kama ilivyopata kutamkwa katika sera ya maendeleo ya michezo.
Leo hii twaifumbia macho lakini ukweli wa mambo ni kwamba siku chache zijazo taifa litalia na kusaga meno.
Kuidharau michezo yetu ya jadi ni kujikana na kulisaliti taifa. Huku ni kupotoka na kwenda katika barabara ya giza.
Mzee wa Busati mara kadhaa ameshashuhudia katika matamasha mbalimbali namna Wabongo walivyosahau mema ya kwao. Watapenda kushabikia nyimbo za ng’ambo na kuzifumbia macho ngoma za kwao.
Wasanii wa ngoma za jadi huangaliwa kama wasiostaarabika. Hawapewi nafasi inayostahili kwa ufundi na ubunifu wao. Wamebaki kuwa mawe ya pembeni.
Leo hata vitegemezi vyetu havitaki kusikia mdundiko wala mdumange. Watakwambia wao wanakwenda na wakati kwa kusikiza muziki kutoka Ulaya na Marekani.
Mzee wa Busati hasemi kwamba nyimbo za ng’ambo zibezwe la hasha! Anachosema ni kwamba mkazo uwekwe kujali na kuthamini mema ya kwetu na hakika inawezekana.
Hivi kweli tutaendelea kujikana namna hii hadi lini? Akili zetu zimewekwa nini? au hizi peremende tunazopewa kutoka ughaibuni? Tatizo li wapi?
Leo hii Mmakonde ukikutana naye mjini hataki umsalimie kwa lugha yake. Yu radhi kusema kwa Kiingereza kuliko lugha yake ya nyumbani. Hata Kiswahili nacho huwa shida kwake. Mtasemaje juu ya hilo? Kama si uzumbukuku ni nini?
Basi na tukae tujipange upya katika hili. Watawala wetu waungane na walio chini yao ili kuendeleza utamaduni wetu.
Wasimame na waseme kwamba tujiweke katika mstari wa kufufua akili zilizodumaa na kusahau mambo ya kijadi. Yakipotea tutakuja kuangamia miaka michache ijayo.
Basi na tuhubiri hayo na wala kusiwe na sababu ya kukwepa majukumu. Twauchimbia kaburi utamaduni wetu kwa kile tunachosema kwenda na wakati. Huu ni ulimbukeni.
Mwaona fahari gani kuwaona watoto wa kiume wakisuka nywele na kuvaa hereni masikioni? Hao wanasema wanakwenda na wakati lakini ukweli wa mambo ni kwamba wamekosa bahati.
Kila walionalo kwenye kioo cha luninga basi ni jema tena jema sana. Hivi ni kweli haya hayaepukiki? Hivi ni kweli kwamba twaona sawia tu vijana kuyumba katika ardhi yao?
Mzee wa Busati anafikia ukomo akiamini kuwa mdumange au sindimba zingali na nafasi nchini Tanzania.
Mwandika Busati atakuwa mwenye faraja kusikia kuwa ngoma za kina Vital Maembe au Zemkala zinagombewa huko Marekani na Ulaya. Hilo litafanikiwa kama tutaweka mkakati maalumu wa kufufua akili zilizolala.
Akili hizo zikifufuka ni wazi kuwa hata michezo ya jadi kama pia, tufe, mieleka na mingi ifananayo na hiyo itanguruma na kupendwa na jamii.
Wasalaam
Monday, October 22, 2007
Lala unono Dube uliyekosa bahati
na innocent munyuku
‘UNLUCKY LUCKY DUBE’ (Dube mwenye bahati aliyekosa bahati) yalikuwa maneno ya mwandishi mkongwe Balinagwe Mwambungu ambaye sasa ni mhariri mshiriki wa gazeti dada la Mtanzania.
Mwambungu ambaye hupenda kuitwa Big Mwa, alikuwa akiteta na Mzee wa Busati mara baada ya kusikia taarifa ya kifo cha mwanamuziki nguli wa muziki wa reggae barani Afrika, Lucy Dube.
Dube alipigwa risasi na majahili mbele ya wanawe wawili katika kitongoji cha Rossettenville jijini Johannesburg na hivyo kusitisha uhai wake.
Katika mazungumzo kati ya Mzee wa Busati na Big Mwa kilichojadiliwa ni namna mwanamuziki huyo alivyopoteza bahati ya kuishi kutokana na ufedhuli wa majahili hao.
Afrika imetikisika na dunia kwa ujumla imeshtushwa na taarifa ya msiba wa mwanamuziki huyo aliyepoteza maisha akiwa na umri wa miaka 43.
Alikuwa kinara na hata sifa zake zikakubalika katika kila ya mabara. Amepotea lakini sifa zake zingali zikienea.
Mzee wa Busati kwa asili yake ni mwenye imani ya rasta akiamini juu ya umoja, upendo na mshikamano. Ndicho alichoshikilia Dube katika tungo zake. Kahubiri haki za binadamu na umuhimu wa kujali wengine pasipo kubaguana.
Kilio kimetanda na hakuna shaka kwamba wengi wanaomlilia Dube wanahuzunika kwa vile wamepoteza kiini cha busara.
Mwanamuziki wa reggae nchini, Ras Innocent Nganyagwa maarufu kama Ras Inno juzi Jumapili alikuwa anatimiza umri wa miaka 42. Mzee wa Busati alikuwa miongoni mwa waliomtumia ujumbe wa kumtakia maisha mengine marefu. Katika majibu yake, Ras Inno alisahau sherehe na alichosema ni kwamba ana majonzi ya Dube.
Wasanii wengi wameshaingia studio kurekodi nyimbo za kumuenzi Dube. Wanahubiri mema yake na namna ya kuishi katika uadilifu.
Dube kishazimika lakini ukweli wa mambo ni kwamba tungali na uwezo wa kuendeleza mema aliyoyaanzisha kama vile amani na mshikamano.
Tuendelee kulia lakini tusisahau kuwa wema katika mitima yetu. Midomo iseme juu ya umoja na kujali shida za wengine. Tusiishie kulia.
Maisha ya reggae kwake yalianza katika miaka ya 1980 akipaza sauti kukemea ubaguzi wa rangi ndani ya Afrika Kusini.
Ni wazi kwamba kutokana na umahiri wake, Dube alikuwa katika nafasi za juu kwenye mauzo ya albamu zake.
Alipoamua kuimba juu ya ubaguzi wa rangi, wazungu walimwona kuwa ni mbaya wao. Akapata upinzani wa hali ya juu.
Upinzani huo ulikwenda mbali ikiwa ni pamoja na kuufungia wimbo wake wa Rasta Never Die usipigwe redioni.
Hakukata tamaa na ndio maana akaendelea kufyatua nyimbo nyingine kibao zikiwa na uzito katika jamii kama vile, Think About The Children na Slave.
Alikuwa mfuasi mkubwa wa Peter Tosh na hata alipofanya ziara nchini Jamaica, baadhi ya mashabiki walistaajabu uwezo wake jukwaani.
Mashabiki hao wakasema kuwa Peter Tosh yu hai akifanya kazi zake barani Afrika. Walimaanisha kwamba uwezo wa Dube ulifanana na wa Tosh.
Alale unono Dube, apumzike kwa amani lakini kuna mengi ya kukumbushana kwamba wafuasi wa mwanamuziki huyo wazidi kuhubiri mema.
Kemeeni ufisadi na ushenzi katika jamii zinazopaswa kuishi kistaarabu. Kuombeleza pasipo kufuata mwelekeo wa Dube ni kukosa nidhamu.
Huu ndio mtazamo wa Mwandika Busati wiki hii. Kwamba Dube katoweka lakini sauti na maneno yake yangali yakiishi.
Mzee wa Busati anafikia ukomo akiamini kwamba wadau wake wanaendelea katika neema hasa katika wakati huu wa mageuzi.
Wengine sasa wameacha ubishi na wamekubali kwamba bila matumizi ya kompyuta dunia haiendi sawia. Hongera Mzee wa Kutibua kwa kuanzisha bulogu yako.
Hiyo ni njia ya kutanua mawasiliano lakini Mzee wa Busati ana hofu na bolugu hiyo kama kweli itaendeleza mema au ni mwamko wa kuleta migogoro katika jamii hasa kwenye klabu za soka asizozipenda.
Vingingevyo Mwandika Busati anaweka kalamu chini akisubiri mwezi ugote arekebishe masuala yake. Si wajua Masiha yu jirani? Pasipo ngwenje kwa wakwe hakuendeki.
Wasalaam,
‘UNLUCKY LUCKY DUBE’ (Dube mwenye bahati aliyekosa bahati) yalikuwa maneno ya mwandishi mkongwe Balinagwe Mwambungu ambaye sasa ni mhariri mshiriki wa gazeti dada la Mtanzania.
Mwambungu ambaye hupenda kuitwa Big Mwa, alikuwa akiteta na Mzee wa Busati mara baada ya kusikia taarifa ya kifo cha mwanamuziki nguli wa muziki wa reggae barani Afrika, Lucy Dube.
Dube alipigwa risasi na majahili mbele ya wanawe wawili katika kitongoji cha Rossettenville jijini Johannesburg na hivyo kusitisha uhai wake.
Katika mazungumzo kati ya Mzee wa Busati na Big Mwa kilichojadiliwa ni namna mwanamuziki huyo alivyopoteza bahati ya kuishi kutokana na ufedhuli wa majahili hao.
Afrika imetikisika na dunia kwa ujumla imeshtushwa na taarifa ya msiba wa mwanamuziki huyo aliyepoteza maisha akiwa na umri wa miaka 43.
Alikuwa kinara na hata sifa zake zikakubalika katika kila ya mabara. Amepotea lakini sifa zake zingali zikienea.
Mzee wa Busati kwa asili yake ni mwenye imani ya rasta akiamini juu ya umoja, upendo na mshikamano. Ndicho alichoshikilia Dube katika tungo zake. Kahubiri haki za binadamu na umuhimu wa kujali wengine pasipo kubaguana.
Kilio kimetanda na hakuna shaka kwamba wengi wanaomlilia Dube wanahuzunika kwa vile wamepoteza kiini cha busara.
Mwanamuziki wa reggae nchini, Ras Innocent Nganyagwa maarufu kama Ras Inno juzi Jumapili alikuwa anatimiza umri wa miaka 42. Mzee wa Busati alikuwa miongoni mwa waliomtumia ujumbe wa kumtakia maisha mengine marefu. Katika majibu yake, Ras Inno alisahau sherehe na alichosema ni kwamba ana majonzi ya Dube.
Wasanii wengi wameshaingia studio kurekodi nyimbo za kumuenzi Dube. Wanahubiri mema yake na namna ya kuishi katika uadilifu.
Dube kishazimika lakini ukweli wa mambo ni kwamba tungali na uwezo wa kuendeleza mema aliyoyaanzisha kama vile amani na mshikamano.
Tuendelee kulia lakini tusisahau kuwa wema katika mitima yetu. Midomo iseme juu ya umoja na kujali shida za wengine. Tusiishie kulia.
Maisha ya reggae kwake yalianza katika miaka ya 1980 akipaza sauti kukemea ubaguzi wa rangi ndani ya Afrika Kusini.
Ni wazi kwamba kutokana na umahiri wake, Dube alikuwa katika nafasi za juu kwenye mauzo ya albamu zake.
Alipoamua kuimba juu ya ubaguzi wa rangi, wazungu walimwona kuwa ni mbaya wao. Akapata upinzani wa hali ya juu.
Upinzani huo ulikwenda mbali ikiwa ni pamoja na kuufungia wimbo wake wa Rasta Never Die usipigwe redioni.
Hakukata tamaa na ndio maana akaendelea kufyatua nyimbo nyingine kibao zikiwa na uzito katika jamii kama vile, Think About The Children na Slave.
Alikuwa mfuasi mkubwa wa Peter Tosh na hata alipofanya ziara nchini Jamaica, baadhi ya mashabiki walistaajabu uwezo wake jukwaani.
Mashabiki hao wakasema kuwa Peter Tosh yu hai akifanya kazi zake barani Afrika. Walimaanisha kwamba uwezo wa Dube ulifanana na wa Tosh.
Alale unono Dube, apumzike kwa amani lakini kuna mengi ya kukumbushana kwamba wafuasi wa mwanamuziki huyo wazidi kuhubiri mema.
Kemeeni ufisadi na ushenzi katika jamii zinazopaswa kuishi kistaarabu. Kuombeleza pasipo kufuata mwelekeo wa Dube ni kukosa nidhamu.
Huu ndio mtazamo wa Mwandika Busati wiki hii. Kwamba Dube katoweka lakini sauti na maneno yake yangali yakiishi.
Mzee wa Busati anafikia ukomo akiamini kwamba wadau wake wanaendelea katika neema hasa katika wakati huu wa mageuzi.
Wengine sasa wameacha ubishi na wamekubali kwamba bila matumizi ya kompyuta dunia haiendi sawia. Hongera Mzee wa Kutibua kwa kuanzisha bulogu yako.
Hiyo ni njia ya kutanua mawasiliano lakini Mzee wa Busati ana hofu na bolugu hiyo kama kweli itaendeleza mema au ni mwamko wa kuleta migogoro katika jamii hasa kwenye klabu za soka asizozipenda.
Vingingevyo Mwandika Busati anaweka kalamu chini akisubiri mwezi ugote arekebishe masuala yake. Si wajua Masiha yu jirani? Pasipo ngwenje kwa wakwe hakuendeki.
Wasalaam,
Thursday, October 18, 2007
Umoja Records yaja na fikra pevu katika sanaa yazidi kujitanua
na innocent munyuku
NILIPOZUNGUMZA naye kiasi cha miezi minne iliyopita, mmoja wa wakurugenzi wa Umoja Records, Gotta Warioba alikuwa na mengi ya kunieleza.
Alisema juu ya mwelekeo wa kampuni yake katika kuinua muziki wenye asili ya Kiafrika na kuusambaza kote duniani.
Midomo yake kwa hakika ilinena kwa kujiamini na alichokusudia kukisema. Wakati huo alikuwa katika kazi ngumu ya kuratibu kazi za wasanii kibao akiwamo Vital Maembe maarufu kama Sumu ya Teja.
Si kama nilikuwa na shaka juu ya msimamo wa Gotta la hasha. Niliwaza mengi na sikuishia kuwaza tu nilimwuliza namna atakavyojipanga katika kutekeleza aliyopanga.
Wakati huo alikuwa na mpango maalumu wa kuandaa albamu ya reggae ikiwakusanya wanamuziki wa aina mbalimbali. Ni wakati huo Gotta alilazimika kulala katika studio za Active ambazo ni sehemu ya Umoja Records.
Katika mpango huo walifanikiwa kupakua albamu ya iliyopewa jina la ‘Bongo Riddims & Style’ ikiwashirikisha wasanii wengi chipukizi.
Wiki iliyopita Gotta amefanya mahojiano na Bingwa na kuelezea mwelekeo wa Umoja Records na maendeleo ya muziki kwa ujumla.
“Umoja Records imetanua wigo wake baada ya kuanza kusaka wanamuziki kutoka Kenya na Uganda,” anasema Gotta.
Anasema ameshafanya mazungumzo na wasanii kadhaa jijini Nairobi zaidi ya wiki moja iliyopita na kwamba makubaliano ni chanya.
Katika ziara hiyo amezungumza na wasanii wengi na kwa kuanzia wawili wanatarajia kuwasili nchini siku chache zijazo kwa ajili ya kuanza kazi ya kurekodi na wasanii wa Tanzania.
“Lengo la ziara yangu lilikuwa kutanua mtandao wa Umoja Records na kusaka vipaji vipya.
“Wasanii watakaokuja wana vipaji vya hali ya juu na tunaamini watashirikiana na hawa waliopo nchini chini ya kampuni yetu.”
Lakini kikubwa anachozungumzia Gotta ni kukuza mkakati wa kampuni yake kwa kuongeza ubunifu katika muziki na kwamba wasanii waliopo wana uwezo mkubwa.
“Tutaangalia namna ya kufikia sehemu nyingine lakini kwa sasa tutaikamata Kenya na Uganda, wasanii hao wakiungana na wa kwetu hakuna shaka kwamba tunakuwa na product nzuri,” anasema.
Lakini anapozungumzia mtazamo mwelekeo wa muziki nchini hasa kwa bongofleva anasema kunatakiwa mapinduzi ya fikra.
“Unakumbuka tulianzisha project hapa ya kuwakusanya wanamuziki kwa ajili ya kutengeneza albamu ya reggae.
“Walikuja wengi na idadi kubwa ni wale wa kizazi kipya, tulielekezana na tukafika mahala tukafanya kazi nzuri pamoja.
“Lakini cha kushangaza kila aliyerekodi wimbo wake aliondoka zake na wengi hawajarudi,” anasema Gotta na kisha kuongeza:
“Walikuja wengi hapa wakarekodi na kuondoka lakini baadhi wamebaki na wana nia ya dhati kuwa nasi.
“Msanii kama Pestman, Ras Mizizi wameonyesha uwezo wa hali ya juu katika kazi zao. Wana fikra pevu na tunajivunia kuwa nao.
“Ras Inno naye anashirikiana nasi na kwa hakika anatupa changamoto nyingi. Kwa hiyo unaweza kuona kuwa ni mchanganyiko uliokomaa,” alisema Gotta.
Anawazungumzia vipi waliorekodi na kukimbia?
“Mimi nasema si tatizo lao, hao waliokimbia ni waathirika wa mfumo mzima wa hali ya utayarishaji wa muziki nchini.
“Kwamba si rahisi sana kuwabadilisha, tunahitaji mapinduzi ya fikra na si kazi ya siku moja.
“Lakini jambo moja liko wazi kwamba kama itatokea siku wakaamua kurejea hapa hatuna kinyongo nao, waje na tutawapokea.
“Wakija bila shaka watakuwa na kitu wamejifunza huko walikokimbilia nasi tutawaonyesha mapya tuliyonayo nadhani hapo tutafundishana na kuwa na kitu bora,” anasema Gotta.
Anapowataja baadhi wa wanamuziki ambao wana mwelekeo chanya katika Umoja Records hasiti kuwataja Pestman, Ras Mizizi, Carola na Ras Mizizi.
“Kwa hakika hawa waliobaki wanaangalia future, nitakupa mfano wa Pestman huyu ana ufahamu mkubwa na mara nyingi hupenda kujifunza mambo mapya.
“Alikuja hapa hajui kupiga gitaa, lakini sasa anaweza kuimba huku akipiga gitaa.
“Cha kufurahisha ni kwamba anaangalia matatizo ya dunia ya kuyajadili na kutoa njia mbadala ya kuyaepuka na wakati huo akiwasiliana na jamii.”
Kwa upande wa Ras Mizizi, Gotta anasema msanii huyo amekolezwa na asili yake ya Afrika na kwamba anapopiga reggae haachi kuzungumzia imani ya rasta na uafrika wake.
“Unaweza kusema kuwa huyu anahubiri imani ya Afrika ndani ya Rastafarian na ni mwepesi katika kurekodi.”
Mbali na hayo, Umoja Records imelenga kuweka uhusiano na mataifa mengine duniani hasa barani Ulaya kwa kuunda sound system na nembo ya pamoja.
“Tutakuwa na production team yetu na kuna kitu kinaitwa mobile disco ambavyo vitatufanya tuwe mahiri katika ziara zetu,” anasema Gotta.
Anasema mpango uliopo ni kuhakikisha kuwa wasanii wanakuwa na uwezo wa kurekodi kwa nembo za nje.
NILIPOZUNGUMZA naye kiasi cha miezi minne iliyopita, mmoja wa wakurugenzi wa Umoja Records, Gotta Warioba alikuwa na mengi ya kunieleza.
Alisema juu ya mwelekeo wa kampuni yake katika kuinua muziki wenye asili ya Kiafrika na kuusambaza kote duniani.
Midomo yake kwa hakika ilinena kwa kujiamini na alichokusudia kukisema. Wakati huo alikuwa katika kazi ngumu ya kuratibu kazi za wasanii kibao akiwamo Vital Maembe maarufu kama Sumu ya Teja.
Si kama nilikuwa na shaka juu ya msimamo wa Gotta la hasha. Niliwaza mengi na sikuishia kuwaza tu nilimwuliza namna atakavyojipanga katika kutekeleza aliyopanga.
Wakati huo alikuwa na mpango maalumu wa kuandaa albamu ya reggae ikiwakusanya wanamuziki wa aina mbalimbali. Ni wakati huo Gotta alilazimika kulala katika studio za Active ambazo ni sehemu ya Umoja Records.
Katika mpango huo walifanikiwa kupakua albamu ya iliyopewa jina la ‘Bongo Riddims & Style’ ikiwashirikisha wasanii wengi chipukizi.
Wiki iliyopita Gotta amefanya mahojiano na Bingwa na kuelezea mwelekeo wa Umoja Records na maendeleo ya muziki kwa ujumla.
“Umoja Records imetanua wigo wake baada ya kuanza kusaka wanamuziki kutoka Kenya na Uganda,” anasema Gotta.
Anasema ameshafanya mazungumzo na wasanii kadhaa jijini Nairobi zaidi ya wiki moja iliyopita na kwamba makubaliano ni chanya.
Katika ziara hiyo amezungumza na wasanii wengi na kwa kuanzia wawili wanatarajia kuwasili nchini siku chache zijazo kwa ajili ya kuanza kazi ya kurekodi na wasanii wa Tanzania.
“Lengo la ziara yangu lilikuwa kutanua mtandao wa Umoja Records na kusaka vipaji vipya.
“Wasanii watakaokuja wana vipaji vya hali ya juu na tunaamini watashirikiana na hawa waliopo nchini chini ya kampuni yetu.”
Lakini kikubwa anachozungumzia Gotta ni kukuza mkakati wa kampuni yake kwa kuongeza ubunifu katika muziki na kwamba wasanii waliopo wana uwezo mkubwa.
“Tutaangalia namna ya kufikia sehemu nyingine lakini kwa sasa tutaikamata Kenya na Uganda, wasanii hao wakiungana na wa kwetu hakuna shaka kwamba tunakuwa na product nzuri,” anasema.
Lakini anapozungumzia mtazamo mwelekeo wa muziki nchini hasa kwa bongofleva anasema kunatakiwa mapinduzi ya fikra.
“Unakumbuka tulianzisha project hapa ya kuwakusanya wanamuziki kwa ajili ya kutengeneza albamu ya reggae.
“Walikuja wengi na idadi kubwa ni wale wa kizazi kipya, tulielekezana na tukafika mahala tukafanya kazi nzuri pamoja.
“Lakini cha kushangaza kila aliyerekodi wimbo wake aliondoka zake na wengi hawajarudi,” anasema Gotta na kisha kuongeza:
“Walikuja wengi hapa wakarekodi na kuondoka lakini baadhi wamebaki na wana nia ya dhati kuwa nasi.
“Msanii kama Pestman, Ras Mizizi wameonyesha uwezo wa hali ya juu katika kazi zao. Wana fikra pevu na tunajivunia kuwa nao.
“Ras Inno naye anashirikiana nasi na kwa hakika anatupa changamoto nyingi. Kwa hiyo unaweza kuona kuwa ni mchanganyiko uliokomaa,” alisema Gotta.
Anawazungumzia vipi waliorekodi na kukimbia?
“Mimi nasema si tatizo lao, hao waliokimbia ni waathirika wa mfumo mzima wa hali ya utayarishaji wa muziki nchini.
“Kwamba si rahisi sana kuwabadilisha, tunahitaji mapinduzi ya fikra na si kazi ya siku moja.
“Lakini jambo moja liko wazi kwamba kama itatokea siku wakaamua kurejea hapa hatuna kinyongo nao, waje na tutawapokea.
“Wakija bila shaka watakuwa na kitu wamejifunza huko walikokimbilia nasi tutawaonyesha mapya tuliyonayo nadhani hapo tutafundishana na kuwa na kitu bora,” anasema Gotta.
Anapowataja baadhi wa wanamuziki ambao wana mwelekeo chanya katika Umoja Records hasiti kuwataja Pestman, Ras Mizizi, Carola na Ras Mizizi.
“Kwa hakika hawa waliobaki wanaangalia future, nitakupa mfano wa Pestman huyu ana ufahamu mkubwa na mara nyingi hupenda kujifunza mambo mapya.
“Alikuja hapa hajui kupiga gitaa, lakini sasa anaweza kuimba huku akipiga gitaa.
“Cha kufurahisha ni kwamba anaangalia matatizo ya dunia ya kuyajadili na kutoa njia mbadala ya kuyaepuka na wakati huo akiwasiliana na jamii.”
Kwa upande wa Ras Mizizi, Gotta anasema msanii huyo amekolezwa na asili yake ya Afrika na kwamba anapopiga reggae haachi kuzungumzia imani ya rasta na uafrika wake.
“Unaweza kusema kuwa huyu anahubiri imani ya Afrika ndani ya Rastafarian na ni mwepesi katika kurekodi.”
Mbali na hayo, Umoja Records imelenga kuweka uhusiano na mataifa mengine duniani hasa barani Ulaya kwa kuunda sound system na nembo ya pamoja.
“Tutakuwa na production team yetu na kuna kitu kinaitwa mobile disco ambavyo vitatufanya tuwe mahiri katika ziara zetu,” anasema Gotta.
Anasema mpango uliopo ni kuhakikisha kuwa wasanii wanakuwa na uwezo wa kurekodi kwa nembo za nje.
Monday, October 15, 2007
Vitambi vya vurugu Jangwani, Msimbazi
na innocent munyuku
HII imekuwa staili ya maisha ya kila siku. Hakuna maendeleo zaidi ya kushikiana bakora kwenye klabu za soka.
Kila unapokanyaga ni mbigili mtindo mmoja. Hadithi ni zile zile, mikwaruzano ndani ya klabu za soka bongo. Yanga na Simba ndizo zinazoongoza.
Mwandika Busati kwa muda mrefu amekuwa shuhuda wa hizo vurugu. Hakuna linalokwenda sawia badala yake ni watu kuumana kwa maslahi yao binafsi.
Yanga msimu huu moto umewaka. Mafahari wanapimana ubavu na wapambe wao pembeni wakisubiri matokeo. Wanachogombea ni ulaji na kujaza matumbo yao.
Kila kukicha hakuna maendeleo zaidi ya kuwasha moto wa mgogoro. Wanaoendesha masuala hayo wanajua wanachotaka na hakika wanakipata.
Mzee wa Busati hushangazwa na mambo haya. Kwamba inawezekanaje waseme wana mapenzi na klabu wakati wanaziangamiza?
Nani atakuwa mwokozi wa haya malumbano? Nani atafanikisha mema ndani ya klabu hizo? Hivi kweli kuna ulazima wa malumbano haya au ni laana ya kipekee?
Mwandika Busati sasa hana shaka tena kuamini kwamba Yanga na Simba ni makaburi ya wachezaji. Hakuna vitalu huko badala yake kumejaa misumari ya moto.
Waliojaa huko kwa kofia za uongozi hawana lolote kwani tambo zao zinatokana na kulishwa mabaya kutoka kwa wapambe wao wanaokaa vijiweni na kupanga mizozo.
Na kwa akili zao huwaza kwamba Tanzania inao ubavu wa kwenda Kombe la Dunia. Nani ataifikisha Tanzania huko wakati wachezaji wamelelewa kwenye migogoro?
Dira yao ni kupanga mbinu za kupambana na migogoro na si kuleta ufundi dimbani. Hilo si kosa lao kwani ndivyo mfumo ulivyo. Wala hakuna haja ya kuwalaumu hao ndiyo makuzi yao.
Kwa mfano timu hizo mbili hazina utaratibu mzuri wa kuleta makocha. Leo kaja huyu kesho kaletwa mwingine. Bila shaka kuna tatizo zaidi ya uendawazimu.
Hakuna umakini katika timu hizo na ndio maana kuna mengi yanafanyika kihuni na kiholela. Kila mwenye ulimi basi anayo fursa ya kutoa tamko hata kama tamko hilo ni pumba.
Midomo ya wapambe huwawezesha kupata ngwenje za kuvimbisha matumbo yao. Vitambi vinakuzwa kwa majungu na uzandiki. Husemwa kila linalowezekana ili wapate shibe. Hakuna lolote la kujenga soka.
Wenye akili zao hubaki wakicheka kwani wakati mwingine si busara kujibizana na wendawazimu. Waache wawehuke na matokeo yataonekana hivi pumbe.
Kama soka imewashinda jaribuni mashindano ya urembo au masumbwi. Kama mpira wa miguu umewashinda jaribuni riadha au kurusha tufe na kama ubavu mnao kajiungeni na wacheza gofu na tenisi.
Mzee wa Busati anatoa ushauri huo kutokana na ukweli kwamba kama kweli hao wanaojiita wadau wa soka wana nia ya kuinua mchezo huo mbona uozo ni ule ule?
Kila kukicha ni mizozo na mitafaruku. Kila uamkapo ni kelele za kugombea madaraka kwenye klabu hizo. Hii maana yake nini?
Tusidanganyane kwamba hao waliopo wana upeo wa kuweka mambo sawa. Kama upeo wanao basi wanaharibiwa na wapambe jambo ambalo ni hatari katika maendeleo ya soka nchini.
Hivi hakuna wa kuamka na kusema sasa yatosha? Kwa staili hii tusahau kuuza wachezaji wetu ng’ambo ya nchi na kama watauzwa basi wataishia Uarabuni ambako baada ya miezi michache huishia kuuza maduka ya Waarabu.
Kuna haja gani basi kujiita wadau wa Yanga na Simba wakati mwaleta mabaya klabuni? Dira za maendeleo hazimo. Kilichopo ni uhuni na uzushi wa migogoro.
Hakuna shaka kwamba huu ni mwanzo wa mwisho wa Simba na Yanga. Hakika huu ni ukomo ili ziibuke timu nyingine ambazo bila shaka zinaweza kuleta mageuzi.
Huu ni utabiri wa Mzee wa Busati na kama utatimia itakuwa neema kwa wapenda soka. Kwamba badala ya kugeukia Arsenal na Manchester United au Liverpool wataketi kuzishangalia timu za nyumbani.
Mwandika Busati anafikia ukomo kwa juma hili ambalo limeanza kwa wengi kubaki na madeni ya sikukuu. Idd el fitr imewatafuna na sasa mji umebaki kama pilipili.
Wasalaam,
HII imekuwa staili ya maisha ya kila siku. Hakuna maendeleo zaidi ya kushikiana bakora kwenye klabu za soka.
Kila unapokanyaga ni mbigili mtindo mmoja. Hadithi ni zile zile, mikwaruzano ndani ya klabu za soka bongo. Yanga na Simba ndizo zinazoongoza.
Mwandika Busati kwa muda mrefu amekuwa shuhuda wa hizo vurugu. Hakuna linalokwenda sawia badala yake ni watu kuumana kwa maslahi yao binafsi.
Yanga msimu huu moto umewaka. Mafahari wanapimana ubavu na wapambe wao pembeni wakisubiri matokeo. Wanachogombea ni ulaji na kujaza matumbo yao.
Kila kukicha hakuna maendeleo zaidi ya kuwasha moto wa mgogoro. Wanaoendesha masuala hayo wanajua wanachotaka na hakika wanakipata.
Mzee wa Busati hushangazwa na mambo haya. Kwamba inawezekanaje waseme wana mapenzi na klabu wakati wanaziangamiza?
Nani atakuwa mwokozi wa haya malumbano? Nani atafanikisha mema ndani ya klabu hizo? Hivi kweli kuna ulazima wa malumbano haya au ni laana ya kipekee?
Mwandika Busati sasa hana shaka tena kuamini kwamba Yanga na Simba ni makaburi ya wachezaji. Hakuna vitalu huko badala yake kumejaa misumari ya moto.
Waliojaa huko kwa kofia za uongozi hawana lolote kwani tambo zao zinatokana na kulishwa mabaya kutoka kwa wapambe wao wanaokaa vijiweni na kupanga mizozo.
Na kwa akili zao huwaza kwamba Tanzania inao ubavu wa kwenda Kombe la Dunia. Nani ataifikisha Tanzania huko wakati wachezaji wamelelewa kwenye migogoro?
Dira yao ni kupanga mbinu za kupambana na migogoro na si kuleta ufundi dimbani. Hilo si kosa lao kwani ndivyo mfumo ulivyo. Wala hakuna haja ya kuwalaumu hao ndiyo makuzi yao.
Kwa mfano timu hizo mbili hazina utaratibu mzuri wa kuleta makocha. Leo kaja huyu kesho kaletwa mwingine. Bila shaka kuna tatizo zaidi ya uendawazimu.
Hakuna umakini katika timu hizo na ndio maana kuna mengi yanafanyika kihuni na kiholela. Kila mwenye ulimi basi anayo fursa ya kutoa tamko hata kama tamko hilo ni pumba.
Midomo ya wapambe huwawezesha kupata ngwenje za kuvimbisha matumbo yao. Vitambi vinakuzwa kwa majungu na uzandiki. Husemwa kila linalowezekana ili wapate shibe. Hakuna lolote la kujenga soka.
Wenye akili zao hubaki wakicheka kwani wakati mwingine si busara kujibizana na wendawazimu. Waache wawehuke na matokeo yataonekana hivi pumbe.
Kama soka imewashinda jaribuni mashindano ya urembo au masumbwi. Kama mpira wa miguu umewashinda jaribuni riadha au kurusha tufe na kama ubavu mnao kajiungeni na wacheza gofu na tenisi.
Mzee wa Busati anatoa ushauri huo kutokana na ukweli kwamba kama kweli hao wanaojiita wadau wa soka wana nia ya kuinua mchezo huo mbona uozo ni ule ule?
Kila kukicha ni mizozo na mitafaruku. Kila uamkapo ni kelele za kugombea madaraka kwenye klabu hizo. Hii maana yake nini?
Tusidanganyane kwamba hao waliopo wana upeo wa kuweka mambo sawa. Kama upeo wanao basi wanaharibiwa na wapambe jambo ambalo ni hatari katika maendeleo ya soka nchini.
Hivi hakuna wa kuamka na kusema sasa yatosha? Kwa staili hii tusahau kuuza wachezaji wetu ng’ambo ya nchi na kama watauzwa basi wataishia Uarabuni ambako baada ya miezi michache huishia kuuza maduka ya Waarabu.
Kuna haja gani basi kujiita wadau wa Yanga na Simba wakati mwaleta mabaya klabuni? Dira za maendeleo hazimo. Kilichopo ni uhuni na uzushi wa migogoro.
Hakuna shaka kwamba huu ni mwanzo wa mwisho wa Simba na Yanga. Hakika huu ni ukomo ili ziibuke timu nyingine ambazo bila shaka zinaweza kuleta mageuzi.
Huu ni utabiri wa Mzee wa Busati na kama utatimia itakuwa neema kwa wapenda soka. Kwamba badala ya kugeukia Arsenal na Manchester United au Liverpool wataketi kuzishangalia timu za nyumbani.
Mwandika Busati anafikia ukomo kwa juma hili ambalo limeanza kwa wengi kubaki na madeni ya sikukuu. Idd el fitr imewatafuna na sasa mji umebaki kama pilipili.
Wasalaam,
Friday, October 12, 2007
Usu Mallya: Jembe jipya makini TGNP
-Akerwa na ubinafsishwaji holela nchini
-Asema maazimio ya Beijing bado changamoto kwa Serikali
Na Innocent Munyuku
KAMA kuna masuala ambayo yamekuwa yakipigiwa zumari katika sehemu nyingi duniani, usawa katika jamii na maisha bora huwezi kuviweka kando.
Zipo asasi nyingi nchini zilizoweka mikakati ya kutatua mambo kama hayo na moja ya asasi hizo ni Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) iliyoanzishwa mwaka 1993.
TGNP ni asasi isiyo ya kiserikali na kuundwa kwake kulilenga zaidi kuleta usawa wa jinsia katika jamii, kuwawezesha wanawake, mafunzo, utafiti na kusambaza taarifa muhimu zinazolenga ustawi wa jamii.
Hivi karibuni TGNP ilipata Mkurugenzi Mtendaji, Usu Mallya anayechukua nafasi ya Mary Rusimbi aliyemaliza muda wake.
Je, mkurugenzi huyo mpya ana mkakati gani baada ya kukalia usukani wa kuipeleka asasi hiyo mbele kimafanikio?
Katika mahojiano maalumu na MTANZANIA Jumapili juzi, Usu anasema mbali na kuwa na jukumu la usimamizi wa asasi hiyo, mfumo wa TGNP unamweka katika mazingira ya kufurahia kazi yake.
“TGNP imejengwa kwa namna kwamba kila jambo linafanywa kwa ushirikiano, hakuna maamuzi ya mtu mmoja.
“Lakini pia niko hapa tangu mwaka 1998 kwa hiyo nimejifunza mengi hapa hasa katika mkakati wa kujenga nguvu za pamoja,” anasema Usu na kisha kuongeza:
“Mtandao wetu umejengwa katika mhimili wa pamoja katika dhamira na dira.”
Pamoja na ukweli kwamba manyanyaso au ubaguzi wa kijinsia upo duniani kwa miaka mingi, nchi nyingi za Afrika ikiwemo Tanzania zilipata mwamko baada ya Mkutano wa Beijing Septemba mwaka 1995.
Katika mkutano huo wa wanawake uliazimia mambo mbalimbali ikiwemo kubadili mtazamo wa jamii katika kutendeana haki pasipo kubaguana.
Pia kujali utu na kumpa mwanamke sauti na kwamba wanaume kwa miaka mingi wamekuwa kikwazo katika maendeleo binafsi ya mwanamke.
Lakini je, baada ya miaka 12 kupita, TGNP inatathimini vipi mafanikio ya azimio la Beijing?
“Zipo fursa nyingi kwa wanawake lakini bado Serikali ina changamoto nyingi kufikia maendeleo.
“Katika elimu kumekuwa na jitihada lakini uwiano ni mdogo katika ngazi ya elimu ya juu. Kwa mfano wasichana wanaovuka kwenda kidato cha tano, sita hadi chuo kikuu inashuka,” anasema Usu.
Anaeleza kuwa kushuka kwa kiwango hicho kunatokana na mazingira au mfumo uliopo katika sheria za nchi.
“Sheria ya ndoa kwa mfano inaweka wazi kuwa mtoto wa kike anaweza kuolewa afikishapo umri wa miaka 14 au 15…sasa huu ndio muda wa mtoto kuwa shule. Akishaolewa safari yake inakuwa imeishia hapo.
“Lakini pia sheria kwamba mtoto wa kike akipata ujauzito abaki nyumbani nayo imechangia kwa kiasi kikubwa kuongeza idadi ya wasichana wenye elimu ya chini katika jamii.”
Hata hivyo, anasema maazimio mengine ya Beijing yanakwamishwa na sera za ubinafsishaji nchini.
Kwamba uchumi sasa ni wa utandawazi unaoongozwa na makampuni kutoka nchi tajiri duniani.
“Mikataba mingi katika eneo hilo ni ya kuwakandamiza wananchi, hii mikataba haijengi nchi changa.
“Nitoe mfano wa hapa kwetu, mkataba wa Bi-water umeshatuumiza, angalia suala la Richmond na umeme wetu au madini.
“Haya mambo yote yametuathiri kwa sababu ya utandawazi, angalia nchi kama Afrika Kusini, imeendelea kwa kiwango kikubwa kwa vile wametumia madini yao kujinufaisha. Hali ni tofauti na Tanzania,” anasema.
Anasema kutokana na mazingira kama hayo, hata jitihada za kuwakomboa Watanzania kutoka katika umasikini zinakuwa ngumu.
“Wanawake kwa mfano wako kwenye uchumi mdogo mdogo. Ninachosema hapa ni kwamba kama Serikali imeshindwa kuhodhi rasilimali basi hata hawa wa chini wataendelea kuumia,” anasema Usu.
Anazungumzia pia sekta ya utalii ambayo kwa mtazamo wake haijampa fursa Mtanzania kunufaika nayo.
“Nani anafaidi matunda ya utalii? Bila shaka ni watu wachache sana,” anasema.
Mbali na uchumi kuwa suala gumu katika kuwaendeleza Watanzania, kuna kikwazo katika sekta ya afya.
“Eneo hili ni changamoto kubwa kwa Serikali kwani linatakiwa kuwezeshwa na anayeumia sana ni mwanamke.
“Vifaa au huduma katika sekta hii bado haijamhakikishia mwanamke hatima njema hasa katika uzazi. Kuna takwimu zinazoonyesha kuwa katika wanawake 560 kati ya 100,000 hufariki dunia kila mwaka kutokana na uzazi usio salama.
“Hii ni dalili au ishara kwamba Serikali inakabiliwa na changamoto kubwa katika sekta ya afya hasa kwa afya ya mwanamke.”
Analalamikia uonevu ambao unachukua sura tofauti kila siku dhidi ya mwanamke.
“Kuna manyanyaso kwa wanawake, wengi wana uwezo mdogo wa kufanya maamuzi kuhusu ngono au idadi ya watoto.
“Ni jambo linalofanywa kuwa ni kawaida kwa mjamzito kufanya kazi za nyumbani huku akiwa na lishe duni hii si ajabu ikachangia vifo wakati mwingine.”
Vipi kuhusu nafasi ya mwanamke katika uongozi?
Usu anasema pamoja kuwa na wabunge wanawake kwa asilimia 30, bado kiwango hicho hakitoshi.
“Wapewe sauti au nafasi pia kuanzia kwenye udiwani…lakini pia naweza kusema kuwa wanawake wanahitaji nafasi pia katika sekta binafsi.
“Hata serikalini ipo haja kwa wanawake kupewa nafasi za juu kama vile ukuu wa mikoa, ukatibu mkuu, ubalozi nje ya nchi, ukurugenzi wa bodi au ujaji,” anasema Usu.
Pamoja na hilo, Usu anasema kuna mambo ambayo lazima yasemwe kwa uwazi au kujadiliwa kitaifa kuhusu utamaduni wa Mtanzania kutokana na ukweli kwamba mengi yanatokana na upotoshwaji wa mila.
Anasema jamii mara nyingi inamwona mwanamke kama chombo cha starehe na hata watoto wanapokua, mtoto wa kike tayari ameshajenga dhana ya kuwa wa chini.
“Hili ni suala nyeti linalopaswa kujadiliwa kitaifa, ni kama ilivyo rushwa lazima lijadiliwe. Hili jambo si la TGNP pekee bali Serikali nayo ihusike.”
Tangu kuanzishwa kwake, TGNP imefanikiwa katika kufikisha ujumbe kwa jamii kwa njia ya semina mbalimbali na kushirikiana na wanaharakati katika ngazi mbalimbali.
Mara nyingi imeshirikiana na FemAct katika kuilemisha jamii na ushirikiano huo upo kwa wanaharakati katika wilaya mbalimbali nchini.
“Tunatambua kazi za wanaharakati katika ngazi husika kwa kufanya semina na nafasi ya elimu kwa watu wa rika mbalimbali,” anasema Usu.
Mbali na semina, kila baada ya miaka miwili, TGNP hufanya tamasha la kijinsia ambalo huwapa fursa washiriki kufanya tathimini.
“Watu mbalimbali hualikwa na kinachofanyika ni kuibua mijadala na kushinikiza mabadiliko.
“Kuna sera kama mgawanyo mbovu wa mali katika familia kama vile ardhi au ukatili nazo hujadiliwa.
“Tumeanza kuishinikiza Serikali ibadili pia Katiba ya nchi kwani haimtendei haki mwanamke linapokuja suala la ndoa.
“Kuna mapungufu kwa mfano Katiba inaruhusu sheria za jadi kutambuliwa, sasa katika hali kama hiyo ni wazi kuwa mwanamke anapewa haki na wakati huo huo kumnyang’anya.
“Unaporuhusu kutumika kwa sheria ya jadi maana yake ni kuruhusu unyanyasaji kwani sheria nyingi za jadi zinamkandamiza mwanamke,” anasema.
TGNP imeshatoa mabango ya aina mbalimbali yanayolenga kuielimisha jamii.
Katika Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge mwaka 2005 walitoa bango la ‘Wakati umefika! Uwezo wa kuongoza tunao! Wanawake tujitokeze’.
Yapo mabango mengine kama la mwaka 2001 linalosomeka ‘Jinsia, demokrasia na maendeleo mbinu mbadala za kukabiliana na kufukarishwa’.
Lipo jingine la mwaka 2004 ‘Tatizo la dunia ya leo si umasikini ni mgawanyiko wa rasilimali wa kinyonyaji’.
Mwaka jana walikemea ubinafsishaji holela wa sekta ya maji.
Na mwaka huu TGNP imekuja na bango la ‘Sema hapana kwa ukatili wa kijinsia’.
Mbali na hayo wamekuwa na machapichopendwa kwa njia ya vitabu kama vile, Kwangu Wapi, Vijana Taifa la Leo, Kondomu Yazua Kasheshe, Utandawazi na Wewe na Ahadi za Uongo.
Pia TGNP imekuwa ikitoa vitabu vya kitaaluma kwa watafiti na wanafunzi. Baadhi ni Gender Profile of Tanzania: Enhancing Gender Family, Activists Voices, Against Neo Liberalism na Gender Budget Analysis in Tanzania 1997-2000.
Kuna maktaba ya kisasa na duka la vitabu katika ofisi hizo zilizopo eneo la Mabibo jijini Dar es Salaam na kila Jumatano huendeshwa semina kwa watu wote katika ofisi hizo kuanzia saa tisa mchana hadi 11 jioni.
Usu Mallya alitokea wapi? Alizaliwa mkoani Shinyanga mwaka 1961 na elimu yake ya msingi aliipata Marangu Sembeti Wilaya ya Moshi Vijijini mkoani Kilimanjaro. Hii ilikuwa kati ya mwaka 1968-74.
Kati ya mwaka 1975-78 alikuwa Shule ya Sekondari ya Kibosho alikohitimu kidato cha nne. Elimu ya juu ya sekondari aliipata Korogwe mkoani Tanga.
Baadaye alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam alikopata shahada ya kwanza ya uongozi wa taasisi za umma, sayansi ya jamii na Kifaransa. Alihitimu mwaka 1985.
Aliwahi kufanya kazi chuoni hapo katika Idara ya Sayansi ya Jamii kati ya mwaka 1990-95.
Alirejea darasani kusomea shahada ya uzamili chuoni hapo akichukua masomo ya sayansi ya jamii. Alihitimu mwaka 1997.
Mwaka mmoja baadaye akajiunga na TGNP.
-Asema maazimio ya Beijing bado changamoto kwa Serikali
Na Innocent Munyuku
KAMA kuna masuala ambayo yamekuwa yakipigiwa zumari katika sehemu nyingi duniani, usawa katika jamii na maisha bora huwezi kuviweka kando.
Zipo asasi nyingi nchini zilizoweka mikakati ya kutatua mambo kama hayo na moja ya asasi hizo ni Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) iliyoanzishwa mwaka 1993.
TGNP ni asasi isiyo ya kiserikali na kuundwa kwake kulilenga zaidi kuleta usawa wa jinsia katika jamii, kuwawezesha wanawake, mafunzo, utafiti na kusambaza taarifa muhimu zinazolenga ustawi wa jamii.
Hivi karibuni TGNP ilipata Mkurugenzi Mtendaji, Usu Mallya anayechukua nafasi ya Mary Rusimbi aliyemaliza muda wake.
Je, mkurugenzi huyo mpya ana mkakati gani baada ya kukalia usukani wa kuipeleka asasi hiyo mbele kimafanikio?
Katika mahojiano maalumu na MTANZANIA Jumapili juzi, Usu anasema mbali na kuwa na jukumu la usimamizi wa asasi hiyo, mfumo wa TGNP unamweka katika mazingira ya kufurahia kazi yake.
“TGNP imejengwa kwa namna kwamba kila jambo linafanywa kwa ushirikiano, hakuna maamuzi ya mtu mmoja.
“Lakini pia niko hapa tangu mwaka 1998 kwa hiyo nimejifunza mengi hapa hasa katika mkakati wa kujenga nguvu za pamoja,” anasema Usu na kisha kuongeza:
“Mtandao wetu umejengwa katika mhimili wa pamoja katika dhamira na dira.”
Pamoja na ukweli kwamba manyanyaso au ubaguzi wa kijinsia upo duniani kwa miaka mingi, nchi nyingi za Afrika ikiwemo Tanzania zilipata mwamko baada ya Mkutano wa Beijing Septemba mwaka 1995.
Katika mkutano huo wa wanawake uliazimia mambo mbalimbali ikiwemo kubadili mtazamo wa jamii katika kutendeana haki pasipo kubaguana.
Pia kujali utu na kumpa mwanamke sauti na kwamba wanaume kwa miaka mingi wamekuwa kikwazo katika maendeleo binafsi ya mwanamke.
Lakini je, baada ya miaka 12 kupita, TGNP inatathimini vipi mafanikio ya azimio la Beijing?
“Zipo fursa nyingi kwa wanawake lakini bado Serikali ina changamoto nyingi kufikia maendeleo.
“Katika elimu kumekuwa na jitihada lakini uwiano ni mdogo katika ngazi ya elimu ya juu. Kwa mfano wasichana wanaovuka kwenda kidato cha tano, sita hadi chuo kikuu inashuka,” anasema Usu.
Anaeleza kuwa kushuka kwa kiwango hicho kunatokana na mazingira au mfumo uliopo katika sheria za nchi.
“Sheria ya ndoa kwa mfano inaweka wazi kuwa mtoto wa kike anaweza kuolewa afikishapo umri wa miaka 14 au 15…sasa huu ndio muda wa mtoto kuwa shule. Akishaolewa safari yake inakuwa imeishia hapo.
“Lakini pia sheria kwamba mtoto wa kike akipata ujauzito abaki nyumbani nayo imechangia kwa kiasi kikubwa kuongeza idadi ya wasichana wenye elimu ya chini katika jamii.”
Hata hivyo, anasema maazimio mengine ya Beijing yanakwamishwa na sera za ubinafsishaji nchini.
Kwamba uchumi sasa ni wa utandawazi unaoongozwa na makampuni kutoka nchi tajiri duniani.
“Mikataba mingi katika eneo hilo ni ya kuwakandamiza wananchi, hii mikataba haijengi nchi changa.
“Nitoe mfano wa hapa kwetu, mkataba wa Bi-water umeshatuumiza, angalia suala la Richmond na umeme wetu au madini.
“Haya mambo yote yametuathiri kwa sababu ya utandawazi, angalia nchi kama Afrika Kusini, imeendelea kwa kiwango kikubwa kwa vile wametumia madini yao kujinufaisha. Hali ni tofauti na Tanzania,” anasema.
Anasema kutokana na mazingira kama hayo, hata jitihada za kuwakomboa Watanzania kutoka katika umasikini zinakuwa ngumu.
“Wanawake kwa mfano wako kwenye uchumi mdogo mdogo. Ninachosema hapa ni kwamba kama Serikali imeshindwa kuhodhi rasilimali basi hata hawa wa chini wataendelea kuumia,” anasema Usu.
Anazungumzia pia sekta ya utalii ambayo kwa mtazamo wake haijampa fursa Mtanzania kunufaika nayo.
“Nani anafaidi matunda ya utalii? Bila shaka ni watu wachache sana,” anasema.
Mbali na uchumi kuwa suala gumu katika kuwaendeleza Watanzania, kuna kikwazo katika sekta ya afya.
“Eneo hili ni changamoto kubwa kwa Serikali kwani linatakiwa kuwezeshwa na anayeumia sana ni mwanamke.
“Vifaa au huduma katika sekta hii bado haijamhakikishia mwanamke hatima njema hasa katika uzazi. Kuna takwimu zinazoonyesha kuwa katika wanawake 560 kati ya 100,000 hufariki dunia kila mwaka kutokana na uzazi usio salama.
“Hii ni dalili au ishara kwamba Serikali inakabiliwa na changamoto kubwa katika sekta ya afya hasa kwa afya ya mwanamke.”
Analalamikia uonevu ambao unachukua sura tofauti kila siku dhidi ya mwanamke.
“Kuna manyanyaso kwa wanawake, wengi wana uwezo mdogo wa kufanya maamuzi kuhusu ngono au idadi ya watoto.
“Ni jambo linalofanywa kuwa ni kawaida kwa mjamzito kufanya kazi za nyumbani huku akiwa na lishe duni hii si ajabu ikachangia vifo wakati mwingine.”
Vipi kuhusu nafasi ya mwanamke katika uongozi?
Usu anasema pamoja kuwa na wabunge wanawake kwa asilimia 30, bado kiwango hicho hakitoshi.
“Wapewe sauti au nafasi pia kuanzia kwenye udiwani…lakini pia naweza kusema kuwa wanawake wanahitaji nafasi pia katika sekta binafsi.
“Hata serikalini ipo haja kwa wanawake kupewa nafasi za juu kama vile ukuu wa mikoa, ukatibu mkuu, ubalozi nje ya nchi, ukurugenzi wa bodi au ujaji,” anasema Usu.
Pamoja na hilo, Usu anasema kuna mambo ambayo lazima yasemwe kwa uwazi au kujadiliwa kitaifa kuhusu utamaduni wa Mtanzania kutokana na ukweli kwamba mengi yanatokana na upotoshwaji wa mila.
Anasema jamii mara nyingi inamwona mwanamke kama chombo cha starehe na hata watoto wanapokua, mtoto wa kike tayari ameshajenga dhana ya kuwa wa chini.
“Hili ni suala nyeti linalopaswa kujadiliwa kitaifa, ni kama ilivyo rushwa lazima lijadiliwe. Hili jambo si la TGNP pekee bali Serikali nayo ihusike.”
Tangu kuanzishwa kwake, TGNP imefanikiwa katika kufikisha ujumbe kwa jamii kwa njia ya semina mbalimbali na kushirikiana na wanaharakati katika ngazi mbalimbali.
Mara nyingi imeshirikiana na FemAct katika kuilemisha jamii na ushirikiano huo upo kwa wanaharakati katika wilaya mbalimbali nchini.
“Tunatambua kazi za wanaharakati katika ngazi husika kwa kufanya semina na nafasi ya elimu kwa watu wa rika mbalimbali,” anasema Usu.
Mbali na semina, kila baada ya miaka miwili, TGNP hufanya tamasha la kijinsia ambalo huwapa fursa washiriki kufanya tathimini.
“Watu mbalimbali hualikwa na kinachofanyika ni kuibua mijadala na kushinikiza mabadiliko.
“Kuna sera kama mgawanyo mbovu wa mali katika familia kama vile ardhi au ukatili nazo hujadiliwa.
“Tumeanza kuishinikiza Serikali ibadili pia Katiba ya nchi kwani haimtendei haki mwanamke linapokuja suala la ndoa.
“Kuna mapungufu kwa mfano Katiba inaruhusu sheria za jadi kutambuliwa, sasa katika hali kama hiyo ni wazi kuwa mwanamke anapewa haki na wakati huo huo kumnyang’anya.
“Unaporuhusu kutumika kwa sheria ya jadi maana yake ni kuruhusu unyanyasaji kwani sheria nyingi za jadi zinamkandamiza mwanamke,” anasema.
TGNP imeshatoa mabango ya aina mbalimbali yanayolenga kuielimisha jamii.
Katika Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge mwaka 2005 walitoa bango la ‘Wakati umefika! Uwezo wa kuongoza tunao! Wanawake tujitokeze’.
Yapo mabango mengine kama la mwaka 2001 linalosomeka ‘Jinsia, demokrasia na maendeleo mbinu mbadala za kukabiliana na kufukarishwa’.
Lipo jingine la mwaka 2004 ‘Tatizo la dunia ya leo si umasikini ni mgawanyiko wa rasilimali wa kinyonyaji’.
Mwaka jana walikemea ubinafsishaji holela wa sekta ya maji.
Na mwaka huu TGNP imekuja na bango la ‘Sema hapana kwa ukatili wa kijinsia’.
Mbali na hayo wamekuwa na machapichopendwa kwa njia ya vitabu kama vile, Kwangu Wapi, Vijana Taifa la Leo, Kondomu Yazua Kasheshe, Utandawazi na Wewe na Ahadi za Uongo.
Pia TGNP imekuwa ikitoa vitabu vya kitaaluma kwa watafiti na wanafunzi. Baadhi ni Gender Profile of Tanzania: Enhancing Gender Family, Activists Voices, Against Neo Liberalism na Gender Budget Analysis in Tanzania 1997-2000.
Kuna maktaba ya kisasa na duka la vitabu katika ofisi hizo zilizopo eneo la Mabibo jijini Dar es Salaam na kila Jumatano huendeshwa semina kwa watu wote katika ofisi hizo kuanzia saa tisa mchana hadi 11 jioni.
Usu Mallya alitokea wapi? Alizaliwa mkoani Shinyanga mwaka 1961 na elimu yake ya msingi aliipata Marangu Sembeti Wilaya ya Moshi Vijijini mkoani Kilimanjaro. Hii ilikuwa kati ya mwaka 1968-74.
Kati ya mwaka 1975-78 alikuwa Shule ya Sekondari ya Kibosho alikohitimu kidato cha nne. Elimu ya juu ya sekondari aliipata Korogwe mkoani Tanga.
Baadaye alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam alikopata shahada ya kwanza ya uongozi wa taasisi za umma, sayansi ya jamii na Kifaransa. Alihitimu mwaka 1985.
Aliwahi kufanya kazi chuoni hapo katika Idara ya Sayansi ya Jamii kati ya mwaka 1990-95.
Alirejea darasani kusomea shahada ya uzamili chuoni hapo akichukua masomo ya sayansi ya jamii. Alihitimu mwaka 1997.
Mwaka mmoja baadaye akajiunga na TGNP.
Amina Chifupa amefariki dunia bila amani moyoni
WATANZANIA kwa muda wamesahau kujadili maumivu ya Bajeti ya Mwaka Mpya wa Fedha wa 2007/8. Wamepunguza kuizumgumzia Taifa Stars na safari yake ya Ghana. Kinachonenwa sasa ni kifo cha Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Amina Chifupa aliyefariki dunia Jumanne wiki hii jijini Dar es Salaam. Katika makala haya waandishi wetu ELIZABETH MJATTA na INNOCENT MUNYUKU wanazungumzia mengi na matarajio aliyokuwa nayo Amina katika uhai wake.
Mwanasiasa huyo machachari aliyekuwa jasiri mdogo kuliko wote bungeni ambaye alipata nafasi hiyo kupitia tiketi ya Umoja wa Vijana wa CCM.
Siku chache kabla ya kuhudhuria Mkutano wa Tano wa Bunge mwaka jana, Amina alifanya mahojiano na gazeti dada la RAI.
Alifika chumba cha habari kwa ajili ya mahojiano maalumu yaliyochukua takribani saa 2. Akiwa amevalia suti yake nyeusi, hereni ndefu za dhahabu kwenye masikio yake, mkufu wa dhahabu ulioshika vema shingo yake, bangili mikononi mwake vilitosha kumpendezesha nyota huyo aliyezimika ghafla.
Kama ilivyokuwa hulka yake, Amina alisema mengi ya msingi kwa kujiamini na hata alipoulizwa juu ya nini kilichompa ujasiri wa kuapa kwa mbingu bungeni kwamba atawafichua wauza dawa za kulevya hakuonekana kujuta.
“Sikuogopa hata kidogo…ninaamini kuwa mimi ni kiongozi hivyo siwezi kuogopa kusema ukweli,” alisema Amina.
Lakini hakuishia hapo akaongeza: “Kama mtu ni mwoga hafai kuingia bungeni, hatuwezi kuwaacha vijana wa Tanzania wakiangamia kwa matumizi ya dawa za kulevya.”
Alitumia fursa hiyo kuzungumzia namna alivyojisikia vibaya baada ya baadhi ya magazeti na watu mbalimbali kuhoji uwezo wake mara alipotangaza kujiingiza katika siasa.
“Siku ya kuapishwa bungeni ilikuwa kazi ngumu kwangu. Pamoja na kuwa mzungumzaji mzuri nilikuwa mwoga nikaona kitu cha ajabu. Nadhani hilo lilitokana na ukweli kwamba baadhi ya magazeti yalishanibeza.
“Baada ya kula kiapo nikaanza kupata ‘vinoti’ vya kunipongeza, mmoja wao alikuwa Kapteni John Komba aliyesema ‘mwanangu umenitoa aibu’.”
Alipoanza kutoa hoja zake bungeni, Amina alionyesha dira njema kwa kuigusa jamii moja kwa moja. Alizungumzia umuhimu wa kuwasaidia wanawake wajawazito na udhibiti wa malaria nchini.
Akawa gumzo kwa walio wengi na hata yale maneno ya kejeli kwamba hakuwa na dira njema zikaanza kuyeyuka. Akavaa koti la umakini na huku akijenga matumaini kwa vijana nchini.
Amina hakuishia katika siasa pekee aliingia kila mahala kwa lengo la kujenga jamii bora. Alihimiza ustawi wa watoto yatima, uendelezwaji wa michezo na sanaa kwa ujumla.
Alikuwa bega kwa bega kuisadia timu ya soka ya taifa (Taifa Stars) lakini pia alikuwa mbioni kuanzisha ligi ya taifa kwa vijana.
Jumatano wiki hii wakati wa kuuga mwili wa marehemu, Ruge Mutahaba ambaye ni mmoja wa wakurugenzi wa Clouds FM ambayo Amina alipata kufanya kazi ya utangazaji, alitaja sifa kubwa ya Amina kuwa ni king’ang’anizi.
“Siwezi kupata lugha rahisi kuelezea ujasiri wake…nitatoa mfano wakati nilipomweleza kuwa anatakiwa kufanya kazi kwa siku sita na kupumzika siku moja akagoma.
“Akatoa wazo kwamba anahitaji kuanzisha kipindi cha taarabu,” anasema Mutahaba na kuongeza kuwa hakuwa na namna ya kumzuia.
“Tukampa nafasi na kweli alifanya vizuri sana katika kipindi hicho cha taarabu na kikubwa zaidi ni kwamba alikuwa mbunifu.”
Naye mtangazaji maarufu nchini, Taji Liundi anayejulikana pia kama ‘Master T’ anamwelezea Amina kuwa mmoja wa wasichana waliokuwa na moyo wa kuthubutu.
“Alikuwa mwenye ujasiri na kuamini kuwa anao uwezo wa kufanya mambo mapya yenye faida kwa jamii.
“Alipenda kuelekezwa kwa kila jambo alilolifanya hata kama alijua kuwa anaweza akalifanya mwenyewe.
“Lakini nasikitika kwamba Amina amefariki dunia bila amani moyoni. Ameondoka wakati mgumu akiwa na msongamano wa mawazo. Hili linaniumiza sana,” anasema Taji.
Wakati fulani alipotembelea kituo kimoja cha watoto yatima jijini Dar es Salaam, Amina aliwahi kumwaga machozi baada ya kuona mazingira waishio watoto hao.
Mapenzi yake kwa watoto yalijionyesha pia wakati akiendesha kipindi cha watoto katika redio.
Katika kipindi chake hicho, alikuwa akipingana sana na baadhi ya wazazi waliokuwa wakifanya matendo mabaya kwa watoto wao. Alikemea unyanyasaji wa watoto.
Lilipokuja suala la mada ya kujadili daima aliibuka mshindi kutokana na uwezo wake wa kujenga hoja na kukubalika. Huo ukawa msingi wa umaarufu wake.
Maelfu ya watu waliofika kuuga mwili wake walionyesha kuwa tayari kuna pengo kubwa katika jamii. Kwamba matarajio na misingi mizuri aliyokuwa ameanza kuijenga Amina bila shaka sasa inakwenda upogo.
Wapo wanaoendelea kushangaa kipaji cha binti huyo kwani katika umri wake mdogo aliweza kufanya mambo makubwa katika jamii tofauti na umri wake.
Amina sasa hatunaye ameshazikwa kijijini kwao Luhanjo-Lupembe Wilaya ya Njombe na kilichobaki sasa ni kuenzi mema yake.
Licha ya kuwa na msimamo katika kupambana na dawa za kulevya, alikuwa mtetezi wa wanawake, vijana, watoto na wanafunzi.
Katika michango yake bungeni. Kwa muda mfupi aliokaa bungeni tangu ale kiapo mjini Dodoma, Desemba 28, 2005, Amina amejipambanua na kuwa miongoni mwa wachangiaji mahiri bungeni, licha ya uchanga wake kisiasa.
Lakini pia alikuwa na mvuto katika jamii na ndiyo maana haikushangaza pale habari zake zilipokuwa zikipewa umuhimu mkubwa katika vyombo vya habari nchini.
Pamoja na hilo, Mei 6 mwaka huu, Amina alianza kuwa kwenye wakati mgumu baada ya kuripotiwa kuwa ametalikiwa na mumewe Mohamed Mpakanjia.
Mpakanjia alikaririwa na vyombo vya habari akisema kuwa ametengana na mkewe huyo aliyedumu naye katika ndoa kwa miaka mitano na kubahatika kupata mtoto mmoja wa kiume.
Kwa bahati mbaya sana mara baada ya taarifa hiyo ya talaka, zikaja taarifa kwamba Amina amelimwa talaka kutokana na kujihusisha kimapenzi na Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe wa Chadema.
Siku tatu baada ya habari za talaka kuripotiwa, baba yake Amina alizungumza na waandishi wa habari kwenye Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Dar es Salaam akisema kuwa suala hilo ni la kisiasa na kwamba CCM inao utaratibu wake wa kutatua mambo yake.
“Masuala yote yanapitia katika mkondo wake. Wazazi hatutaki kuharibu pensheni yetu, si mnajua kuwa siku hizi watoto ndio pensheni?” alisema Mzee Chifupa.
Lakini wanahabari wengi walishangazwa na hatua ya Mzee Chifupa kuitisha kuzungumza katika mkutano huo kwani jana yake Amina aliahidi kuzungumza yeye.
Waandishi walikuwa na shauku ya kukutana na Amina ana kwa ana kwani wiki moja kabla ya kuthibitishwa kwa taarifa za kutalikiwa, anadaiwa alisambaza ujumbe wa maandishi katika simu za mkononi.
Inadaiwa kuwa ujumbe huo ulikwenda kwa baadhi ya watu wanaoaminika kuwa karibu na Naibu Waziri mmoja aliyemtuhumu kusababisha kuvunjika kwa ndoa yake.
Ujumbe ulisomeka hivi: “Alichounganisha Mwenyezi Mungu binadamu hawezi kukitenganisha. Nakuheshimu sana kama kiongozi wangu, Mwenyekiti wangu, Naibu Waziri, M-NEC, M-CCM, mkubwa wangu kiumri, mbunge na kadhalika.
“Nimesikitishwa sana na jitihada za kutaka kuvuruga ndoa yangu, nakutakia kila la heri, lakini usisahau malipo ni hapa hapa duniani na kila mwenye kufanyia wenzake mabaya na yeye hulipwa kwa ubaya.
“Nampenda sana mume wangu na ntailinda ndoa yangu kwa gharama yoyote cko tayari kumpoteza, mi ni zaidi ya mwanamke. Asante sana, kila la heri na kazi njema katika kulifanikisha hilo, wizara
yako nyeti sana, ina mambo mengi sana. Bye.”
Kuna wakati ikasemwa kwamba kuachika kwake kulikuja baada ya Naibu Waziri mmoja kudaiwa kwenda kumchomea utambi kwa mumewe. Baada ya tukio hilo, Amina alitoa ahadi ya kumtaja mbaya wake jambo ambalo halikutimia.
Yapo madai kuwa Naibu Waziri huyo alikuwa na mipango ya kumpaka matope katika siasa kutokana na nia aliyoitangaza ya kutaka kugombea uenyekiti wa taifa wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM).
Amina pia alikuwa ameomba ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC), kupitia Kundi la Vijana katika Uchaguzi Mkuu wa CCM unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.
Juni 22, mwaka huu, Amina aliuliza bungeni kwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, akitaka kufahamishwa hatua gani zinazochukuliwa na Serikali katika kudhibiti uvujaji wa mitihani. Liliulizwa kwa niaba yake na Mbunge wa Muleba Kaskazini, Ruth Msafiri (CCM).
Amina aliyezaliwa Mei 20 mwaka 1981 alikuwa mcheshi na katika moja ya mikakati yake alipata kutamka kuwa ipo siku atajitumbukiza katika kinyang’anyiro katika jimbo.
Hakuishia katika kulitamani jimbo. Alipata kusema pia kuwa anaamini anao ubavu wa kuwa rais wa nchi katika miaka ijayo. Kauli hiyo aliitoa wakati alipohojiwa katika kipindi cha Jahazi cha Radio Clouds FM Mei mwaka huu.
Alisema wanasiasa wengi dunia huwa na ndoto ya kupanda ngazi hadi kufikia urais.
Aliongeza kuwa maisha ya kila mwanadamu huenda kwa malengo. Kwa hakika yaweza kusemwa kuwa maisha ya Amina yalikwenda kwa utaratibu wa kufikiria mambo chanya daima.
Pamoja na hayo, atakumbukwa kwa tukio lililomsibu bungeni mwaka jana wakati alipoagizwa na Spika kutoka nje ya ukumbi wa Bunge kutokana na kuvaa suti ya kike na kofia ya pama bila glovu kwa mujibu wa kanuni.
Mwanasiasa huyo machachari aliyekuwa jasiri mdogo kuliko wote bungeni ambaye alipata nafasi hiyo kupitia tiketi ya Umoja wa Vijana wa CCM.
Siku chache kabla ya kuhudhuria Mkutano wa Tano wa Bunge mwaka jana, Amina alifanya mahojiano na gazeti dada la RAI.
Alifika chumba cha habari kwa ajili ya mahojiano maalumu yaliyochukua takribani saa 2. Akiwa amevalia suti yake nyeusi, hereni ndefu za dhahabu kwenye masikio yake, mkufu wa dhahabu ulioshika vema shingo yake, bangili mikononi mwake vilitosha kumpendezesha nyota huyo aliyezimika ghafla.
Kama ilivyokuwa hulka yake, Amina alisema mengi ya msingi kwa kujiamini na hata alipoulizwa juu ya nini kilichompa ujasiri wa kuapa kwa mbingu bungeni kwamba atawafichua wauza dawa za kulevya hakuonekana kujuta.
“Sikuogopa hata kidogo…ninaamini kuwa mimi ni kiongozi hivyo siwezi kuogopa kusema ukweli,” alisema Amina.
Lakini hakuishia hapo akaongeza: “Kama mtu ni mwoga hafai kuingia bungeni, hatuwezi kuwaacha vijana wa Tanzania wakiangamia kwa matumizi ya dawa za kulevya.”
Alitumia fursa hiyo kuzungumzia namna alivyojisikia vibaya baada ya baadhi ya magazeti na watu mbalimbali kuhoji uwezo wake mara alipotangaza kujiingiza katika siasa.
“Siku ya kuapishwa bungeni ilikuwa kazi ngumu kwangu. Pamoja na kuwa mzungumzaji mzuri nilikuwa mwoga nikaona kitu cha ajabu. Nadhani hilo lilitokana na ukweli kwamba baadhi ya magazeti yalishanibeza.
“Baada ya kula kiapo nikaanza kupata ‘vinoti’ vya kunipongeza, mmoja wao alikuwa Kapteni John Komba aliyesema ‘mwanangu umenitoa aibu’.”
Alipoanza kutoa hoja zake bungeni, Amina alionyesha dira njema kwa kuigusa jamii moja kwa moja. Alizungumzia umuhimu wa kuwasaidia wanawake wajawazito na udhibiti wa malaria nchini.
Akawa gumzo kwa walio wengi na hata yale maneno ya kejeli kwamba hakuwa na dira njema zikaanza kuyeyuka. Akavaa koti la umakini na huku akijenga matumaini kwa vijana nchini.
Amina hakuishia katika siasa pekee aliingia kila mahala kwa lengo la kujenga jamii bora. Alihimiza ustawi wa watoto yatima, uendelezwaji wa michezo na sanaa kwa ujumla.
Alikuwa bega kwa bega kuisadia timu ya soka ya taifa (Taifa Stars) lakini pia alikuwa mbioni kuanzisha ligi ya taifa kwa vijana.
Jumatano wiki hii wakati wa kuuga mwili wa marehemu, Ruge Mutahaba ambaye ni mmoja wa wakurugenzi wa Clouds FM ambayo Amina alipata kufanya kazi ya utangazaji, alitaja sifa kubwa ya Amina kuwa ni king’ang’anizi.
“Siwezi kupata lugha rahisi kuelezea ujasiri wake…nitatoa mfano wakati nilipomweleza kuwa anatakiwa kufanya kazi kwa siku sita na kupumzika siku moja akagoma.
“Akatoa wazo kwamba anahitaji kuanzisha kipindi cha taarabu,” anasema Mutahaba na kuongeza kuwa hakuwa na namna ya kumzuia.
“Tukampa nafasi na kweli alifanya vizuri sana katika kipindi hicho cha taarabu na kikubwa zaidi ni kwamba alikuwa mbunifu.”
Naye mtangazaji maarufu nchini, Taji Liundi anayejulikana pia kama ‘Master T’ anamwelezea Amina kuwa mmoja wa wasichana waliokuwa na moyo wa kuthubutu.
“Alikuwa mwenye ujasiri na kuamini kuwa anao uwezo wa kufanya mambo mapya yenye faida kwa jamii.
“Alipenda kuelekezwa kwa kila jambo alilolifanya hata kama alijua kuwa anaweza akalifanya mwenyewe.
“Lakini nasikitika kwamba Amina amefariki dunia bila amani moyoni. Ameondoka wakati mgumu akiwa na msongamano wa mawazo. Hili linaniumiza sana,” anasema Taji.
Wakati fulani alipotembelea kituo kimoja cha watoto yatima jijini Dar es Salaam, Amina aliwahi kumwaga machozi baada ya kuona mazingira waishio watoto hao.
Mapenzi yake kwa watoto yalijionyesha pia wakati akiendesha kipindi cha watoto katika redio.
Katika kipindi chake hicho, alikuwa akipingana sana na baadhi ya wazazi waliokuwa wakifanya matendo mabaya kwa watoto wao. Alikemea unyanyasaji wa watoto.
Lilipokuja suala la mada ya kujadili daima aliibuka mshindi kutokana na uwezo wake wa kujenga hoja na kukubalika. Huo ukawa msingi wa umaarufu wake.
Maelfu ya watu waliofika kuuga mwili wake walionyesha kuwa tayari kuna pengo kubwa katika jamii. Kwamba matarajio na misingi mizuri aliyokuwa ameanza kuijenga Amina bila shaka sasa inakwenda upogo.
Wapo wanaoendelea kushangaa kipaji cha binti huyo kwani katika umri wake mdogo aliweza kufanya mambo makubwa katika jamii tofauti na umri wake.
Amina sasa hatunaye ameshazikwa kijijini kwao Luhanjo-Lupembe Wilaya ya Njombe na kilichobaki sasa ni kuenzi mema yake.
Licha ya kuwa na msimamo katika kupambana na dawa za kulevya, alikuwa mtetezi wa wanawake, vijana, watoto na wanafunzi.
Katika michango yake bungeni. Kwa muda mfupi aliokaa bungeni tangu ale kiapo mjini Dodoma, Desemba 28, 2005, Amina amejipambanua na kuwa miongoni mwa wachangiaji mahiri bungeni, licha ya uchanga wake kisiasa.
Lakini pia alikuwa na mvuto katika jamii na ndiyo maana haikushangaza pale habari zake zilipokuwa zikipewa umuhimu mkubwa katika vyombo vya habari nchini.
Pamoja na hilo, Mei 6 mwaka huu, Amina alianza kuwa kwenye wakati mgumu baada ya kuripotiwa kuwa ametalikiwa na mumewe Mohamed Mpakanjia.
Mpakanjia alikaririwa na vyombo vya habari akisema kuwa ametengana na mkewe huyo aliyedumu naye katika ndoa kwa miaka mitano na kubahatika kupata mtoto mmoja wa kiume.
Kwa bahati mbaya sana mara baada ya taarifa hiyo ya talaka, zikaja taarifa kwamba Amina amelimwa talaka kutokana na kujihusisha kimapenzi na Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe wa Chadema.
Siku tatu baada ya habari za talaka kuripotiwa, baba yake Amina alizungumza na waandishi wa habari kwenye Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Dar es Salaam akisema kuwa suala hilo ni la kisiasa na kwamba CCM inao utaratibu wake wa kutatua mambo yake.
“Masuala yote yanapitia katika mkondo wake. Wazazi hatutaki kuharibu pensheni yetu, si mnajua kuwa siku hizi watoto ndio pensheni?” alisema Mzee Chifupa.
Lakini wanahabari wengi walishangazwa na hatua ya Mzee Chifupa kuitisha kuzungumza katika mkutano huo kwani jana yake Amina aliahidi kuzungumza yeye.
Waandishi walikuwa na shauku ya kukutana na Amina ana kwa ana kwani wiki moja kabla ya kuthibitishwa kwa taarifa za kutalikiwa, anadaiwa alisambaza ujumbe wa maandishi katika simu za mkononi.
Inadaiwa kuwa ujumbe huo ulikwenda kwa baadhi ya watu wanaoaminika kuwa karibu na Naibu Waziri mmoja aliyemtuhumu kusababisha kuvunjika kwa ndoa yake.
Ujumbe ulisomeka hivi: “Alichounganisha Mwenyezi Mungu binadamu hawezi kukitenganisha. Nakuheshimu sana kama kiongozi wangu, Mwenyekiti wangu, Naibu Waziri, M-NEC, M-CCM, mkubwa wangu kiumri, mbunge na kadhalika.
“Nimesikitishwa sana na jitihada za kutaka kuvuruga ndoa yangu, nakutakia kila la heri, lakini usisahau malipo ni hapa hapa duniani na kila mwenye kufanyia wenzake mabaya na yeye hulipwa kwa ubaya.
“Nampenda sana mume wangu na ntailinda ndoa yangu kwa gharama yoyote cko tayari kumpoteza, mi ni zaidi ya mwanamke. Asante sana, kila la heri na kazi njema katika kulifanikisha hilo, wizara
yako nyeti sana, ina mambo mengi sana. Bye.”
Kuna wakati ikasemwa kwamba kuachika kwake kulikuja baada ya Naibu Waziri mmoja kudaiwa kwenda kumchomea utambi kwa mumewe. Baada ya tukio hilo, Amina alitoa ahadi ya kumtaja mbaya wake jambo ambalo halikutimia.
Yapo madai kuwa Naibu Waziri huyo alikuwa na mipango ya kumpaka matope katika siasa kutokana na nia aliyoitangaza ya kutaka kugombea uenyekiti wa taifa wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM).
Amina pia alikuwa ameomba ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC), kupitia Kundi la Vijana katika Uchaguzi Mkuu wa CCM unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.
Juni 22, mwaka huu, Amina aliuliza bungeni kwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, akitaka kufahamishwa hatua gani zinazochukuliwa na Serikali katika kudhibiti uvujaji wa mitihani. Liliulizwa kwa niaba yake na Mbunge wa Muleba Kaskazini, Ruth Msafiri (CCM).
Amina aliyezaliwa Mei 20 mwaka 1981 alikuwa mcheshi na katika moja ya mikakati yake alipata kutamka kuwa ipo siku atajitumbukiza katika kinyang’anyiro katika jimbo.
Hakuishia katika kulitamani jimbo. Alipata kusema pia kuwa anaamini anao ubavu wa kuwa rais wa nchi katika miaka ijayo. Kauli hiyo aliitoa wakati alipohojiwa katika kipindi cha Jahazi cha Radio Clouds FM Mei mwaka huu.
Alisema wanasiasa wengi dunia huwa na ndoto ya kupanda ngazi hadi kufikia urais.
Aliongeza kuwa maisha ya kila mwanadamu huenda kwa malengo. Kwa hakika yaweza kusemwa kuwa maisha ya Amina yalikwenda kwa utaratibu wa kufikiria mambo chanya daima.
Pamoja na hayo, atakumbukwa kwa tukio lililomsibu bungeni mwaka jana wakati alipoagizwa na Spika kutoka nje ya ukumbi wa Bunge kutokana na kuvaa suti ya kike na kofia ya pama bila glovu kwa mujibu wa kanuni.
Monday, October 8, 2007
Mapatano pwani, baharini ni uvuvi
na innocent munyuku
JUMA la kula na kusaza limeanza. Wenye matumbo na nguvu ya kushika tonge wajiandae. Wajiweke kwa ajili ya kutafuna vinono wakati wa Sikukuu ya Idd el Fitr.
Mzee wa Busati naye anaomba uhai afike mwisho wa juma aungane na wengine katika ulaji la unywaji. Kwa masela siku kama hiyo hawana haja ya kuumiza vichwa manake kila nyumba huwa huru kukaribisha wageni.
Badala ya kula chips dume na maji ya kwenye mifuko ya plastiki siku hiyo ni kutafuna vipapatio vya kuku, pilau na vinywaji vyenye ubora. Mambo ya shangwe hayo.
Wiki hii Mzee wa Busati anaingia ulingoni akiwa na maswali kibao yenye mshangao pia kuhusu kauli ya kiungo wa zamani wa Yanga, Sekilojo Chambua.
Chambua kalalama kwenye vyombo vya habari kwamba uongozi wa Yanga haujatekeleza ahadi zake kwake baada ya kustaafu kuichezea timu hiyo kwa takribani miaka 10.
Nyota huyo alipoamua kupumzika kuichezea Yanga akaahidiwa mema kama vile kulipiwa pango la nyumba kwa mwaka mzima, kununuliwa kiwanja na kusomeshwa ukocha nje ya nchi.
Miaka minne sasa imepita tangu ahadi hizo zitolewe na kwa mujibu wa Chambua hakuna lililotekelezwa. Waliotia saini barua ya ahadi kwa mwanasoka huyo wameingia mitini na kukaa kimya.
Ni habari ya kusikitisha kuona kwamba mchezaji aliyeitumikia timu kwa moyo wake wote akilipwa mshahara na posho hafifu anapewa ahadi hewa kama hizo.
Mzee wa Busati hakika angeishangaa Yanga kama wangetimiza ahadi hizo. Angeshangaa kwa sababu kwa uzoefu wa klabu za Kibongo suala la masilahi kwa wachezaji limekuwa sugu.
Vinara wa klabu daima wamekuwa wenye kupenda sifa kuliko utekelezaji wa masuala muhimu kwa wanaojenga klabu.
Chambua bila shaka ana haki ya kudai kilichoahidiwa kwake na klabu. Waliohusika kumfanyia uhuni mwanasoka huyo waanikwe na ikibidi wachapwe bakora ili uwe mfano kwa wengine.
Husemwa kwamba mapatano kwa kawaida hufanyika pwani ukishaingia habarini ni uvuvi tu hakuna mjadala mwingine labda kama kutatoka dhoruba.
Kwa maana hiyo Yanga inapaswa kutekeleza kilichoandikwa kwenye barua ya ahadi kwa Chambua na si kumletea longolongo.
Kwani kulikuwa na ulazima gani wa kumpa moyo Chambua kama mlijua kuwa mlichoahidi hakitekelezeki? Au mwalitaka kumwiga tembo?
Chambua mbali na kupewa ahadi hewa anadai pia malimbukizo ya mishahara yake na hadi leo hakuna kiongozi wa Yanga anayesimama kutetea haki ya mwanasoka huyo. Wamelala na bila shaka hata majalada hayapo.
Mwandika Busati hasiti kusema kuwa kuna uhuni umefanyika. Dhuluma imedhihirika na watu wanapaswa kuwajibika katika hili.
Anachosema Mzee wa Busati ni kwamba anayolalamikia Chambua yawezekana yametokea kwa wachezaji wengi wa Yanga na klabu nyingine.
Haya ni mambo ambayo yameendelea kwa muda mrefu. Wahusika wamekaa kimya na hivyo kuhalalisha ubaya wa hali hiyo kwa kiwango cha kutisha. Matokeo yake wachezaji hugeuka kuwa ombaomba.
Nani atasimama na kuweka mambo sawia? Hata katika hili twamsubiri Masiha? Kwanini hekima isitumike kuondoa dhuluma hii?
Waungwana daima hutimiza ahadi zao hata kama walifanya makosa katika tamko la awali. Hutekeleza walichosema na kama waliteleza hujipanga upya.
Kwamba Chambua apewe alichoahidiwa na wala hakuna haja ya kwenda njia ndefu apewe chake atulie.
Mzee wa Busati anaelekea ukomo wa Jumanne hii akitoa salamu kwa wadau wake. Kwa waliojaliwa kufunga Ramadhan endeleeni kupata neema.
Kila jema liwakute katika maandalizi ya kumaliza mfungo lakini msije mkaleta balaa kwa kuzidisha kipimo cha furaha siku ikifika.
Wasalaam,
JUMA la kula na kusaza limeanza. Wenye matumbo na nguvu ya kushika tonge wajiandae. Wajiweke kwa ajili ya kutafuna vinono wakati wa Sikukuu ya Idd el Fitr.
Mzee wa Busati naye anaomba uhai afike mwisho wa juma aungane na wengine katika ulaji la unywaji. Kwa masela siku kama hiyo hawana haja ya kuumiza vichwa manake kila nyumba huwa huru kukaribisha wageni.
Badala ya kula chips dume na maji ya kwenye mifuko ya plastiki siku hiyo ni kutafuna vipapatio vya kuku, pilau na vinywaji vyenye ubora. Mambo ya shangwe hayo.
Wiki hii Mzee wa Busati anaingia ulingoni akiwa na maswali kibao yenye mshangao pia kuhusu kauli ya kiungo wa zamani wa Yanga, Sekilojo Chambua.
Chambua kalalama kwenye vyombo vya habari kwamba uongozi wa Yanga haujatekeleza ahadi zake kwake baada ya kustaafu kuichezea timu hiyo kwa takribani miaka 10.
Nyota huyo alipoamua kupumzika kuichezea Yanga akaahidiwa mema kama vile kulipiwa pango la nyumba kwa mwaka mzima, kununuliwa kiwanja na kusomeshwa ukocha nje ya nchi.
Miaka minne sasa imepita tangu ahadi hizo zitolewe na kwa mujibu wa Chambua hakuna lililotekelezwa. Waliotia saini barua ya ahadi kwa mwanasoka huyo wameingia mitini na kukaa kimya.
Ni habari ya kusikitisha kuona kwamba mchezaji aliyeitumikia timu kwa moyo wake wote akilipwa mshahara na posho hafifu anapewa ahadi hewa kama hizo.
Mzee wa Busati hakika angeishangaa Yanga kama wangetimiza ahadi hizo. Angeshangaa kwa sababu kwa uzoefu wa klabu za Kibongo suala la masilahi kwa wachezaji limekuwa sugu.
Vinara wa klabu daima wamekuwa wenye kupenda sifa kuliko utekelezaji wa masuala muhimu kwa wanaojenga klabu.
Chambua bila shaka ana haki ya kudai kilichoahidiwa kwake na klabu. Waliohusika kumfanyia uhuni mwanasoka huyo waanikwe na ikibidi wachapwe bakora ili uwe mfano kwa wengine.
Husemwa kwamba mapatano kwa kawaida hufanyika pwani ukishaingia habarini ni uvuvi tu hakuna mjadala mwingine labda kama kutatoka dhoruba.
Kwa maana hiyo Yanga inapaswa kutekeleza kilichoandikwa kwenye barua ya ahadi kwa Chambua na si kumletea longolongo.
Kwani kulikuwa na ulazima gani wa kumpa moyo Chambua kama mlijua kuwa mlichoahidi hakitekelezeki? Au mwalitaka kumwiga tembo?
Chambua mbali na kupewa ahadi hewa anadai pia malimbukizo ya mishahara yake na hadi leo hakuna kiongozi wa Yanga anayesimama kutetea haki ya mwanasoka huyo. Wamelala na bila shaka hata majalada hayapo.
Mwandika Busati hasiti kusema kuwa kuna uhuni umefanyika. Dhuluma imedhihirika na watu wanapaswa kuwajibika katika hili.
Anachosema Mzee wa Busati ni kwamba anayolalamikia Chambua yawezekana yametokea kwa wachezaji wengi wa Yanga na klabu nyingine.
Haya ni mambo ambayo yameendelea kwa muda mrefu. Wahusika wamekaa kimya na hivyo kuhalalisha ubaya wa hali hiyo kwa kiwango cha kutisha. Matokeo yake wachezaji hugeuka kuwa ombaomba.
Nani atasimama na kuweka mambo sawia? Hata katika hili twamsubiri Masiha? Kwanini hekima isitumike kuondoa dhuluma hii?
Waungwana daima hutimiza ahadi zao hata kama walifanya makosa katika tamko la awali. Hutekeleza walichosema na kama waliteleza hujipanga upya.
Kwamba Chambua apewe alichoahidiwa na wala hakuna haja ya kwenda njia ndefu apewe chake atulie.
Mzee wa Busati anaelekea ukomo wa Jumanne hii akitoa salamu kwa wadau wake. Kwa waliojaliwa kufunga Ramadhan endeleeni kupata neema.
Kila jema liwakute katika maandalizi ya kumaliza mfungo lakini msije mkaleta balaa kwa kuzidisha kipimo cha furaha siku ikifika.
Wasalaam,
Monday, October 1, 2007
Safari hii msikubali matege
na innocent munyuku
KUMEKUCHA na bila shaka mambo yanakwenda katika unyoofu wake. Kama kuna matatizo hayo hayakwepeki kwa vile ni mpango wa maisha ya kila siku.
Mzee wa Busati yu katika mlolongo wake wa kuwapa porojo zake za kila wiki. Hii yaweza kuitwa wiki ya vicheko kwani walio wengi nafuu ingalipo. Mapato ya mwezi Septemba yangali yakionekana kibindoni. Si haba!
Linalomweka Mwandika Busati leo hii ni huu ujio wa kocha mpya wa Yanga Wojciech Lazarek wa nchini Poland. Kocha huyo mpya anakuja kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Milutin Sredejovic `Micho`.
Kwa wapenzi wa mpira hasa mashabiki wa Yanga kuja kwa Mpoland huyo ni ishara ya pambazuko kwa masilahi ya timu hiyo.
Mzee wa Busati kama walivyo wadau wengine katika eneo hilo hana budi kutoa mawazo yake kuhusiana na ujio wa kocha huyo mpya. Hasemi kwa mabaya bali kuwekana sawa ili mambo yakiwa sivyo basi wenye Yanga wasilalame kwamba hawakuambiwa.
Kwa mtazamo mwepesi tu ni kwamba licha ya kuwa Mpoland huyo wasifu wake unatia moyo katika soka, bado anahitaji kupewa nafasi ya kujitanua katika kutimiza wajibu wake.
Kuna hila ndani ya klabu za soka nchini Tanzania. Kwamba hapa kwa Wadanganyika kila jambo hufanywa kwa mazoea tena mazoea mabaya.
Kazi kubwa ya hao wanaojiita mashabiki na wenye Yanga yao ni kutoa kasoro kwa walimu hata kama kocha huyo ana siku mbili kambini na wachezaji.
Jukumu lao ni kupiga soga barazani wakipanga kile wanachokiita ubora wa timu lakini ukweli wa mambo ni kwamba wengi wao ni watengenezaji wa fitina ndani ya soka.
Hawana lolote la maana ndani ya mitima yao. Badala yake wamejaa porojo zilizokosa miguu na fikra pevu. Hawa ndio wa kwanza kupiga kelele kwamba fulani hafai lakini ukiwauliza mbadala hawana.
Hupayuka kwamba timu fulani ni yao lakini ukiwaambia watoe hapo senti 10 kwa ajili ya wachezaji wanakimbia mithili ya duma nyikani. Hawataki majukumu huku wakisisitiza kuwa hiyo ni timu yao.
Basi kama mambo ni hayo, kocha mpya ajaye Yanga apewe nafasi ya kutimiza majukumu yake na kamwe asitengenezewe vigingi vya hapa na pale.
Ni wazi kwamba mpira wa Kibongo ni mgumu kutokana na ukweli kwamba hakuna mwekezaji makini aliyejitokeza na kuweka vitalu vya soka.
Timu zote zimebaki kuwakusanya wachezaji kwa kutumia vigezo dhaifu na ndio maana si jambo la ajabu kusikia Mwambungu kasajiliwa Simba leo na kesho ukaambiwa kiwango chake kimeshuka.
Wanaosema fulani kashuka kiwango ni mashabiki na hapo kama mwalimu si makini basi kesho yake ataanza kumweka mchezaji benchi badala ya kumsaidia mwanasoka huyo arejee kileleni.
Hoja hapa ni kwamba midomo ya mashabiki kwa kawaida imekuwa ikiwaponza hata viongozi wa klabu husika na kufanya maamuzi yasiyofaa.
Kwa maneno mengine ni kwamba imefika pahala viongozi wa soka nchini wakafanana uamuzi na mashabiki wao. Hapo hakuna jipya zaidi ya kupanga timu wapendavyo.
Hujapata kusikia kuwa mchezaji fulani ni kipenzi cha kiongozi fulani? Kwa hiyo kama mchezaji huyo hakupangwa basi hapo kocha huingia matatani. Atasemwa kwa ubaya na hata atengwe na kaya.
Huu si muda wa kuendeleza fitina ndani ya soka kwa maana hiyo ujio wa kocha mpya kwa Wanajangwani kujengwe kwa uzio wa subira na nidhamu kwa mwalimu huyo.
Mzee wa Busati anayasema hayo kwa vile anaelewa baadhi ya mambo ya kihuni ndani ya klabu za soka nchini. Huko kila mmoja ana uamuzi wake atakavyo hata kama ni kupoteza dira ya maendeleo.
Wanachoangalia ni masilahi ya leo na si kujenga soka kwa ajili ya maisha mema ya wachezaji na ustawi wa nchi. Wao wanaharibu na ukiwauliza watakwambia atakayekuja atajenga ukuta baada ya wao kupuuzia nyufa.
Kama mpira wa kusutana na kuwashambulia makocha utaendelea katika uso wa Wadanganyika basi mjue kuwa hiyo ni laana katika mpira wa miguu nchini na hata kama atakuja Dunga kuwafundisha bado mtakwama.
Mtazidi kukwamba kutokana na ukweli kwamba masikio yenu yamejaa nta na hamtaki kukubali kwamba kuna umuhimu wa mabadiliko.
Kinachosemwa na Mwandika Busati ni kwamba suala la makocha kuzikimbia timu baada ya muda mfupi si la kupuuzia. Kuna haja ya kuangalia wapi kuna tatizo.
Hawa wanaokimbia si wendawazimu hata kidogo, wana akili timamu na wanapoona makubaliano hafifu hulazimika kukitoa ili kulinda heshima zao.
Basi kwa wenye upeo wa utambuzi wa mema wadake haya yasemwayo na Mzee wa Busati kwamba safari hii Yanga msikubali matege katika kushirikiana na kocha mpya ajaye.
Wenye dhamana ya kuitawala Yanga, enendeni mkahubiri uvumilivu na moyo wa ushirikiano kwa mashabiki wenu. Vinginevyo itabaki hadithi ile ile ya kale kwamba Jangwani na Msimbazi hakukaliki.
Wasalaam,
KUMEKUCHA na bila shaka mambo yanakwenda katika unyoofu wake. Kama kuna matatizo hayo hayakwepeki kwa vile ni mpango wa maisha ya kila siku.
Mzee wa Busati yu katika mlolongo wake wa kuwapa porojo zake za kila wiki. Hii yaweza kuitwa wiki ya vicheko kwani walio wengi nafuu ingalipo. Mapato ya mwezi Septemba yangali yakionekana kibindoni. Si haba!
Linalomweka Mwandika Busati leo hii ni huu ujio wa kocha mpya wa Yanga Wojciech Lazarek wa nchini Poland. Kocha huyo mpya anakuja kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Milutin Sredejovic `Micho`.
Kwa wapenzi wa mpira hasa mashabiki wa Yanga kuja kwa Mpoland huyo ni ishara ya pambazuko kwa masilahi ya timu hiyo.
Mzee wa Busati kama walivyo wadau wengine katika eneo hilo hana budi kutoa mawazo yake kuhusiana na ujio wa kocha huyo mpya. Hasemi kwa mabaya bali kuwekana sawa ili mambo yakiwa sivyo basi wenye Yanga wasilalame kwamba hawakuambiwa.
Kwa mtazamo mwepesi tu ni kwamba licha ya kuwa Mpoland huyo wasifu wake unatia moyo katika soka, bado anahitaji kupewa nafasi ya kujitanua katika kutimiza wajibu wake.
Kuna hila ndani ya klabu za soka nchini Tanzania. Kwamba hapa kwa Wadanganyika kila jambo hufanywa kwa mazoea tena mazoea mabaya.
Kazi kubwa ya hao wanaojiita mashabiki na wenye Yanga yao ni kutoa kasoro kwa walimu hata kama kocha huyo ana siku mbili kambini na wachezaji.
Jukumu lao ni kupiga soga barazani wakipanga kile wanachokiita ubora wa timu lakini ukweli wa mambo ni kwamba wengi wao ni watengenezaji wa fitina ndani ya soka.
Hawana lolote la maana ndani ya mitima yao. Badala yake wamejaa porojo zilizokosa miguu na fikra pevu. Hawa ndio wa kwanza kupiga kelele kwamba fulani hafai lakini ukiwauliza mbadala hawana.
Hupayuka kwamba timu fulani ni yao lakini ukiwaambia watoe hapo senti 10 kwa ajili ya wachezaji wanakimbia mithili ya duma nyikani. Hawataki majukumu huku wakisisitiza kuwa hiyo ni timu yao.
Basi kama mambo ni hayo, kocha mpya ajaye Yanga apewe nafasi ya kutimiza majukumu yake na kamwe asitengenezewe vigingi vya hapa na pale.
Ni wazi kwamba mpira wa Kibongo ni mgumu kutokana na ukweli kwamba hakuna mwekezaji makini aliyejitokeza na kuweka vitalu vya soka.
Timu zote zimebaki kuwakusanya wachezaji kwa kutumia vigezo dhaifu na ndio maana si jambo la ajabu kusikia Mwambungu kasajiliwa Simba leo na kesho ukaambiwa kiwango chake kimeshuka.
Wanaosema fulani kashuka kiwango ni mashabiki na hapo kama mwalimu si makini basi kesho yake ataanza kumweka mchezaji benchi badala ya kumsaidia mwanasoka huyo arejee kileleni.
Hoja hapa ni kwamba midomo ya mashabiki kwa kawaida imekuwa ikiwaponza hata viongozi wa klabu husika na kufanya maamuzi yasiyofaa.
Kwa maneno mengine ni kwamba imefika pahala viongozi wa soka nchini wakafanana uamuzi na mashabiki wao. Hapo hakuna jipya zaidi ya kupanga timu wapendavyo.
Hujapata kusikia kuwa mchezaji fulani ni kipenzi cha kiongozi fulani? Kwa hiyo kama mchezaji huyo hakupangwa basi hapo kocha huingia matatani. Atasemwa kwa ubaya na hata atengwe na kaya.
Huu si muda wa kuendeleza fitina ndani ya soka kwa maana hiyo ujio wa kocha mpya kwa Wanajangwani kujengwe kwa uzio wa subira na nidhamu kwa mwalimu huyo.
Mzee wa Busati anayasema hayo kwa vile anaelewa baadhi ya mambo ya kihuni ndani ya klabu za soka nchini. Huko kila mmoja ana uamuzi wake atakavyo hata kama ni kupoteza dira ya maendeleo.
Wanachoangalia ni masilahi ya leo na si kujenga soka kwa ajili ya maisha mema ya wachezaji na ustawi wa nchi. Wao wanaharibu na ukiwauliza watakwambia atakayekuja atajenga ukuta baada ya wao kupuuzia nyufa.
Kama mpira wa kusutana na kuwashambulia makocha utaendelea katika uso wa Wadanganyika basi mjue kuwa hiyo ni laana katika mpira wa miguu nchini na hata kama atakuja Dunga kuwafundisha bado mtakwama.
Mtazidi kukwamba kutokana na ukweli kwamba masikio yenu yamejaa nta na hamtaki kukubali kwamba kuna umuhimu wa mabadiliko.
Kinachosemwa na Mwandika Busati ni kwamba suala la makocha kuzikimbia timu baada ya muda mfupi si la kupuuzia. Kuna haja ya kuangalia wapi kuna tatizo.
Hawa wanaokimbia si wendawazimu hata kidogo, wana akili timamu na wanapoona makubaliano hafifu hulazimika kukitoa ili kulinda heshima zao.
Basi kwa wenye upeo wa utambuzi wa mema wadake haya yasemwayo na Mzee wa Busati kwamba safari hii Yanga msikubali matege katika kushirikiana na kocha mpya ajaye.
Wenye dhamana ya kuitawala Yanga, enendeni mkahubiri uvumilivu na moyo wa ushirikiano kwa mashabiki wenu. Vinginevyo itabaki hadithi ile ile ya kale kwamba Jangwani na Msimbazi hakukaliki.
Wasalaam,
Tuesday, September 25, 2007
Vunju sasa limewekwa hadharani
na innocent munyuku
VUNJU husemwa na Waswahili kuwa ni vumbi linatokea kwenye maji baada ya kutibuliwa. Kwamba waweza ona maji yako safi lakini ukishayatibua vumbi hujitokeza na taka nyinginezo.
Ndicho kilichotokea wakati wa mechi za awali za Ligi Kuu Tanzania Bara kwa wakongwe wa soka nchini Simba na Yanga baada ya kukubali kufungwa.
Walitinga dimbani wakijiona wasafi wa soka na wenye ubavu lakini kumbe ndani yake kungali vumbi kibao. Yanga ndiyo iliyoanza kupokea kipigo.
Lakini kwa mshangao Simba wakasahau kwamba mwenzako akinyolewa nawe tia maji.
Jumamosi iliyopita, mashabiki wa Yanga hakika walikuwa kwenye wakati mgumu baada ya timu yao kutekenywa kwa bao 1-0 na Ashanti United kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Vijiwe vikagauka kuwa vichungu kwani mahasimu wao walikuwa wakitamba kwa kejeli kwamba Jangwani kwisha habari yao. Wekundu wa Msimbazi, Simba ya Darisalama ikawa mstari wa mbele kukenua wakifurahia kichapo walichopata Yanga.
Hao waliotamba jana yake nao kesho yake wakapata kipigo kama cha masahiba kutoka kwa wagosi wa kaya, Coastal Union. Nani wa kumcheka mwenzake?
Hapa kwa Mzee wa Busati mambo ni murua kwa sababu kila jambo laenda sawia. Pengine Mwandika Busati aseme tu kwamba mwanzo wa ligi umewafumbua macho wengi.
Kwamba kitendo cha Yanga na Simba kuyeyuka kama konokono kwenye chumvi kimeleta neema na upeo kwamba majina makubwa kwenye soka si lolote bali ufanisi.
Hiyo imekuwa faraja kwa wengi na bila shaka mwanzo mzuri wa timu nyingine zinazoshiriki ligi hiyo. Kwamba sasa huenda wamejua kuwa soka si kwa Simba na Yanga tu hata wao wanaweza kuwa vinara dimbani.
Tuseme nini Jumanne hii ambayo wengi wanaishi kwa matumaini ya kujazwa sarafu mifukoni ili wazidi kujinafasi kwa sababu mifuko yao itawaruhusu kufanya hivyo.
Leo watakuwa baa ile na kesho watahamia kwingine na wapambe wao pembeni. Wanakula raha na kuponda mali kwa vile kufa kwaja! Mambo hayo wakwetu.
Hoja kuu ya Mzee wa Busati wiki hii ya neema ni kwamba kusiwe na hoja ya kujenga ukuta kwamba fulani anaweza na mwingine hajui. Kwa vile wote mpo katika kapu moja la ligi kila timu iwe na jukumu la kutoa burudani kwa mashabiki wake.
Soka si la Simba na Yanga tu. Kwa maana hiyo hata wageni wa ligi msimu huu nao wafanye mambo ya maana ili kubadilisha soka nchini.
Kwani hamkuwahi kuambiwa kwamba Simba na Yanga ni kaburi la wachezaji? Hamkuwahi kusikia kuwa wakongwe hao wa soka nchini hawana jipya zaidi ya sifa za historia?
Angalia ulimbukeni wao kwenye usajili kila msimu. Ni mgogoro kwa kwenda mbele. Wakati mwingine wanaingizwa mjini kama Simba wakati uleee walipoingizwa mjini na Ssentongo.
Limekuwa tatizo sugu hapa kwa wabongo kila msimu na kutokana na hali hiyo ndiyo maana baadhi ya timu kama Simba na Yanga zimejikuta zikiwa kama makaburi ya wachezaji.
Hii ni kwa vile usajili wao kwa kawaida hutawaliwa na mizengwe ya makomandoo na wanachama wanaojiita wakongwe.
Imekuwa ni fitna mtindo mmoja na kutokana na hilo si ajabu kwa Simba na Yanga kusajili wachezaji na kabla msimu haujakoma ukasikia maneno mengine kwamba mchezaji huyo kachuja.
Baada ya kipigo cha Morogoro na Tanga maneno yameshaanza na kwa hakika kinachosemwa ni kwamba usajili wao mwaka huu ni mbovu. Hawachelewi kulalama hawa. Wakiguswa kidogo tu lazima waruke.
Nani anabisha hili? Mifano yaweza kujaa vikapu hadi kutapika. Ni mambo yasiyofichika kwa sababu wenye macho wanaona na wenye masikio wanasikia vishindo vya uvundo huo.
Lakini nani basi atakuja na dawa ya masuala haya? Ni nani ataibuka na kutokomeza hali hii ya wachezaji kutumika kama makopo ya chooni? Je, ni malaika wa Kimakonde au wale kutoka juu mbinguni?
Usajili wa Simba na Yanga unategemea zaidi makapi ya wachezaji kutoka nchi jirani. Eti wenyewe wanawaita kuwa ni wachezaji wa kulipwa!
Kama kungelikuwa na vya soka ni nani leo hii angewababakia wachezaji makapi kutoka nchi jirani? Wachezaji ambao huko kwao si lolote. Kama wangelikuwa lulu wasingelithubutu kuja kwa Wabongo.
Kama kweli hao ni wa kulipwa mbona hawaendi Ulaya na nchi nyingine zilizo juu katika soka? Hao nao wanaganga njaa tu.
Lakini yote heri kwani sasa maji yameshatibuka na vunju laonekana. Kwamba utulivu uliokuwa umezoeleka ni batili kwani ndani ya maji yanayoitwa Simba na Yanga kuna vumbi kibao na hilo ndilo vunju linalosemwa na Mzee wa Busati.
Wasalaam,
VUNJU husemwa na Waswahili kuwa ni vumbi linatokea kwenye maji baada ya kutibuliwa. Kwamba waweza ona maji yako safi lakini ukishayatibua vumbi hujitokeza na taka nyinginezo.
Ndicho kilichotokea wakati wa mechi za awali za Ligi Kuu Tanzania Bara kwa wakongwe wa soka nchini Simba na Yanga baada ya kukubali kufungwa.
Walitinga dimbani wakijiona wasafi wa soka na wenye ubavu lakini kumbe ndani yake kungali vumbi kibao. Yanga ndiyo iliyoanza kupokea kipigo.
Lakini kwa mshangao Simba wakasahau kwamba mwenzako akinyolewa nawe tia maji.
Jumamosi iliyopita, mashabiki wa Yanga hakika walikuwa kwenye wakati mgumu baada ya timu yao kutekenywa kwa bao 1-0 na Ashanti United kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Vijiwe vikagauka kuwa vichungu kwani mahasimu wao walikuwa wakitamba kwa kejeli kwamba Jangwani kwisha habari yao. Wekundu wa Msimbazi, Simba ya Darisalama ikawa mstari wa mbele kukenua wakifurahia kichapo walichopata Yanga.
Hao waliotamba jana yake nao kesho yake wakapata kipigo kama cha masahiba kutoka kwa wagosi wa kaya, Coastal Union. Nani wa kumcheka mwenzake?
Hapa kwa Mzee wa Busati mambo ni murua kwa sababu kila jambo laenda sawia. Pengine Mwandika Busati aseme tu kwamba mwanzo wa ligi umewafumbua macho wengi.
Kwamba kitendo cha Yanga na Simba kuyeyuka kama konokono kwenye chumvi kimeleta neema na upeo kwamba majina makubwa kwenye soka si lolote bali ufanisi.
Hiyo imekuwa faraja kwa wengi na bila shaka mwanzo mzuri wa timu nyingine zinazoshiriki ligi hiyo. Kwamba sasa huenda wamejua kuwa soka si kwa Simba na Yanga tu hata wao wanaweza kuwa vinara dimbani.
Tuseme nini Jumanne hii ambayo wengi wanaishi kwa matumaini ya kujazwa sarafu mifukoni ili wazidi kujinafasi kwa sababu mifuko yao itawaruhusu kufanya hivyo.
Leo watakuwa baa ile na kesho watahamia kwingine na wapambe wao pembeni. Wanakula raha na kuponda mali kwa vile kufa kwaja! Mambo hayo wakwetu.
Hoja kuu ya Mzee wa Busati wiki hii ya neema ni kwamba kusiwe na hoja ya kujenga ukuta kwamba fulani anaweza na mwingine hajui. Kwa vile wote mpo katika kapu moja la ligi kila timu iwe na jukumu la kutoa burudani kwa mashabiki wake.
Soka si la Simba na Yanga tu. Kwa maana hiyo hata wageni wa ligi msimu huu nao wafanye mambo ya maana ili kubadilisha soka nchini.
Kwani hamkuwahi kuambiwa kwamba Simba na Yanga ni kaburi la wachezaji? Hamkuwahi kusikia kuwa wakongwe hao wa soka nchini hawana jipya zaidi ya sifa za historia?
Angalia ulimbukeni wao kwenye usajili kila msimu. Ni mgogoro kwa kwenda mbele. Wakati mwingine wanaingizwa mjini kama Simba wakati uleee walipoingizwa mjini na Ssentongo.
Limekuwa tatizo sugu hapa kwa wabongo kila msimu na kutokana na hali hiyo ndiyo maana baadhi ya timu kama Simba na Yanga zimejikuta zikiwa kama makaburi ya wachezaji.
Hii ni kwa vile usajili wao kwa kawaida hutawaliwa na mizengwe ya makomandoo na wanachama wanaojiita wakongwe.
Imekuwa ni fitna mtindo mmoja na kutokana na hilo si ajabu kwa Simba na Yanga kusajili wachezaji na kabla msimu haujakoma ukasikia maneno mengine kwamba mchezaji huyo kachuja.
Baada ya kipigo cha Morogoro na Tanga maneno yameshaanza na kwa hakika kinachosemwa ni kwamba usajili wao mwaka huu ni mbovu. Hawachelewi kulalama hawa. Wakiguswa kidogo tu lazima waruke.
Nani anabisha hili? Mifano yaweza kujaa vikapu hadi kutapika. Ni mambo yasiyofichika kwa sababu wenye macho wanaona na wenye masikio wanasikia vishindo vya uvundo huo.
Lakini nani basi atakuja na dawa ya masuala haya? Ni nani ataibuka na kutokomeza hali hii ya wachezaji kutumika kama makopo ya chooni? Je, ni malaika wa Kimakonde au wale kutoka juu mbinguni?
Usajili wa Simba na Yanga unategemea zaidi makapi ya wachezaji kutoka nchi jirani. Eti wenyewe wanawaita kuwa ni wachezaji wa kulipwa!
Kama kungelikuwa na vya soka ni nani leo hii angewababakia wachezaji makapi kutoka nchi jirani? Wachezaji ambao huko kwao si lolote. Kama wangelikuwa lulu wasingelithubutu kuja kwa Wabongo.
Kama kweli hao ni wa kulipwa mbona hawaendi Ulaya na nchi nyingine zilizo juu katika soka? Hao nao wanaganga njaa tu.
Lakini yote heri kwani sasa maji yameshatibuka na vunju laonekana. Kwamba utulivu uliokuwa umezoeleka ni batili kwani ndani ya maji yanayoitwa Simba na Yanga kuna vumbi kibao na hilo ndilo vunju linalosemwa na Mzee wa Busati.
Wasalaam,
Subscribe to:
Posts (Atom)