Friday, January 19, 2007

Haya ndiyo maajabu ya Dk. Mwiko

Na Mwandishi Wetu
ALIANZIA kuvuma jijini Dar es Salaam lakini sasa jina lake limepaa na kuvuka mipaka ya Tanzania. Huyu si mwingine bali Dk. Mwiko Kuona mganga maarufu wa tiba za asili nchini.

Aliposimama na kuwafichua wachawi siku ya kwanza katika viunga vya Keko jijini Dar es Salaam ilionekana wazi kuwa alikuwa na mwelekeo mzuri katika tiba na hivyo kuokoa maisha ya watu.

Hakuishia kuwakomesha magagula bali alizidisha huduma za tiba kwa wateja wake na hilo ndilo jambo analoendelea nalo kila leo.

Wiki hii amezungumza na gazeti hili na kubainisha kuwa mwaka huu wa 2007 atakuwa na jukumu zito zaidi kwani amepanga kupanua wigo wa huduma zake katika sehemu mbalimbali za Tanzania.

"Nimekaa Dar es Salaam kwa muda mrefu lakini kwa jinsi watu wanavyozidi kunihitaji siwezi kubakia hapa nilipo yanipasa niwafuate huko waliko manake wengine hawamudu gharama za kuja nilipo," anasema Dk. Mwiko.

Inawezekana ulishakumbwa na matatizo kama vile kukosa uzazi, kutokuwa na hamu ya kula, magonjwa yatokanayo na ukimwi, malaria sugu au kudhulumiwa haki yako. Hayo yote yana suluhu kwa Dk.Mwiko.

Si hayo tu hata kama kuna mpenzi wako anayekuchezea akili kwa kutembea nje ya mapenzi yenu, Dk. Mwiko anao uwezo wa kurejesha uhusiano uliovunjika na hilo linafanyika kwa muda wa siku chache.

Pengine ulishateswa usingizini na wakati mwingine kuandamwa na wezi katika mashamba au nyumbani, Dk. Mwiko ana ubavu wa kukuwekea zindiko na kukuepusha na matatizo hayo.

Katika siku za mwanzo kabisa, Dk. Mwiko hakupenda kujihusisha na masuala ya uganga wa tiba za asili. Alitamani kufanya kazi nyingine. Lakini kadri siku zilivyokuwa zinasonga mbele, mambo yalibadilika kwani mizimu ya mababu ilimvuta arithi tiba kama ilivyokuwa kwa babu yake.

"Si unajua mambo ya ujana bwana, mimi sikutaka kujihusisha na uganga ingawa babu ndio ilikuwa shughuli zake.

"Lakini kila nilipojaribu kukwepa jukumu hilo, kichwa kilikuwa kinaendelea kupata maumivu makubwa kiasi cha kushindwa kufanya kazi. Ndipo nikaanza kujiuliza tatizo nini?

"Kwa hiyo baada ya kurejea Chalinze nikaambiwa kuna kitu natakiwa kukifanya na sijafanya na kwamba salama yangu nikubali kubeba mikoba ya uganga kutoka kwa babu," anakumbuka Dk. Mwiko Kuona.

Anasema baada ya kufanyiwa zindiko porini, ile hali ya kuumwa kichwa ikapotea na ndiyo maana aliamua kuacha kazi ya kuajiriwa na kuamua kuwapa watu tiba za asili kwa wanaohitaji.

Alishaalikwa kuondoa majini sehemu moja huko Ugweno na katika ziara yake hiyo anasema alipata mafanikio makubwa kwani wanakijiji walifurahi kwa vile aliwanusuru na mateso waliyokuwa wakikumbana nayo.

"Hapa unaponiona hakuna lisilowezekana katika tiba za asili, nafanya kila jitihada kuhakikisha kuwa wateja wangu wanaridhika na tiba zangu na hilo nalifanya kwa umakini mkubwa kwa sababu sitaki kuharibu jina," anaeleza.

Katika shughuli za kuondoa 'vitu' kwenye majumba ya watu na kuwasitisha wachawi huambatana na wasaidizi wake wanne pamoja na walinzi zaidi ya 10.

"Walinzi hawa kazi yao ni kudhibiti msongamano wa watu manake katika hizi kazi hasa ya kuwashika wachawi watu wanakuwa na usongo wa kuona nini kinaendelea...sasa kama huna ulinzi watakuharibia shughuli kwani msongamano huo utaingilia utaratibu mzima," anasema.

Kama unasumbuliwa na magonjwa mbalimbali au mfarakano wa kimapenzi, biashara haiendi vizuri usisite kuwasiliana na Dk. Mwiko Kuona kwa simu namba
0754 602629 au 0787 602629.

No comments: