Friday, January 19, 2007

Haya ndiyo maajabu ya Dk. Mwiko

Na Mwandishi Wetu
ALIANZIA kuvuma jijini Dar es Salaam lakini sasa jina lake limepaa na kuvuka mipaka ya Tanzania. Huyu si mwingine bali Dk. Mwiko Kuona mganga maarufu wa tiba za asili nchini.

Aliposimama na kuwafichua wachawi siku ya kwanza katika viunga vya Keko jijini Dar es Salaam ilionekana wazi kuwa alikuwa na mwelekeo mzuri katika tiba na hivyo kuokoa maisha ya watu.

Hakuishia kuwakomesha magagula bali alizidisha huduma za tiba kwa wateja wake na hilo ndilo jambo analoendelea nalo kila leo.

Wiki hii amezungumza na gazeti hili na kubainisha kuwa mwaka huu wa 2007 atakuwa na jukumu zito zaidi kwani amepanga kupanua wigo wa huduma zake katika sehemu mbalimbali za Tanzania.

"Nimekaa Dar es Salaam kwa muda mrefu lakini kwa jinsi watu wanavyozidi kunihitaji siwezi kubakia hapa nilipo yanipasa niwafuate huko waliko manake wengine hawamudu gharama za kuja nilipo," anasema Dk. Mwiko.

Inawezekana ulishakumbwa na matatizo kama vile kukosa uzazi, kutokuwa na hamu ya kula, magonjwa yatokanayo na ukimwi, malaria sugu au kudhulumiwa haki yako. Hayo yote yana suluhu kwa Dk.Mwiko.

Si hayo tu hata kama kuna mpenzi wako anayekuchezea akili kwa kutembea nje ya mapenzi yenu, Dk. Mwiko anao uwezo wa kurejesha uhusiano uliovunjika na hilo linafanyika kwa muda wa siku chache.

Pengine ulishateswa usingizini na wakati mwingine kuandamwa na wezi katika mashamba au nyumbani, Dk. Mwiko ana ubavu wa kukuwekea zindiko na kukuepusha na matatizo hayo.

Katika siku za mwanzo kabisa, Dk. Mwiko hakupenda kujihusisha na masuala ya uganga wa tiba za asili. Alitamani kufanya kazi nyingine. Lakini kadri siku zilivyokuwa zinasonga mbele, mambo yalibadilika kwani mizimu ya mababu ilimvuta arithi tiba kama ilivyokuwa kwa babu yake.

"Si unajua mambo ya ujana bwana, mimi sikutaka kujihusisha na uganga ingawa babu ndio ilikuwa shughuli zake.

"Lakini kila nilipojaribu kukwepa jukumu hilo, kichwa kilikuwa kinaendelea kupata maumivu makubwa kiasi cha kushindwa kufanya kazi. Ndipo nikaanza kujiuliza tatizo nini?

"Kwa hiyo baada ya kurejea Chalinze nikaambiwa kuna kitu natakiwa kukifanya na sijafanya na kwamba salama yangu nikubali kubeba mikoba ya uganga kutoka kwa babu," anakumbuka Dk. Mwiko Kuona.

Anasema baada ya kufanyiwa zindiko porini, ile hali ya kuumwa kichwa ikapotea na ndiyo maana aliamua kuacha kazi ya kuajiriwa na kuamua kuwapa watu tiba za asili kwa wanaohitaji.

Alishaalikwa kuondoa majini sehemu moja huko Ugweno na katika ziara yake hiyo anasema alipata mafanikio makubwa kwani wanakijiji walifurahi kwa vile aliwanusuru na mateso waliyokuwa wakikumbana nayo.

"Hapa unaponiona hakuna lisilowezekana katika tiba za asili, nafanya kila jitihada kuhakikisha kuwa wateja wangu wanaridhika na tiba zangu na hilo nalifanya kwa umakini mkubwa kwa sababu sitaki kuharibu jina," anaeleza.

Katika shughuli za kuondoa 'vitu' kwenye majumba ya watu na kuwasitisha wachawi huambatana na wasaidizi wake wanne pamoja na walinzi zaidi ya 10.

"Walinzi hawa kazi yao ni kudhibiti msongamano wa watu manake katika hizi kazi hasa ya kuwashika wachawi watu wanakuwa na usongo wa kuona nini kinaendelea...sasa kama huna ulinzi watakuharibia shughuli kwani msongamano huo utaingilia utaratibu mzima," anasema.

Kama unasumbuliwa na magonjwa mbalimbali au mfarakano wa kimapenzi, biashara haiendi vizuri usisite kuwasiliana na Dk. Mwiko Kuona kwa simu namba
0754 602629 au 0787 602629.

Kifimbo: Tusibeze tiba za asili

na innocent munyuku

HISTORIA inaonyesha kuwa binadamu kabla ya kuibuka kwa teknolojia za kisasa alitumia vitu vingi vya asili. Kuanzia chakula na dawa kwa magonjwa mbalimbali.

Kuibuka kwa mbinu mpya katika nyanja za kila aina kukasababisha utengenezwaji wa dawa viwandani na hivyo kurahishisha ufungaji na usambazaji pia.

Pamoja na uvumbuzi wa viwanda vya dawa, ukweli wa mambo ni kwamba tiba za asili zingali na umuhimu mkubwa kwa binadamu na mataifa mengi yanaendelea kuzitumia dawa hizo.

Tanzania ni moja ya nchi ambazo zimeendelea kutumia tiba za asili kwa magonjwa mbalimbali ikiwemo zile za kupunguza makali ya ugonjwa wa ukimwi, homa na ngiri.

Hata hivyo, kumekuwa na wimbi la watoa tiba za asili ambao wengi wao si waaminifu. Hili ni kundi ambalo limejiwekea mizizi ya kuwatapeli watu badala ya kutoa tiba halisi kwa wagonjwa.

Katika mahojiano na gazeti hili mapema wiki hii, mganga maarufu wa tiba za asili nchini Dk. Haruna Kifimbo anasema ujio wa kundi la ‘makanjanja’ katika tiba za asili ni kero kubwa kwa jamii.

“Mimi ninachoomba ni mamlaka za Serikali hapa nchini kuwadhibiti hawa wahalifu wa tiba za asili. Wanaharibu maana ya huduma hii.

“Si kila mtu anaweza kuwa mganga wa tiba za asili hilo lazima tukubaliane na kwa vile hawa wanaoharibu sekta hii tunaishi nao mitaani ni suala la kuwakamata na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria ili kuokoa maisha ya Watanzania,” anasema Dk. Kifimbo.

Dk. Kifimbo anaeleza kuwa kama waharibifu wa aina hiyo hawatadhibitiwa, Tanzania itajikuta iko kwenye janga litakalolidhoofisha taifa.

Akizungumzia uwezo wa tiba hizo katika jamii, Kifimbo anasema dawa hizo zimekuwa zikiokoa maisha watu kila siku. Anayataja maradhi ambayo wamekuwa wakikabiliana nayo kuwa ni pamoja na upungufu wa nguvu za nguvu za kiume.

“Ukweli ni kwamba katika miaka ya hivi karibuni, wanaume wengi wamekuwa wakipungukiwa nguvu za kiume na tiba zipo. Matatizo kama haya mara nyingi hutokana na vyakula tunavyokula hasa vilivyopoteza uasili wake, mtu mwenye kisukari, ngiri, presha au ugonjwa wa figo anaweza kukumbwa na tatizo hili,” anasema.

Dk. Kifimbo anasema wakati umefika kwa jamii kutambua umuhimu wa matumizi ya dawa za asili kwani uzoefu unaonyesha kuwa ni nzuri kwa matumizi ya binadamu na hukomesha kabisa magonjwa sugu.

Anatolea mfano magonjwa kama kuwashwa sehemu za siri, chunusi sugu na mabaka, maumivu ya mara kwa mara ya mgongo au kiuno, kukojoa kitandani, kukosa usingizi homa ya matumbo au magonjwa nyemelezi.

“Angalia Wachina wanavyoendelea kutumia dawa za asili, wanajua ubora wake ndio maana wamezing’ang’ania. Sasa sisi tunazibeza nadhani hii ni hatari kwetu kama hatutakuwa makini.

“Amerika ya Kusini nao wako mstari wa mbele katika kudumisha matumizi ya dawa hizi. Kwa hiyo ni jukumu letu kama wataalamu wa tiba kuhakikisha kuwa tunakuwa wabunifu kila siku na kuwadhibiti wanaoharibu sekta hii, hiki ni kilio changu.”

Mbali na kutoa huduma ya tiba, Dk. Kifimbo amekuwa akijitolea kuisaidia jamii katika mambo mbalimbali. “Naamini katika jamii bora na ndio maana ninachokipata nagawana na wengine,” anasema Kifimbo.

Zurry Chuchu umetuokoa wengi

na innocent munyuku
KATIKA maisha ya binadamu wapo majasiri na kundi jingine la watu wenye hofu huku wengine wakibaki kuwa ÔvuguvuguÕ hawajulikani wako upande upi.
Ujasiri ninaomaanisha hapa ni ule wa kusema jambo bila kigugumizi kama alivyofanya mwimbaji Easter Bugado maarufu kama Zurry Chuchu.
Wiki iliyopita nilisoma gazetini habari ya mwanadada huyo kwamba amejitangaza kuwa mwenye virusi vya ugonjwa wa ukimwi.
Kauli yake hiyo ilinivuta na sikuona kama nitakuwa natenda haki kwa kuiacha habari hiyo itokee sikio la pili bila ya kumpa salamu za pongezi msanii huyo.
Naam anastahili pongezi kwa kuwa amekuwa wazi kusema ana virusi vya ukimwi tofauti na wasanii wengine na hata watu wengine katika nyanja mbalimbali.
Uwazi wa Zurry ni wa kuigwa kwani kwa kujiweka wazi kiasi hicho, atakuwa anaokoa maisha ya watu wengi katika jamii inayomzunguka.
Kauli ya msanii huyo inanifanya nimkumbuke Mkurugenzi wa TOT Plus, Kapteni John Komba ambaye Mei 28 mwaka 2002 alisema kuwa baadhi ya wasanii wake wamefariki kwa ugonjwa wa ukimwi.
Kapteni Komba alitoa kauli hiyo mjini Bagamoyo katika risala yake baada ya kundi hilo kuhitimu mafunzo ya sanaa katika Chuo cha Sanaa cha Bagamoyo.
ÒKatika kipindi cha miaka 10 ya uhai wa TOT zaidi ya wasanii 15 wamefariki kwa ukimwi,Ó alisema Kapteni Komba wakati huo.
Nilimwona kuwa shujaa anayestahili kuigwa kwa kuthubutu kwake kuvunja ukimya.
Komba aliitoa kauli hiyo mbele ya mgeni rasmi William Lukuvi wakati huo akiwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu.
Lukuvi ambaye alikuwa akimwakilisha aliyekuwa Waziri Mkuu Frederick Sumaye aliposimama na kutoa hotuba yake alisisitiza kuwa lazima wasanii wawe mstari wa mbele kuupiga vita ukimwi.
Ninapoyatafakari hayo narejea kumwona Zurry kuwa msanii anayepaswa kuigwa kwani kufanya hivyo kutasaidia kupunguza maambukizi.
Tuwe wazi kusema kama tumeathirika ili kuwasaidia wengine ambao hawajaathirika. Tusione aibu kujitangaza na huu uwe utaratibu wa kudumu.
Kukaa kimya na kuufanya ukimwi kuwa ugonjwa wa siri ni kuendeleza maambukizi ambayo yangeweza kuepukika.
Tuseme ili wengine wajihadhari na kuacha tamaa ya kufanya mapenzi. Ni nani leo hii atasimama na kuomba tendo la ngono kwa mtu ambaye ameshajitangaza kuishi na virusi vya ukimwi?
Licha ya kwamba kila mmoja anayo nafasi ya kuushambulia ukimwi, si vibaya tukaanza kujiweka wazi kama alivyofanya Zurry.
Hata hivyo, bado ipo haja ya kuyakumbuka maneno ya Lukuvi kwamba wasanii wawe mstari wa mbele kutunga nyimbo za kuielimisha jamii kuhusu ugonjwa huo.
Tuache habari ya kusifia wanawake wazuri au kusifia pombe kama wafanyavyo baadhi ya wasanii wa muziki wa kizazi kipya maarufu kama bongofleva.
Tujiweke kando na malumbano na majungu katika vikundi vya sanaa na badala yake muda huo tuutumie kuwapa somo raia wengine juu ya kuepukana na janga la ukimwi.
Ya nini kuimba juu ya mavazi mazuri au mambo mengine yasiyofaa wakati ndugu zetu wanaangamia?
Kuna raha gani kukata mauno jukwaani na vivazi vya aibu wakati kuna maelfu wanakufa kwa sababu pengine walikosa elimu juu ya ugonjwa huo?
Wasanii simameni sasa na kuwakemea wasiotaka mabadiliko. Hakuna kulala kwani vita hii ni pana.
Tumieni vipaji vyenu kuliokoa taifa linalozidi kuandamwa na watu wasiokuwa tayari kuacha tabia chafu zinazozidi kuufanya ukimwi ukithiri.
Alichofanya Zurry ni cha kuungwa mkono na ni heri kumwona kama shujaa aliye tayari kuwaokoa watu wake.
Kamwe asitengwe Zurry, asilani! Asibaguliwe kwa kunena ukweli. Pia asiandamwe kwa ÔvijembeÕ na badala yake tufuate moyo wake wa kishujaa wa kujitangaza kwa uwazi.
munyuku@gmail.com
0754 471 920

Tunahofu juu ya ukimwi lakini kemikali nazo ni tishio

na innocent munyuku
WARSHA nyingi zimefanyika juu ya ugonjwa wa ukimwi. Mada mbalimbali zimetolewa kuhusu ugonjwa huo unaoangamiza mamilioni ya watu sehemu mbalimbali duniani. Lakini wakati tunawaza kuhusu ukimwi, walio wengi hawajaona hatari ya chemikali zenye sumu zilizozagaa katika nchi zinazoendelea.
Kemikali hizo kwa kiasi kikubwa zimeendelea kuwaangamiza maelfu katika nchi mbalimbali barani Afrika ambako kwa miaka mingi zimekuwa zikitumika katika kilimo, mifugo na mambo mengine.
Mamilioni ya tani ya kemikali hizo zilizozagaa barani Afrika zimekuwa zikidhuru maisha ya watu kutokana na uelewa mdogo wa watu wake ambao wengi wao hawajapewa elimu ya kutosha kuhusu ubaya wa dawa hizo hasa pale zinapotumika isivyo.
Hivi karibuni ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwa ufadhili wa GTZ, WWF na AGENDA iliandaa warsha kwa waandishi wa habari wa ndani na nje ya nchi juu ya usalama wa kemikali na mpango wa uondoshaji wa dawa barani Afrika (ASP). Warsha hiyo ilifanyika kwenye Hoteli ya Paradise mjini Bagamoyo.
Katika mada yake Mkemia Mkuu wa Serikali, Dk. Ernest Mashimba alisema kemikali ni muhimu katika maisha ya watu lakini pia ni hatari kwani sumu hizo mara nyingi zimesababisha maafa au uharibifu wa mazingira na wakati mwingine kuharibu ngozi.
ÒDawa hizi ziko sehemu mbalimbali na ni muhimu katika maisha ya kila siku lakini zina madhara makubwa kama hazitatumika ipasavyo.
ÒChangamoto kubwa tuliyonayo ni kuwa na elimu juu ya kemikali kwa sababu ni muhimu kuwa na ufahamu na uelewa wa kutosha kuhusu dawa hizi.Ó
Kwamba kwa vile wengi hawana elimu ndio maana utunzaji wake umekuwa wa hovyo huku watu wengine wakiyatumia kinyume cha makusudio.
Inakadiriwa kuwa kwa mwaka zaidi ya tani milioni 500 huzalishwa katika viwanda katika nchi zilizoendelea na kusambazwa katika nchi zinazoendelea ikiwamo Tanzania na kwa bahati mbaya matumizi ya dawa hizo ni madogo.
Kwa maana hiyo kemikali hizo zimekuwa zikiharibu mazingira na kubadilisha hali ya hewa na wakati huo huo kuharibu maji, vyakula vinavyotumika kwa binadamu na wanyama pia.
Yapo magonjwa yatokanayo na matumizi mabaya ya kemikali hizo kama vile saratani ya ngozi, upofu, kuharibu akili, kansa ya damu, kutoka mimba au kujifungua kabla ya muda.
Inasemekana kuwa kemikali zimekuwapo katika uso wa dunia kwa zaidi ya miaka 200 iliyopita na katika tani milioni 500 zinazozalishwa kila mwaka, aina kati ya 70,000 na 100,000 ziko sokoni huku aina mpya kati ya 1,500 na 2,000 zikiendelea kuota mizizi sokoni kila mwaka.
Kemikali hizo kwa hali ilivyo sasa wazalishaji wakubwa barani Ulaya na Marekani ndio wanaoendelea kunufaika kutokana na mauzo. Kwa mfano Marekani hupata kiasi cha dola trilioni 1.6 kwa mwaka.
Pamoja na ukweli kwamba kemikali zimekuwa zikisaidia kudhibiti magonjwa mbalimbali na kukuza mimea mashambani, bado Afrika inaangamia kutokana na madhara makubwa ya kemikali hizo. Waathirika wakubwa katika jamii ni watoto, wajawazito na wazee.
Huu ni mzigo kwa bara la Afrika kwani sasa hivi taratibu zinafanywa kupata pesa za kutosha kwa ajili ya kuzikusanya kemikali hizo na kuzirejesha barani Ulaya ili ziharibiwe.
Tanzania imeshapata dola za Marekani milioni 6.7 kutoka kwa wahisani mbalimbali lengo likiwa kuhakikisha sumu hizo zinakusanywa kwa uangalifu mkubwa na kuzisafirisha kwenda Ulaya. Ikumbukwe kuwa sumu hizo ni zile ambazo zimebaki katika ardhi ya Afrika bila matumizi kwa muda mrefu.
Mfano Septemba 11 mwaka huu nchini Ivory Coast watu 10 walipoteza maisha na zaidi ya 100,000 wakihitaji uangalizi wa madaktari kutokana na athari za kemikali zilizomwagwa.
Upo uwezekano pia kuwa janga kama hilo linaweza kutokea katika eneo jingine ndani ya Afrika kutokana na ukweli kwamba bado watu wake hawajapata elimu ya kutosha juu ya kemikali kama hizo.
Katika Tanzania utatifi uliofanywa kati ya mwaka 1998-2000 umebaini kuwepo kwa maghala 325 ya kemikali sehemu mbalimbali nchini. Si ajabu yakabainika maghala mengine yenye kemikali zisizofaa.
Tatizo kama hili halipo Tanzania pekee, nchini Mali, Morocco, Ethiopia na Afrika Kusini ziko katika shida hii. Uzito wa tatizo hili umelifanya bara la Afrika kuwa katika mkakati wa makusudi kuhakikisha kuwa linafikia ukomo.
Hatuwezi kuendelea kuhatarisha maisha ya Waafrika kwa kuziachia kemikali hizi zisizofaa ziwepo katika maisha yetu ya kila siku.
Kama alivyowahi kusema mtoa mada mwingine katika warsha hiyo, Wolfgang Schimpf kutoka GTZ kwamba kukosekana kwa elimu ya utunzaji wa kemikali kutasababisha madhara makubwa na kwamba ipo haja ya kudhibiti hali hiyo.
Lakini akaonya kuwa si jambo sahihi kumwaga au kutupa kemikali hizo baharini kwani huko ni kuharibu maisha ya viumbe hai vinavyotegemea maji hayo.
Dawa kama DDT, Aldrin, Chlordane, Dieldrin, Endrin, Heptachlor, Hexachlobenzene (HCB) zimekuwa zikitishia uhai wa Afrika na kwa maana hiyo, ulazima wa kuwapa Waafrika elimu unabaki kuwa changamoto kwa wakazi wake.
Tangu miaka ya 1960 kumekuwa na kesi mbalimbali juu ya madhara ya matumizi ya kemikali katika uso wa dunia. Kwa mfano kati ya mwaka 1960-1963 katika mji wa Minamata nchini Japan, watu 1,714 waliathirika na Methyl Mercury kati ya hao 267 walifariki dunia.
Mwaka 1974 kulipuka mtambo wa kemikali kulisababisha kusambaa kwa cyclohexane katika eneo la Flixborough, England. Katika tukio hilo watu 28 walipoteza maisha. Kulipuka kwa mtambo wa nuklia Chernobly, nchini Ukraine mwaka 1986 kuliangamiza maisha ya watu 1,000.

Tunahofu juu ya ukimwi lakini kemikali nazo ni tishio

na innocent munyuku
WARSHA nyingi zimefanyika juu ya ugonjwa wa ukimwi. Mada mbalimbali zimetolewa kuhusu ugonjwa huo unaoangamiza mamilioni ya watu sehemu mbalimbali duniani. Lakini wakati tunawaza kuhusu ukimwi, walio wengi hawajaona hatari ya chemikali zenye sumu zilizozagaa katika nchi zinazoendelea.
Kemikali hizo kwa kiasi kikubwa zimeendelea kuwaangamiza maelfu katika nchi mbalimbali barani Afrika ambako kwa miaka mingi zimekuwa zikitumika katika kilimo, mifugo na mambo mengine.
Mamilioni ya tani ya kemikali hizo zilizozagaa barani Afrika zimekuwa zikidhuru maisha ya watu kutokana na uelewa mdogo wa watu wake ambao wengi wao hawajapewa elimu ya kutosha kuhusu ubaya wa dawa hizo hasa pale zinapotumika isivyo.
Hivi karibuni ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwa ufadhili wa GTZ, WWF na AGENDA iliandaa warsha kwa waandishi wa habari wa ndani na nje ya nchi juu ya usalama wa kemikali na mpango wa uondoshaji wa dawa barani Afrika (ASP). Warsha hiyo ilifanyika kwenye Hoteli ya Paradise mjini Bagamoyo.
Katika mada yake Mkemia Mkuu wa Serikali, Dk. Ernest Mashimba alisema kemikali ni muhimu katika maisha ya watu lakini pia ni hatari kwani sumu hizo mara nyingi zimesababisha maafa au uharibifu wa mazingira na wakati mwingine kuharibu ngozi.
ÒDawa hizi ziko sehemu mbalimbali na ni muhimu katika maisha ya kila siku lakini zina madhara makubwa kama hazitatumika ipasavyo.
ÒChangamoto kubwa tuliyonayo ni kuwa na elimu juu ya kemikali kwa sababu ni muhimu kuwa na ufahamu na uelewa wa kutosha kuhusu dawa hizi.Ó
Kwamba kwa vile wengi hawana elimu ndio maana utunzaji wake umekuwa wa hovyo huku watu wengine wakiyatumia kinyume cha makusudio.
Inakadiriwa kuwa kwa mwaka zaidi ya tani milioni 500 huzalishwa katika viwanda katika nchi zilizoendelea na kusambazwa katika nchi zinazoendelea ikiwamo Tanzania na kwa bahati mbaya matumizi ya dawa hizo ni madogo.
Kwa maana hiyo kemikali hizo zimekuwa zikiharibu mazingira na kubadilisha hali ya hewa na wakati huo huo kuharibu maji, vyakula vinavyotumika kwa binadamu na wanyama pia.
Yapo magonjwa yatokanayo na matumizi mabaya ya kemikali hizo kama vile saratani ya ngozi, upofu, kuharibu akili, kansa ya damu, kutoka mimba au kujifungua kabla ya muda.
Inasemekana kuwa kemikali zimekuwapo katika uso wa dunia kwa zaidi ya miaka 200 iliyopita na katika tani milioni 500 zinazozalishwa kila mwaka, aina kati ya 70,000 na 100,000 ziko sokoni huku aina mpya kati ya 1,500 na 2,000 zikiendelea kuota mizizi sokoni kila mwaka.
Kemikali hizo kwa hali ilivyo sasa wazalishaji wakubwa barani Ulaya na Marekani ndio wanaoendelea kunufaika kutokana na mauzo. Kwa mfano Marekani hupata kiasi cha dola trilioni 1.6 kwa mwaka.
Pamoja na ukweli kwamba kemikali zimekuwa zikisaidia kudhibiti magonjwa mbalimbali na kukuza mimea mashambani, bado Afrika inaangamia kutokana na madhara makubwa ya kemikali hizo. Waathirika wakubwa katika jamii ni watoto, wajawazito na wazee.
Huu ni mzigo kwa bara la Afrika kwani sasa hivi taratibu zinafanywa kupata pesa za kutosha kwa ajili ya kuzikusanya kemikali hizo na kuzirejesha barani Ulaya ili ziharibiwe.
Tanzania imeshapata dola za Marekani milioni 6.7 kutoka kwa wahisani mbalimbali lengo likiwa kuhakikisha sumu hizo zinakusanywa kwa uangalifu mkubwa na kuzisafirisha kwenda Ulaya. Ikumbukwe kuwa sumu hizo ni zile ambazo zimebaki katika ardhi ya Afrika bila matumizi kwa muda mrefu.
Mfano Septemba 11 mwaka huu nchini Ivory Coast watu 10 walipoteza maisha na zaidi ya 100,000 wakihitaji uangalizi wa madaktari kutokana na athari za kemikali zilizomwagwa.
Upo uwezekano pia kuwa janga kama hilo linaweza kutokea katika eneo jingine ndani ya Afrika kutokana na ukweli kwamba bado watu wake hawajapata elimu ya kutosha juu ya kemikali kama hizo.
Katika Tanzania utatifi uliofanywa kati ya mwaka 1998-2000 umebaini kuwepo kwa maghala 325 ya kemikali sehemu mbalimbali nchini. Si ajabu yakabainika maghala mengine yenye kemikali zisizofaa.
Tatizo kama hili halipo Tanzania pekee, nchini Mali, Morocco, Ethiopia na Afrika Kusini ziko katika shida hii. Uzito wa tatizo hili umelifanya bara la Afrika kuwa katika mkakati wa makusudi kuhakikisha kuwa linafikia ukomo.
Hatuwezi kuendelea kuhatarisha maisha ya Waafrika kwa kuziachia kemikali hizi zisizofaa ziwepo katika maisha yetu ya kila siku.
Kama alivyowahi kusema mtoa mada mwingine katika warsha hiyo, Wolfgang Schimpf kutoka GTZ kwamba kukosekana kwa elimu ya utunzaji wa kemikali kutasababisha madhara makubwa na kwamba ipo haja ya kudhibiti hali hiyo.
Lakini akaonya kuwa si jambo sahihi kumwaga au kutupa kemikali hizo baharini kwani huko ni kuharibu maisha ya viumbe hai vinavyotegemea maji hayo.
Dawa kama DDT, Aldrin, Chlordane, Dieldrin, Endrin, Heptachlor, Hexachlobenzene (HCB) zimekuwa zikitishia uhai wa Afrika na kwa maana hiyo, ulazima wa kuwapa Waafrika elimu unabaki kuwa changamoto kwa wakazi wake.
Tangu miaka ya 1960 kumekuwa na kesi mbalimbali juu ya madhara ya matumizi ya kemikali katika uso wa dunia. Kwa mfano kati ya mwaka 1960-1963 katika mji wa Minamata nchini Japan, watu 1,714 waliathirika na Methyl Mercury kati ya hao 267 walifariki dunia.
Mwaka 1974 kulipuka mtambo wa kemikali kulisababisha kusambaa kwa cyclohexane katika eneo la Flixborough, England. Katika tukio hilo watu 28 walipoteza maisha. Kulipuka kwa mtambo wa nuklia Chernobly, nchini Ukraine mwaka 1986 kuliangamiza maisha ya watu 1,000.

Tuwapongeze wabunge wa upinzani kwa lipi?-Dk Mvungi

na innocent munyuku

ALIYEKUWA mgombea urais katika Uchaguzi Mkuu wa Rais na wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa tiketi ya NCCR-Mageuzi mwaka jana, Dk. Edmund Sengondo Mvungi amesema chama chake hakikuona sababu ya kuandamana kuwapongeza wabunge wa upinzani waliomaliza Bunge la Bajeti kwa kuwa hakuna ujasiri wowote waliouonyesha.

Dk. Mvungi alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita katika mahojiano maalum na Rai, kwenye Makao Makuu ya NCCR-Mageuzi Mtaa wa Kilosa, Ilala jijini Dar es Salaam.

“Tuwapongeze hawa kwa ushujaa upi? Tunawapongeza kwa lipi kubwa?,”alihoji Mvungi na kuongeza:

“Kwangu mimi wamekuwa kati ya watu waliopitisha bajeti ambayo ilikuwa ya hovyo kabisa…angalia suala la mikopo kwa elimu ya juu, kwa nini ukubali vipitishwe vigezo vya kukopeshwa kwa madaraja? Hawa watoto wengine watakwenda wapi?”.

Alhamisi iliyopita vyama vya Upinzani vilifanya maandamano jijini Dar es Salaam na baadaye kufanya mkutano wa hadhara kwenye viwanja vya Jangwani baada ya kuwapokea wabunge wa kambi hiyo waliotokea mjini Dodoma kuhudhuria Bunge la Bajeti.

Akizungumzia upinzani nchini, Dk. Mvungi amesema vyama vingi vya upinzani havisemi lugha moja katika mageuzi halisi kwa Watanzania.

Alisema tatizo la upande wa upinzani ni kwamba viongozi wengi wanakuwa na ndoto ya kwenda Ikulu moja kwa moja bila kuweka wazi nini kinawapeleka huko.

“Mnakaa mnajadiliana kwamba hivi tukikuachia nafasi utawafanyia nini wananchi, una malengo gani utasikia mmoja akisema ahh acha tu tutajua huko huko nikifika.

“Huu si utaratibu mzuri, lazima tuelezwe kwamba wananchi utawafanyia nini na wewe mwenyewe umejiandaa vipi kutekeleza unayoahidi,” alisema na kuongeza:

“Binafsi sikuzunguka Tanzania nzima wakati wa kampeni kwa lengo la kuwa katika historia ya nchi kwamba niliwahi kuwa rais. Hapana. Nilizunguka ili kuwapa raia fikra juu ya nini Watanzania tunatakiwa tuwe.

“Ndio maana nasema hivi kwanza tukae tuambizane, tuaminiane halafu twende mbele. Mageuzi si ya Mvungi tu bali ni yetu sote.”

Akizungumza mafanikio katika miezi takribani minane ya uongozi mpya wa awamu ya nne, Dk. Mvungi anasema hawezi kusema kuwa kuna mafanikio makubwa.

“Jambo jema ninaloweza kusema ni kwamba tumebaki na amani ile ile tuliyoizoea Watanzania. Lakini kwa kweli matumaini katika huduma ya jamii hakuna, hali ni mbaya.

“Tulipoamua kufanya uchaguzi tulitegemea mabadiliko ya maisha ya watu na hatuchagui serikali itupeleke nyuma, bali mbele kimaendeleo.

“Lakini hofu yangu pia ni kuwa huenda kuna waliokwenda kuwachagua watu ili nao waendelee kunufaika na ulaji.”

Pamoja na hayo Dk. Mvungi anasema katika uchaguzi uliopita Chama Cha Mapinduzi kilifanya mapinduzi makubwa ndani ya chama. Mapinduzi ambayo kama yanalenga dhamira njema yanaweza kuisaidia Tanzania.

“Ndiyo kulikuwa na mapinduzi makubwa ndani ya CCM, hawa waliofanya mapinduzi walikuwa makini sana. Hawa ndio wanaojiita ‘wanamtandao’.

“CCM imebadilika, watu wapya kabisa wenye matamanio mapya na ndio maana nasema mchakato wa CCM haukuwa wa kizembe na wala halikuwa jambo dogo lililofanywa na wanamtandao.

“Lakini mimi nasema hawa wanamtandao wana lengo ambalo bila shaka ni kula na bila shaka zile bilioni 21 zilizotengwa kwa ajili ya kusambazwa mikoani zitawanufaisha hawa watu.

“Wanamtandao ni wengi, Rais kishachagua baraza la mawiziri, wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya sasa wengine waliobaki watapewa nini? Bila shaka ni hizi pesa za kifuta machozi.”

Alisema katika mfumo huu wa chama dola, ni CCM ndicho kitakachoamua nani apewe pesa hizo. “Nafikiri wanajipanga hivyo.”

Mikumi Sound ‘Wanatekenya’ walioiteka Moro

na mwandishi wetu

BAADA ya kufifia kwa bendi maarufu mkoani Morogoro kama Moro Jazz iliyotamba na marehemu Mbaraka Mwinshehe, mkoa huo ulibaki kama yatima katika masuala ya muziki.

Hii ilitokana na wadau kutotaka au kutokuwa na ari au uwezo wa kumiliki bendi za muziki wa dansi. Matokeo yake, burudani ya aina hiyo ikazidi kushamiri katika jiji la Dar es Salaam.

Lakini leo hii, Morogoro si yatima tena katika muziki wa dansi. Hilo linajihidhirisha baada ya kuibuka kwa bendi mpya ya Mikumi Sound iliyojikita mkoani humo kiasi cha mwaka mmoja uliopita.

Wiki iliyopita nimekuwa shuhuda wa makali ya bendi hiyo inayotumia mtindo wa Tekenya katika mapigo yake wakati ilipotumbuiza kwenye Ukumbi a VIP mjini Morogoro.

Umahiri wao jukwaani huwezi kuamiani kuwa bendi hii inaundwa na wanamuziki wenye usongo wa kujitangaza kimataifa.

Hao ni Sadiq Jakaya anayepiga gitaa la solo, Balely Mohamed anayevuma na gitaa la bass, Toto Site (kinanda), Abeid Said anayepiga drums huku Jose Kigenda ambaye ni rais wa bendi hiyo. Kuna washambuliaji wa jukwaa katika unenguaji hawa ni Monter Bige, Cool Mud, Dogoo Kaisi na Hamis Makata.

Kama ulikuwa ukiwaza kushabikia bendi za Kikongo, bila shaka nuna sababu tena ya kufanya hivyo kutokana na ukweli kwamba muziki wa Mikumi Sound ni kiboko yao. Hawatanii katika fani na wako makini. Wameshafyatua albamu mbili sasa nazo ni Cheo ni Dhamana yenye vibao sita na Mama Mkwe yenye nyimbo tano.

Rais wa bendi hiyo, Jose Kigenda katika mahojiamo maalumu anasema kuwa wanamuziki wake wamekuwa wabunifu kutokana na maelewano baina yao.

“Mikumi Sound si ya wababaishaji na tunawaomba mashabiki waelewe kuwa tumekuja kamili na tumeiva kimuziki,” anasema Kigenda na kuongeza:

“Tunajua mashabiki wanataka nini na hapa Morogoro tumegundua kuwa hawataki mambo ya kuwaiga Wakongo na ndio maana sisi tumeitikia wito kwa kuthamini utamaduni wa Mtanzania.

“Ndio maana kila siku nawaambia kuwa wanaodhani wamesimama kimuziki wakae chonjo, mwendo wetu ni wa taratibu lakini tuko makini sana,” anasema.

Mapema Juni mwaka huu, bendi hiyo iliandaa onyesho maalumu kuipongeza timu ya soka ya Moro United kwa kushika nafasi ya pili katika michuano ya Kombe la Kagame.

Katika onyesho hilo, bendi hiyo iliwapagawisha mashabiki wake kwa vibao kemkem kutoka kwenye albamu ya Mama Mkwe inayoundwa pia na nyimbo za Usiku wa
Deni, Dunia Duara, Mchumba Mwema na Afrika Tekenya
Twist.

Katika kuhakikisha kuwa inabeba mashabiki wengi zaidi, bendi hiyo imeshazuru mikoa mbalimbali nchini kujitangaza. Moja ya ziara iliyofana ni ile ya kuitangaza albamu yake Mama Mkwe.

Lakini hayo yote yasingewezekana kama sio ubavu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Mikumi Sound, Rena Vegula. Huyu kwa watu wengine wanaweza kumwita mwanamke wa shoka kutokana na kutokuwa na woga katika uendeshaji wa masuala ya maendeleo.

“Wazo la bendi lilianzia mjini Arusha mwaka 2003 na lengo hasa lilikuwa kuitangaza Mikumi kama mbuga nzuri Tanzania na ndio maana tukaamua kuipa jina hili,” anasema Rena mama wa watoto wanne; Abel, Erick, Peter na Aneth.

Wakati wazo hilo linaanza mwaka 2003, Rena alikuwa jijini Arusha akiendesha biashara zake. “Nina ukumbi wa starehe pale Arusha unaitwa Ricks Club sasa wakati ule bendi ya Olduvai ilikuwa ikipiga pale.

“Baadhi ya wanamuziki wetu wakawa wanaonyesha moyo wa kuendeleza muziki lakini vifaa hatukuwa navyo, ndipo tukaamua kununua vifaa vyetu.”

Alipoulizwa kama haoni kikwazo kuendesha bendi ya muziki wa dansi, Rena anasema kuwa haoni kikwazo kwa sababu dhamira yake ni kuona muziki wa Tanzania unakua na wanamuziki wake wanapata neema.

“Nikwambie kitu kwamba matarajio yetu ni makubwa sana hadi utashangaa,” anasema. “Mipango tuliyo nayo ni mizuri na tunasikilizana.”

Anasema kuwa hadi sasa, bendi hiyo inajiendesha na hakuna mzigo mkubwa sana kama hapo awali.

Kwa nini basi Mikumi Sound ikahamia Morogoro?

Rena anaeleza kuwa mwaka jana walipata nafasi ya kuiendesha hoteli ya Masuka Village iliyopo barabara ya Boma mjini Morogoro, kwa hiyo wakaamua kuihamishia bendi mjini hapo ili kuwa nayo karibu.

“Hapa tukaona nafasi nzuri ya kuikarabati bendi na hii ilitokana na kupokewa vizuri hapa Morogoro, mashabiki wanakubali na kuipenda kazi yetu.”

Lakini Rena ana msimamo ambao kwa hakika unajenga asili yetu kama Watanzania pale anaposema kuwa hatakubali kuwaajiri Wakongo kwenye bendi yake.

Anasema kimsingi kumwacha Mtanzania na kumwajiri Mkongo katika bendi ni dhambi kwani unamnyima mtu wako wa karibu mkate wa kila siku.

Anasema umefika wakati sasa kwa Watanzania kuthamini watu na vipaji vyao na kwamba hao wa nje hawana muujiza zaidi ya kwamba wanajituma katika kazi zao za muziki.

“Ndio maana ukiingia katika maonyesho yetu moja kwa moja unapata ladha ya muziki wetu na hatutaki kuiga,” anasema na kuongeza kuwa wanataka kuziba pengo la Mbaraka Mwinshehe.

“Tanzania kuna vipaji vingi mno katika muziki, ni suala la kuwaibua hawa wasanii na kila jambo linawezekana, hakuna sababu ya kuiga nyimbo za wanamuziki wa Kongo hii ni aibu kwa taifa.”

Ni mwanamke jasiri ambaye daima ulimi wake hulenga katika ari ya kuthubutu kutenda na kutekeleza masuala ya maendeleo na hilo amefanikiwa kutokana na malengo yake kukubalika pia kwa mumewe anayekwenda kwa jina la Henry Vegula.

“Mume ananielewa na hata watoto pia wanaelewa kwamba kazi ina manufaa kwetu sote,” anasema Rena.

Si lazima wote waimbe

Si lazima wote waimbe
YAPO mambo ambayo kila yanapotokea katika hii dunia, basi huwa gumzo kwa mitazamo tofauti. Aghalabu mambo hayo yanaweza kuwa mema au mabaya.Watendaji wa mambo hayo wakati mwingine hulenga kupata umaarufu katika jamii. Na ndio maana katika baadhi ya nyimbo za muziki hapa kwetu zimekuwa zikitaja majina ya watu kuanzia mwanzo hadi mwisho.Kuna tetesi kwamba hao wanaotajwa hulipia kiasi fulani cha ngwenje ili wapate kurushwa hewani kupitia maikrofoni. Utasikia wakipayuka ‘Papaa Mkechee wapi Papaa Lusajo’ au ‘Papaa Kidume wapi Mukulu Ndago’.Inawezekana ni staili ya miaka mingi katika sanaa ya muziki lakini je, hao wanaotajwa wana kitu gani kipya kwa jamii? Ana mchango upi ambao msikilizaji wa tungo husika atakunwa kusikiliza?Kwa mtazamo wa Mzee wa Busati huu ni sawa na ulofa. Muziki gani huu wa kutajana majina kuanzia ubeti wa kwanza hadi wa mwisho? Maana yake nini hasa?Pengine kwa mtazamo wa Mwandika Busati staili hii ni bardani. Hakuna uzito wowote ndani yake na ni sawa na debe tupu ambalo halikosi kupiga kelele.Kama noma na iwe noma! Huu ni ubabaishaji katika sanaa. Imbeni kitu kinachoeleweka si kutajana majina tu. Imbeni mema kwa nchi kama vile vita dhidi ya maradhi mbalimbali na umaskini.Enendeni mkaseme maovu ya serikali mbalimbali za Afrika na hata huko Ulaya na kwingineko. Kemeeni wabakaji na walawiti kwani hayo yote ni kinyume na taratibu katika kaya nyingi.Wakemeeni na kuwaasa wafanyakazi wavivu wanaotumia vibaya nafasi zao kwa kujilimbikizia mali huku wengine wakila mlo mmoja kwa siku.Mwadhani kwa staili hii ya kutajana majina mtaweza kuuza tungo zenu kwa pesa nyingi ndani na nje ya nchi? Mtaishia kukaa kwenye viti virefu na kukamata chupa za bia. Mkienda mbali sana mtanunua mikweche ya magari kutoka Mashariki ya Mbali.Hakuna shaka kwamba ukosefu wa ubunifu ndicho chanzo cha muziki wa Tanzania kukosa kutamba nchi za mbali.Lakini pia muda huo mnaotumia kutaja majina ya watu wasio na jipya katika jamii, ingefaa basi mketi kupanga mikakati ya kuboresha muziki wetu na namna ya kuwabana wasambazaji wa kazi zenu ambao wakati mwingine wamekuwa kero kwa baadhi ya wanamuziki wanaofanya vizuri sokoni.Mzee wa Busati ataendelea kuyaweka haya bila hofu kwani tangu siku ya kwanza alipoanza kuyoyoma katika safu yake hii ambayo walau sasa itagota miaka sita aliahidi kuwa mkweli pasipo ukandamizaji.Ndio maana kero kama hizi zinapigiwa zumari ziende kuzimu. Walio wengi wanakerwa na mtindo wenu wa wanamuziki kutaja taja majina katika tungo.Mwenye Busati anayasema haya kwani ana hofu kwamba ipo siku baadhi ya hawa wanamuziki wataanza kuimba habari za wake zao na nyumba ndogo.Wataanza kutaja majina ya watu wao wa ukoo kwa sababu ndimi zao zimekuwa na shauku ya kutaja watu katika nyimbo. Wakishamaliza kutaja hayo watatueleza pia na umri wa familia zao.Mzee wa Busati angepita kuona siku moja akitua New York aulizwe habari za wanamuziki wa hapa kwetu ambao tayari kwa wakati huo watakuwa wameteka soko la muziki huko.Hiyo ndiyo ndoto endelevu ya Mzee wa Busati kwamba ije siku akiwa Congo Brazzaville aulizwe juu ya akina Dudu Baya au Banza Stone na Ally Choki.Kwamba ifike mahala wanamuziki wetu wajulikane kama ilivyo kwa nyota wa DRC ambao wanatamba barani Ulaya wakiingiza mamilioni ya faranga kwenye mifuko yao.Wamefikia mahala ambako hata kama hawatapiga ukumbini mwaka mzima, wanaendelea kunawiri kwa sababu mauzo ya albamu zao sokoni ni mazuri. Hawana haja ya kuumiza kichwa na viingilio vya buku tatu kwa kila kichwa kama ilivyo hapa kwetu.Uwezo wa kufikia walipo na hata kuwapiku upo ikiwa wanamuziki watakubali kutumia vichwa vyao ipasavyo. Wakibuni na kujipangia mikakati ya ushindi katika majukwaa ya muziki.Mikakati ni muhimu badala ya kupikiana majungu kila siku na kupishana kwa sangoma kusaka mbinu chafu za kuangushana.Huo ndio mtazamo wa Mzee wa Busati. Kwamba wakati wa mageuzi katika muziki ni huu na hakuna haja ya kusubiri miujiza kutoka sehemu nyingine. Ni suala la ubunifu katika tungo na mambo mengine yanayoambatana na muziki.Mwenye Busati anafikia ukomo kwa juma hili akisubiri kwa hamu kuangalia vituko kwenye viunga mbalimbali vya Darisalama na Mji Kasoro Bahari ambako wikiendi huwa njema ajabu.Hakuna kuulizana kila mmoja hujitanua kwa nafasi yake apendavyo na huwezi kujua kama wengine wanavinjari na pesa za mikopo au mafao ya wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki.Kuuliza hakuna kwani kila mwenye chake hujipinda awezavyo ila maji yenye rangi ya mende yakishatoweka kichwani ndipo majuto hujaa tele.Lakini kwa kumalizia tu ni kwamba Mzee wa Busati anaomba wapenzi na mashabiki wa Yanga wasiisuse timu hiyo licha ya kutolewa mapema katika Ligi ya Mabingwa Afrika. Endeleeni kushikamana ili kuleta mafanikio katika Ligi Kuu.
Wasalaam,
munyuku@gmail.com
0754 471 920

Eti pesa za Uhuru zililiwa na waliovaa suti!

Na Innocent Munyuku

YAWEZEKANA mkashangaa haya mapinduzi kwenye safu hii. Kwamba iweje kaja mtawala mwingine ghafla bin vuu? Jibu la swali kama hilo ni rahisi. Mwasisi wa ‘Mtaani Kwetu’ kaona jambo la heri kwenda kwao kuongeza nguvu kwani inasemekana ndumba zimegoma kutii amri.

Haya ni maneno ya ‘Mtaani Kwetu’ nami kama mmoja wa waliosikia sina budi kuwahabarisha wengine kwamba mzee mzima kakimbilia Umakondeni kuweka mambo sawa.

Lakini tukiachana na hilo, huku ‘Mtaani Kwetu’ kuna mambo yamekuwa yakisemwa na kwa hakika wanaonguruma na maneno hayo wanaonekana kukerwa kwa siku nyingi. Hawaogopi hawa watu. Ni kama vile wamevaa mabomu tayari kwa kujilipua.

Kinachosemwa ‘Mtaani Kwetu’ ni kwamba kitendo cha kuchangia sherehe za Uhuru wa Tanganyika mwaka jana kimewakera huku mtaani. Wanasema badala ya kukusanya hizo pesa kwa ajili ya tiba hospitalini wao wamezikusanya na kuzitumbua kwa saa chache.

Aliyeanza kunena kero hiyo ni jamaa mmoja ambaye kajitambulisha kuwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam sehemu ya Mlimani. Kasema yeye kanyimwa mkopo kwa ajili ya elimu lakini kumbe Serikali inayo uwezo wa kuwahamasisha wafanyabiashara na kuchangia sherehe badala ya elimu.

‘Mtaani Kwetu’ wamekerwa na jambo hili na kama wangemwona Waziri Mkuu na bosi wake ana kwa ana huku mtaani basi sijui wangemsalimia kwa lugha gani.

Sherehe zimepita na wao kinachowafanya walalame ni kwamba ugumu wa maisha unaendelea. Mwingine akasema eti hayo mabilioni ya shilingi yaliyochangishwa yeye hakuwahi hata kupata maji ya sh 200 pale kwenye Uwanja wa Taifa. Aliambulia ukali wa jua la utosi na kupakana jasho na shombo.

Hayo ndiyo mambo ya ‘Mtaani Kwetu’ ambako si ajabu ukakutana na mtu akaanza kulia tu. Kisa? Ugumu wa maisha! Lakini wapo wanaosema kwamba nafuu basi hizo pesa za Uhuru zingenunua dawa kwa ajili ya wagonjwa hospitalini.

Wangezipeleka hata Mwanamanyala, au Amana na sehemu nyingine zenye kuhitaji ubora wa afya. Hilo fungu lingeweza kununua vitanda na kuwapa nafuu kina mama wajawazito ambao kwa nyakati fulani huku ‘Mtaani Kwetu’ tulisikia habari kwamba kina mama hao hulala mzungu wa nne kwa sababu vitanda havitoshi.

Maneno ya huku ‘Mtaani Kwetu’ wakati mwingine unaweza ukashika kichwa kwa mshtuko manake watu wanatema cheche pasipo hofu. Rafiki zangu Mmachinga ndio kabisa usithubutu kuwasikiliza.

Hawa jamaa baada ya ule mpango wa bomoa bomoa na kuwahamisha kwenye makao mapya, hivi sasa wana hasira na Serikali yao. Wengine imefikia hatua hata ya kujutia kura zao wakati wa Uchaguzi Mkuu uliopita.

Wangali wakilalama kwamba hawakutendewa haki kuhamishwa. Njoo ‘Mtaani Kwetu’ uwasikilize wanavyosema. Wanasema wamepoteza nguvu zao nyingi na hivyo vibanda vilivyovunjwa hawa jamaa wanaokusanya kodi (TRA) walipitisha bakuli zao kutaka malipo.

Ghafla Serikali imewageuka. Wametemwa na huko walikopelekwa wanadai hakuna lolote la maana zaidi ya kuambulia vumbi. Ukija ‘Mtaani Kwetu’ utasikia mengi hadi ukome ubishi.

‘Mtaani Kwetu’ walio wengi ni kama vile wamevuta bangi ya Malawi. Manake husemwa kuwa hii ni kiboko kuzidi ya Musoma au Morocco. Hii ya Malawi ina ubora wa aina yake. Ukivuta ‘inakubangua’ kweli kweli haina utani.

Basi hawa wavutaji ndio waliojaa huku ‘Mtaani Kwetu’ lakini naomba niseme kwamba hizi ni hisia zangu kwani sijawahi kuwafuma wakiwa na hizo bangi ila kwa jinsi wanavyojiamini naona kama vile wana nguvu ya ziada kwenye bongo zao.

Ukija ‘Mtaani Kwetu’ wanaolia sana ni wale wenye matumbo yaso na uhakika wa kumeza kitu kwa kila siku iendayo kwa Mungu. Hawa wanakula wanachokipata na si wanachokitaka.

Ndio manaa huku ‘Mtaani Kwetu’ ni rahisi kuwakuta ‘wanasiasa’ mahiri kwa kupanga safu ya uongozi. Utawasikia wakisema ahh fulani ndiye alifaa kuwa Mkuu wa Kaya. Kisa? Maisha bora waliyoambiwa wakati wa Uchaguzi Mkuu hayaonekani.

Waliambiwa habari za kuongezeka kwa ajira, lakini leo hii huku ‘Mtaani Kwetu’ wanazidi kuteseka. Wamebaki kutafakari kero. Lakini nani alaumiwe? Ajira gani watapewa hawa watu wakati hawana elimu ya kutosha katika vichwa vyao? Wanasubiri rehema za Allah.

Kilichobaki ni kulilia pesa za Uhuru, lawama kwa Serikali kwa kuwakimbiza Mmachinga. Hizi ni nyimbo za kila siku kibwagizo kinaweza kuwa chochote kati hivi vifuatavyo; rushwa, huduma mbovu za jamii hasa katika sekta ya afya.

Mie kama mpiga mbiu sitaacha kuwaeleza wengine juu ya hiki kinachoendelea kusemwa huku ‘Mtaani Kwetu’ ni heri mkayajua manake isije siku mnakuja mnashangaa raia wamenuna na hawataki salamu zenu.

Msije mkashangaa kuona jamaa wamejifungia kwenye vibanda vyao vya ‘mbavu za mbwa’ hawatoki kuwalaki kwenye ziara zenu. Hawakufurahishwa na michango ya Uhuru manake wanasema fedha hizo zililiwa na wenye ubavu wa kuvaa suti na si walalahoi.

Naam, ni lazima tuwajulishe ya huku mtaani kwa sababu wakati mwingi mko katika kupanga mikakati ya kuijenga nchi. Mkitoka ofisini mwaelekea kwenye makazi yenu ambako watu wa huku ‘Mtaani Kwetu’ hawawezi kuja kuwasalimia kwenye makazi yenu.

Mvamizi wa safu hii amefikia ukomo. Kama mapinduzi haya yatapewa baraka basi atabakia ulingoni kwa muda mrefu ujayo. Na hapo itaundwa upya serikali ya mapinduzi ya Mtaani Kwetu. Aliyepinduliwa ataambulia kuwa mshauri mkuu.

Wasalaam,
munyuku@gmail.com
0754 471 920

Thursday, January 18, 2007

Haya ndiyo maajabu ya Dk. Mwiko

Na Mwandishi Wetu
ALIANZIA kuvuma jijini Dar es Salaam lakini sasa jina lake limepaa na kuvuka mipaka ya Tanzania. Huyu si mwingine bali Dk. Mwiko Kuona mganga maarufu wa tiba za asili nchini.

Aliposimama na kuwafichua wachawi siku ya kwanza katika viunga vya Keko jijini Dar es Salaam ilionekana wazi kuwa alikuwa na mwelekeo mzuri katika tiba na hivyo kuokoa maisha ya watu.

Hakuishia kuwakomesha magagula bali alizidisha huduma za tiba kwa wateja wake na hilo ndilo jambo analoendelea nalo kila leo.

Wiki hii amezungumza na gazeti hili na kubainisha kuwa mwaka huu wa 2007 atakuwa na jukumu zito zaidi kwani amepanga kupanua wigo wa huduma zake katika sehemu mbalimbali za Tanzania.

"Nimekaa Dar es Salaam kwa muda mrefu lakini kwa jinsi watu wanavyozidi kunihitaji siwezi kubakia hapa nilipo yanipasa niwafuate huko waliko manake wengine hawamudu gharama za kuja nilipo," anasema Dk. Mwiko.

Inawezekana ulishakumbwa na matatizo kama vile kukosa uzazi, kutokuwa na hamu ya kula, magonjwa yatokanayo na ukimwi, malaria sugu au kudhulumiwa haki yako. Hayo yote yana suluhu kwa Dk.Mwiko.

Si hayo tu hata kama kuna mpenzi wako anayekuchezea akili kwa kutembea nje ya mapenzi yenu, Dk. Mwiko anao uwezo wa kurejesha uhusiano uliovunjika na hilo linafanyika kwa muda wa siku chache.

Pengine ulishateswa usingizini na wakati mwingine kuandamwa na wezi katika mashamba au nyumbani, Dk. Mwiko ana ubavu wa kukuwekea zindiko na kukuepusha na matatizo hayo.

Katika siku za mwanzo kabisa, Dk. Mwiko hakupenda kujihusisha na masuala ya uganga wa tiba za asili. Alitamani kufanya kazi nyingine. Lakini kadri siku zilivyokuwa zinasonga mbele, mambo yalibadilika kwani mizimu ya mababu ilimvuta arithi tiba kama ilivyokuwa kwa babu yake.

"Si unajua mambo ya ujana bwana, mimi sikutaka kujihusisha na uganga ingawa babu ndio ilikuwa shughuli zake.

"Lakini kila nilipojaribu kukwepa jukumu hilo, kichwa kilikuwa kinaendelea kupata maumivu makubwa kiasi cha kushindwa kufanya kazi. Ndipo nikaanza kujiuliza tatizo nini?

"Kwa hiyo baada ya kurejea Chalinze nikaambiwa kuna kitu natakiwa kukifanya na sijafanya na kwamba salama yangu nikubali kubeba mikoba ya uganga kutoka kwa babu," anakumbuka Dk. Mwiko Kuona.

Anasema baada ya kufanyiwa zindiko porini, ile hali ya kuumwa kichwa ikapotea na ndiyo maana aliamua kuacha kazi ya kuajiriwa na kuamua kuwapa watu tiba za asili kwa wanaohitaji.

Alishaalikwa kuondoa majini sehemu moja huko Ugweno na katika ziara yake hiyo anasema alipata mafanikio makubwa kwani wanakijiji walifurahi kwa vile aliwanusuru na mateso waliyokuwa wakikumbana nayo.

"Hapa unaponiona hakuna lisilowezekana katika tiba za asili, nafanya kila jitihada kuhakikisha kuwa wateja wangu wanaridhika na tiba zangu na hilo nalifanya kwa umakini mkubwa kwa sababu sitaki kuharibu jina," anaeleza.

Katika shughuli za kuondoa 'vitu' kwenye majumba ya watu na kuwasitisha wachawi huambatana na wasaidizi wake wanne pamoja na walinzi zaidi ya 10.

"Walinzi hawa kazi yao ni kudhibiti msongamano wa watu manake katika hizi kazi hasa ya kuwashika wachawi watu wanakuwa na usongo wa kuona nini kinaendelea...sasa kama huna ulinzi watakuharibia shughuli kwani msongamano huo utaingilia utaratibu mzima," anasema.

Kama unasumbuliwa na magonjwa mbalimbali au mfarakano wa kimapenzi, biashara haiendi vizuri usisite kuwasiliana na Dk. Mwiko Kuona kwa simu namba
0754 602629 au 0787 602629.

Kifimbo: Tusibeze tiba za asili

na innocent munyuku

HISTORIA inaonyesha kuwa binadamu kabla ya kuibuka kwa teknolojia za kisasa alitumia vitu vingi vya asili. Kuanzia chakula na dawa kwa magonjwa mbalimbali.

Kuibuka kwa mbinu mpya katika nyanja za kila aina kukasababisha utengenezwaji wa dawa viwandani na hivyo kurahishisha ufungaji na usambazaji pia.

Pamoja na uvumbuzi wa viwanda vya dawa, ukweli wa mambo ni kwamba tiba za asili zingali na umuhimu mkubwa kwa binadamu na mataifa mengi yanaendelea kuzitumia dawa hizo.

Tanzania ni moja ya nchi ambazo zimeendelea kutumia tiba za asili kwa magonjwa mbalimbali ikiwemo zile za kupunguza makali ya ugonjwa wa ukimwi, homa na ngiri.

Hata hivyo, kumekuwa na wimbi la watoa tiba za asili ambao wengi wao si waaminifu. Hili ni kundi ambalo limejiwekea mizizi ya kuwatapeli watu badala ya kutoa tiba halisi kwa wagonjwa.

Katika mahojiano na gazeti hili mapema wiki hii, mganga maarufu wa tiba za asili nchini Dk. Haruna Kifimbo anasema ujio wa kundi la ‘makanjanja’ katika tiba za asili ni kero kubwa kwa jamii.

“Mimi ninachoomba ni mamlaka za Serikali hapa nchini kuwadhibiti hawa wahalifu wa tiba za asili. Wanaharibu maana ya huduma hii.

“Si kila mtu anaweza kuwa mganga wa tiba za asili hilo lazima tukubaliane na kwa vile hawa wanaoharibu sekta hii tunaishi nao mitaani ni suala la kuwakamata na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria ili kuokoa maisha ya Watanzania,” anasema Dk. Kifimbo.

Dk. Kifimbo anaeleza kuwa kama waharibifu wa aina hiyo hawatadhibitiwa, Tanzania itajikuta iko kwenye janga litakalolidhoofisha taifa.

Akizungumzia uwezo wa tiba hizo katika jamii, Kifimbo anasema dawa hizo zimekuwa zikiokoa maisha watu kila siku. Anayataja maradhi ambayo wamekuwa wakikabiliana nayo kuwa ni pamoja na upungufu wa nguvu za nguvu za kiume.

“Ukweli ni kwamba katika miaka ya hivi karibuni, wanaume wengi wamekuwa wakipungukiwa nguvu za kiume na tiba zipo. Matatizo kama haya mara nyingi hutokana na vyakula tunavyokula hasa vilivyopoteza uasili wake, mtu mwenye kisukari, ngiri, presha au ugonjwa wa figo anaweza kukumbwa na tatizo hili,” anasema.

Dk. Kifimbo anasema wakati umefika kwa jamii kutambua umuhimu wa matumizi ya dawa za asili kwani uzoefu unaonyesha kuwa ni nzuri kwa matumizi ya binadamu na hukomesha kabisa magonjwa sugu.

Anatolea mfano magonjwa kama kuwashwa sehemu za siri, chunusi sugu na mabaka, maumivu ya mara kwa mara ya mgongo au kiuno, kukojoa kitandani, kukosa usingizi homa ya matumbo au magonjwa nyemelezi.

“Angalia Wachina wanavyoendelea kutumia dawa za asili, wanajua ubora wake ndio maana wamezing’ang’ania. Sasa sisi tunazibeza nadhani hii ni hatari kwetu kama hatutakuwa makini.

“Amerika ya Kusini nao wako mstari wa mbele katika kudumisha matumizi ya dawa hizi. Kwa hiyo ni jukumu letu kama wataalamu wa tiba kuhakikisha kuwa tunakuwa wabunifu kila siku na kuwadhibiti wanaoharibu sekta hii, hiki ni kilio changu.”

Mbali na kutoa huduma ya tiba, Dk. Kifimbo amekuwa akijitolea kuisaidia jamii katika mambo mbalimbali. “Naamini katika jamii bora na ndio maana ninachokipata nagawana na wengine,” anasema Kifimbo.

Tunahofu juu ya ukimwi lakini kemikali nazo ni tishio

na innocent munyuku
WARSHA nyingi zimefanyika juu ya ugonjwa wa ukimwi. Mada mbalimbali zimetolewa kuhusu ugonjwa huo unaoangamiza mamilioni ya watu sehemu mbalimbali duniani. Lakini wakati tunawaza kuhusu ukimwi, walio wengi hawajaona hatari ya chemikali zenye sumu zilizozagaa katika nchi zinazoendelea.
Kemikali hizo kwa kiasi kikubwa zimeendelea kuwaangamiza maelfu katika nchi mbalimbali barani Afrika ambako kwa miaka mingi zimekuwa zikitumika katika kilimo, mifugo na mambo mengine.
Mamilioni ya tani ya kemikali hizo zilizozagaa barani Afrika zimekuwa zikidhuru maisha ya watu kutokana na uelewa mdogo wa watu wake ambao wengi wao hawajapewa elimu ya kutosha kuhusu ubaya wa dawa hizo hasa pale zinapotumika isivyo.
Hivi karibuni ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwa ufadhili wa GTZ, WWF na AGENDA iliandaa warsha kwa waandishi wa habari wa ndani na nje ya nchi juu ya usalama wa kemikali na mpango wa uondoshaji wa dawa barani Afrika (ASP). Warsha hiyo ilifanyika kwenye Hoteli ya Paradise mjini Bagamoyo.
Katika mada yake Mkemia Mkuu wa Serikali, Dk. Ernest Mashimba alisema kemikali ni muhimu katika maisha ya watu lakini pia ni hatari kwani sumu hizo mara nyingi zimesababisha maafa au uharibifu wa mazingira na wakati mwingine kuharibu ngozi.
ÒDawa hizi ziko sehemu mbalimbali na ni muhimu katika maisha ya kila siku lakini zina madhara makubwa kama hazitatumika ipasavyo.
ÒChangamoto kubwa tuliyonayo ni kuwa na elimu juu ya kemikali kwa sababu ni muhimu kuwa na ufahamu na uelewa wa kutosha kuhusu dawa hizi.Ó
Kwamba kwa vile wengi hawana elimu ndio maana utunzaji wake umekuwa wa hovyo huku watu wengine wakiyatumia kinyume cha makusudio.
Inakadiriwa kuwa kwa mwaka zaidi ya tani milioni 500 huzalishwa katika viwanda katika nchi zilizoendelea na kusambazwa katika nchi zinazoendelea ikiwamo Tanzania na kwa bahati mbaya matumizi ya dawa hizo ni madogo.
Kwa maana hiyo kemikali hizo zimekuwa zikiharibu mazingira na kubadilisha hali ya hewa na wakati huo huo kuharibu maji, vyakula vinavyotumika kwa binadamu na wanyama pia.
Yapo magonjwa yatokanayo na matumizi mabaya ya kemikali hizo kama vile saratani ya ngozi, upofu, kuharibu akili, kansa ya damu, kutoka mimba au kujifungua kabla ya muda.
Inasemekana kuwa kemikali zimekuwapo katika uso wa dunia kwa zaidi ya miaka 200 iliyopita na katika tani milioni 500 zinazozalishwa kila mwaka, aina kati ya 70,000 na 100,000 ziko sokoni huku aina mpya kati ya 1,500 na 2,000 zikiendelea kuota mizizi sokoni kila mwaka.
Kemikali hizo kwa hali ilivyo sasa wazalishaji wakubwa barani Ulaya na Marekani ndio wanaoendelea kunufaika kutokana na mauzo. Kwa mfano Marekani hupata kiasi cha dola trilioni 1.6 kwa mwaka.
Pamoja na ukweli kwamba kemikali zimekuwa zikisaidia kudhibiti magonjwa mbalimbali na kukuza mimea mashambani, bado Afrika inaangamia kutokana na madhara makubwa ya kemikali hizo. Waathirika wakubwa katika jamii ni watoto, wajawazito na wazee.
Huu ni mzigo kwa bara la Afrika kwani sasa hivi taratibu zinafanywa kupata pesa za kutosha kwa ajili ya kuzikusanya kemikali hizo na kuzirejesha barani Ulaya ili ziharibiwe.
Tanzania imeshapata dola za Marekani milioni 6.7 kutoka kwa wahisani mbalimbali lengo likiwa kuhakikisha sumu hizo zinakusanywa kwa uangalifu mkubwa na kuzisafirisha kwenda Ulaya. Ikumbukwe kuwa sumu hizo ni zile ambazo zimebaki katika ardhi ya Afrika bila matumizi kwa muda mrefu.
Mfano Septemba 11 mwaka huu nchini Ivory Coast watu 10 walipoteza maisha na zaidi ya 100,000 wakihitaji uangalizi wa madaktari kutokana na athari za kemikali zilizomwagwa.
Upo uwezekano pia kuwa janga kama hilo linaweza kutokea katika eneo jingine ndani ya Afrika kutokana na ukweli kwamba bado watu wake hawajapata elimu ya kutosha juu ya kemikali kama hizo.
Katika Tanzania utatifi uliofanywa kati ya mwaka 1998-2000 umebaini kuwepo kwa maghala 325 ya kemikali sehemu mbalimbali nchini. Si ajabu yakabainika maghala mengine yenye kemikali zisizofaa.
Tatizo kama hili halipo Tanzania pekee, nchini Mali, Morocco, Ethiopia na Afrika Kusini ziko katika shida hii. Uzito wa tatizo hili umelifanya bara la Afrika kuwa katika mkakati wa makusudi kuhakikisha kuwa linafikia ukomo.
Hatuwezi kuendelea kuhatarisha maisha ya Waafrika kwa kuziachia kemikali hizi zisizofaa ziwepo katika maisha yetu ya kila siku.
Kama alivyowahi kusema mtoa mada mwingine katika warsha hiyo, Wolfgang Schimpf kutoka GTZ kwamba kukosekana kwa elimu ya utunzaji wa kemikali kutasababisha madhara makubwa na kwamba ipo haja ya kudhibiti hali hiyo.
Lakini akaonya kuwa si jambo sahihi kumwaga au kutupa kemikali hizo baharini kwani huko ni kuharibu maisha ya viumbe hai vinavyotegemea maji hayo.
Dawa kama DDT, Aldrin, Chlordane, Dieldrin, Endrin, Heptachlor, Hexachlobenzene (HCB) zimekuwa zikitishia uhai wa Afrika na kwa maana hiyo, ulazima wa kuwapa Waafrika elimu unabaki kuwa changamoto kwa wakazi wake.
Tangu miaka ya 1960 kumekuwa na kesi mbalimbali juu ya madhara ya matumizi ya kemikali katika uso wa dunia. Kwa mfano kati ya mwaka 1960-1963 katika mji wa Minamata nchini Japan, watu 1,714 waliathirika na Methyl Mercury kati ya hao 267 walifariki dunia.
Mwaka 1974 kulipuka mtambo wa kemikali kulisababisha kusambaa kwa cyclohexane katika eneo la Flixborough, England. Katika tukio hilo watu 28 walipoteza maisha. Kulipuka kwa mtambo wa nuklia Chernobly, nchini Ukraine mwaka 1986 kuliangamiza maisha ya watu 1,000.

Mikumi Sound ‘Wanatekenya’ walioiteka Moro

na mwandishi wetu

BAADA ya kufifia kwa bendi maarufu mkoani Morogoro kama Moro Jazz iliyotamba na marehemu Mbaraka Mwinshehe, mkoa huo ulibaki kama yatima katika masuala ya muziki.

Hii ilitokana na wadau kutotaka au kutokuwa na ari au uwezo wa kumiliki bendi za muziki wa dansi. Matokeo yake, burudani ya aina hiyo ikazidi kushamiri katika jiji la Dar es Salaam.

Lakini leo hii, Morogoro si yatima tena katika muziki wa dansi. Hilo linajihidhirisha baada ya kuibuka kwa bendi mpya ya Mikumi Sound iliyojikita mkoani humo kiasi cha mwaka mmoja uliopita.

Wiki iliyopita nimekuwa shuhuda wa makali ya bendi hiyo inayotumia mtindo wa Tekenya katika mapigo yake wakati ilipotumbuiza kwenye Ukumbi a VIP mjini Morogoro.

Umahiri wao jukwaani huwezi kuamiani kuwa bendi hii inaundwa na wanamuziki wenye usongo wa kujitangaza kimataifa.

Hao ni Sadiq Jakaya anayepiga gitaa la solo, Balely Mohamed anayevuma na gitaa la bass, Toto Site (kinanda), Abeid Said anayepiga drums huku Jose Kigenda ambaye ni rais wa bendi hiyo. Kuna washambuliaji wa jukwaa katika unenguaji hawa ni Monter Bige, Cool Mud, Dogoo Kaisi na Hamis Makata.

Kama ulikuwa ukiwaza kushabikia bendi za Kikongo, bila shaka nuna sababu tena ya kufanya hivyo kutokana na ukweli kwamba muziki wa Mikumi Sound ni kiboko yao. Hawatanii katika fani na wako makini. Wameshafyatua albamu mbili sasa nazo ni Cheo ni Dhamana yenye vibao sita na Mama Mkwe yenye nyimbo tano.

Rais wa bendi hiyo, Jose Kigenda katika mahojiamo maalumu anasema kuwa wanamuziki wake wamekuwa wabunifu kutokana na maelewano baina yao.

“Mikumi Sound si ya wababaishaji na tunawaomba mashabiki waelewe kuwa tumekuja kamili na tumeiva kimuziki,” anasema Kigenda na kuongeza:

“Tunajua mashabiki wanataka nini na hapa Morogoro tumegundua kuwa hawataki mambo ya kuwaiga Wakongo na ndio maana sisi tumeitikia wito kwa kuthamini utamaduni wa Mtanzania.

“Ndio maana kila siku nawaambia kuwa wanaodhani wamesimama kimuziki wakae chonjo, mwendo wetu ni wa taratibu lakini tuko makini sana,” anasema.

Mapema Juni mwaka huu, bendi hiyo iliandaa onyesho maalumu kuipongeza timu ya soka ya Moro United kwa kushika nafasi ya pili katika michuano ya Kombe la Kagame.

Katika onyesho hilo, bendi hiyo iliwapagawisha mashabiki wake kwa vibao kemkem kutoka kwenye albamu ya Mama Mkwe inayoundwa pia na nyimbo za Usiku wa
Deni, Dunia Duara, Mchumba Mwema na Afrika Tekenya
Twist.

Katika kuhakikisha kuwa inabeba mashabiki wengi zaidi, bendi hiyo imeshazuru mikoa mbalimbali nchini kujitangaza. Moja ya ziara iliyofana ni ile ya kuitangaza albamu yake Mama Mkwe.

Lakini hayo yote yasingewezekana kama sio ubavu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Mikumi Sound, Rena Vegula. Huyu kwa watu wengine wanaweza kumwita mwanamke wa shoka kutokana na kutokuwa na woga katika uendeshaji wa masuala ya maendeleo.

“Wazo la bendi lilianzia mjini Arusha mwaka 2003 na lengo hasa lilikuwa kuitangaza Mikumi kama mbuga nzuri Tanzania na ndio maana tukaamua kuipa jina hili,” anasema Rena mama wa watoto wanne; Abel, Erick, Peter na Aneth.

Wakati wazo hilo linaanza mwaka 2003, Rena alikuwa jijini Arusha akiendesha biashara zake. “Nina ukumbi wa starehe pale Arusha unaitwa Ricks Club sasa wakati ule bendi ya Olduvai ilikuwa ikipiga pale.

“Baadhi ya wanamuziki wetu wakawa wanaonyesha moyo wa kuendeleza muziki lakini vifaa hatukuwa navyo, ndipo tukaamua kununua vifaa vyetu.”

Alipoulizwa kama haoni kikwazo kuendesha bendi ya muziki wa dansi, Rena anasema kuwa haoni kikwazo kwa sababu dhamira yake ni kuona muziki wa Tanzania unakua na wanamuziki wake wanapata neema.

“Nikwambie kitu kwamba matarajio yetu ni makubwa sana hadi utashangaa,” anasema. “Mipango tuliyo nayo ni mizuri na tunasikilizana.”

Anasema kuwa hadi sasa, bendi hiyo inajiendesha na hakuna mzigo mkubwa sana kama hapo awali.

Kwa nini basi Mikumi Sound ikahamia Morogoro?

Rena anaeleza kuwa mwaka jana walipata nafasi ya kuiendesha hoteli ya Masuka Village iliyopo barabara ya Boma mjini Morogoro, kwa hiyo wakaamua kuihamishia bendi mjini hapo ili kuwa nayo karibu.

“Hapa tukaona nafasi nzuri ya kuikarabati bendi na hii ilitokana na kupokewa vizuri hapa Morogoro, mashabiki wanakubali na kuipenda kazi yetu.”

Lakini Rena ana msimamo ambao kwa hakika unajenga asili yetu kama Watanzania pale anaposema kuwa hatakubali kuwaajiri Wakongo kwenye bendi yake.

Anasema kimsingi kumwacha Mtanzania na kumwajiri Mkongo katika bendi ni dhambi kwani unamnyima mtu wako wa karibu mkate wa kila siku.

Anasema umefika wakati sasa kwa Watanzania kuthamini watu na vipaji vyao na kwamba hao wa nje hawana muujiza zaidi ya kwamba wanajituma katika kazi zao za muziki.

“Ndio maana ukiingia katika maonyesho yetu moja kwa moja unapata ladha ya muziki wetu na hatutaki kuiga,” anasema na kuongeza kuwa wanataka kuziba pengo la Mbaraka Mwinshehe.

“Tanzania kuna vipaji vingi mno katika muziki, ni suala la kuwaibua hawa wasanii na kila jambo linawezekana, hakuna sababu ya kuiga nyimbo za wanamuziki wa Kongo hii ni aibu kwa taifa.”

Ni mwanamke jasiri ambaye daima ulimi wake hulenga katika ari ya kuthubutu kutenda na kutekeleza masuala ya maendeleo na hilo amefanikiwa kutokana na malengo yake kukubalika pia kwa mumewe anayekwenda kwa jina la Henry Vegula.

“Mume ananielewa na hata watoto pia wanaelewa kwamba kazi ina manufaa kwetu sote,” anasema Rena.

Twawapima wakuu wetu kwa mizani ya pesa?

na innocent munyuku

MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini Tanzania Albert Motika maarufu kama Mr. Ebbo alipata kufyatua kibao ambacho wengi walikifurahia kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ni porojo zilizojaa kwenye wimbo huo uliopachikwa jina la Mnisamehe.

Katika wimbo huo, Mr. Ebbo anaeleza baadhi ya mambo ambayo kwa akili ya kawaida hayatekelezeki na kama yatatekelezwa basi itakuwa balaa. Kama pale anaposema angefurahi kuona magazeti yote yameandikwa kwa lugha ya Kimasai au mnada wa ng’ombe wa Pugu usogezwe hadi Mtaa wa Samora jijini Dar es Salaam.

Lakini msanii huyo anaendelea kuimba kwamba hata gari moshi zisiwe na honi kwenye safari zake na anaomba apande gari lisilo na breki. Kila anachosema mwisho wake humalizia kwa kutaka asamehewe kwa kauli yake hiyo. Bila shaka ujumbe ulishafika.

Nami kabla sijajikita katika msingi wa makala yangu hii leo naomba nisamehewe kwa hoja yangu kwamba tuzo kwa marais wa nchi iliyoandaliwa na tajiri Mohamed Ibrahim, kwa mtazamo wangu hailengi kufichua ama kuutokomeza ufisadi katika Afrika.

Kwa zaidi ya wiki mbili sasa, vyombo mbalimbali vya habari vimekuwa vikiandika kwa kina taarifa hiyo ya tajiri huyo anayependa kuitwa Mo Ibrahim ambaye asili yake ni nchini Sudan ingawa mwaka 1975 alipewa uraia wa Uingereza.

Tajiri huyo bila shaka kwa nia njema kama alivyoona katika dhamira yake ametangaza kuanzishwa kwa tuzo maalumu ya marais wa Afrika na kwamba rais atakayebainika kuwa anafuata misingi ya utawala bora na kuwawezesha raia wake kuwa na maisha mazuri basi atajinyakulia kitita cha dola za Marekani milioni 5 (zaidi ya shilingi bilioni 5 za Tanzania).

Lakini mshindi wa tuzo hiyo atakuwa pia akilipwa dola za Marekani 200, 000 (zaidi ya shilingi milioni 200) kila mwaka hadi ukomo wa maisha yake.

Binafsi niliposikia habari hizo nilijiuliza mambo mengi na baadaye nikaona si jambo jema kwa watawala wetu kupimwa uwezo wao wa kazi za kuwaongoza wananchi kwa mashindano na ahadi ya mamilioni ya pesa. Hapakuwa na haja hiyo na wala sioni kama umuhimu wa aina hiyo upo katika jamii zetu.

Hata hivyo, wakati naendelea kuwaza jambo hilo nikaikumbuka moja ya hotuba ya mtawala wa zamani wa Afrika Kusini P.W. Botha. Huyu ndiye mwasisi wa siasa za kibaguzi za rangi nchini humo aliyerejea kuzimu hivi karibuni akiwa na umri wa miaka 90. Botha katika moja ya hotuba yake alipata kusema kuwa njia rahisi ya kuziteka akili za mtu mweusi basi mpe mwanamke wa Kizungu na hapo atakupa siri zote.

Lakini Botha hakuishia kusema hayo, katika hotuba yake hiyo na hata katika mazungumzo yake ya kawaida mara kwa mara alisema njia nyingine ya kuuteka ubongo wa mtu Mweusi, mpe zawadi ya pesa na hapo atawajibika hata kama litakuwa suala la kumnyima usingizi.

Katika hilo, Botha hakumaanisha kuwa hakuna mwanadamu asiyependa pesa la hasha! Alichosema ni kuwa ni mazoea kwamba kwa mtu Mweusi hata jambo ambalo ni wajibu wake alifanye katika misingi fulani atapenda apewe ‘kitu kidogo’ ili aendelee kuwajibika. Kwamba anapopigwa ‘mjeledi’ wa pesa mambo hayaendi kombo.

Siku ile nilipoyafumbua macho yangu na kusoma habari kwamba kuna tuzo kwa ajili ya viongozi watakaoonekana kufuata utawala bora, nilipata mshangao kwamba iweje leo hii kuibuke na kitu kama hicho kwa watawala wetu. Nikasema ndani ya mtima wangu kuwa kumbe Botha pamoja na ufedhuli wake alilonena lina ukweli kiasi chake.

Je, urais sasa ni kama mashindano ya Miss World ambako warembo hujiandaa kuanzia ngazi za chini lengo likiwa ni kuibuka kinara kwa wengine? Au urais wa Afrika umekuwa kama michuano ya Klabu Bingwa Afrika?

Kwa ufahamu wangu, viongozi wengi barani Afrika wameingia madarakani kwa kupigiwa kura za ndiyo na wananchi. Hawakuvamia Ikulu na kwa maana hiyo kulikuwa na maandalizi ya uchaguzi kwa kampeni za kuwania nafasi hiyo, kampeni ambazo bila shaka ziliambatana na ahadi juu ya nini watawafanyia raia wao pindi watakapopata ridhaa ya kutawala.

Leo hii, linaibuka la kuibuka kwamba marais wapimwe utendaji wao na kisha wapewe pesa kama zawadi. Huku ni kupotoka! Hawa wamekuwa watoto kwamba hawaendi kuoga hadi wapewe ahadi ya peremende? Wamekuwa watumwa kwamba hawawezi kufanya kazi hadi wachapwe na mijeledi kwenye migongo yao?

Huyu Mo Ibrahim ambaye pia ni mwanzilishi wa Kampuni ya Simu za mkononi ya Celtel kama kweli ana nia ya kuwasaidia watu wake ndani ya Afrika, angeanzia nchini mwake alikozaliwa huko Sudan ambako hali si shwari katika Darfur. Angeanzia huko kama Waingereza wanavyoamini kuwa charity starts at home.

Nionavyo mimi, zawadi ya pesa kwa marais haiwezi kuijenga Afrika hata siku moja. Huo ndio mtazamo wangu na hicho ndicho ninachokiamini. Fisadi ni fisadi tu na hawezi kubadilika eti kwa sababu kaona pesa mbele yake. Kiongozi mwenye nia ya dhati huzaliwa na moyo wa aina hiyo na hujipanga kuwatumikia watu wake kwa haki hata kama itamlazimu kulala sehemu isiyo ya kifahari.

Ninachokiona ni kuudhalilisha utu kwa kigezo cha pesa. Kwamba kinachoonekana hapa si changamoto kama baadhi ya watu wanavyojaribu kuamini bali ni udhalilishaji kwa wakuu wa Afrika.

Kama nilivyodokeza hapo juu kuwa kigezo cha pesa kisiwe hoja ya msingi kuwapima watawala wetu. Mtu mwadilifu aliyepewa dhamana ya utawala wa nchi anatarajiwa kuwa mwenye kuumia na umaskini wa watu, mwadilifu sharti asilale usingizi pale anapoona raia wake wanakufa kwa magonjwa au njaa.

Mwadilifu anapaswa kutokuwa mwenye makuu kwa kujinufaisha yeye wakati raia wake wakikosa elimu na huduma nyingine muhimu za jamii. Lakini katika hili, mwadifu pia ni yule ambaye atafanya na kutimiza majukumu yake pasipo kuwekewa mfuko wa mamilioni ya dola za Marekani mbele yake. Huyu ndiye anayetufaa.

Wenye kuandaa utaratibu huo wamepanga zawadi hizo kwa hao watakaoonekana kuwa watawala bora lakini je, na hao marais wazandiki na wadhalimu watapewa adhabu na nani? Bila shaka kuna mahala mpango huu utakwenda upogo.

Hivi kweli palikuwa na umuhimu wa kuanzisha tuzo hizi kwa wakati huu? Waandaaji hawakuona kuwa upo umuhimu wa kuwajengea mazingira mazuri raia wa kawaida kabisa ambao wamekuwa wakipata wakati mgumu kukabiliana na maisha ya kila siku?

Au tuseme kwamba yale yaliyopatwa kunenwa na Manabii kwamba mwenye nacho huongezewa yanaendelea kutimia? Rais wa nchi awaye yote anapostaafu hupewa mafao yanayomwezesha kuwa na maisha bora kwa kipindi kirefu lakini si mwananchi wa kawaida.

I wapi basi mipango ya kuwakomboa Waafrika kama mambo yenyewe ni haya? Zumari la kuwakataza hao wanaojifanya kuwa wanaidai Afrika madeni makubwa mbona halipigwi tena? Badala yake twaibuka na mambo ambayo kwa mtazamo binafsi hauna jema katika maendeleo ya Afrika zaidi ya kuwadhalilisha watawala wetu.

Sina hakika na akiba ya Mo Ibrahim katika akaunti zake za benki, lakini kama nilingelijua ningelimshauri jambo moja nalo ni kujenga shule za aina mbalimbali ndani ya bara hilo ili kufuta ujinga kwa mamilioni ya watu barani humo.

Lakini pia angeweza kujenga misingi ya kuwainua Waafrika moja kwa moja kwa kuanzisha kampuni ambazo zitatoa ajira kama alivyofanikiwa katika Celtel ambayo kwa sasa imeuzwa kwa wawekezaji wa Kuwait. Hili la kuwashindanisha wakuu wetu wa nchi kwa ahadi ya pesa kamwe sikubaliano nalo. Naomba kutofautiana!

munyuku@gmail.com

0754 471 920

Tuchangie harusi hadi lini?

na innocent munyuku

KIASI cha miaka miwili nyuma, rafiki yangu wa karibu alipata kuniambia namna alivyojijengea ukuta mgumu dhidi ya ndugu, jamaa na marafiki baada ya kuweka wazi msimamo wake juu ya kutochangia harusi.

Katika simulizi zake, jamaa huyo akanieleza kuwa ilifika mahala akashindwa kuchangia pesa kwa ajili ya harusi kwa vile aliangalia hesabu ya bajeti yake kwa mwezi, akakuta anatumia kiasi kikubwa cha pesa katika kuchangia harusi badala ya mambo mengine ambayo anaamini ni ya msingi zaidi.

Akatoa mfano kwamba kama kila mwezi watu sita wanaoa au kuolewa na kila mmoja atamchangia Sh 20,000 ina maana kila mwezi atenge Sh 120,000. Hivyo basi kwa mwaka mzima itamgharimu Sh 1,440,000. Hiyo ilikuwa miaka miwili iliyopita na kuna uwezekano mkubwa gharama kwa ajili ya shughuli hizo zimepanda.

Nimelazimika kuandika makala hii kutokana na kuguswa na hali halisi ya maisha ya Mtanzania wa kawaida na ukweli kwamba, kila siku michango ya harusi imeendelea kushamiri miongoni mwetu.

Kwamba kwa vile gharama ya maisha imepanda kwa kiwango kikubwa ni heri tukaangalia maeneo muhimu ya kuchangia ili kuleta tija kwa kila Mtanzania. Nasema hivyo kwa sababu dhamira yangu inanituma kuamini kuwa, michango mikubwa katika harusi haina neema kwa wahusika. Kama kuna wanaonufaika katika michango hiyo ni wachache na kwa muda mfupi.

Imebainika kuwa, michango mingi hasa ya pesa huishia kwa waliochangia na si kwa maharusi. Kwamba fedha zinazokusanywa hatimaye huishia kwenye matumbo ya waliochanga kwa kunywa na kula siku ya harusi na baadaye kile kinachoitwa kuvunja kamati.

Binafsi ningeunga mkono kuendelea kwa michango hiyo kama pesa zingewanufaisha moja kwa moja maharusi. Kwa mfano zimepatikana shilingi milioni nne basi wapewe maharusi kwa ajili ya kuendelea na maisha yao.

Ya nini basi tuchangishane mamilioni ya pesa halafu tuzitumbue pesa hizo kwa kunywa bia na kula pilau? Kuna maana gani basi kuwaona maharusi baada ya siku chache wanalia njaa kwa sababu pesa zimeshatumika kukamilisha sherehe ya wao kuungana katika ndoa? Ni heri tubadilike sasa kwani huko tuendako siko.

Nitatetea hoja yangu hii kwa msingi mkuu mmoja nao ni kuwa, naamini wanaojiandaa kufunga ndoa kwa mujibu wa sheria wamefikisha umri wa kufanya hivyo na wanapojiandaa katika muungano huo wa hiari wawili hao wameshaweka maandalizi ya maisha yao mapya.

Kwa maana hiyo, katika mazingira kama hayo ni jambo lililo wazi kuwa wanaooana lazima watakuwa kwenye nafasi ya kukabiliana na majukumu ya ndoa ikiwa ni pamoja na maisha ya kila siku. Wanachotakiwa ni kujiandaa kama afanyanyo mwanafunzi darasani kukabiliana na mitihani yake.

Si mara moja au mbili, kumekuwa na matukio ya kuchefua roho baada ya kumalizika kwa harusi. Utasikia bwana na bibi harusi wanakabiliwa na madeni yaliyotakana na ‘kuzidi kwa bajeti’ ya harusi yao. Wanabaki kukuna vichwa wasijue watalizipaje pesa hizo. Huu si uungwana!

Kwa hakika si uungwana na ndio maana napiga zumari hili lenye sauti ya kupinga kuchangishana pesa kwa ajili ya harusi na baadaye kuzitumia pesa hizo kwa ajili ya kushibisha matumbo na kuwaacha wanandoa ambao ni wahusika wakuu wa shughuli hiyo wakienda nyumbani mikono mitupu.

Kama kweli tuna mapenzi ya dhati na maharusi kwa nini basi pesa zinazochanganywa wasipewe ili wajue nini cha kufanya mara baada ya kutoka kwa kasisi au sheikh? Huu ni muda wa kubadilika, matarumbeta na kukodi kumbi za kifahari tuwaachie wengine ambao wana uwezo wa kutenda pasipo kutembeza bakuli.

Badala yake tuchangie katika masuala mengine ambayo naamini kuwa ni muhimu kuliko hili la kuchangishana ili watu wapate kushiba kwenye harusi. Tulipe mgongo suala la harusi na tuangalie maeneo mengine kama elimu au afya.

Kuna mifano hai kwamba, wapo watu walioshindwa kuendelea na masomo kwa sababu tu hawana pesa za kuwawezesha kusonga mbele. Hao wamejaa kwenye ardhi ya Tanzania. Wamefumbiwa macho kwa sababu dhamira za walio wengi ni kutoa pesa ambayo baada ya mwezi mmoja ataitumia kwa kunywa bia na kutafuna vipapatio vya kuku.

Jaribu leo kuitisha kikao kwamba unataka kujiendeleza shule na unahitaji kuchangiwa pesa kwa ajili ya kukidhi gharama za masomo. Hata marafiki zako wa karibu wanaweza kukupiga chenga. Naam watapiga chenga kwa sababu huo utamaduni ni mpya katika mioyo yao. Wamezoea kuchanga ili siku chache baadaye wazirejeshe pesa hizo kwa faida yao. Hawaangalii matokeo mema yanayolengwa kuja kwa miaka walau minne ijayo.

Naamini kabisa kuwa pesa zinazotumika katika kufanikisha harusi zingewasaidia wahitaji wengine kama wagonjwa waliolazwa hospitalini. Inawezekana wakajitokeza wengine wakadai kuwa hilo ni jukumu la Serikali. Huko ni kupotoka, kwani kama tuna ubavu wa kufanya harusi za kifahari kwa kuchangishana pesa kwanini tushindwe kuwasaidia watu wengine katika masuala muhimu?

Leo hii nikiamua kwenda kanisani kufunga ndoa na kisha kuingia kwenye banda langu la uani na mke wangu bado nitakuwa na amani kwamba jambo la msingi limeshafanyika nalo ni uhalali wa ndoa hiyo mbele ya kasisi na baraka kutoka kwa mashuhuda wanaotambulika kwa mujibu wa sheria. Sitakuwa na kinyongo bali furaha tele moyoni.

Watanzania tumekuwa wepesi wa kuiga mengi kutoka Ulaya na Marekani kwanini basi utaratibu wa ndoa za ‘kimya kimya’ nao tusiige kutoka kwao? Kwamba huko ughaibuni mtu anajikuna anapofikia na kufanikisha harusi yake na wala hana haja ya kulia shida kwa wengine. La maana ni cheti cha ndoa kwa mujibu wa sheria zilizopo.

Raila kapiga zumari Kenya, tulicheze Tanzania

na innocent munyuku

WANASEMA uzee ni dalili ya hekima lakini pamoja na ukweli huo uzee hauhalalishi kuziba vipaji au mianya ya wengine kuonyesha uwezo wao katika masuala mbalimbali yahusuyo jamii. Basi tuseme pia katika hili uzee waweza kutumika kama mwongozo au mifano sahihi kwa ustawi wa jamii.

Katika hilo ndio maana hadi hii leo kwa baadhi ya kaya huwatumia wazee katika kufanya suluhisho kwenye eneo husika hasa kama kutatokea kutokuelewana baina yao. Pengine kutokana na hilo inawezekana wengine wakadiriki kusema kuwa ukubwa ni jalala.

Lakini katika nyanja za siasa hasa barani Afrika hali ni tofauti. Wazee wameonyesha njia mbaya kwa kung’ang’ania madaraka na huu kwa mtazamo wa kawaida kabisa ni ishara na mwongozo usiofaa kwa vijana wanaochipukia katika siasa na hata waliosimama kabisa.

Nimeamua kuandika haya kwa kusimamia hoja ya Mbunge wa Jimbo la Lang’ata nchini Kenya, Raila Odinga aliyependekeza hivi karibuni kuwa ni vema wanasiasa wa nchini mwake ambao wamekuwa madarakani kwa muda mrefu waachie ngazi na kupisha damu changa.

Odinga alisema kuwa anashangaa kuwaona wanasiasa wa jinsi hiyo ambao hadi hii leo wangali wakishika utawala tangu enzi ya marehemu baba yake Jaramongi Oginga Odinga.

Ingawa Odinga alikuwa akiyasema hayo kukipigia debe chama chake cha Orange for Democratic Movement-Kenya (ODM-K), maneno yake yalitosha kuwa changamoto kwa ajili ya kujenga vyama vyenye damu mpya na mawazo mapya katika siasa.

Nchini humo kwa mfano, Makamu wa Rais Moody Awori ana umri wa miaka 79, huku kukiwa na mawaziri wengine wenye umri mkubwa kama yeye akiwemo Njenga Karume (80), Simone Nyachae (75) na John Michuki (74).

Kimsingi hoja ya Raila si ya kuachwa ipite hivi hivi pasipo kuungwa mkono na katika hili ndio maana nasema kuwa mwanasiasa huyo machachari amelenga sehemu husika kutokana na ukweli kwamba sehemu mbalimbali barani Afrika lina tatizo kama hilo.

Tanzania kama ilivyo Kenya pia ina wanasiasa ambao leo hii wana rekodi ya kubakia katika ulingo huo huku wakiziba ya damu changa zisiweze kuonyesha upeo wao katika nyanya mbalimbali. Hao wamejaa tele na ni kama wamepigiliwa misumari.

Ndani ya Tanzania wapo wanasiasa ambao tangu wengine hatujazaliwa wapo katika ulingo huo wakiendesha maisha yao kwa mgongo wa siasa na hadi hii wangali madarakani kama vile hakuna Mtanzania kijana mwenye uwezo wa kuyatenda hayo ayatendayo huyo aliyeko madarakani.

Naungana na Raila kusema kuwa hii ni dalili mbaya kwa mustakabali wa taifa letu kwani ukweli ni kwamba wanasiasa wa aina hii hawana jipya katika mioyo yao. Hawana jipya la kutueleza, wamebaki na mbinu za kale ambazo kwa nyakati hizi hatuwezi kukubaliana nazo.

Kwamba hawana fikra pevu tena, vichwa vyao pamoja na kwamba wanaweza kuwa na hekima, hawana jema la kuwafundisha wengine. Ni heri kwao wakakubali mabadiliko kuliko kung’ang’ania siasa. Huu uwe wakati wa kuwafundisha wengine. Na kufundisha kuzuri ni kwa kumpisha mwanafunzi kitini na kumwelekeza namna ya kuliongoza jahazi.

Kama wanasiasa wa jinsi hii wameshindwa kuleta maendeleo au kuishauri Serikali husika kwa kipindi cha miaka 20 au 30 leo hii watakuwa na miujiza gani katika kulisukuma gurudumu mbele gurudumu la maendeleo na tija halisi kwa Watanzania?

Hawa wazee wa siasa wana jipya gani leo hii? Watasimama waseme kitu ambacho kwa wakati huu watu watakubali kuwa wanachokinena ndicho sahihi? Lakini hakuna shaka kwamba salamu wamezipata wakati ule wa kampeni za Uchaguzi Mkuu mwaka jana. Baadhi yao nasikia walizomewa na wakalazimika kushuka jukwaani wakiwa wamevaa sura za aibu.

Hivi kwani ni lazima wote wawe wanasiasa? Kwanini wengine wasibaki pembeni na kuangalia vichwa vingine vikiongoza jahazi? Bila shaka zumari la Raila lafaa lisikizwe kwa makini na lichezwe hapa kwenye ardhi yetu ya Tanzania. Tusipuuze kwani alichokisema nchini Kenya ndicho kilichopo hapa kwetu.

Sileti siasa za kibaguzi lakini kwa mtazamo, ufike wakati wazee wakubali mabadiliko si kwa kuwapiga watoto wao (wa damu) bali pia kuwapa nafasi wengine wajaribu kujiwekea rekodi zao. Ninachotarajia kwa muda huu ni hawa wazee wajenge vitalu bora kwa kuwapika vijana kisiasa badala ya kuwawekea vizingiti ambavyo kimsingi vinaliangamiza taifa.

Kwamba wakati huu uwe mwafaka kwa Watanzania kujifunza kutokana na changamoto ya kina Raila na kundi lake. Kwani hawa vijana wasipojifunza leo watapata wapi nafasi hiyo? Wasipojaribu leo watajaribu lini?

Tusione aibu kuwapisha vijana waonyeshe walichonacho kwenye vichwa vyao na kama watateleza huo utakuwa muda mwafaka kuwarekebisha na kuwaelekeza wapite wapi na watufikishe wapi. Kuwabana ni kuwanyima haki yao na huu si utaratibu mzuri wa kukuza maendeleo. Tuwape nafasi hii leo.

Niseme pia kuwa hatujachelewa kufikia kuwapa vijana nafasi. Ni suala la maandalizi ambayo yakianza sasa bila shaka katika Uchaguzi Mkuu ujao wazee watakubali kukaa pembeni na kuwapisha vijana waendelee kukimbiza kijiti cha maendeleo.

Hakika tusione aibu kabisa kuanza kulicheza zumari la Raila. Huo ndio uungwana, kubalini mabadiliko mapema ili heshima yenu isipotee.

munyuku@gmail.com

0754 471 920

Zurry Chuchu umetuokoa wengi

na innocent munyuku
KATIKA maisha ya binadamu wapo majasiri na kundi jingine la watu wenye hofu huku wengine wakibaki kuwa ÔvuguvuguÕ hawajulikani wako upande upi.
Ujasiri ninaomaanisha hapa ni ule wa kusema jambo bila kigugumizi kama alivyofanya mwimbaji Easter Bugado maarufu kama Zurry Chuchu.
Wiki iliyopita nilisoma gazetini habari ya mwanadada huyo kwamba amejitangaza kuwa mwenye virusi vya ugonjwa wa ukimwi.
Kauli yake hiyo ilinivuta na sikuona kama nitakuwa natenda haki kwa kuiacha habari hiyo itokee sikio la pili bila ya kumpa salamu za pongezi msanii huyo.
Naam anastahili pongezi kwa kuwa amekuwa wazi kusema ana virusi vya ukimwi tofauti na wasanii wengine na hata watu wengine katika nyanja mbalimbali.
Uwazi wa Zurry ni wa kuigwa kwani kwa kujiweka wazi kiasi hicho, atakuwa anaokoa maisha ya watu wengi katika jamii inayomzunguka.
Kauli ya msanii huyo inanifanya nimkumbuke Mkurugenzi wa TOT Plus, Kapteni John Komba ambaye Mei 28 mwaka 2002 alisema kuwa baadhi ya wasanii wake wamefariki kwa ugonjwa wa ukimwi.
Kapteni Komba alitoa kauli hiyo mjini Bagamoyo katika risala yake baada ya kundi hilo kuhitimu mafunzo ya sanaa katika Chuo cha Sanaa cha Bagamoyo.
ÒKatika kipindi cha miaka 10 ya uhai wa TOT zaidi ya wasanii 15 wamefariki kwa ukimwi,Ó alisema Kapteni Komba wakati huo.
Nilimwona kuwa shujaa anayestahili kuigwa kwa kuthubutu kwake kuvunja ukimya.
Komba aliitoa kauli hiyo mbele ya mgeni rasmi William Lukuvi wakati huo akiwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu.
Lukuvi ambaye alikuwa akimwakilisha aliyekuwa Waziri Mkuu Frederick Sumaye aliposimama na kutoa hotuba yake alisisitiza kuwa lazima wasanii wawe mstari wa mbele kuupiga vita ukimwi.
Ninapoyatafakari hayo narejea kumwona Zurry kuwa msanii anayepaswa kuigwa kwani kufanya hivyo kutasaidia kupunguza maambukizi.
Tuwe wazi kusema kama tumeathirika ili kuwasaidia wengine ambao hawajaathirika. Tusione aibu kujitangaza na huu uwe utaratibu wa kudumu.
Kukaa kimya na kuufanya ukimwi kuwa ugonjwa wa siri ni kuendeleza maambukizi ambayo yangeweza kuepukika.
Tuseme ili wengine wajihadhari na kuacha tamaa ya kufanya mapenzi. Ni nani leo hii atasimama na kuomba tendo la ngono kwa mtu ambaye ameshajitangaza kuishi na virusi vya ukimwi?
Licha ya kwamba kila mmoja anayo nafasi ya kuushambulia ukimwi, si vibaya tukaanza kujiweka wazi kama alivyofanya Zurry.
Hata hivyo, bado ipo haja ya kuyakumbuka maneno ya Lukuvi kwamba wasanii wawe mstari wa mbele kutunga nyimbo za kuielimisha jamii kuhusu ugonjwa huo.
Tuache habari ya kusifia wanawake wazuri au kusifia pombe kama wafanyavyo baadhi ya wasanii wa muziki wa kizazi kipya maarufu kama bongofleva.
Tujiweke kando na malumbano na majungu katika vikundi vya sanaa na badala yake muda huo tuutumie kuwapa somo raia wengine juu ya kuepukana na janga la ukimwi.
Ya nini kuimba juu ya mavazi mazuri au mambo mengine yasiyofaa wakati ndugu zetu wanaangamia?
Kuna raha gani kukata mauno jukwaani na vivazi vya aibu wakati kuna maelfu wanakufa kwa sababu pengine walikosa elimu juu ya ugonjwa huo?
Wasanii simameni sasa na kuwakemea wasiotaka mabadiliko. Hakuna kulala kwani vita hii ni pana.
Tumieni vipaji vyenu kuliokoa taifa linalozidi kuandamwa na watu wasiokuwa tayari kuacha tabia chafu zinazozidi kuufanya ukimwi ukithiri.
Alichofanya Zurry ni cha kuungwa mkono na ni heri kumwona kama shujaa aliye tayari kuwaokoa watu wake.
Kamwe asitengwe Zurry, asilani! Asibaguliwe kwa kunena ukweli. Pia asiandamwe kwa ÔvijembeÕ na badala yake tufuate moyo wake wa kishujaa wa kujitangaza kwa uwazi.
munyuku@gmail.com

0754 471 920

Zemkala: Vichwa sita vyenye upeo wa juu

Na Innocent Munyuku

UZOEFU unaonyesha kuwa watu wengi waliotimiza ndoto zao katika maisha hawakuwa na shaka na wanachowazia. Walijipanga na kuhakikisha kuwa mipangilio yao ya maisha inakuwa kama walivyokusudia. Lije jua au mvua.

Hivyo ndivyo ilivyo kwa wasanii wa ngoma na nyimbo za asili ya Tanzania wanaojulikana kama Zemkala. Ni kundi linaloundwa na wasanii sita ambao bado umri wao haujavuka miaka 30. Wangali na damu mbichi katika kueneza mila na utamaduni wa Mtanzania katika nchi mbalimbali duniani.

Wanaounda kundi hilo ni Yuster Nyakachara, Havintishi Baraza, Fadhili Mkenda, Yusuf Chambuso, Maulid Mastir na Kasembe Ungani.

Kwa mujibu wa kiongozi wa kundi hilo, Yusta Nyakachara, walianza kupata uhai mwaka 2002, waanzilishi wakiwa Ungani na Mkenda ambao walijieungua kutoka katika kundi lililowahi kuvuma wakati la Sisi Tambala. Wasanii wengine walijumuika na Zemkala wakitokea Splendid Theatre.

Katika miaka minne ya uhai wa kundi hilo, Zemkala imefanya mambo mengi ndani na nje ya nchi kwa kulitangaza taifa katika maonyesho ya sanaa kila lilipopata nafasi ya kufanya hivyo.

Cha kufurahisha kuhusu wasanii hawa ni kwamba si rahisi kujua kama wamepeana majukumu tofauti jukwaani. Hawana mzaha wawapo katika pilikapilika za kuleta burudani huku kila mmoja akijaribu ‘kuivaa’ kazi ya msanii mwingine.

Chambuso ni hodari katika kupiga ngoma nane, lakini usishangae kumwona akiziacha ngoma hizo na kujiunga na wachezaji ambao ni Yusta na Havintishi ambao ni mahiri katika kulishambilia jukwaa.

Si Chambuso tu mwenye hulka hiyo, Mastir ambaye ni kiboko ya njia katika kupiga marimba, hasiti kuacha marimba hayo na kuwavaa mashabiki akiwaonyesha uwezo wake mwingine wa kucheza na kuruka sarakasi na baadaye atamweka pembeni Chambuso naye kuanza kupiga ngoma tena kwa ustadi mkubwa kabisa. Wakati huo filimbi yake inakwenda pamoja na mirindimo ya drums kutoka kwa Mkenda.

Lakini uhondo huo unakuwa haujakamilika pasipo kumhusisha Ungani. Huyu ni kinara katika kupiga ngoma ndogo maarufu kama jembe. Mara chache utamwona akicheza lakini uso wake wa tabasamu na umakini utakufanya mara kwa mara kuangalia namna anavyokwenda vyema na wapigaji wa vyombo vingine.

Tangu kuundwa kwa kundi hilo, wameshazuru Sweden, Msumbiji, Kenya na Zanzibar katika kufanya maonyesho mbalimbali kupitia matamasha ya sanaa. Huko kote wameacha sifa njema na kujizolea mashabiki lukuki.

Unapowauliza katika maonyesho hayo ni lipi ambalo wanalikumbuka zaidi hawasiti kulitaja onyesho la mjini Kisumu kiasi cha miaka miwili iliyopita. Kwa nini wanalikumbuka? Swali kama hilo linawafanya wote waangue kicheko kinachofuatiwa na maelezo kutoka kwa Yusta.

“Kule katika siku ya kwanza ya maonyesho yetu tulipata wakati mgumu sana. Unabadilisha nguo hapo ili uvae za kuingilia jukwaani unasikia mtu pembeni yako akisema ‘cheki hiyo bonge ya raba lazima tutoke nayo.

“Sasa katika mazingira hayo unapanda jukwaani pasipo umakini, kwani unawaza kuibiwa viatu au vifaa vingine,” anasema Yusta.

Lakini baada ya kulalamika kwa waandaaji wa shughuli hiyo mambo yakabadilika siku iliyofuata. “Hata hivyo, bado ikawa adhabu kwetu…ni sawa tulipewa ulinzi wa kutosha lakini shughuli ilikuwa pevu,” anakumbuka Mastir.

Kwamba kwa vile onyesho lao lililotangulia walivipiku vikundi vingine kutoka nchi nyingine, walijikuta wakiwa na mashabiki wengi ambao kila walipopanda jukwaani walilazimisha waendelee kutoa burudani pasipo kupumzika.

“Kwa hakika ilikuwa hali ngumu na kama tusingekuwa na mazeozi ya kutosha hali ingekuwa mbaya sana, unacheza jukwaani kwa dakika 60 lengo likiwa kumaliza kiu ya watazamaji wako,” anasema Yusta.

Mbali na ushujaa wao jukwaani, Zemkala wamepikwa katika msimamo wa kulinda na kujivunia utamaduni wa Mtanzania na Mwafrika kwa ujumla. Maneno yao yamejawa na hamasa kama ya Dk. J Aggrey ambaye anasifika sehemu nyingi duniani kwa kujivunia ngozi yake nyeusi.

Dk. Aggrey alipata kukaririwa akisema kuwa kama angelikwenda mbinguni na Mungu angelimwuliza kama anataka kurejea duniani kama mtu mweupe angeligoma. Na kwamba kama angeulizwa kwa nini hataki kurudi kama mtu mweupe, angesema bado ana kibarua cha kufanya kama mtu mweusi na anajivunia rangi hiyo na kwamba kama kuna asiyejivunia rangi yake basi huyo hastahili kuwa na pumzi ya uzima.

Unaweza kuwataja Zemkala kuwa ni wasanii wasio na aibu kutangaza ngoma za asili ya Tanzania. Wamefanikiwa kuchanganya ngoma za makabila tofauti katika maonyesho yao kote walikopata nafasi ya kufanya hivyo.

Lengo ni kwamba ifike siku Tanzania ijulikane kupitia ngoma zake kama walivyofanikiwa Wakongo au mataifa ya Afrika Magharibi.

Wanashangaa kuona hadi hii leo baadhi ya Watanzania hasa vijana wanakataa kucheza ngoma za asili na badala yake kukimbilia disko na kuiga utamaduni wa Kimagharibi.

“Huu ni msimamo wetu kwamba lazima tuitangaze Tanzania kwa kutumia ngoma na nyimbo zetu,” anasema Yusta. “Lazima nia iwepo na wengine naamini watafuata nyayo zetu katika kujivunia mambo yetu ya asili.”

Katika jitihada zao hizo za kuing’arisha Tanzania kimataifa, wameshaanza kupenya kibiashara katika bara la Ulaya na Marekani Kaskazini.

Meneja wa Zemkala, Jotham ‘Gota’ Warioba, amekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa kundi hilo linasonga mbele kwa hali na mali.

Amelidokeza gazeti hili kuwa ameshaanza mazungumzo na kampuni moja ya inayojishughulisha na usambazaji wa muziki nchini Ujerumani ili kuingia nayo mkataba wa kibiashara.

Kampuni hiyo ina matawi sehemu mbalimbali barani Ulaya na kusambaa hadi Marekani Kaskazini. Hata hivyo, hakuwa tayari kuitaja kwa vile kuna mambo ya msingi wanayotakiwa kuwekana sawa kabla ya kuutangazia umma.

“Wameonyesha nia ya dhati kujumuika nasi na sisiti kusema kuwa hii ni njia mojawapo kuelekea katika mafanikio ya Zemkala,” alisema Gota.

Pamoja na hayo, Gota aliongeza kuwa anaweka mkakati wa kulifanya kundi lake hilo liwe na maonyesho ya ndani ya nchi badala ya kuwaburudisha watu wa nje pekee.

“Tanzania hakuna utamaduni wa kupenda kuangalia ngoma za asili, wamezoea dansi au disko lakini sisi tunadhani upo umuhimu wa kuwa na show (onyesho) walau mara moja kila wiki hapa kwetu ili watu waone uzuri wake…wasikimbilie kwingine.”

Zemkala hujikita katika mazoezi kila Jumatatu, Jumatano na Ijumaa kuanzia asubuhi hadi mchana katika Ukumbi wa Utamaduni wa Russia uliopo Sea View jijini Dar es Salaam.

munyuku@gmail.com
+255 471 920

Tuwapongeze wabunge wa upinzani kwa lipi?-Dk Mvungi

na innocent munyuku

ALIYEKUWA mgombea urais katika Uchaguzi Mkuu wa Rais na wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa tiketi ya NCCR-Mageuzi mwaka jana, Dk. Edmund Sengondo Mvungi amesema chama chake hakikuona sababu ya kuandamana kuwapongeza wabunge wa upinzani waliomaliza Bunge la Bajeti kwa kuwa hakuna ujasiri wowote waliouonyesha.

Dk. Mvungi alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita katika mahojiano maalum na Rai, kwenye Makao Makuu ya NCCR-Mageuzi Mtaa wa Kilosa, Ilala jijini Dar es Salaam.

“Tuwapongeze hawa kwa ushujaa upi? Tunawapongeza kwa lipi kubwa?,”alihoji Mvungi na kuongeza:

“Kwangu mimi wamekuwa kati ya watu waliopitisha bajeti ambayo ilikuwa ya hovyo kabisa…angalia suala la mikopo kwa elimu ya juu, kwa nini ukubali vipitishwe vigezo vya kukopeshwa kwa madaraja? Hawa watoto wengine watakwenda wapi?”.

Alhamisi iliyopita vyama vya Upinzani vilifanya maandamano jijini Dar es Salaam na baadaye kufanya mkutano wa hadhara kwenye viwanja vya Jangwani baada ya kuwapokea wabunge wa kambi hiyo waliotokea mjini Dodoma kuhudhuria Bunge la Bajeti.

Akizungumzia upinzani nchini, Dk. Mvungi amesema vyama vingi vya upinzani havisemi lugha moja katika mageuzi halisi kwa Watanzania.

Alisema tatizo la upande wa upinzani ni kwamba viongozi wengi wanakuwa na ndoto ya kwenda Ikulu moja kwa moja bila kuweka wazi nini kinawapeleka huko.

“Mnakaa mnajadiliana kwamba hivi tukikuachia nafasi utawafanyia nini wananchi, una malengo gani utasikia mmoja akisema ahh acha tu tutajua huko huko nikifika.

“Huu si utaratibu mzuri, lazima tuelezwe kwamba wananchi utawafanyia nini na wewe mwenyewe umejiandaa vipi kutekeleza unayoahidi,” alisema na kuongeza:

“Binafsi sikuzunguka Tanzania nzima wakati wa kampeni kwa lengo la kuwa katika historia ya nchi kwamba niliwahi kuwa rais. Hapana. Nilizunguka ili kuwapa raia fikra juu ya nini Watanzania tunatakiwa tuwe.

“Ndio maana nasema hivi kwanza tukae tuambizane, tuaminiane halafu twende mbele. Mageuzi si ya Mvungi tu bali ni yetu sote.”

Akizungumza mafanikio katika miezi takribani minane ya uongozi mpya wa awamu ya nne, Dk. Mvungi anasema hawezi kusema kuwa kuna mafanikio makubwa.

“Jambo jema ninaloweza kusema ni kwamba tumebaki na amani ile ile tuliyoizoea Watanzania. Lakini kwa kweli matumaini katika huduma ya jamii hakuna, hali ni mbaya.

“Tulipoamua kufanya uchaguzi tulitegemea mabadiliko ya maisha ya watu na hatuchagui serikali itupeleke nyuma, bali mbele kimaendeleo.

“Lakini hofu yangu pia ni kuwa huenda kuna waliokwenda kuwachagua watu ili nao waendelee kunufaika na ulaji.”

Pamoja na hayo Dk. Mvungi anasema katika uchaguzi uliopita Chama Cha Mapinduzi kilifanya mapinduzi makubwa ndani ya chama. Mapinduzi ambayo kama yanalenga dhamira njema yanaweza kuisaidia Tanzania.

“Ndiyo kulikuwa na mapinduzi makubwa ndani ya CCM, hawa waliofanya mapinduzi walikuwa makini sana. Hawa ndio wanaojiita ‘wanamtandao’.

“CCM imebadilika, watu wapya kabisa wenye matamanio mapya na ndio maana nasema mchakato wa CCM haukuwa wa kizembe na wala halikuwa jambo dogo lililofanywa na wanamtandao.

“Lakini mimi nasema hawa wanamtandao wana lengo ambalo bila shaka ni kula na bila shaka zile bilioni 21 zilizotengwa kwa ajili ya kusambazwa mikoani zitawanufaisha hawa watu.

“Wanamtandao ni wengi, Rais kishachagua baraza la mawiziri, wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya sasa wengine waliobaki watapewa nini? Bila shaka ni hizi pesa za kifuta machozi.”

Alisema katika mfumo huu wa chama dola, ni CCM ndicho kitakachoamua nani apewe pesa hizo. “Nafikiri wanajipanga hivyo.”

munyuku@gmail.com
+255 754 471 920

Profesa Ishengoma: Si lazima wote twende bungeni

na innocent munyuku
NI asubuhi ya saa mbili na nusu hivi. Jumamosi iliyotulia, siku ambayo nimejaa shauku ya kukutana na msomi aliyebobea katika masuala ya kilimo lakini akaamua kuwania nafasi ya chini katika siasa.
Huyu si mwingine bali ni Profesa Romanus Ishengoma (54), Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine Morogoro ambaye hivi karibuni iliyopita amefanya mahojiano maalumu na RAI na kutoboa kisa cha yeye kujiingiza katika siasa akiwania nafasi ya chini kabisa.
Akiwa amevalia vazi la kaptula na shati la bluu ananifuata katika lango kuu la kuingilia nyumbani kwake eneo la Falkland mjini Morogoro. Ananikaribisha baada ya utambulisho mfupi. Ni mwingi wa mazungumzo lakini kila anachozungumza hasiti kukitolea mifano na wakati mwingine kukushirikisha katika mazungumzo kwa kuuliza maswali.
ÒUnaujua huu ni mti gani?Ó ananiuliza akinionyesha mti mmojawapo unaopendezesha nyumba yake iliyozungukwa na mti. Mti huo anaouliza ni wa aina ya cacao ambao kwa mazoea haulimwi nchini Tanzania.
Lakini baadaye ananieleza kuwa anaelewa fika kwamba si kwenda kuangalia miti aliyoipanda na hivyo ananipisha niendelee na kiini cha safari yangu.
Nami bila kusita namjibu kwamba kilichonileta ni habari ya miti pia kwa hiyo hana haja ya kuacha kuzungumzia suala la mazingira. Tunashirikiana kicheko na kuketi katika viti nje ya nyumba yake.
Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana, wengi hawakuelewa pale waliposoma kwenye magazeti au kupata habari kupitia vyombo vingine kwamba Profesa wa Chuo Kikuu anawania nafasi ya udiwani wa Kata ya Mbuyuni mjini Morogoro.
Prof. Ishengoma analielezea jambo hilo kuwa ni msimamo wake katika maisha.
ÒSiwezi kuwa driven (kuendeshwa) na mkumbo, na hii ni kwa sababu nina elimu ambayo ndio msingi mkubwa wa maisha.
ÒKusema tu kwamba mimi ni profesa haitoshi, mchango wangu ni nini katika jamiiÉmaendeleo daima huanzia katika grass roots na huu ndio mchango,Ó anasema na kisha kuongeza:
ÒKwa hiyo unapozungumzia udiwani unazungumzia msingi wa mambo mengi ya jamii, na labda niwakumbushe wanaonishangaa kwamba udiwani hauniondelei uprofesa nilionao.Ó
Anasema aliona ni vema aanzie na udiwani kwani ipo haja ya kujenga msingi.
ÒNawashauri wasomi au niseme maprofesa wenzangu, tuache kulalamika na badala yake tuanze kuwaletea maendeleo wananchi sehemu tunazoishi.
ÒLakini hapa pia tuwekane sawa kwamba si lazima wote twende bungeni. Maprofesa wamebaki kulalamika na wengi hawataki kuwatumikia wananchi,Ó anasema.
Je, katika uchaguzi huo wa mwaka jana hakutengwa na wananchi wa Morogoro kwa ukabila hasa ikizingatiwa kwamba yeye ni mtu wa Bukoba?
ÒWananchi wa Morogoro si wakabila, naomba tusiwapakazie. Lakini niliwahi kusikia minongÕono juu ya jambo hilo. Lakini hawa mimi ni ndugu zangu.
ÒHili nalisema kwa uwazi kabisa, Waluguru ni ndugu zangu. Nimekaa hapa kwa miaka zaidi ya 30 na sioni kama natengwa kama wapo wenye hulka hiyo ni wachache. Sasa hatuwezi kusema Waluguru ni wakabila wakati wenye tabia hiyo si wengi.Ó
Anazungumziaje Serikali ya Rais Jakaya Kikwete hasa katika kipindi hiki cha kuelekea mwaka mmoja madarakani?
Prof. Ishengoma ambaye Januari 19 mwaka huu alichaguliwa kuwa Meya wa Manispaa ya Morogoro anasema Kikwete kaanza vizuri katika uongozi wake.
ÒHuu mwaka mmoja wa Kikwete vya kusifiwa ni vingi kuliko lawama, kuna kasi ya maendeleoÉkuna attitude ya uwajibikaji kwa viongozi.
ÒAmekuwa Rais ambaye hakai chini katika utendaji. Sasa kama Rais anakosa muda wa kupumzika wewe wa chini utalalaje?Ó anahoji Prof. Ishengoma.
Anasema pia katika nyanja za kiusalama, Serikali ya Kikwete imefanya jitihada na imefanikiwa kupunguza nguvu za ujambazi.ÒUsalama wa raia upo ingawa sehemu za Magharibi bado kuna tatizo.Ó
Lakini je, vipi kuhusu tatizo la umeme linalowakabili Watanzania na uchumi wao? Prof. Ishengoma anasema si jambo jema kumtupia lawama Rais Kikwete pekee.
ÒTusimtafute mchawi, hili suala la umeme lina uhusiano mkubwa na mazingira. Sisi tunazalisha umeme wa maji, watu wanaharibu mazingira unategemea nini?
ÒHatuna reserves za majiÉlazima tujifunze kutunza mazingira na hili si la kuzembea kabisa ni vizuri kuvisaidia vyanzo vya maji.
ÒMimi nipo Morogoro tangu mwaka 1973 wakati huo kulikuwa na maji yanatiririka milimani na hata marehemu Mbaraka Mwinshehe aliimba. Leo hii hakuna kitu kama hicho. Tuwajibike sasa kwa pamoja.Ó
Anapozungumzia suala la Tanzania kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki, anasema Watanzania hawana haja kuwa waoga na muungano huo.
ÒNi kweli tuna suala la Muungano wetu na Zanzibar ambalo linasumbua kidogo, lakini huwezi kukataa Jumuiya kwa kigezo cha Zanzibar.
ÒTunatakiwa kuelewa kuwa kuna mambo ya bed room (chumba cha kulala) na sitting room (sebuleni) sasa mazungumzo ya vyumba ni tofauti kabisa.
ÒKuleta hoja ya woga hapa huu ni ujinga na hatuwezi kusema kuwa hatuendi huko. Sisi kama nchi hatuwezi kukwepa mabadiliko. You change or changes will change you. Mimi naona tusisubiri mabadiliko yatubadilishe ni heri tubadilike sasa,Ó anasema na kuongeza:
ÒDunia inakwenda na wakati kwa njia ya muungano. Sasa kama dunia inaungana sisi tunasubiri nini?
ÒSuala hapa basi liwe ku-survive na tujiulize how do we join. Je, tunakubaliana nini huko? Tunafanyaje? Lakini isiletwe hoja ya kipuuzi kwamba tukwepe kuungana. Tutakwisha.Ó
Anaongeza kuwa jambo la msingi katika Jumuiya ya Afrika Mashariki ni kuangalia Tanzania inapeleka kitu gani sokoni. Anasema kwa mfano kama Wakenya wana uhaba wa mahindi ni jukumu la Watanzania kulima mahindi na kuyasambaza katika soko la Kenya.
ÒMbona leo hii tunakula apples za Afrika Kusini? Hapa sasa tuangalie nafasi yetu kisoko na si kukwepa muungano huu.Ó
Mbali na kuungwa kwake Jumuiya ya Afrika Mashariki, Prof. Ishengoma ni mtu wa karibu anayependa kuona wanawake wanapewa nafasi katika jamii.
Anasema si jambo jema kuwafungia wanawake kwenye chupa. ÒWape uhuru waonyeshe vipaji vyao na tuache dharau dhidi yao.Ó
Lakini kuna jambo jingine linalomkera sana. Nalo ni vijana kupotoka kimaadili. Anasema vijana wengi wanataka kuwa Wamarekani; hawautaki Utanzania.
ÒWako brain washed kabisa lakini wameharibiwa na sinema wanadhani kuwa hayo ndiyo maisha halisi. Vijana hawa ni kama kuku broilers, sisi tunataka kuku wa kienyeji.Ó
Katika maisha ya kawaida, Prof. Ishengoma ametumia elimu yake ya misitu kuyatengeneza mazingira ya makazi yake.
Kuna miti mbalimbali mojawapo ni cacao ambao wengi wanaamini kuwa miti hiyo haiwezi kustawi hapa nchini. Ana miti aina ya mdalasini, miembe na bwawa la samaki.
Kimsingi hakuna zao la bustani ambalo utalikosa kwa Prof. Ishengoma na anajivunia jambo hilo na kwamba amefanya hivyo kupunguza gharama za maisha.
ÒLitakuwa ni jambo la ajabu sana kama nitakwenda sokoni au mtu wa familia yangu anakwenda sokoni kutafuta nyanya, ndizi au pilipili. Nina kila kitu humu ndani,Ó anasema Prof. Ishengoma.
Profesa Ishengoma alizaliwa mkoani Kagera Aprili 4, 1952 alikopata elimu yake ya msingi kabla ya kujiunga na sekondari ya Nyakato mkoani Mwanza.
Alimaliza kidato cha sita katika Shule ya Sekondari ya Mazengo mkoani Dodoma mwaka 1972 na mwaka uliofuata Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kampasi ya Morogoro ambayo baadaye ndiyo ilizaa SUA.
Mwaka 1986 alipata udaktari wa sayansi ya kilimo kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo cha Norway na mwaka 1996 akawa profesa kamili. Msomi huyo ambaye yuko kazini kwa miaka 30, mke wake ndiye Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Dk. Christine Ishengoma.

munyuku@gmail.com
+255 754 471 920

Kirigini: Serikali ya Tanganyika itarudi

na innocent munyuku

HERMAN Kirigini si jina geni katika ulimwengu wa siasa nchini Tanzania. Ameshaliwakilisha bungeni jimbo la Musoma Vijijini kuanzia mwaka 1975 hadi 1985. Hivi karibuni mkongwe huyo wa siasa amezungumza na RAI katika mahojiano maalumu kuhusu mustakabali wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na kagusia Muungano na kurejeshwa kwa Serikali ya Tanganyika.

Akizungumzia juu ya mchakato wa Shirikisho la Mashariki, Kirigini anasema kimsingi watawala wa nchi zote tatu yaani Kenya, Uganda na Tanzania wamewaburuza wananchi wake.

Kwa mtazamo wake, nchi kama Tanzania inaburuzwa kuingia katika muungano huo na kwamba rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa anastahili lawama kwa kuridhia jambo hilo.

“Huyu wa kwetu niseme kwa uwazi kabisa aliburuzwa. Ndiyo! Mkapa aliburuzwa kwa sababu alikuwa dhaifu,” anasema na kuongeza kuwa Tanzania inakimbilia huko pasipo kujua udhaifu wao kiuchumi.

Anasema kuwa kwa kasi ya ukuaji wa uchumi unaofanywa na Kenya ni wazi Tanzania itamezwa katika jumuiya hiyo.

Kwamba Tanzania na Uganda si ajabu zikawa dampo la bidhaa kutoka Kenya kutokana na takwimu za mwaka uliopita juu ya bidhaa zinazouzwa nje ya nchi.

Mwaka jana, Kenya iliiuzia Tanzania na Uganda bidhaa mbalimbali za viwandani zenye thamani ya dola za Marekani milioni 593.351 wakati Tanzania na Uganda zikiiuzia Kenya bidhaa zenye thamani ya dola za Marekani milioni 186.200.

Katika mwaka huo huo, Uganda na Tanzania ziliagiza kutoka Kenya bidhaa zenye thamani ya dola za Marekani milioni 638.992 na hii kwa mtazamo wa Kirigini nchi hizi hazina uwezo sawa kiushindani.

“Uchumi wa Tanzania na Uganda unategemea zaidi kilimo cha mazao wakati ule wa Kenya ukitegemea viwanda na huduma,” anasema Kirigini na kisha kuongeza:

“Hali hii inaufanya uchumi wa Kenya kuwa imara zaidi kushinda wa Tanzania na Uganda unaotegemea hali ya hewa wakati ule Kenya ambao daima unategemea uzalishaji wa bidhaa za viwandani.”

Lakini pia Kirigini anasema kuwa nchi hizi tatu katika suala la mapato na bajeti zake kwa mwaka hayalingani. Kwamba Kenya inapata dola bilioni 3.715 na matumizi yao ni dola 3.88.

Tanzania inapata dola za Marekani bilioni 2.235 huku matumizi yake yakiwa dola 2.669. Uganda inapata dola bilioni 1.845 na inatumia dola bilioni 1.904 kwa mwaka.

“Ndiyo maana nasema wananchi wanaburuzwa na viongozi wa kisiasa katika jambo hili,” anasema.

Hata hivyo, anasisitiza kuwa hili suala la watu kutangaza kutaka maoni juu ya wananchi kuhusu shirikisho ni hadaa kwani maamuzi yalishafanywa.

“Leo hii unawauliza wananchi inasaidia nini? Hii ni hadaa, wangepewa nafasi ya kwanza kutoa maoni. Hivi kweli hatukumbuki tulivyoumia baada ya Jumuiya ya awali iliyovunjika mwaka 1977? Nani walifaidika zaidi kama sio Wakenya?”

Anasema wakati jumuiya inavunjika njia kuu za uchumi zilikuwa zikishikiliwa Kenya na wao wakaziendeleza kwa maslahi yao.

“Tuliumwa na nyoka na je, leo tuna uhakika gani kama muungano huu hautavunjika?” anahoji Kirigini.

Akizungumzia suala la Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Kirigini anaeleza kuwa Rais Jakaya Kikwete ameachwa peke yake.

“Kikwete analia peke yake katika kutatua mgogoro wa kisiasa Visiwani na kasoro za Muungano. Hawa viongozi wa CCM hawampi ushirikiano kukemea maovu ya Zanzibar.

“Kasimama bungeni (Kikwete) na kusema kuwa kuna mpasuko wa kisiasa Zanzibar lakini mbona hawamsaidii kuyakemea?

“Zanzibar kuna tatizo kubwa sana, Karume ni sawa na Salmin Amour wanalewa madaraka.”

Anasema kutokana na kasoro hizo ipo siku hoja ya Serikali ya Tanganyika itaibuka upya.

“Mimi nasema Serikali ya Tanganyika lazima itarudi na kosa alilofanya Nyerere ni kutokubali kubaki na Tanganyika, amefariki dunia akilijua hilo na hakuweza kurudi nyuma,” anasema Kirigini.

“Lakini mbali na jambo hilo, jambo jingine ni kwamba wengi waliomfuata Nyerere walikuwa wanafiki, walimwogopa badala ya kumshauri.

“Mimi sikutaka kuwa katika mkumbo huo na ndio maana wakati fulani bungeni nilichachamaa kwa kuwatetea wakulima wa pamba.

“Hili si Bunge, nakumbuka katika utetezi wangu kwa wakulima, Mwalimu alitaka kunikamata, alidai mimi na wenzangu tunapinga chama ndani ya Bunge.”

Anasema alichofunza katika miaka yake kama mwanasiasa ni kwamba CCM haitaki kuukubali upinzani na kutokana na misimamo yake, wana-CCM wengi wamekuwa wakimtenga kwa kumwona msaliti.

“Mwaka 1987 niliomba ujumbe wa NEC nikapewa alama ya E na kwamba mimi ni msaliti wa kisiasa, nikaandika barua Halmashauri Kuu lakini hadi hii leo sijajibiwa.

“Nikaonekana mbaya kwa watu wa mkoa wangu lakini upinzani ule leo hii ndio huo ambao umekubalika. Kuna chama kama CUF ni vema kikaendelea kuwepo ili pawe na criticism.”

Anaeleza kuwa mawazo makongwe hasa kutoka kwa baadhi ya wanasiasa wasiokubali mabadiliko yamesababisha CCM wakati mwingine kukosa mwamko.

“Lakini bado nakubali kwamba hawa walioko CCM baadhi yao wakitoka na kuunda chama kingine chama hicho kitakuwa bora kwani wapinzani wa kweli wangali humo.”

Kuhusu mwaka mmoja wa Serikali ya Kikwete, Kirigini anaeleza kuwa mtawala huyo anakubalika na wengi lakini kasi yake wengi hawaiwezi.

“Kikwete ana kasi ya ajabu na mtu mzuri lakini watu wake (viongozi) hawaendi naye. Wameachwa nyuma na kama mpiganaji, anatakiwa arudi nyuma aangalie majeshi yake mfano ni hizi Serikali za Mitaa zimeoza.”

Hata hivyo, anapingana na utaratibu wa Serikali kuwachangisha wananchi kwa ajili ya sherehe za Uhuru. Anasema kimsingi ni heri jambo hilo likawa katika bajeti.

“Waliochanga wengi ni wafanyabiashara na kwa kawaida wafanyabiashara hawana nia nzuri, wanakuwa na lao jambo.”

Kirigini ambaye kitaaluma ni Bwanashamba alizaliwa Desemba 22, 1955 ameoa na ana watoto wanane mmoja kati ya hao ni Rosemary Kirigini ambaye ni Mbunge wa Viti Maalumu (CCM).

Kirigini amewahi kuwa Waziri wa Mifugo kati ya mwaka 1980-83 na kati ya mwaka 1983-85 akawa Waziri wa Nchi anayeshughulikia mifugo.

Amewahi pia kuwa Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga na Arusha kati ya mwaka 1993-96. Ana shahada ya kilimo aliyoipata Chuo Kikuu cha Makerere mwaka 1970.

munyuku@gmail.com
+255 754 471 920