na innocent munyuku
BARAKA ziko mlangoni na shari kisogoni. Nyakati za kulalama kwamba maharagwe yanakaribia kuota tumboni zimekwenda likizo. Kilichopo ni tungo na vibwagizo vyenye utamu kwenye ndimi.
Siku kama hizi Mzee wa Busati huwa makini sana katika mikusanyiko. Iwe kwenye daladala au kwenye kilauri. Manake walio wengi wanatembea kwa matao wakijivunia ujazo kwenye mifuko yao.
Tarehe kama hizi, ubabe wa kila aina hutokea na anayekufanyia ubabe hudiriki kutamba kwamba anaweza kukupoteza mjini. Kisa? Anazo za kupandia taksi kwa siku mbili hizi.
Dada zetu ndo usiseme wameshasahu nywele zao za kipilipili. Siku hizi wanapanga foleni kwenye saluni kuzibadili nywele zao zifanane za kina Victoria Beckham au Jennifer Lopez. Si vibaya kwani ndivyo dunia inavyokwenda.
Tulidai uhuru wa kujitawala tukapewa lakini waliotupa uhuru huo wakaongeza mbinu kuhakikisha kuwa wanaziteka bongo zetu. Ndio maana Mzee wa Busati amekuwa akikemea utumwa wa akili ambao ni mbaya kuliko utumwa wa aina nyingine.
Tumefunzwa kuamini kuwa kila litokalo majuu ni jema na halina kasoro. Pita mitaa ya bongo utashangaa kuona kuwa hadi hii leo mitaa hupachikwa majina ya kigeni. Twakimbilia wapi?
Hoja ya Mwandika Busati juma hili ni kwamba jamii ya Kitanzania inapaswa kuthamini utamaduni wake na katika hili michezo ya jadi isisahauliwe.
Husemwa kwamba nchi haiwezi kutambulika kama taifa huru pasipo kuwa na utamaduni wake kama vile michezo na mengine yafananayo na hayo.
Ni kutokana na hilo, mwaka 1967 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha Sheria Na. 12 iliyobariki kuanzishwa kwa Baraza la Michezo la Taifa (BMT).
Lakini kwa bahati mbaya michezo mingi ya jadi imekuwa ikiachwa kando na kuendeleza michezo mingine.
Ipo haja ya kuunda mkakati wa kuendeleza michezo mbalimbali ya jadi na kuifanyia utafiti kama ilivyopata kutamkwa katika sera ya maendeleo ya michezo.
Leo hii twaifumbia macho lakini ukweli wa mambo ni kwamba siku chache zijazo taifa litalia na kusaga meno.
Kuidharau michezo yetu ya jadi ni kujikana na kulisaliti taifa. Huku ni kupotoka na kwenda katika barabara ya giza.
Mzee wa Busati mara kadhaa ameshashuhudia katika matamasha mbalimbali namna Wabongo walivyosahau mema ya kwao. Watapenda kushabikia nyimbo za ng’ambo na kuzifumbia macho ngoma za kwao.
Wasanii wa ngoma za jadi huangaliwa kama wasiostaarabika. Hawapewi nafasi inayostahili kwa ufundi na ubunifu wao. Wamebaki kuwa mawe ya pembeni.
Leo hata vitegemezi vyetu havitaki kusikia mdundiko wala mdumange. Watakwambia wao wanakwenda na wakati kwa kusikiza muziki kutoka Ulaya na Marekani.
Mzee wa Busati hasemi kwamba nyimbo za ng’ambo zibezwe la hasha! Anachosema ni kwamba mkazo uwekwe kujali na kuthamini mema ya kwetu na hakika inawezekana.
Hivi kweli tutaendelea kujikana namna hii hadi lini? Akili zetu zimewekwa nini? au hizi peremende tunazopewa kutoka ughaibuni? Tatizo li wapi?
Leo hii Mmakonde ukikutana naye mjini hataki umsalimie kwa lugha yake. Yu radhi kusema kwa Kiingereza kuliko lugha yake ya nyumbani. Hata Kiswahili nacho huwa shida kwake. Mtasemaje juu ya hilo? Kama si uzumbukuku ni nini?
Basi na tukae tujipange upya katika hili. Watawala wetu waungane na walio chini yao ili kuendeleza utamaduni wetu.
Wasimame na waseme kwamba tujiweke katika mstari wa kufufua akili zilizodumaa na kusahau mambo ya kijadi. Yakipotea tutakuja kuangamia miaka michache ijayo.
Basi na tuhubiri hayo na wala kusiwe na sababu ya kukwepa majukumu. Twauchimbia kaburi utamaduni wetu kwa kile tunachosema kwenda na wakati. Huu ni ulimbukeni.
Mwaona fahari gani kuwaona watoto wa kiume wakisuka nywele na kuvaa hereni masikioni? Hao wanasema wanakwenda na wakati lakini ukweli wa mambo ni kwamba wamekosa bahati.
Kila walionalo kwenye kioo cha luninga basi ni jema tena jema sana. Hivi ni kweli haya hayaepukiki? Hivi ni kweli kwamba twaona sawia tu vijana kuyumba katika ardhi yao?
Mzee wa Busati anafikia ukomo akiamini kuwa mdumange au sindimba zingali na nafasi nchini Tanzania.
Mwandika Busati atakuwa mwenye faraja kusikia kuwa ngoma za kina Vital Maembe au Zemkala zinagombewa huko Marekani na Ulaya. Hilo litafanikiwa kama tutaweka mkakati maalumu wa kufufua akili zilizolala.
Akili hizo zikifufuka ni wazi kuwa hata michezo ya jadi kama pia, tufe, mieleka na mingi ifananayo na hiyo itanguruma na kupendwa na jamii.
Wasalaam
Monday, October 29, 2007
Monday, October 22, 2007
Lala unono Dube uliyekosa bahati
na innocent munyuku
‘UNLUCKY LUCKY DUBE’ (Dube mwenye bahati aliyekosa bahati) yalikuwa maneno ya mwandishi mkongwe Balinagwe Mwambungu ambaye sasa ni mhariri mshiriki wa gazeti dada la Mtanzania.
Mwambungu ambaye hupenda kuitwa Big Mwa, alikuwa akiteta na Mzee wa Busati mara baada ya kusikia taarifa ya kifo cha mwanamuziki nguli wa muziki wa reggae barani Afrika, Lucy Dube.
Dube alipigwa risasi na majahili mbele ya wanawe wawili katika kitongoji cha Rossettenville jijini Johannesburg na hivyo kusitisha uhai wake.
Katika mazungumzo kati ya Mzee wa Busati na Big Mwa kilichojadiliwa ni namna mwanamuziki huyo alivyopoteza bahati ya kuishi kutokana na ufedhuli wa majahili hao.
Afrika imetikisika na dunia kwa ujumla imeshtushwa na taarifa ya msiba wa mwanamuziki huyo aliyepoteza maisha akiwa na umri wa miaka 43.
Alikuwa kinara na hata sifa zake zikakubalika katika kila ya mabara. Amepotea lakini sifa zake zingali zikienea.
Mzee wa Busati kwa asili yake ni mwenye imani ya rasta akiamini juu ya umoja, upendo na mshikamano. Ndicho alichoshikilia Dube katika tungo zake. Kahubiri haki za binadamu na umuhimu wa kujali wengine pasipo kubaguana.
Kilio kimetanda na hakuna shaka kwamba wengi wanaomlilia Dube wanahuzunika kwa vile wamepoteza kiini cha busara.
Mwanamuziki wa reggae nchini, Ras Innocent Nganyagwa maarufu kama Ras Inno juzi Jumapili alikuwa anatimiza umri wa miaka 42. Mzee wa Busati alikuwa miongoni mwa waliomtumia ujumbe wa kumtakia maisha mengine marefu. Katika majibu yake, Ras Inno alisahau sherehe na alichosema ni kwamba ana majonzi ya Dube.
Wasanii wengi wameshaingia studio kurekodi nyimbo za kumuenzi Dube. Wanahubiri mema yake na namna ya kuishi katika uadilifu.
Dube kishazimika lakini ukweli wa mambo ni kwamba tungali na uwezo wa kuendeleza mema aliyoyaanzisha kama vile amani na mshikamano.
Tuendelee kulia lakini tusisahau kuwa wema katika mitima yetu. Midomo iseme juu ya umoja na kujali shida za wengine. Tusiishie kulia.
Maisha ya reggae kwake yalianza katika miaka ya 1980 akipaza sauti kukemea ubaguzi wa rangi ndani ya Afrika Kusini.
Ni wazi kwamba kutokana na umahiri wake, Dube alikuwa katika nafasi za juu kwenye mauzo ya albamu zake.
Alipoamua kuimba juu ya ubaguzi wa rangi, wazungu walimwona kuwa ni mbaya wao. Akapata upinzani wa hali ya juu.
Upinzani huo ulikwenda mbali ikiwa ni pamoja na kuufungia wimbo wake wa Rasta Never Die usipigwe redioni.
Hakukata tamaa na ndio maana akaendelea kufyatua nyimbo nyingine kibao zikiwa na uzito katika jamii kama vile, Think About The Children na Slave.
Alikuwa mfuasi mkubwa wa Peter Tosh na hata alipofanya ziara nchini Jamaica, baadhi ya mashabiki walistaajabu uwezo wake jukwaani.
Mashabiki hao wakasema kuwa Peter Tosh yu hai akifanya kazi zake barani Afrika. Walimaanisha kwamba uwezo wa Dube ulifanana na wa Tosh.
Alale unono Dube, apumzike kwa amani lakini kuna mengi ya kukumbushana kwamba wafuasi wa mwanamuziki huyo wazidi kuhubiri mema.
Kemeeni ufisadi na ushenzi katika jamii zinazopaswa kuishi kistaarabu. Kuombeleza pasipo kufuata mwelekeo wa Dube ni kukosa nidhamu.
Huu ndio mtazamo wa Mwandika Busati wiki hii. Kwamba Dube katoweka lakini sauti na maneno yake yangali yakiishi.
Mzee wa Busati anafikia ukomo akiamini kwamba wadau wake wanaendelea katika neema hasa katika wakati huu wa mageuzi.
Wengine sasa wameacha ubishi na wamekubali kwamba bila matumizi ya kompyuta dunia haiendi sawia. Hongera Mzee wa Kutibua kwa kuanzisha bulogu yako.
Hiyo ni njia ya kutanua mawasiliano lakini Mzee wa Busati ana hofu na bolugu hiyo kama kweli itaendeleza mema au ni mwamko wa kuleta migogoro katika jamii hasa kwenye klabu za soka asizozipenda.
Vingingevyo Mwandika Busati anaweka kalamu chini akisubiri mwezi ugote arekebishe masuala yake. Si wajua Masiha yu jirani? Pasipo ngwenje kwa wakwe hakuendeki.
Wasalaam,
‘UNLUCKY LUCKY DUBE’ (Dube mwenye bahati aliyekosa bahati) yalikuwa maneno ya mwandishi mkongwe Balinagwe Mwambungu ambaye sasa ni mhariri mshiriki wa gazeti dada la Mtanzania.
Mwambungu ambaye hupenda kuitwa Big Mwa, alikuwa akiteta na Mzee wa Busati mara baada ya kusikia taarifa ya kifo cha mwanamuziki nguli wa muziki wa reggae barani Afrika, Lucy Dube.
Dube alipigwa risasi na majahili mbele ya wanawe wawili katika kitongoji cha Rossettenville jijini Johannesburg na hivyo kusitisha uhai wake.
Katika mazungumzo kati ya Mzee wa Busati na Big Mwa kilichojadiliwa ni namna mwanamuziki huyo alivyopoteza bahati ya kuishi kutokana na ufedhuli wa majahili hao.
Afrika imetikisika na dunia kwa ujumla imeshtushwa na taarifa ya msiba wa mwanamuziki huyo aliyepoteza maisha akiwa na umri wa miaka 43.
Alikuwa kinara na hata sifa zake zikakubalika katika kila ya mabara. Amepotea lakini sifa zake zingali zikienea.
Mzee wa Busati kwa asili yake ni mwenye imani ya rasta akiamini juu ya umoja, upendo na mshikamano. Ndicho alichoshikilia Dube katika tungo zake. Kahubiri haki za binadamu na umuhimu wa kujali wengine pasipo kubaguana.
Kilio kimetanda na hakuna shaka kwamba wengi wanaomlilia Dube wanahuzunika kwa vile wamepoteza kiini cha busara.
Mwanamuziki wa reggae nchini, Ras Innocent Nganyagwa maarufu kama Ras Inno juzi Jumapili alikuwa anatimiza umri wa miaka 42. Mzee wa Busati alikuwa miongoni mwa waliomtumia ujumbe wa kumtakia maisha mengine marefu. Katika majibu yake, Ras Inno alisahau sherehe na alichosema ni kwamba ana majonzi ya Dube.
Wasanii wengi wameshaingia studio kurekodi nyimbo za kumuenzi Dube. Wanahubiri mema yake na namna ya kuishi katika uadilifu.
Dube kishazimika lakini ukweli wa mambo ni kwamba tungali na uwezo wa kuendeleza mema aliyoyaanzisha kama vile amani na mshikamano.
Tuendelee kulia lakini tusisahau kuwa wema katika mitima yetu. Midomo iseme juu ya umoja na kujali shida za wengine. Tusiishie kulia.
Maisha ya reggae kwake yalianza katika miaka ya 1980 akipaza sauti kukemea ubaguzi wa rangi ndani ya Afrika Kusini.
Ni wazi kwamba kutokana na umahiri wake, Dube alikuwa katika nafasi za juu kwenye mauzo ya albamu zake.
Alipoamua kuimba juu ya ubaguzi wa rangi, wazungu walimwona kuwa ni mbaya wao. Akapata upinzani wa hali ya juu.
Upinzani huo ulikwenda mbali ikiwa ni pamoja na kuufungia wimbo wake wa Rasta Never Die usipigwe redioni.
Hakukata tamaa na ndio maana akaendelea kufyatua nyimbo nyingine kibao zikiwa na uzito katika jamii kama vile, Think About The Children na Slave.
Alikuwa mfuasi mkubwa wa Peter Tosh na hata alipofanya ziara nchini Jamaica, baadhi ya mashabiki walistaajabu uwezo wake jukwaani.
Mashabiki hao wakasema kuwa Peter Tosh yu hai akifanya kazi zake barani Afrika. Walimaanisha kwamba uwezo wa Dube ulifanana na wa Tosh.
Alale unono Dube, apumzike kwa amani lakini kuna mengi ya kukumbushana kwamba wafuasi wa mwanamuziki huyo wazidi kuhubiri mema.
Kemeeni ufisadi na ushenzi katika jamii zinazopaswa kuishi kistaarabu. Kuombeleza pasipo kufuata mwelekeo wa Dube ni kukosa nidhamu.
Huu ndio mtazamo wa Mwandika Busati wiki hii. Kwamba Dube katoweka lakini sauti na maneno yake yangali yakiishi.
Mzee wa Busati anafikia ukomo akiamini kwamba wadau wake wanaendelea katika neema hasa katika wakati huu wa mageuzi.
Wengine sasa wameacha ubishi na wamekubali kwamba bila matumizi ya kompyuta dunia haiendi sawia. Hongera Mzee wa Kutibua kwa kuanzisha bulogu yako.
Hiyo ni njia ya kutanua mawasiliano lakini Mzee wa Busati ana hofu na bolugu hiyo kama kweli itaendeleza mema au ni mwamko wa kuleta migogoro katika jamii hasa kwenye klabu za soka asizozipenda.
Vingingevyo Mwandika Busati anaweka kalamu chini akisubiri mwezi ugote arekebishe masuala yake. Si wajua Masiha yu jirani? Pasipo ngwenje kwa wakwe hakuendeki.
Wasalaam,
Thursday, October 18, 2007
Umoja Records yaja na fikra pevu katika sanaa yazidi kujitanua
na innocent munyuku
NILIPOZUNGUMZA naye kiasi cha miezi minne iliyopita, mmoja wa wakurugenzi wa Umoja Records, Gotta Warioba alikuwa na mengi ya kunieleza.
Alisema juu ya mwelekeo wa kampuni yake katika kuinua muziki wenye asili ya Kiafrika na kuusambaza kote duniani.
Midomo yake kwa hakika ilinena kwa kujiamini na alichokusudia kukisema. Wakati huo alikuwa katika kazi ngumu ya kuratibu kazi za wasanii kibao akiwamo Vital Maembe maarufu kama Sumu ya Teja.
Si kama nilikuwa na shaka juu ya msimamo wa Gotta la hasha. Niliwaza mengi na sikuishia kuwaza tu nilimwuliza namna atakavyojipanga katika kutekeleza aliyopanga.
Wakati huo alikuwa na mpango maalumu wa kuandaa albamu ya reggae ikiwakusanya wanamuziki wa aina mbalimbali. Ni wakati huo Gotta alilazimika kulala katika studio za Active ambazo ni sehemu ya Umoja Records.
Katika mpango huo walifanikiwa kupakua albamu ya iliyopewa jina la ‘Bongo Riddims & Style’ ikiwashirikisha wasanii wengi chipukizi.
Wiki iliyopita Gotta amefanya mahojiano na Bingwa na kuelezea mwelekeo wa Umoja Records na maendeleo ya muziki kwa ujumla.
“Umoja Records imetanua wigo wake baada ya kuanza kusaka wanamuziki kutoka Kenya na Uganda,” anasema Gotta.
Anasema ameshafanya mazungumzo na wasanii kadhaa jijini Nairobi zaidi ya wiki moja iliyopita na kwamba makubaliano ni chanya.
Katika ziara hiyo amezungumza na wasanii wengi na kwa kuanzia wawili wanatarajia kuwasili nchini siku chache zijazo kwa ajili ya kuanza kazi ya kurekodi na wasanii wa Tanzania.
“Lengo la ziara yangu lilikuwa kutanua mtandao wa Umoja Records na kusaka vipaji vipya.
“Wasanii watakaokuja wana vipaji vya hali ya juu na tunaamini watashirikiana na hawa waliopo nchini chini ya kampuni yetu.”
Lakini kikubwa anachozungumzia Gotta ni kukuza mkakati wa kampuni yake kwa kuongeza ubunifu katika muziki na kwamba wasanii waliopo wana uwezo mkubwa.
“Tutaangalia namna ya kufikia sehemu nyingine lakini kwa sasa tutaikamata Kenya na Uganda, wasanii hao wakiungana na wa kwetu hakuna shaka kwamba tunakuwa na product nzuri,” anasema.
Lakini anapozungumzia mtazamo mwelekeo wa muziki nchini hasa kwa bongofleva anasema kunatakiwa mapinduzi ya fikra.
“Unakumbuka tulianzisha project hapa ya kuwakusanya wanamuziki kwa ajili ya kutengeneza albamu ya reggae.
“Walikuja wengi na idadi kubwa ni wale wa kizazi kipya, tulielekezana na tukafika mahala tukafanya kazi nzuri pamoja.
“Lakini cha kushangaza kila aliyerekodi wimbo wake aliondoka zake na wengi hawajarudi,” anasema Gotta na kisha kuongeza:
“Walikuja wengi hapa wakarekodi na kuondoka lakini baadhi wamebaki na wana nia ya dhati kuwa nasi.
“Msanii kama Pestman, Ras Mizizi wameonyesha uwezo wa hali ya juu katika kazi zao. Wana fikra pevu na tunajivunia kuwa nao.
“Ras Inno naye anashirikiana nasi na kwa hakika anatupa changamoto nyingi. Kwa hiyo unaweza kuona kuwa ni mchanganyiko uliokomaa,” alisema Gotta.
Anawazungumzia vipi waliorekodi na kukimbia?
“Mimi nasema si tatizo lao, hao waliokimbia ni waathirika wa mfumo mzima wa hali ya utayarishaji wa muziki nchini.
“Kwamba si rahisi sana kuwabadilisha, tunahitaji mapinduzi ya fikra na si kazi ya siku moja.
“Lakini jambo moja liko wazi kwamba kama itatokea siku wakaamua kurejea hapa hatuna kinyongo nao, waje na tutawapokea.
“Wakija bila shaka watakuwa na kitu wamejifunza huko walikokimbilia nasi tutawaonyesha mapya tuliyonayo nadhani hapo tutafundishana na kuwa na kitu bora,” anasema Gotta.
Anapowataja baadhi wa wanamuziki ambao wana mwelekeo chanya katika Umoja Records hasiti kuwataja Pestman, Ras Mizizi, Carola na Ras Mizizi.
“Kwa hakika hawa waliobaki wanaangalia future, nitakupa mfano wa Pestman huyu ana ufahamu mkubwa na mara nyingi hupenda kujifunza mambo mapya.
“Alikuja hapa hajui kupiga gitaa, lakini sasa anaweza kuimba huku akipiga gitaa.
“Cha kufurahisha ni kwamba anaangalia matatizo ya dunia ya kuyajadili na kutoa njia mbadala ya kuyaepuka na wakati huo akiwasiliana na jamii.”
Kwa upande wa Ras Mizizi, Gotta anasema msanii huyo amekolezwa na asili yake ya Afrika na kwamba anapopiga reggae haachi kuzungumzia imani ya rasta na uafrika wake.
“Unaweza kusema kuwa huyu anahubiri imani ya Afrika ndani ya Rastafarian na ni mwepesi katika kurekodi.”
Mbali na hayo, Umoja Records imelenga kuweka uhusiano na mataifa mengine duniani hasa barani Ulaya kwa kuunda sound system na nembo ya pamoja.
“Tutakuwa na production team yetu na kuna kitu kinaitwa mobile disco ambavyo vitatufanya tuwe mahiri katika ziara zetu,” anasema Gotta.
Anasema mpango uliopo ni kuhakikisha kuwa wasanii wanakuwa na uwezo wa kurekodi kwa nembo za nje.
NILIPOZUNGUMZA naye kiasi cha miezi minne iliyopita, mmoja wa wakurugenzi wa Umoja Records, Gotta Warioba alikuwa na mengi ya kunieleza.
Alisema juu ya mwelekeo wa kampuni yake katika kuinua muziki wenye asili ya Kiafrika na kuusambaza kote duniani.
Midomo yake kwa hakika ilinena kwa kujiamini na alichokusudia kukisema. Wakati huo alikuwa katika kazi ngumu ya kuratibu kazi za wasanii kibao akiwamo Vital Maembe maarufu kama Sumu ya Teja.
Si kama nilikuwa na shaka juu ya msimamo wa Gotta la hasha. Niliwaza mengi na sikuishia kuwaza tu nilimwuliza namna atakavyojipanga katika kutekeleza aliyopanga.
Wakati huo alikuwa na mpango maalumu wa kuandaa albamu ya reggae ikiwakusanya wanamuziki wa aina mbalimbali. Ni wakati huo Gotta alilazimika kulala katika studio za Active ambazo ni sehemu ya Umoja Records.
Katika mpango huo walifanikiwa kupakua albamu ya iliyopewa jina la ‘Bongo Riddims & Style’ ikiwashirikisha wasanii wengi chipukizi.
Wiki iliyopita Gotta amefanya mahojiano na Bingwa na kuelezea mwelekeo wa Umoja Records na maendeleo ya muziki kwa ujumla.
“Umoja Records imetanua wigo wake baada ya kuanza kusaka wanamuziki kutoka Kenya na Uganda,” anasema Gotta.
Anasema ameshafanya mazungumzo na wasanii kadhaa jijini Nairobi zaidi ya wiki moja iliyopita na kwamba makubaliano ni chanya.
Katika ziara hiyo amezungumza na wasanii wengi na kwa kuanzia wawili wanatarajia kuwasili nchini siku chache zijazo kwa ajili ya kuanza kazi ya kurekodi na wasanii wa Tanzania.
“Lengo la ziara yangu lilikuwa kutanua mtandao wa Umoja Records na kusaka vipaji vipya.
“Wasanii watakaokuja wana vipaji vya hali ya juu na tunaamini watashirikiana na hawa waliopo nchini chini ya kampuni yetu.”
Lakini kikubwa anachozungumzia Gotta ni kukuza mkakati wa kampuni yake kwa kuongeza ubunifu katika muziki na kwamba wasanii waliopo wana uwezo mkubwa.
“Tutaangalia namna ya kufikia sehemu nyingine lakini kwa sasa tutaikamata Kenya na Uganda, wasanii hao wakiungana na wa kwetu hakuna shaka kwamba tunakuwa na product nzuri,” anasema.
Lakini anapozungumzia mtazamo mwelekeo wa muziki nchini hasa kwa bongofleva anasema kunatakiwa mapinduzi ya fikra.
“Unakumbuka tulianzisha project hapa ya kuwakusanya wanamuziki kwa ajili ya kutengeneza albamu ya reggae.
“Walikuja wengi na idadi kubwa ni wale wa kizazi kipya, tulielekezana na tukafika mahala tukafanya kazi nzuri pamoja.
“Lakini cha kushangaza kila aliyerekodi wimbo wake aliondoka zake na wengi hawajarudi,” anasema Gotta na kisha kuongeza:
“Walikuja wengi hapa wakarekodi na kuondoka lakini baadhi wamebaki na wana nia ya dhati kuwa nasi.
“Msanii kama Pestman, Ras Mizizi wameonyesha uwezo wa hali ya juu katika kazi zao. Wana fikra pevu na tunajivunia kuwa nao.
“Ras Inno naye anashirikiana nasi na kwa hakika anatupa changamoto nyingi. Kwa hiyo unaweza kuona kuwa ni mchanganyiko uliokomaa,” alisema Gotta.
Anawazungumzia vipi waliorekodi na kukimbia?
“Mimi nasema si tatizo lao, hao waliokimbia ni waathirika wa mfumo mzima wa hali ya utayarishaji wa muziki nchini.
“Kwamba si rahisi sana kuwabadilisha, tunahitaji mapinduzi ya fikra na si kazi ya siku moja.
“Lakini jambo moja liko wazi kwamba kama itatokea siku wakaamua kurejea hapa hatuna kinyongo nao, waje na tutawapokea.
“Wakija bila shaka watakuwa na kitu wamejifunza huko walikokimbilia nasi tutawaonyesha mapya tuliyonayo nadhani hapo tutafundishana na kuwa na kitu bora,” anasema Gotta.
Anapowataja baadhi wa wanamuziki ambao wana mwelekeo chanya katika Umoja Records hasiti kuwataja Pestman, Ras Mizizi, Carola na Ras Mizizi.
“Kwa hakika hawa waliobaki wanaangalia future, nitakupa mfano wa Pestman huyu ana ufahamu mkubwa na mara nyingi hupenda kujifunza mambo mapya.
“Alikuja hapa hajui kupiga gitaa, lakini sasa anaweza kuimba huku akipiga gitaa.
“Cha kufurahisha ni kwamba anaangalia matatizo ya dunia ya kuyajadili na kutoa njia mbadala ya kuyaepuka na wakati huo akiwasiliana na jamii.”
Kwa upande wa Ras Mizizi, Gotta anasema msanii huyo amekolezwa na asili yake ya Afrika na kwamba anapopiga reggae haachi kuzungumzia imani ya rasta na uafrika wake.
“Unaweza kusema kuwa huyu anahubiri imani ya Afrika ndani ya Rastafarian na ni mwepesi katika kurekodi.”
Mbali na hayo, Umoja Records imelenga kuweka uhusiano na mataifa mengine duniani hasa barani Ulaya kwa kuunda sound system na nembo ya pamoja.
“Tutakuwa na production team yetu na kuna kitu kinaitwa mobile disco ambavyo vitatufanya tuwe mahiri katika ziara zetu,” anasema Gotta.
Anasema mpango uliopo ni kuhakikisha kuwa wasanii wanakuwa na uwezo wa kurekodi kwa nembo za nje.
Monday, October 15, 2007
Vitambi vya vurugu Jangwani, Msimbazi
na innocent munyuku
HII imekuwa staili ya maisha ya kila siku. Hakuna maendeleo zaidi ya kushikiana bakora kwenye klabu za soka.
Kila unapokanyaga ni mbigili mtindo mmoja. Hadithi ni zile zile, mikwaruzano ndani ya klabu za soka bongo. Yanga na Simba ndizo zinazoongoza.
Mwandika Busati kwa muda mrefu amekuwa shuhuda wa hizo vurugu. Hakuna linalokwenda sawia badala yake ni watu kuumana kwa maslahi yao binafsi.
Yanga msimu huu moto umewaka. Mafahari wanapimana ubavu na wapambe wao pembeni wakisubiri matokeo. Wanachogombea ni ulaji na kujaza matumbo yao.
Kila kukicha hakuna maendeleo zaidi ya kuwasha moto wa mgogoro. Wanaoendesha masuala hayo wanajua wanachotaka na hakika wanakipata.
Mzee wa Busati hushangazwa na mambo haya. Kwamba inawezekanaje waseme wana mapenzi na klabu wakati wanaziangamiza?
Nani atakuwa mwokozi wa haya malumbano? Nani atafanikisha mema ndani ya klabu hizo? Hivi kweli kuna ulazima wa malumbano haya au ni laana ya kipekee?
Mwandika Busati sasa hana shaka tena kuamini kwamba Yanga na Simba ni makaburi ya wachezaji. Hakuna vitalu huko badala yake kumejaa misumari ya moto.
Waliojaa huko kwa kofia za uongozi hawana lolote kwani tambo zao zinatokana na kulishwa mabaya kutoka kwa wapambe wao wanaokaa vijiweni na kupanga mizozo.
Na kwa akili zao huwaza kwamba Tanzania inao ubavu wa kwenda Kombe la Dunia. Nani ataifikisha Tanzania huko wakati wachezaji wamelelewa kwenye migogoro?
Dira yao ni kupanga mbinu za kupambana na migogoro na si kuleta ufundi dimbani. Hilo si kosa lao kwani ndivyo mfumo ulivyo. Wala hakuna haja ya kuwalaumu hao ndiyo makuzi yao.
Kwa mfano timu hizo mbili hazina utaratibu mzuri wa kuleta makocha. Leo kaja huyu kesho kaletwa mwingine. Bila shaka kuna tatizo zaidi ya uendawazimu.
Hakuna umakini katika timu hizo na ndio maana kuna mengi yanafanyika kihuni na kiholela. Kila mwenye ulimi basi anayo fursa ya kutoa tamko hata kama tamko hilo ni pumba.
Midomo ya wapambe huwawezesha kupata ngwenje za kuvimbisha matumbo yao. Vitambi vinakuzwa kwa majungu na uzandiki. Husemwa kila linalowezekana ili wapate shibe. Hakuna lolote la kujenga soka.
Wenye akili zao hubaki wakicheka kwani wakati mwingine si busara kujibizana na wendawazimu. Waache wawehuke na matokeo yataonekana hivi pumbe.
Kama soka imewashinda jaribuni mashindano ya urembo au masumbwi. Kama mpira wa miguu umewashinda jaribuni riadha au kurusha tufe na kama ubavu mnao kajiungeni na wacheza gofu na tenisi.
Mzee wa Busati anatoa ushauri huo kutokana na ukweli kwamba kama kweli hao wanaojiita wadau wa soka wana nia ya kuinua mchezo huo mbona uozo ni ule ule?
Kila kukicha ni mizozo na mitafaruku. Kila uamkapo ni kelele za kugombea madaraka kwenye klabu hizo. Hii maana yake nini?
Tusidanganyane kwamba hao waliopo wana upeo wa kuweka mambo sawa. Kama upeo wanao basi wanaharibiwa na wapambe jambo ambalo ni hatari katika maendeleo ya soka nchini.
Hivi hakuna wa kuamka na kusema sasa yatosha? Kwa staili hii tusahau kuuza wachezaji wetu ng’ambo ya nchi na kama watauzwa basi wataishia Uarabuni ambako baada ya miezi michache huishia kuuza maduka ya Waarabu.
Kuna haja gani basi kujiita wadau wa Yanga na Simba wakati mwaleta mabaya klabuni? Dira za maendeleo hazimo. Kilichopo ni uhuni na uzushi wa migogoro.
Hakuna shaka kwamba huu ni mwanzo wa mwisho wa Simba na Yanga. Hakika huu ni ukomo ili ziibuke timu nyingine ambazo bila shaka zinaweza kuleta mageuzi.
Huu ni utabiri wa Mzee wa Busati na kama utatimia itakuwa neema kwa wapenda soka. Kwamba badala ya kugeukia Arsenal na Manchester United au Liverpool wataketi kuzishangalia timu za nyumbani.
Mwandika Busati anafikia ukomo kwa juma hili ambalo limeanza kwa wengi kubaki na madeni ya sikukuu. Idd el fitr imewatafuna na sasa mji umebaki kama pilipili.
Wasalaam,
HII imekuwa staili ya maisha ya kila siku. Hakuna maendeleo zaidi ya kushikiana bakora kwenye klabu za soka.
Kila unapokanyaga ni mbigili mtindo mmoja. Hadithi ni zile zile, mikwaruzano ndani ya klabu za soka bongo. Yanga na Simba ndizo zinazoongoza.
Mwandika Busati kwa muda mrefu amekuwa shuhuda wa hizo vurugu. Hakuna linalokwenda sawia badala yake ni watu kuumana kwa maslahi yao binafsi.
Yanga msimu huu moto umewaka. Mafahari wanapimana ubavu na wapambe wao pembeni wakisubiri matokeo. Wanachogombea ni ulaji na kujaza matumbo yao.
Kila kukicha hakuna maendeleo zaidi ya kuwasha moto wa mgogoro. Wanaoendesha masuala hayo wanajua wanachotaka na hakika wanakipata.
Mzee wa Busati hushangazwa na mambo haya. Kwamba inawezekanaje waseme wana mapenzi na klabu wakati wanaziangamiza?
Nani atakuwa mwokozi wa haya malumbano? Nani atafanikisha mema ndani ya klabu hizo? Hivi kweli kuna ulazima wa malumbano haya au ni laana ya kipekee?
Mwandika Busati sasa hana shaka tena kuamini kwamba Yanga na Simba ni makaburi ya wachezaji. Hakuna vitalu huko badala yake kumejaa misumari ya moto.
Waliojaa huko kwa kofia za uongozi hawana lolote kwani tambo zao zinatokana na kulishwa mabaya kutoka kwa wapambe wao wanaokaa vijiweni na kupanga mizozo.
Na kwa akili zao huwaza kwamba Tanzania inao ubavu wa kwenda Kombe la Dunia. Nani ataifikisha Tanzania huko wakati wachezaji wamelelewa kwenye migogoro?
Dira yao ni kupanga mbinu za kupambana na migogoro na si kuleta ufundi dimbani. Hilo si kosa lao kwani ndivyo mfumo ulivyo. Wala hakuna haja ya kuwalaumu hao ndiyo makuzi yao.
Kwa mfano timu hizo mbili hazina utaratibu mzuri wa kuleta makocha. Leo kaja huyu kesho kaletwa mwingine. Bila shaka kuna tatizo zaidi ya uendawazimu.
Hakuna umakini katika timu hizo na ndio maana kuna mengi yanafanyika kihuni na kiholela. Kila mwenye ulimi basi anayo fursa ya kutoa tamko hata kama tamko hilo ni pumba.
Midomo ya wapambe huwawezesha kupata ngwenje za kuvimbisha matumbo yao. Vitambi vinakuzwa kwa majungu na uzandiki. Husemwa kila linalowezekana ili wapate shibe. Hakuna lolote la kujenga soka.
Wenye akili zao hubaki wakicheka kwani wakati mwingine si busara kujibizana na wendawazimu. Waache wawehuke na matokeo yataonekana hivi pumbe.
Kama soka imewashinda jaribuni mashindano ya urembo au masumbwi. Kama mpira wa miguu umewashinda jaribuni riadha au kurusha tufe na kama ubavu mnao kajiungeni na wacheza gofu na tenisi.
Mzee wa Busati anatoa ushauri huo kutokana na ukweli kwamba kama kweli hao wanaojiita wadau wa soka wana nia ya kuinua mchezo huo mbona uozo ni ule ule?
Kila kukicha ni mizozo na mitafaruku. Kila uamkapo ni kelele za kugombea madaraka kwenye klabu hizo. Hii maana yake nini?
Tusidanganyane kwamba hao waliopo wana upeo wa kuweka mambo sawa. Kama upeo wanao basi wanaharibiwa na wapambe jambo ambalo ni hatari katika maendeleo ya soka nchini.
Hivi hakuna wa kuamka na kusema sasa yatosha? Kwa staili hii tusahau kuuza wachezaji wetu ng’ambo ya nchi na kama watauzwa basi wataishia Uarabuni ambako baada ya miezi michache huishia kuuza maduka ya Waarabu.
Kuna haja gani basi kujiita wadau wa Yanga na Simba wakati mwaleta mabaya klabuni? Dira za maendeleo hazimo. Kilichopo ni uhuni na uzushi wa migogoro.
Hakuna shaka kwamba huu ni mwanzo wa mwisho wa Simba na Yanga. Hakika huu ni ukomo ili ziibuke timu nyingine ambazo bila shaka zinaweza kuleta mageuzi.
Huu ni utabiri wa Mzee wa Busati na kama utatimia itakuwa neema kwa wapenda soka. Kwamba badala ya kugeukia Arsenal na Manchester United au Liverpool wataketi kuzishangalia timu za nyumbani.
Mwandika Busati anafikia ukomo kwa juma hili ambalo limeanza kwa wengi kubaki na madeni ya sikukuu. Idd el fitr imewatafuna na sasa mji umebaki kama pilipili.
Wasalaam,
Friday, October 12, 2007
Usu Mallya: Jembe jipya makini TGNP
-Akerwa na ubinafsishwaji holela nchini
-Asema maazimio ya Beijing bado changamoto kwa Serikali
Na Innocent Munyuku
KAMA kuna masuala ambayo yamekuwa yakipigiwa zumari katika sehemu nyingi duniani, usawa katika jamii na maisha bora huwezi kuviweka kando.
Zipo asasi nyingi nchini zilizoweka mikakati ya kutatua mambo kama hayo na moja ya asasi hizo ni Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) iliyoanzishwa mwaka 1993.
TGNP ni asasi isiyo ya kiserikali na kuundwa kwake kulilenga zaidi kuleta usawa wa jinsia katika jamii, kuwawezesha wanawake, mafunzo, utafiti na kusambaza taarifa muhimu zinazolenga ustawi wa jamii.
Hivi karibuni TGNP ilipata Mkurugenzi Mtendaji, Usu Mallya anayechukua nafasi ya Mary Rusimbi aliyemaliza muda wake.
Je, mkurugenzi huyo mpya ana mkakati gani baada ya kukalia usukani wa kuipeleka asasi hiyo mbele kimafanikio?
Katika mahojiano maalumu na MTANZANIA Jumapili juzi, Usu anasema mbali na kuwa na jukumu la usimamizi wa asasi hiyo, mfumo wa TGNP unamweka katika mazingira ya kufurahia kazi yake.
“TGNP imejengwa kwa namna kwamba kila jambo linafanywa kwa ushirikiano, hakuna maamuzi ya mtu mmoja.
“Lakini pia niko hapa tangu mwaka 1998 kwa hiyo nimejifunza mengi hapa hasa katika mkakati wa kujenga nguvu za pamoja,” anasema Usu na kisha kuongeza:
“Mtandao wetu umejengwa katika mhimili wa pamoja katika dhamira na dira.”
Pamoja na ukweli kwamba manyanyaso au ubaguzi wa kijinsia upo duniani kwa miaka mingi, nchi nyingi za Afrika ikiwemo Tanzania zilipata mwamko baada ya Mkutano wa Beijing Septemba mwaka 1995.
Katika mkutano huo wa wanawake uliazimia mambo mbalimbali ikiwemo kubadili mtazamo wa jamii katika kutendeana haki pasipo kubaguana.
Pia kujali utu na kumpa mwanamke sauti na kwamba wanaume kwa miaka mingi wamekuwa kikwazo katika maendeleo binafsi ya mwanamke.
Lakini je, baada ya miaka 12 kupita, TGNP inatathimini vipi mafanikio ya azimio la Beijing?
“Zipo fursa nyingi kwa wanawake lakini bado Serikali ina changamoto nyingi kufikia maendeleo.
“Katika elimu kumekuwa na jitihada lakini uwiano ni mdogo katika ngazi ya elimu ya juu. Kwa mfano wasichana wanaovuka kwenda kidato cha tano, sita hadi chuo kikuu inashuka,” anasema Usu.
Anaeleza kuwa kushuka kwa kiwango hicho kunatokana na mazingira au mfumo uliopo katika sheria za nchi.
“Sheria ya ndoa kwa mfano inaweka wazi kuwa mtoto wa kike anaweza kuolewa afikishapo umri wa miaka 14 au 15…sasa huu ndio muda wa mtoto kuwa shule. Akishaolewa safari yake inakuwa imeishia hapo.
“Lakini pia sheria kwamba mtoto wa kike akipata ujauzito abaki nyumbani nayo imechangia kwa kiasi kikubwa kuongeza idadi ya wasichana wenye elimu ya chini katika jamii.”
Hata hivyo, anasema maazimio mengine ya Beijing yanakwamishwa na sera za ubinafsishaji nchini.
Kwamba uchumi sasa ni wa utandawazi unaoongozwa na makampuni kutoka nchi tajiri duniani.
“Mikataba mingi katika eneo hilo ni ya kuwakandamiza wananchi, hii mikataba haijengi nchi changa.
“Nitoe mfano wa hapa kwetu, mkataba wa Bi-water umeshatuumiza, angalia suala la Richmond na umeme wetu au madini.
“Haya mambo yote yametuathiri kwa sababu ya utandawazi, angalia nchi kama Afrika Kusini, imeendelea kwa kiwango kikubwa kwa vile wametumia madini yao kujinufaisha. Hali ni tofauti na Tanzania,” anasema.
Anasema kutokana na mazingira kama hayo, hata jitihada za kuwakomboa Watanzania kutoka katika umasikini zinakuwa ngumu.
“Wanawake kwa mfano wako kwenye uchumi mdogo mdogo. Ninachosema hapa ni kwamba kama Serikali imeshindwa kuhodhi rasilimali basi hata hawa wa chini wataendelea kuumia,” anasema Usu.
Anazungumzia pia sekta ya utalii ambayo kwa mtazamo wake haijampa fursa Mtanzania kunufaika nayo.
“Nani anafaidi matunda ya utalii? Bila shaka ni watu wachache sana,” anasema.
Mbali na uchumi kuwa suala gumu katika kuwaendeleza Watanzania, kuna kikwazo katika sekta ya afya.
“Eneo hili ni changamoto kubwa kwa Serikali kwani linatakiwa kuwezeshwa na anayeumia sana ni mwanamke.
“Vifaa au huduma katika sekta hii bado haijamhakikishia mwanamke hatima njema hasa katika uzazi. Kuna takwimu zinazoonyesha kuwa katika wanawake 560 kati ya 100,000 hufariki dunia kila mwaka kutokana na uzazi usio salama.
“Hii ni dalili au ishara kwamba Serikali inakabiliwa na changamoto kubwa katika sekta ya afya hasa kwa afya ya mwanamke.”
Analalamikia uonevu ambao unachukua sura tofauti kila siku dhidi ya mwanamke.
“Kuna manyanyaso kwa wanawake, wengi wana uwezo mdogo wa kufanya maamuzi kuhusu ngono au idadi ya watoto.
“Ni jambo linalofanywa kuwa ni kawaida kwa mjamzito kufanya kazi za nyumbani huku akiwa na lishe duni hii si ajabu ikachangia vifo wakati mwingine.”
Vipi kuhusu nafasi ya mwanamke katika uongozi?
Usu anasema pamoja kuwa na wabunge wanawake kwa asilimia 30, bado kiwango hicho hakitoshi.
“Wapewe sauti au nafasi pia kuanzia kwenye udiwani…lakini pia naweza kusema kuwa wanawake wanahitaji nafasi pia katika sekta binafsi.
“Hata serikalini ipo haja kwa wanawake kupewa nafasi za juu kama vile ukuu wa mikoa, ukatibu mkuu, ubalozi nje ya nchi, ukurugenzi wa bodi au ujaji,” anasema Usu.
Pamoja na hilo, Usu anasema kuna mambo ambayo lazima yasemwe kwa uwazi au kujadiliwa kitaifa kuhusu utamaduni wa Mtanzania kutokana na ukweli kwamba mengi yanatokana na upotoshwaji wa mila.
Anasema jamii mara nyingi inamwona mwanamke kama chombo cha starehe na hata watoto wanapokua, mtoto wa kike tayari ameshajenga dhana ya kuwa wa chini.
“Hili ni suala nyeti linalopaswa kujadiliwa kitaifa, ni kama ilivyo rushwa lazima lijadiliwe. Hili jambo si la TGNP pekee bali Serikali nayo ihusike.”
Tangu kuanzishwa kwake, TGNP imefanikiwa katika kufikisha ujumbe kwa jamii kwa njia ya semina mbalimbali na kushirikiana na wanaharakati katika ngazi mbalimbali.
Mara nyingi imeshirikiana na FemAct katika kuilemisha jamii na ushirikiano huo upo kwa wanaharakati katika wilaya mbalimbali nchini.
“Tunatambua kazi za wanaharakati katika ngazi husika kwa kufanya semina na nafasi ya elimu kwa watu wa rika mbalimbali,” anasema Usu.
Mbali na semina, kila baada ya miaka miwili, TGNP hufanya tamasha la kijinsia ambalo huwapa fursa washiriki kufanya tathimini.
“Watu mbalimbali hualikwa na kinachofanyika ni kuibua mijadala na kushinikiza mabadiliko.
“Kuna sera kama mgawanyo mbovu wa mali katika familia kama vile ardhi au ukatili nazo hujadiliwa.
“Tumeanza kuishinikiza Serikali ibadili pia Katiba ya nchi kwani haimtendei haki mwanamke linapokuja suala la ndoa.
“Kuna mapungufu kwa mfano Katiba inaruhusu sheria za jadi kutambuliwa, sasa katika hali kama hiyo ni wazi kuwa mwanamke anapewa haki na wakati huo huo kumnyang’anya.
“Unaporuhusu kutumika kwa sheria ya jadi maana yake ni kuruhusu unyanyasaji kwani sheria nyingi za jadi zinamkandamiza mwanamke,” anasema.
TGNP imeshatoa mabango ya aina mbalimbali yanayolenga kuielimisha jamii.
Katika Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge mwaka 2005 walitoa bango la ‘Wakati umefika! Uwezo wa kuongoza tunao! Wanawake tujitokeze’.
Yapo mabango mengine kama la mwaka 2001 linalosomeka ‘Jinsia, demokrasia na maendeleo mbinu mbadala za kukabiliana na kufukarishwa’.
Lipo jingine la mwaka 2004 ‘Tatizo la dunia ya leo si umasikini ni mgawanyiko wa rasilimali wa kinyonyaji’.
Mwaka jana walikemea ubinafsishaji holela wa sekta ya maji.
Na mwaka huu TGNP imekuja na bango la ‘Sema hapana kwa ukatili wa kijinsia’.
Mbali na hayo wamekuwa na machapichopendwa kwa njia ya vitabu kama vile, Kwangu Wapi, Vijana Taifa la Leo, Kondomu Yazua Kasheshe, Utandawazi na Wewe na Ahadi za Uongo.
Pia TGNP imekuwa ikitoa vitabu vya kitaaluma kwa watafiti na wanafunzi. Baadhi ni Gender Profile of Tanzania: Enhancing Gender Family, Activists Voices, Against Neo Liberalism na Gender Budget Analysis in Tanzania 1997-2000.
Kuna maktaba ya kisasa na duka la vitabu katika ofisi hizo zilizopo eneo la Mabibo jijini Dar es Salaam na kila Jumatano huendeshwa semina kwa watu wote katika ofisi hizo kuanzia saa tisa mchana hadi 11 jioni.
Usu Mallya alitokea wapi? Alizaliwa mkoani Shinyanga mwaka 1961 na elimu yake ya msingi aliipata Marangu Sembeti Wilaya ya Moshi Vijijini mkoani Kilimanjaro. Hii ilikuwa kati ya mwaka 1968-74.
Kati ya mwaka 1975-78 alikuwa Shule ya Sekondari ya Kibosho alikohitimu kidato cha nne. Elimu ya juu ya sekondari aliipata Korogwe mkoani Tanga.
Baadaye alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam alikopata shahada ya kwanza ya uongozi wa taasisi za umma, sayansi ya jamii na Kifaransa. Alihitimu mwaka 1985.
Aliwahi kufanya kazi chuoni hapo katika Idara ya Sayansi ya Jamii kati ya mwaka 1990-95.
Alirejea darasani kusomea shahada ya uzamili chuoni hapo akichukua masomo ya sayansi ya jamii. Alihitimu mwaka 1997.
Mwaka mmoja baadaye akajiunga na TGNP.
-Asema maazimio ya Beijing bado changamoto kwa Serikali
Na Innocent Munyuku
KAMA kuna masuala ambayo yamekuwa yakipigiwa zumari katika sehemu nyingi duniani, usawa katika jamii na maisha bora huwezi kuviweka kando.
Zipo asasi nyingi nchini zilizoweka mikakati ya kutatua mambo kama hayo na moja ya asasi hizo ni Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) iliyoanzishwa mwaka 1993.
TGNP ni asasi isiyo ya kiserikali na kuundwa kwake kulilenga zaidi kuleta usawa wa jinsia katika jamii, kuwawezesha wanawake, mafunzo, utafiti na kusambaza taarifa muhimu zinazolenga ustawi wa jamii.
Hivi karibuni TGNP ilipata Mkurugenzi Mtendaji, Usu Mallya anayechukua nafasi ya Mary Rusimbi aliyemaliza muda wake.
Je, mkurugenzi huyo mpya ana mkakati gani baada ya kukalia usukani wa kuipeleka asasi hiyo mbele kimafanikio?
Katika mahojiano maalumu na MTANZANIA Jumapili juzi, Usu anasema mbali na kuwa na jukumu la usimamizi wa asasi hiyo, mfumo wa TGNP unamweka katika mazingira ya kufurahia kazi yake.
“TGNP imejengwa kwa namna kwamba kila jambo linafanywa kwa ushirikiano, hakuna maamuzi ya mtu mmoja.
“Lakini pia niko hapa tangu mwaka 1998 kwa hiyo nimejifunza mengi hapa hasa katika mkakati wa kujenga nguvu za pamoja,” anasema Usu na kisha kuongeza:
“Mtandao wetu umejengwa katika mhimili wa pamoja katika dhamira na dira.”
Pamoja na ukweli kwamba manyanyaso au ubaguzi wa kijinsia upo duniani kwa miaka mingi, nchi nyingi za Afrika ikiwemo Tanzania zilipata mwamko baada ya Mkutano wa Beijing Septemba mwaka 1995.
Katika mkutano huo wa wanawake uliazimia mambo mbalimbali ikiwemo kubadili mtazamo wa jamii katika kutendeana haki pasipo kubaguana.
Pia kujali utu na kumpa mwanamke sauti na kwamba wanaume kwa miaka mingi wamekuwa kikwazo katika maendeleo binafsi ya mwanamke.
Lakini je, baada ya miaka 12 kupita, TGNP inatathimini vipi mafanikio ya azimio la Beijing?
“Zipo fursa nyingi kwa wanawake lakini bado Serikali ina changamoto nyingi kufikia maendeleo.
“Katika elimu kumekuwa na jitihada lakini uwiano ni mdogo katika ngazi ya elimu ya juu. Kwa mfano wasichana wanaovuka kwenda kidato cha tano, sita hadi chuo kikuu inashuka,” anasema Usu.
Anaeleza kuwa kushuka kwa kiwango hicho kunatokana na mazingira au mfumo uliopo katika sheria za nchi.
“Sheria ya ndoa kwa mfano inaweka wazi kuwa mtoto wa kike anaweza kuolewa afikishapo umri wa miaka 14 au 15…sasa huu ndio muda wa mtoto kuwa shule. Akishaolewa safari yake inakuwa imeishia hapo.
“Lakini pia sheria kwamba mtoto wa kike akipata ujauzito abaki nyumbani nayo imechangia kwa kiasi kikubwa kuongeza idadi ya wasichana wenye elimu ya chini katika jamii.”
Hata hivyo, anasema maazimio mengine ya Beijing yanakwamishwa na sera za ubinafsishaji nchini.
Kwamba uchumi sasa ni wa utandawazi unaoongozwa na makampuni kutoka nchi tajiri duniani.
“Mikataba mingi katika eneo hilo ni ya kuwakandamiza wananchi, hii mikataba haijengi nchi changa.
“Nitoe mfano wa hapa kwetu, mkataba wa Bi-water umeshatuumiza, angalia suala la Richmond na umeme wetu au madini.
“Haya mambo yote yametuathiri kwa sababu ya utandawazi, angalia nchi kama Afrika Kusini, imeendelea kwa kiwango kikubwa kwa vile wametumia madini yao kujinufaisha. Hali ni tofauti na Tanzania,” anasema.
Anasema kutokana na mazingira kama hayo, hata jitihada za kuwakomboa Watanzania kutoka katika umasikini zinakuwa ngumu.
“Wanawake kwa mfano wako kwenye uchumi mdogo mdogo. Ninachosema hapa ni kwamba kama Serikali imeshindwa kuhodhi rasilimali basi hata hawa wa chini wataendelea kuumia,” anasema Usu.
Anazungumzia pia sekta ya utalii ambayo kwa mtazamo wake haijampa fursa Mtanzania kunufaika nayo.
“Nani anafaidi matunda ya utalii? Bila shaka ni watu wachache sana,” anasema.
Mbali na uchumi kuwa suala gumu katika kuwaendeleza Watanzania, kuna kikwazo katika sekta ya afya.
“Eneo hili ni changamoto kubwa kwa Serikali kwani linatakiwa kuwezeshwa na anayeumia sana ni mwanamke.
“Vifaa au huduma katika sekta hii bado haijamhakikishia mwanamke hatima njema hasa katika uzazi. Kuna takwimu zinazoonyesha kuwa katika wanawake 560 kati ya 100,000 hufariki dunia kila mwaka kutokana na uzazi usio salama.
“Hii ni dalili au ishara kwamba Serikali inakabiliwa na changamoto kubwa katika sekta ya afya hasa kwa afya ya mwanamke.”
Analalamikia uonevu ambao unachukua sura tofauti kila siku dhidi ya mwanamke.
“Kuna manyanyaso kwa wanawake, wengi wana uwezo mdogo wa kufanya maamuzi kuhusu ngono au idadi ya watoto.
“Ni jambo linalofanywa kuwa ni kawaida kwa mjamzito kufanya kazi za nyumbani huku akiwa na lishe duni hii si ajabu ikachangia vifo wakati mwingine.”
Vipi kuhusu nafasi ya mwanamke katika uongozi?
Usu anasema pamoja kuwa na wabunge wanawake kwa asilimia 30, bado kiwango hicho hakitoshi.
“Wapewe sauti au nafasi pia kuanzia kwenye udiwani…lakini pia naweza kusema kuwa wanawake wanahitaji nafasi pia katika sekta binafsi.
“Hata serikalini ipo haja kwa wanawake kupewa nafasi za juu kama vile ukuu wa mikoa, ukatibu mkuu, ubalozi nje ya nchi, ukurugenzi wa bodi au ujaji,” anasema Usu.
Pamoja na hilo, Usu anasema kuna mambo ambayo lazima yasemwe kwa uwazi au kujadiliwa kitaifa kuhusu utamaduni wa Mtanzania kutokana na ukweli kwamba mengi yanatokana na upotoshwaji wa mila.
Anasema jamii mara nyingi inamwona mwanamke kama chombo cha starehe na hata watoto wanapokua, mtoto wa kike tayari ameshajenga dhana ya kuwa wa chini.
“Hili ni suala nyeti linalopaswa kujadiliwa kitaifa, ni kama ilivyo rushwa lazima lijadiliwe. Hili jambo si la TGNP pekee bali Serikali nayo ihusike.”
Tangu kuanzishwa kwake, TGNP imefanikiwa katika kufikisha ujumbe kwa jamii kwa njia ya semina mbalimbali na kushirikiana na wanaharakati katika ngazi mbalimbali.
Mara nyingi imeshirikiana na FemAct katika kuilemisha jamii na ushirikiano huo upo kwa wanaharakati katika wilaya mbalimbali nchini.
“Tunatambua kazi za wanaharakati katika ngazi husika kwa kufanya semina na nafasi ya elimu kwa watu wa rika mbalimbali,” anasema Usu.
Mbali na semina, kila baada ya miaka miwili, TGNP hufanya tamasha la kijinsia ambalo huwapa fursa washiriki kufanya tathimini.
“Watu mbalimbali hualikwa na kinachofanyika ni kuibua mijadala na kushinikiza mabadiliko.
“Kuna sera kama mgawanyo mbovu wa mali katika familia kama vile ardhi au ukatili nazo hujadiliwa.
“Tumeanza kuishinikiza Serikali ibadili pia Katiba ya nchi kwani haimtendei haki mwanamke linapokuja suala la ndoa.
“Kuna mapungufu kwa mfano Katiba inaruhusu sheria za jadi kutambuliwa, sasa katika hali kama hiyo ni wazi kuwa mwanamke anapewa haki na wakati huo huo kumnyang’anya.
“Unaporuhusu kutumika kwa sheria ya jadi maana yake ni kuruhusu unyanyasaji kwani sheria nyingi za jadi zinamkandamiza mwanamke,” anasema.
TGNP imeshatoa mabango ya aina mbalimbali yanayolenga kuielimisha jamii.
Katika Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge mwaka 2005 walitoa bango la ‘Wakati umefika! Uwezo wa kuongoza tunao! Wanawake tujitokeze’.
Yapo mabango mengine kama la mwaka 2001 linalosomeka ‘Jinsia, demokrasia na maendeleo mbinu mbadala za kukabiliana na kufukarishwa’.
Lipo jingine la mwaka 2004 ‘Tatizo la dunia ya leo si umasikini ni mgawanyiko wa rasilimali wa kinyonyaji’.
Mwaka jana walikemea ubinafsishaji holela wa sekta ya maji.
Na mwaka huu TGNP imekuja na bango la ‘Sema hapana kwa ukatili wa kijinsia’.
Mbali na hayo wamekuwa na machapichopendwa kwa njia ya vitabu kama vile, Kwangu Wapi, Vijana Taifa la Leo, Kondomu Yazua Kasheshe, Utandawazi na Wewe na Ahadi za Uongo.
Pia TGNP imekuwa ikitoa vitabu vya kitaaluma kwa watafiti na wanafunzi. Baadhi ni Gender Profile of Tanzania: Enhancing Gender Family, Activists Voices, Against Neo Liberalism na Gender Budget Analysis in Tanzania 1997-2000.
Kuna maktaba ya kisasa na duka la vitabu katika ofisi hizo zilizopo eneo la Mabibo jijini Dar es Salaam na kila Jumatano huendeshwa semina kwa watu wote katika ofisi hizo kuanzia saa tisa mchana hadi 11 jioni.
Usu Mallya alitokea wapi? Alizaliwa mkoani Shinyanga mwaka 1961 na elimu yake ya msingi aliipata Marangu Sembeti Wilaya ya Moshi Vijijini mkoani Kilimanjaro. Hii ilikuwa kati ya mwaka 1968-74.
Kati ya mwaka 1975-78 alikuwa Shule ya Sekondari ya Kibosho alikohitimu kidato cha nne. Elimu ya juu ya sekondari aliipata Korogwe mkoani Tanga.
Baadaye alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam alikopata shahada ya kwanza ya uongozi wa taasisi za umma, sayansi ya jamii na Kifaransa. Alihitimu mwaka 1985.
Aliwahi kufanya kazi chuoni hapo katika Idara ya Sayansi ya Jamii kati ya mwaka 1990-95.
Alirejea darasani kusomea shahada ya uzamili chuoni hapo akichukua masomo ya sayansi ya jamii. Alihitimu mwaka 1997.
Mwaka mmoja baadaye akajiunga na TGNP.
Amina Chifupa amefariki dunia bila amani moyoni
WATANZANIA kwa muda wamesahau kujadili maumivu ya Bajeti ya Mwaka Mpya wa Fedha wa 2007/8. Wamepunguza kuizumgumzia Taifa Stars na safari yake ya Ghana. Kinachonenwa sasa ni kifo cha Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Amina Chifupa aliyefariki dunia Jumanne wiki hii jijini Dar es Salaam. Katika makala haya waandishi wetu ELIZABETH MJATTA na INNOCENT MUNYUKU wanazungumzia mengi na matarajio aliyokuwa nayo Amina katika uhai wake.
Mwanasiasa huyo machachari aliyekuwa jasiri mdogo kuliko wote bungeni ambaye alipata nafasi hiyo kupitia tiketi ya Umoja wa Vijana wa CCM.
Siku chache kabla ya kuhudhuria Mkutano wa Tano wa Bunge mwaka jana, Amina alifanya mahojiano na gazeti dada la RAI.
Alifika chumba cha habari kwa ajili ya mahojiano maalumu yaliyochukua takribani saa 2. Akiwa amevalia suti yake nyeusi, hereni ndefu za dhahabu kwenye masikio yake, mkufu wa dhahabu ulioshika vema shingo yake, bangili mikononi mwake vilitosha kumpendezesha nyota huyo aliyezimika ghafla.
Kama ilivyokuwa hulka yake, Amina alisema mengi ya msingi kwa kujiamini na hata alipoulizwa juu ya nini kilichompa ujasiri wa kuapa kwa mbingu bungeni kwamba atawafichua wauza dawa za kulevya hakuonekana kujuta.
“Sikuogopa hata kidogo…ninaamini kuwa mimi ni kiongozi hivyo siwezi kuogopa kusema ukweli,” alisema Amina.
Lakini hakuishia hapo akaongeza: “Kama mtu ni mwoga hafai kuingia bungeni, hatuwezi kuwaacha vijana wa Tanzania wakiangamia kwa matumizi ya dawa za kulevya.”
Alitumia fursa hiyo kuzungumzia namna alivyojisikia vibaya baada ya baadhi ya magazeti na watu mbalimbali kuhoji uwezo wake mara alipotangaza kujiingiza katika siasa.
“Siku ya kuapishwa bungeni ilikuwa kazi ngumu kwangu. Pamoja na kuwa mzungumzaji mzuri nilikuwa mwoga nikaona kitu cha ajabu. Nadhani hilo lilitokana na ukweli kwamba baadhi ya magazeti yalishanibeza.
“Baada ya kula kiapo nikaanza kupata ‘vinoti’ vya kunipongeza, mmoja wao alikuwa Kapteni John Komba aliyesema ‘mwanangu umenitoa aibu’.”
Alipoanza kutoa hoja zake bungeni, Amina alionyesha dira njema kwa kuigusa jamii moja kwa moja. Alizungumzia umuhimu wa kuwasaidia wanawake wajawazito na udhibiti wa malaria nchini.
Akawa gumzo kwa walio wengi na hata yale maneno ya kejeli kwamba hakuwa na dira njema zikaanza kuyeyuka. Akavaa koti la umakini na huku akijenga matumaini kwa vijana nchini.
Amina hakuishia katika siasa pekee aliingia kila mahala kwa lengo la kujenga jamii bora. Alihimiza ustawi wa watoto yatima, uendelezwaji wa michezo na sanaa kwa ujumla.
Alikuwa bega kwa bega kuisadia timu ya soka ya taifa (Taifa Stars) lakini pia alikuwa mbioni kuanzisha ligi ya taifa kwa vijana.
Jumatano wiki hii wakati wa kuuga mwili wa marehemu, Ruge Mutahaba ambaye ni mmoja wa wakurugenzi wa Clouds FM ambayo Amina alipata kufanya kazi ya utangazaji, alitaja sifa kubwa ya Amina kuwa ni king’ang’anizi.
“Siwezi kupata lugha rahisi kuelezea ujasiri wake…nitatoa mfano wakati nilipomweleza kuwa anatakiwa kufanya kazi kwa siku sita na kupumzika siku moja akagoma.
“Akatoa wazo kwamba anahitaji kuanzisha kipindi cha taarabu,” anasema Mutahaba na kuongeza kuwa hakuwa na namna ya kumzuia.
“Tukampa nafasi na kweli alifanya vizuri sana katika kipindi hicho cha taarabu na kikubwa zaidi ni kwamba alikuwa mbunifu.”
Naye mtangazaji maarufu nchini, Taji Liundi anayejulikana pia kama ‘Master T’ anamwelezea Amina kuwa mmoja wa wasichana waliokuwa na moyo wa kuthubutu.
“Alikuwa mwenye ujasiri na kuamini kuwa anao uwezo wa kufanya mambo mapya yenye faida kwa jamii.
“Alipenda kuelekezwa kwa kila jambo alilolifanya hata kama alijua kuwa anaweza akalifanya mwenyewe.
“Lakini nasikitika kwamba Amina amefariki dunia bila amani moyoni. Ameondoka wakati mgumu akiwa na msongamano wa mawazo. Hili linaniumiza sana,” anasema Taji.
Wakati fulani alipotembelea kituo kimoja cha watoto yatima jijini Dar es Salaam, Amina aliwahi kumwaga machozi baada ya kuona mazingira waishio watoto hao.
Mapenzi yake kwa watoto yalijionyesha pia wakati akiendesha kipindi cha watoto katika redio.
Katika kipindi chake hicho, alikuwa akipingana sana na baadhi ya wazazi waliokuwa wakifanya matendo mabaya kwa watoto wao. Alikemea unyanyasaji wa watoto.
Lilipokuja suala la mada ya kujadili daima aliibuka mshindi kutokana na uwezo wake wa kujenga hoja na kukubalika. Huo ukawa msingi wa umaarufu wake.
Maelfu ya watu waliofika kuuga mwili wake walionyesha kuwa tayari kuna pengo kubwa katika jamii. Kwamba matarajio na misingi mizuri aliyokuwa ameanza kuijenga Amina bila shaka sasa inakwenda upogo.
Wapo wanaoendelea kushangaa kipaji cha binti huyo kwani katika umri wake mdogo aliweza kufanya mambo makubwa katika jamii tofauti na umri wake.
Amina sasa hatunaye ameshazikwa kijijini kwao Luhanjo-Lupembe Wilaya ya Njombe na kilichobaki sasa ni kuenzi mema yake.
Licha ya kuwa na msimamo katika kupambana na dawa za kulevya, alikuwa mtetezi wa wanawake, vijana, watoto na wanafunzi.
Katika michango yake bungeni. Kwa muda mfupi aliokaa bungeni tangu ale kiapo mjini Dodoma, Desemba 28, 2005, Amina amejipambanua na kuwa miongoni mwa wachangiaji mahiri bungeni, licha ya uchanga wake kisiasa.
Lakini pia alikuwa na mvuto katika jamii na ndiyo maana haikushangaza pale habari zake zilipokuwa zikipewa umuhimu mkubwa katika vyombo vya habari nchini.
Pamoja na hilo, Mei 6 mwaka huu, Amina alianza kuwa kwenye wakati mgumu baada ya kuripotiwa kuwa ametalikiwa na mumewe Mohamed Mpakanjia.
Mpakanjia alikaririwa na vyombo vya habari akisema kuwa ametengana na mkewe huyo aliyedumu naye katika ndoa kwa miaka mitano na kubahatika kupata mtoto mmoja wa kiume.
Kwa bahati mbaya sana mara baada ya taarifa hiyo ya talaka, zikaja taarifa kwamba Amina amelimwa talaka kutokana na kujihusisha kimapenzi na Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe wa Chadema.
Siku tatu baada ya habari za talaka kuripotiwa, baba yake Amina alizungumza na waandishi wa habari kwenye Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Dar es Salaam akisema kuwa suala hilo ni la kisiasa na kwamba CCM inao utaratibu wake wa kutatua mambo yake.
“Masuala yote yanapitia katika mkondo wake. Wazazi hatutaki kuharibu pensheni yetu, si mnajua kuwa siku hizi watoto ndio pensheni?” alisema Mzee Chifupa.
Lakini wanahabari wengi walishangazwa na hatua ya Mzee Chifupa kuitisha kuzungumza katika mkutano huo kwani jana yake Amina aliahidi kuzungumza yeye.
Waandishi walikuwa na shauku ya kukutana na Amina ana kwa ana kwani wiki moja kabla ya kuthibitishwa kwa taarifa za kutalikiwa, anadaiwa alisambaza ujumbe wa maandishi katika simu za mkononi.
Inadaiwa kuwa ujumbe huo ulikwenda kwa baadhi ya watu wanaoaminika kuwa karibu na Naibu Waziri mmoja aliyemtuhumu kusababisha kuvunjika kwa ndoa yake.
Ujumbe ulisomeka hivi: “Alichounganisha Mwenyezi Mungu binadamu hawezi kukitenganisha. Nakuheshimu sana kama kiongozi wangu, Mwenyekiti wangu, Naibu Waziri, M-NEC, M-CCM, mkubwa wangu kiumri, mbunge na kadhalika.
“Nimesikitishwa sana na jitihada za kutaka kuvuruga ndoa yangu, nakutakia kila la heri, lakini usisahau malipo ni hapa hapa duniani na kila mwenye kufanyia wenzake mabaya na yeye hulipwa kwa ubaya.
“Nampenda sana mume wangu na ntailinda ndoa yangu kwa gharama yoyote cko tayari kumpoteza, mi ni zaidi ya mwanamke. Asante sana, kila la heri na kazi njema katika kulifanikisha hilo, wizara
yako nyeti sana, ina mambo mengi sana. Bye.”
Kuna wakati ikasemwa kwamba kuachika kwake kulikuja baada ya Naibu Waziri mmoja kudaiwa kwenda kumchomea utambi kwa mumewe. Baada ya tukio hilo, Amina alitoa ahadi ya kumtaja mbaya wake jambo ambalo halikutimia.
Yapo madai kuwa Naibu Waziri huyo alikuwa na mipango ya kumpaka matope katika siasa kutokana na nia aliyoitangaza ya kutaka kugombea uenyekiti wa taifa wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM).
Amina pia alikuwa ameomba ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC), kupitia Kundi la Vijana katika Uchaguzi Mkuu wa CCM unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.
Juni 22, mwaka huu, Amina aliuliza bungeni kwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, akitaka kufahamishwa hatua gani zinazochukuliwa na Serikali katika kudhibiti uvujaji wa mitihani. Liliulizwa kwa niaba yake na Mbunge wa Muleba Kaskazini, Ruth Msafiri (CCM).
Amina aliyezaliwa Mei 20 mwaka 1981 alikuwa mcheshi na katika moja ya mikakati yake alipata kutamka kuwa ipo siku atajitumbukiza katika kinyang’anyiro katika jimbo.
Hakuishia katika kulitamani jimbo. Alipata kusema pia kuwa anaamini anao ubavu wa kuwa rais wa nchi katika miaka ijayo. Kauli hiyo aliitoa wakati alipohojiwa katika kipindi cha Jahazi cha Radio Clouds FM Mei mwaka huu.
Alisema wanasiasa wengi dunia huwa na ndoto ya kupanda ngazi hadi kufikia urais.
Aliongeza kuwa maisha ya kila mwanadamu huenda kwa malengo. Kwa hakika yaweza kusemwa kuwa maisha ya Amina yalikwenda kwa utaratibu wa kufikiria mambo chanya daima.
Pamoja na hayo, atakumbukwa kwa tukio lililomsibu bungeni mwaka jana wakati alipoagizwa na Spika kutoka nje ya ukumbi wa Bunge kutokana na kuvaa suti ya kike na kofia ya pama bila glovu kwa mujibu wa kanuni.
Mwanasiasa huyo machachari aliyekuwa jasiri mdogo kuliko wote bungeni ambaye alipata nafasi hiyo kupitia tiketi ya Umoja wa Vijana wa CCM.
Siku chache kabla ya kuhudhuria Mkutano wa Tano wa Bunge mwaka jana, Amina alifanya mahojiano na gazeti dada la RAI.
Alifika chumba cha habari kwa ajili ya mahojiano maalumu yaliyochukua takribani saa 2. Akiwa amevalia suti yake nyeusi, hereni ndefu za dhahabu kwenye masikio yake, mkufu wa dhahabu ulioshika vema shingo yake, bangili mikononi mwake vilitosha kumpendezesha nyota huyo aliyezimika ghafla.
Kama ilivyokuwa hulka yake, Amina alisema mengi ya msingi kwa kujiamini na hata alipoulizwa juu ya nini kilichompa ujasiri wa kuapa kwa mbingu bungeni kwamba atawafichua wauza dawa za kulevya hakuonekana kujuta.
“Sikuogopa hata kidogo…ninaamini kuwa mimi ni kiongozi hivyo siwezi kuogopa kusema ukweli,” alisema Amina.
Lakini hakuishia hapo akaongeza: “Kama mtu ni mwoga hafai kuingia bungeni, hatuwezi kuwaacha vijana wa Tanzania wakiangamia kwa matumizi ya dawa za kulevya.”
Alitumia fursa hiyo kuzungumzia namna alivyojisikia vibaya baada ya baadhi ya magazeti na watu mbalimbali kuhoji uwezo wake mara alipotangaza kujiingiza katika siasa.
“Siku ya kuapishwa bungeni ilikuwa kazi ngumu kwangu. Pamoja na kuwa mzungumzaji mzuri nilikuwa mwoga nikaona kitu cha ajabu. Nadhani hilo lilitokana na ukweli kwamba baadhi ya magazeti yalishanibeza.
“Baada ya kula kiapo nikaanza kupata ‘vinoti’ vya kunipongeza, mmoja wao alikuwa Kapteni John Komba aliyesema ‘mwanangu umenitoa aibu’.”
Alipoanza kutoa hoja zake bungeni, Amina alionyesha dira njema kwa kuigusa jamii moja kwa moja. Alizungumzia umuhimu wa kuwasaidia wanawake wajawazito na udhibiti wa malaria nchini.
Akawa gumzo kwa walio wengi na hata yale maneno ya kejeli kwamba hakuwa na dira njema zikaanza kuyeyuka. Akavaa koti la umakini na huku akijenga matumaini kwa vijana nchini.
Amina hakuishia katika siasa pekee aliingia kila mahala kwa lengo la kujenga jamii bora. Alihimiza ustawi wa watoto yatima, uendelezwaji wa michezo na sanaa kwa ujumla.
Alikuwa bega kwa bega kuisadia timu ya soka ya taifa (Taifa Stars) lakini pia alikuwa mbioni kuanzisha ligi ya taifa kwa vijana.
Jumatano wiki hii wakati wa kuuga mwili wa marehemu, Ruge Mutahaba ambaye ni mmoja wa wakurugenzi wa Clouds FM ambayo Amina alipata kufanya kazi ya utangazaji, alitaja sifa kubwa ya Amina kuwa ni king’ang’anizi.
“Siwezi kupata lugha rahisi kuelezea ujasiri wake…nitatoa mfano wakati nilipomweleza kuwa anatakiwa kufanya kazi kwa siku sita na kupumzika siku moja akagoma.
“Akatoa wazo kwamba anahitaji kuanzisha kipindi cha taarabu,” anasema Mutahaba na kuongeza kuwa hakuwa na namna ya kumzuia.
“Tukampa nafasi na kweli alifanya vizuri sana katika kipindi hicho cha taarabu na kikubwa zaidi ni kwamba alikuwa mbunifu.”
Naye mtangazaji maarufu nchini, Taji Liundi anayejulikana pia kama ‘Master T’ anamwelezea Amina kuwa mmoja wa wasichana waliokuwa na moyo wa kuthubutu.
“Alikuwa mwenye ujasiri na kuamini kuwa anao uwezo wa kufanya mambo mapya yenye faida kwa jamii.
“Alipenda kuelekezwa kwa kila jambo alilolifanya hata kama alijua kuwa anaweza akalifanya mwenyewe.
“Lakini nasikitika kwamba Amina amefariki dunia bila amani moyoni. Ameondoka wakati mgumu akiwa na msongamano wa mawazo. Hili linaniumiza sana,” anasema Taji.
Wakati fulani alipotembelea kituo kimoja cha watoto yatima jijini Dar es Salaam, Amina aliwahi kumwaga machozi baada ya kuona mazingira waishio watoto hao.
Mapenzi yake kwa watoto yalijionyesha pia wakati akiendesha kipindi cha watoto katika redio.
Katika kipindi chake hicho, alikuwa akipingana sana na baadhi ya wazazi waliokuwa wakifanya matendo mabaya kwa watoto wao. Alikemea unyanyasaji wa watoto.
Lilipokuja suala la mada ya kujadili daima aliibuka mshindi kutokana na uwezo wake wa kujenga hoja na kukubalika. Huo ukawa msingi wa umaarufu wake.
Maelfu ya watu waliofika kuuga mwili wake walionyesha kuwa tayari kuna pengo kubwa katika jamii. Kwamba matarajio na misingi mizuri aliyokuwa ameanza kuijenga Amina bila shaka sasa inakwenda upogo.
Wapo wanaoendelea kushangaa kipaji cha binti huyo kwani katika umri wake mdogo aliweza kufanya mambo makubwa katika jamii tofauti na umri wake.
Amina sasa hatunaye ameshazikwa kijijini kwao Luhanjo-Lupembe Wilaya ya Njombe na kilichobaki sasa ni kuenzi mema yake.
Licha ya kuwa na msimamo katika kupambana na dawa za kulevya, alikuwa mtetezi wa wanawake, vijana, watoto na wanafunzi.
Katika michango yake bungeni. Kwa muda mfupi aliokaa bungeni tangu ale kiapo mjini Dodoma, Desemba 28, 2005, Amina amejipambanua na kuwa miongoni mwa wachangiaji mahiri bungeni, licha ya uchanga wake kisiasa.
Lakini pia alikuwa na mvuto katika jamii na ndiyo maana haikushangaza pale habari zake zilipokuwa zikipewa umuhimu mkubwa katika vyombo vya habari nchini.
Pamoja na hilo, Mei 6 mwaka huu, Amina alianza kuwa kwenye wakati mgumu baada ya kuripotiwa kuwa ametalikiwa na mumewe Mohamed Mpakanjia.
Mpakanjia alikaririwa na vyombo vya habari akisema kuwa ametengana na mkewe huyo aliyedumu naye katika ndoa kwa miaka mitano na kubahatika kupata mtoto mmoja wa kiume.
Kwa bahati mbaya sana mara baada ya taarifa hiyo ya talaka, zikaja taarifa kwamba Amina amelimwa talaka kutokana na kujihusisha kimapenzi na Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe wa Chadema.
Siku tatu baada ya habari za talaka kuripotiwa, baba yake Amina alizungumza na waandishi wa habari kwenye Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Dar es Salaam akisema kuwa suala hilo ni la kisiasa na kwamba CCM inao utaratibu wake wa kutatua mambo yake.
“Masuala yote yanapitia katika mkondo wake. Wazazi hatutaki kuharibu pensheni yetu, si mnajua kuwa siku hizi watoto ndio pensheni?” alisema Mzee Chifupa.
Lakini wanahabari wengi walishangazwa na hatua ya Mzee Chifupa kuitisha kuzungumza katika mkutano huo kwani jana yake Amina aliahidi kuzungumza yeye.
Waandishi walikuwa na shauku ya kukutana na Amina ana kwa ana kwani wiki moja kabla ya kuthibitishwa kwa taarifa za kutalikiwa, anadaiwa alisambaza ujumbe wa maandishi katika simu za mkononi.
Inadaiwa kuwa ujumbe huo ulikwenda kwa baadhi ya watu wanaoaminika kuwa karibu na Naibu Waziri mmoja aliyemtuhumu kusababisha kuvunjika kwa ndoa yake.
Ujumbe ulisomeka hivi: “Alichounganisha Mwenyezi Mungu binadamu hawezi kukitenganisha. Nakuheshimu sana kama kiongozi wangu, Mwenyekiti wangu, Naibu Waziri, M-NEC, M-CCM, mkubwa wangu kiumri, mbunge na kadhalika.
“Nimesikitishwa sana na jitihada za kutaka kuvuruga ndoa yangu, nakutakia kila la heri, lakini usisahau malipo ni hapa hapa duniani na kila mwenye kufanyia wenzake mabaya na yeye hulipwa kwa ubaya.
“Nampenda sana mume wangu na ntailinda ndoa yangu kwa gharama yoyote cko tayari kumpoteza, mi ni zaidi ya mwanamke. Asante sana, kila la heri na kazi njema katika kulifanikisha hilo, wizara
yako nyeti sana, ina mambo mengi sana. Bye.”
Kuna wakati ikasemwa kwamba kuachika kwake kulikuja baada ya Naibu Waziri mmoja kudaiwa kwenda kumchomea utambi kwa mumewe. Baada ya tukio hilo, Amina alitoa ahadi ya kumtaja mbaya wake jambo ambalo halikutimia.
Yapo madai kuwa Naibu Waziri huyo alikuwa na mipango ya kumpaka matope katika siasa kutokana na nia aliyoitangaza ya kutaka kugombea uenyekiti wa taifa wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM).
Amina pia alikuwa ameomba ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC), kupitia Kundi la Vijana katika Uchaguzi Mkuu wa CCM unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.
Juni 22, mwaka huu, Amina aliuliza bungeni kwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, akitaka kufahamishwa hatua gani zinazochukuliwa na Serikali katika kudhibiti uvujaji wa mitihani. Liliulizwa kwa niaba yake na Mbunge wa Muleba Kaskazini, Ruth Msafiri (CCM).
Amina aliyezaliwa Mei 20 mwaka 1981 alikuwa mcheshi na katika moja ya mikakati yake alipata kutamka kuwa ipo siku atajitumbukiza katika kinyang’anyiro katika jimbo.
Hakuishia katika kulitamani jimbo. Alipata kusema pia kuwa anaamini anao ubavu wa kuwa rais wa nchi katika miaka ijayo. Kauli hiyo aliitoa wakati alipohojiwa katika kipindi cha Jahazi cha Radio Clouds FM Mei mwaka huu.
Alisema wanasiasa wengi dunia huwa na ndoto ya kupanda ngazi hadi kufikia urais.
Aliongeza kuwa maisha ya kila mwanadamu huenda kwa malengo. Kwa hakika yaweza kusemwa kuwa maisha ya Amina yalikwenda kwa utaratibu wa kufikiria mambo chanya daima.
Pamoja na hayo, atakumbukwa kwa tukio lililomsibu bungeni mwaka jana wakati alipoagizwa na Spika kutoka nje ya ukumbi wa Bunge kutokana na kuvaa suti ya kike na kofia ya pama bila glovu kwa mujibu wa kanuni.
Monday, October 8, 2007
Mapatano pwani, baharini ni uvuvi
na innocent munyuku
JUMA la kula na kusaza limeanza. Wenye matumbo na nguvu ya kushika tonge wajiandae. Wajiweke kwa ajili ya kutafuna vinono wakati wa Sikukuu ya Idd el Fitr.
Mzee wa Busati naye anaomba uhai afike mwisho wa juma aungane na wengine katika ulaji la unywaji. Kwa masela siku kama hiyo hawana haja ya kuumiza vichwa manake kila nyumba huwa huru kukaribisha wageni.
Badala ya kula chips dume na maji ya kwenye mifuko ya plastiki siku hiyo ni kutafuna vipapatio vya kuku, pilau na vinywaji vyenye ubora. Mambo ya shangwe hayo.
Wiki hii Mzee wa Busati anaingia ulingoni akiwa na maswali kibao yenye mshangao pia kuhusu kauli ya kiungo wa zamani wa Yanga, Sekilojo Chambua.
Chambua kalalama kwenye vyombo vya habari kwamba uongozi wa Yanga haujatekeleza ahadi zake kwake baada ya kustaafu kuichezea timu hiyo kwa takribani miaka 10.
Nyota huyo alipoamua kupumzika kuichezea Yanga akaahidiwa mema kama vile kulipiwa pango la nyumba kwa mwaka mzima, kununuliwa kiwanja na kusomeshwa ukocha nje ya nchi.
Miaka minne sasa imepita tangu ahadi hizo zitolewe na kwa mujibu wa Chambua hakuna lililotekelezwa. Waliotia saini barua ya ahadi kwa mwanasoka huyo wameingia mitini na kukaa kimya.
Ni habari ya kusikitisha kuona kwamba mchezaji aliyeitumikia timu kwa moyo wake wote akilipwa mshahara na posho hafifu anapewa ahadi hewa kama hizo.
Mzee wa Busati hakika angeishangaa Yanga kama wangetimiza ahadi hizo. Angeshangaa kwa sababu kwa uzoefu wa klabu za Kibongo suala la masilahi kwa wachezaji limekuwa sugu.
Vinara wa klabu daima wamekuwa wenye kupenda sifa kuliko utekelezaji wa masuala muhimu kwa wanaojenga klabu.
Chambua bila shaka ana haki ya kudai kilichoahidiwa kwake na klabu. Waliohusika kumfanyia uhuni mwanasoka huyo waanikwe na ikibidi wachapwe bakora ili uwe mfano kwa wengine.
Husemwa kwamba mapatano kwa kawaida hufanyika pwani ukishaingia habarini ni uvuvi tu hakuna mjadala mwingine labda kama kutatoka dhoruba.
Kwa maana hiyo Yanga inapaswa kutekeleza kilichoandikwa kwenye barua ya ahadi kwa Chambua na si kumletea longolongo.
Kwani kulikuwa na ulazima gani wa kumpa moyo Chambua kama mlijua kuwa mlichoahidi hakitekelezeki? Au mwalitaka kumwiga tembo?
Chambua mbali na kupewa ahadi hewa anadai pia malimbukizo ya mishahara yake na hadi leo hakuna kiongozi wa Yanga anayesimama kutetea haki ya mwanasoka huyo. Wamelala na bila shaka hata majalada hayapo.
Mwandika Busati hasiti kusema kuwa kuna uhuni umefanyika. Dhuluma imedhihirika na watu wanapaswa kuwajibika katika hili.
Anachosema Mzee wa Busati ni kwamba anayolalamikia Chambua yawezekana yametokea kwa wachezaji wengi wa Yanga na klabu nyingine.
Haya ni mambo ambayo yameendelea kwa muda mrefu. Wahusika wamekaa kimya na hivyo kuhalalisha ubaya wa hali hiyo kwa kiwango cha kutisha. Matokeo yake wachezaji hugeuka kuwa ombaomba.
Nani atasimama na kuweka mambo sawia? Hata katika hili twamsubiri Masiha? Kwanini hekima isitumike kuondoa dhuluma hii?
Waungwana daima hutimiza ahadi zao hata kama walifanya makosa katika tamko la awali. Hutekeleza walichosema na kama waliteleza hujipanga upya.
Kwamba Chambua apewe alichoahidiwa na wala hakuna haja ya kwenda njia ndefu apewe chake atulie.
Mzee wa Busati anaelekea ukomo wa Jumanne hii akitoa salamu kwa wadau wake. Kwa waliojaliwa kufunga Ramadhan endeleeni kupata neema.
Kila jema liwakute katika maandalizi ya kumaliza mfungo lakini msije mkaleta balaa kwa kuzidisha kipimo cha furaha siku ikifika.
Wasalaam,
JUMA la kula na kusaza limeanza. Wenye matumbo na nguvu ya kushika tonge wajiandae. Wajiweke kwa ajili ya kutafuna vinono wakati wa Sikukuu ya Idd el Fitr.
Mzee wa Busati naye anaomba uhai afike mwisho wa juma aungane na wengine katika ulaji la unywaji. Kwa masela siku kama hiyo hawana haja ya kuumiza vichwa manake kila nyumba huwa huru kukaribisha wageni.
Badala ya kula chips dume na maji ya kwenye mifuko ya plastiki siku hiyo ni kutafuna vipapatio vya kuku, pilau na vinywaji vyenye ubora. Mambo ya shangwe hayo.
Wiki hii Mzee wa Busati anaingia ulingoni akiwa na maswali kibao yenye mshangao pia kuhusu kauli ya kiungo wa zamani wa Yanga, Sekilojo Chambua.
Chambua kalalama kwenye vyombo vya habari kwamba uongozi wa Yanga haujatekeleza ahadi zake kwake baada ya kustaafu kuichezea timu hiyo kwa takribani miaka 10.
Nyota huyo alipoamua kupumzika kuichezea Yanga akaahidiwa mema kama vile kulipiwa pango la nyumba kwa mwaka mzima, kununuliwa kiwanja na kusomeshwa ukocha nje ya nchi.
Miaka minne sasa imepita tangu ahadi hizo zitolewe na kwa mujibu wa Chambua hakuna lililotekelezwa. Waliotia saini barua ya ahadi kwa mwanasoka huyo wameingia mitini na kukaa kimya.
Ni habari ya kusikitisha kuona kwamba mchezaji aliyeitumikia timu kwa moyo wake wote akilipwa mshahara na posho hafifu anapewa ahadi hewa kama hizo.
Mzee wa Busati hakika angeishangaa Yanga kama wangetimiza ahadi hizo. Angeshangaa kwa sababu kwa uzoefu wa klabu za Kibongo suala la masilahi kwa wachezaji limekuwa sugu.
Vinara wa klabu daima wamekuwa wenye kupenda sifa kuliko utekelezaji wa masuala muhimu kwa wanaojenga klabu.
Chambua bila shaka ana haki ya kudai kilichoahidiwa kwake na klabu. Waliohusika kumfanyia uhuni mwanasoka huyo waanikwe na ikibidi wachapwe bakora ili uwe mfano kwa wengine.
Husemwa kwamba mapatano kwa kawaida hufanyika pwani ukishaingia habarini ni uvuvi tu hakuna mjadala mwingine labda kama kutatoka dhoruba.
Kwa maana hiyo Yanga inapaswa kutekeleza kilichoandikwa kwenye barua ya ahadi kwa Chambua na si kumletea longolongo.
Kwani kulikuwa na ulazima gani wa kumpa moyo Chambua kama mlijua kuwa mlichoahidi hakitekelezeki? Au mwalitaka kumwiga tembo?
Chambua mbali na kupewa ahadi hewa anadai pia malimbukizo ya mishahara yake na hadi leo hakuna kiongozi wa Yanga anayesimama kutetea haki ya mwanasoka huyo. Wamelala na bila shaka hata majalada hayapo.
Mwandika Busati hasiti kusema kuwa kuna uhuni umefanyika. Dhuluma imedhihirika na watu wanapaswa kuwajibika katika hili.
Anachosema Mzee wa Busati ni kwamba anayolalamikia Chambua yawezekana yametokea kwa wachezaji wengi wa Yanga na klabu nyingine.
Haya ni mambo ambayo yameendelea kwa muda mrefu. Wahusika wamekaa kimya na hivyo kuhalalisha ubaya wa hali hiyo kwa kiwango cha kutisha. Matokeo yake wachezaji hugeuka kuwa ombaomba.
Nani atasimama na kuweka mambo sawia? Hata katika hili twamsubiri Masiha? Kwanini hekima isitumike kuondoa dhuluma hii?
Waungwana daima hutimiza ahadi zao hata kama walifanya makosa katika tamko la awali. Hutekeleza walichosema na kama waliteleza hujipanga upya.
Kwamba Chambua apewe alichoahidiwa na wala hakuna haja ya kwenda njia ndefu apewe chake atulie.
Mzee wa Busati anaelekea ukomo wa Jumanne hii akitoa salamu kwa wadau wake. Kwa waliojaliwa kufunga Ramadhan endeleeni kupata neema.
Kila jema liwakute katika maandalizi ya kumaliza mfungo lakini msije mkaleta balaa kwa kuzidisha kipimo cha furaha siku ikifika.
Wasalaam,
Monday, October 1, 2007
Safari hii msikubali matege
na innocent munyuku
KUMEKUCHA na bila shaka mambo yanakwenda katika unyoofu wake. Kama kuna matatizo hayo hayakwepeki kwa vile ni mpango wa maisha ya kila siku.
Mzee wa Busati yu katika mlolongo wake wa kuwapa porojo zake za kila wiki. Hii yaweza kuitwa wiki ya vicheko kwani walio wengi nafuu ingalipo. Mapato ya mwezi Septemba yangali yakionekana kibindoni. Si haba!
Linalomweka Mwandika Busati leo hii ni huu ujio wa kocha mpya wa Yanga Wojciech Lazarek wa nchini Poland. Kocha huyo mpya anakuja kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Milutin Sredejovic `Micho`.
Kwa wapenzi wa mpira hasa mashabiki wa Yanga kuja kwa Mpoland huyo ni ishara ya pambazuko kwa masilahi ya timu hiyo.
Mzee wa Busati kama walivyo wadau wengine katika eneo hilo hana budi kutoa mawazo yake kuhusiana na ujio wa kocha huyo mpya. Hasemi kwa mabaya bali kuwekana sawa ili mambo yakiwa sivyo basi wenye Yanga wasilalame kwamba hawakuambiwa.
Kwa mtazamo mwepesi tu ni kwamba licha ya kuwa Mpoland huyo wasifu wake unatia moyo katika soka, bado anahitaji kupewa nafasi ya kujitanua katika kutimiza wajibu wake.
Kuna hila ndani ya klabu za soka nchini Tanzania. Kwamba hapa kwa Wadanganyika kila jambo hufanywa kwa mazoea tena mazoea mabaya.
Kazi kubwa ya hao wanaojiita mashabiki na wenye Yanga yao ni kutoa kasoro kwa walimu hata kama kocha huyo ana siku mbili kambini na wachezaji.
Jukumu lao ni kupiga soga barazani wakipanga kile wanachokiita ubora wa timu lakini ukweli wa mambo ni kwamba wengi wao ni watengenezaji wa fitina ndani ya soka.
Hawana lolote la maana ndani ya mitima yao. Badala yake wamejaa porojo zilizokosa miguu na fikra pevu. Hawa ndio wa kwanza kupiga kelele kwamba fulani hafai lakini ukiwauliza mbadala hawana.
Hupayuka kwamba timu fulani ni yao lakini ukiwaambia watoe hapo senti 10 kwa ajili ya wachezaji wanakimbia mithili ya duma nyikani. Hawataki majukumu huku wakisisitiza kuwa hiyo ni timu yao.
Basi kama mambo ni hayo, kocha mpya ajaye Yanga apewe nafasi ya kutimiza majukumu yake na kamwe asitengenezewe vigingi vya hapa na pale.
Ni wazi kwamba mpira wa Kibongo ni mgumu kutokana na ukweli kwamba hakuna mwekezaji makini aliyejitokeza na kuweka vitalu vya soka.
Timu zote zimebaki kuwakusanya wachezaji kwa kutumia vigezo dhaifu na ndio maana si jambo la ajabu kusikia Mwambungu kasajiliwa Simba leo na kesho ukaambiwa kiwango chake kimeshuka.
Wanaosema fulani kashuka kiwango ni mashabiki na hapo kama mwalimu si makini basi kesho yake ataanza kumweka mchezaji benchi badala ya kumsaidia mwanasoka huyo arejee kileleni.
Hoja hapa ni kwamba midomo ya mashabiki kwa kawaida imekuwa ikiwaponza hata viongozi wa klabu husika na kufanya maamuzi yasiyofaa.
Kwa maneno mengine ni kwamba imefika pahala viongozi wa soka nchini wakafanana uamuzi na mashabiki wao. Hapo hakuna jipya zaidi ya kupanga timu wapendavyo.
Hujapata kusikia kuwa mchezaji fulani ni kipenzi cha kiongozi fulani? Kwa hiyo kama mchezaji huyo hakupangwa basi hapo kocha huingia matatani. Atasemwa kwa ubaya na hata atengwe na kaya.
Huu si muda wa kuendeleza fitina ndani ya soka kwa maana hiyo ujio wa kocha mpya kwa Wanajangwani kujengwe kwa uzio wa subira na nidhamu kwa mwalimu huyo.
Mzee wa Busati anayasema hayo kwa vile anaelewa baadhi ya mambo ya kihuni ndani ya klabu za soka nchini. Huko kila mmoja ana uamuzi wake atakavyo hata kama ni kupoteza dira ya maendeleo.
Wanachoangalia ni masilahi ya leo na si kujenga soka kwa ajili ya maisha mema ya wachezaji na ustawi wa nchi. Wao wanaharibu na ukiwauliza watakwambia atakayekuja atajenga ukuta baada ya wao kupuuzia nyufa.
Kama mpira wa kusutana na kuwashambulia makocha utaendelea katika uso wa Wadanganyika basi mjue kuwa hiyo ni laana katika mpira wa miguu nchini na hata kama atakuja Dunga kuwafundisha bado mtakwama.
Mtazidi kukwamba kutokana na ukweli kwamba masikio yenu yamejaa nta na hamtaki kukubali kwamba kuna umuhimu wa mabadiliko.
Kinachosemwa na Mwandika Busati ni kwamba suala la makocha kuzikimbia timu baada ya muda mfupi si la kupuuzia. Kuna haja ya kuangalia wapi kuna tatizo.
Hawa wanaokimbia si wendawazimu hata kidogo, wana akili timamu na wanapoona makubaliano hafifu hulazimika kukitoa ili kulinda heshima zao.
Basi kwa wenye upeo wa utambuzi wa mema wadake haya yasemwayo na Mzee wa Busati kwamba safari hii Yanga msikubali matege katika kushirikiana na kocha mpya ajaye.
Wenye dhamana ya kuitawala Yanga, enendeni mkahubiri uvumilivu na moyo wa ushirikiano kwa mashabiki wenu. Vinginevyo itabaki hadithi ile ile ya kale kwamba Jangwani na Msimbazi hakukaliki.
Wasalaam,
KUMEKUCHA na bila shaka mambo yanakwenda katika unyoofu wake. Kama kuna matatizo hayo hayakwepeki kwa vile ni mpango wa maisha ya kila siku.
Mzee wa Busati yu katika mlolongo wake wa kuwapa porojo zake za kila wiki. Hii yaweza kuitwa wiki ya vicheko kwani walio wengi nafuu ingalipo. Mapato ya mwezi Septemba yangali yakionekana kibindoni. Si haba!
Linalomweka Mwandika Busati leo hii ni huu ujio wa kocha mpya wa Yanga Wojciech Lazarek wa nchini Poland. Kocha huyo mpya anakuja kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Milutin Sredejovic `Micho`.
Kwa wapenzi wa mpira hasa mashabiki wa Yanga kuja kwa Mpoland huyo ni ishara ya pambazuko kwa masilahi ya timu hiyo.
Mzee wa Busati kama walivyo wadau wengine katika eneo hilo hana budi kutoa mawazo yake kuhusiana na ujio wa kocha huyo mpya. Hasemi kwa mabaya bali kuwekana sawa ili mambo yakiwa sivyo basi wenye Yanga wasilalame kwamba hawakuambiwa.
Kwa mtazamo mwepesi tu ni kwamba licha ya kuwa Mpoland huyo wasifu wake unatia moyo katika soka, bado anahitaji kupewa nafasi ya kujitanua katika kutimiza wajibu wake.
Kuna hila ndani ya klabu za soka nchini Tanzania. Kwamba hapa kwa Wadanganyika kila jambo hufanywa kwa mazoea tena mazoea mabaya.
Kazi kubwa ya hao wanaojiita mashabiki na wenye Yanga yao ni kutoa kasoro kwa walimu hata kama kocha huyo ana siku mbili kambini na wachezaji.
Jukumu lao ni kupiga soga barazani wakipanga kile wanachokiita ubora wa timu lakini ukweli wa mambo ni kwamba wengi wao ni watengenezaji wa fitina ndani ya soka.
Hawana lolote la maana ndani ya mitima yao. Badala yake wamejaa porojo zilizokosa miguu na fikra pevu. Hawa ndio wa kwanza kupiga kelele kwamba fulani hafai lakini ukiwauliza mbadala hawana.
Hupayuka kwamba timu fulani ni yao lakini ukiwaambia watoe hapo senti 10 kwa ajili ya wachezaji wanakimbia mithili ya duma nyikani. Hawataki majukumu huku wakisisitiza kuwa hiyo ni timu yao.
Basi kama mambo ni hayo, kocha mpya ajaye Yanga apewe nafasi ya kutimiza majukumu yake na kamwe asitengenezewe vigingi vya hapa na pale.
Ni wazi kwamba mpira wa Kibongo ni mgumu kutokana na ukweli kwamba hakuna mwekezaji makini aliyejitokeza na kuweka vitalu vya soka.
Timu zote zimebaki kuwakusanya wachezaji kwa kutumia vigezo dhaifu na ndio maana si jambo la ajabu kusikia Mwambungu kasajiliwa Simba leo na kesho ukaambiwa kiwango chake kimeshuka.
Wanaosema fulani kashuka kiwango ni mashabiki na hapo kama mwalimu si makini basi kesho yake ataanza kumweka mchezaji benchi badala ya kumsaidia mwanasoka huyo arejee kileleni.
Hoja hapa ni kwamba midomo ya mashabiki kwa kawaida imekuwa ikiwaponza hata viongozi wa klabu husika na kufanya maamuzi yasiyofaa.
Kwa maneno mengine ni kwamba imefika pahala viongozi wa soka nchini wakafanana uamuzi na mashabiki wao. Hapo hakuna jipya zaidi ya kupanga timu wapendavyo.
Hujapata kusikia kuwa mchezaji fulani ni kipenzi cha kiongozi fulani? Kwa hiyo kama mchezaji huyo hakupangwa basi hapo kocha huingia matatani. Atasemwa kwa ubaya na hata atengwe na kaya.
Huu si muda wa kuendeleza fitina ndani ya soka kwa maana hiyo ujio wa kocha mpya kwa Wanajangwani kujengwe kwa uzio wa subira na nidhamu kwa mwalimu huyo.
Mzee wa Busati anayasema hayo kwa vile anaelewa baadhi ya mambo ya kihuni ndani ya klabu za soka nchini. Huko kila mmoja ana uamuzi wake atakavyo hata kama ni kupoteza dira ya maendeleo.
Wanachoangalia ni masilahi ya leo na si kujenga soka kwa ajili ya maisha mema ya wachezaji na ustawi wa nchi. Wao wanaharibu na ukiwauliza watakwambia atakayekuja atajenga ukuta baada ya wao kupuuzia nyufa.
Kama mpira wa kusutana na kuwashambulia makocha utaendelea katika uso wa Wadanganyika basi mjue kuwa hiyo ni laana katika mpira wa miguu nchini na hata kama atakuja Dunga kuwafundisha bado mtakwama.
Mtazidi kukwamba kutokana na ukweli kwamba masikio yenu yamejaa nta na hamtaki kukubali kwamba kuna umuhimu wa mabadiliko.
Kinachosemwa na Mwandika Busati ni kwamba suala la makocha kuzikimbia timu baada ya muda mfupi si la kupuuzia. Kuna haja ya kuangalia wapi kuna tatizo.
Hawa wanaokimbia si wendawazimu hata kidogo, wana akili timamu na wanapoona makubaliano hafifu hulazimika kukitoa ili kulinda heshima zao.
Basi kwa wenye upeo wa utambuzi wa mema wadake haya yasemwayo na Mzee wa Busati kwamba safari hii Yanga msikubali matege katika kushirikiana na kocha mpya ajaye.
Wenye dhamana ya kuitawala Yanga, enendeni mkahubiri uvumilivu na moyo wa ushirikiano kwa mashabiki wenu. Vinginevyo itabaki hadithi ile ile ya kale kwamba Jangwani na Msimbazi hakukaliki.
Wasalaam,
Subscribe to:
Posts (Atom)