Na Innocent Munyuku
WAKATI fulani mwaka jana nilipata kuandika habari ya mwanamuziki Vitali Maembe na kundi lake la Bagamoyo Spirits. Nikamweka msanii huyo miongoni mwa wakali waliopata kutokea katika uso wa dunia.
Huo ni mtazamo wangu kwamba kwa namna anavyosonga mbele kwa kasi ya ajabu, ni wazi kuwa Maembe na kundi lake anayo nafasi ya kufanya vema katika safari yake ya muziki huko aendako.
Hilo linatokana na ukweli kwamba tofauti na wanamuziki wengi wa kizazi kipya nchini Tanzania, Maembe na kundi lake wanapiga vyombo vya asili. Midundo ukiisikiliza huwezi kupata ladha ya Kimagharibi.
Vitali Maembe? Pengine wengi watajiuliza. Ndio ni Maembe yule aliyevuma na kibao cha Sumu ya Teja na baadaye akaja na wimbo wa Kariakoo. Hivi karibuni kaibuka upya na kibao cha Shangilia Taifa Stars pamoja na Mchakamchaka.
Hata hivyo, ukweli wa mambo ni kwamba katika mafanikio yote hayo, Maembe naweza kutamka kuwa anabebwa kwa kiasi kikubwa na mmoja wa wasanii chipukizi. Huyu ni Manyama Nyambasi mwenye umri wa miaka 15.
Pengine neno kubebwa laweza kuleta ukakasi kwa mashabiki wa Maembe ila kusudio langu ni kuweka bayana moja ya siri za mafanikio kwa mwanamuziki huyo.
Nyambasi kwa umri wake huo mdogo ndiye kinara wa upigaji ngoma katika kundi hilo. Kijana huyo ambaye alianza kuchomoza kwenye vyombo vya habari zaidi ya miaka mitano nyuma anamudu kupiga ngoma 12.
Msanii huyo chipukizi kwa hakika ni nuru kwa Maembe na kundi lake. Daima ni makini katika upigaji wa ngoma zake anazozipiga kwa ustadi mkubwa.
Cha kufurahisha ni kwamba licha ya uwingi wa ngoma hizo, Manyama anamudu kuzipiga mfululizo kwa zaidi ya dakika 20.
Pengine huyu aweza kuitwa mrithi sahihi wa msanii aliyewahi kuvuma nchini Tanzania, marehemu Morris Nyunyusa kutokana na umahiri wake huo.
Pamoja na uwepo wa Manyama katika kundi la Bagamoyo Spirits, bado anahitaji msaada wa kunogesha midundo ya ngoma zake. Rafiki yake mkubwa jukwaani ni Salum Mpute.
Mpute kama alivyo Manyama, ana umri wa miaka 15 na kazi yake kubwa jukwaani licha ya kuimba baadhi ya mashairi, hupiga manyanga. Ukali wao waweza kufananishwa na pilipili au moto wa kuotea mbali kama wengine wanavyosema.
Hii ni hazina ya Bagamoyo Spirits kwani kama ulivyo msimamo wa kiongozi wao, Maembe hawana haja ya kukimbilia midundo ya Ulaya na Marekani.
Hawako tayari kusahau asili yao ambayo ni bara la Afrika. Hawabezi ngoma wala manyanga.
Hawataki kuwa miongoni mwa vijana wenye akili za utumwa. Vijana ambao wanaendelea kuamini kwamba kila wakionacho kwenye runinga basi ni cha kuigwa.
Kutokana na hilo ndio maana wengi wao hawajui kupiga ala mbalimbali za muziki. Je, na hawa tuwaite wanamuziki? Hapana!
Kwa muungano huo wa Bagamoyo Spirits, hawana cha kujuta kwa sababu kitendo chao cha kuweka lafudhi za Kiafrika kwenye kazi zao vibao vyao vinavuma katika kona nyingi duniani.
Katika albamu ya BAGAMOYO unaweza kuwa shuhuda wa uhondo wa midundo ya kiafrika katika nyimbo hizo. Kuna vibao kama Afrika Shilingi Tano, Sumu ya Teja, Toka na Asalaam Aleykhum. Hizi ziko katika video huko Mbwa wa Kiombwe, Naropoka, Kipande cha Papa, Kinoo na Hamia Ndege zikisubiri.
Tumwangalie Maembe na Bagamoyo Spirits lakini pia tuwapaishe kina Manyama na Mpute waendeleze vipaji vyao wakiwa ndani ya kundi hilo linalotamba na mtindo wa Motokaa.
Sunday, April 29, 2007
Zemkala: Twatetea utamaduni wa Mtanzania
Na Innocent Munyuku
NAWAITA marafiki wa sanaa lakini wao hujiita Zemkala. Hili ni kundi la muziki asilia lenye maskani yake jijini Dar es Salaam.
Nimeshakutana nao mara nyingi katika matamasha mbalimbali. Pia wakati mwingine hujumuika nao kwenye mazoezi yao.
Ijumaa ya Aprili 6 mwaka huu nilikutana tena na wasanii hawa katika Ukumbi wa Hoteli ya Rombo Green View barabara ya Shekilango jijini Dar es Salaam. Walikuwa hapo kupendezesha hafla ya kuwatunuku waandishi bora wa habari za utamaduni na sanaa kwa mwaka uliopita.
Tofauti na nilivyowaona kiasi cha miezi miwili nyuma, Zemkala wamepaa. Wameongeza uwezo katika nyanja mbalimbali kama vile kutawala jukwaa na vyombo pia.
Moyo wangu ulifarijika kuona kuwa kile walichonieleza zaidi ya mwaka mmoja uliopita kuwa wameingia ulingoni kwa ajili ya kuhakikisha wanautangaza utamaduni wa Mtanzania.
Lakini mbali na hili walichonieleza siku ya kwanza kuonana nao ni kwamba wanalenga pia kujikwamua kimaisha na kuachana na mpango wa kukaa vijiweni kupiga soga.
Ni kundi linaloundwa na wasanii wanane ambao bado umri wao haujavuka miaka 30. Wangali na damu mbichi katika kueneza mila na utamaduni wa Mtanzania katika nchi mbalimbali duniani.
Wanaounda kundi hilo ni Yuster Nyakachara, Havintishi Baraza, Fadhili Mkenda, Yusuf Chambuso, Maulid Mastir, Kasembe Ungani, Shabaan Mugado na Fred Saganda.
Uzuri wa kundi hili ni kwamba karibu kila msaani ana uwezo wa kuimba, kupiga ala.
Kundi lilianza kupata uhai mwaka 2002, waanzilishi wakiwa Ungani na Mkenda. Hawa walijiengua kutoka Sisi Tambala.
Ni zaidi ya miaka minne sasa tangu liibuke na kwa hakika unapozungumza nao wanasema kila siku inaleta neema mpya.
Hilo lina ukweli kwani wameshasafiri katika nchi mbalimbali kuitangaza Tanzania kupitia ngoma na sauti zao za kuvutia.
Wameshafanya maonyesho Sweden, Msumbiji, Kenya na Zanzibar na katika ziara zote hizo wameacha gumzo kwa mashabiki wao.
Wanachosema Zemkala ni kwamba ifike siku Tanzania ijulikane kupitia ngoma zake kama walivyofanikiwa Wakongo au mataifa ya Afrika Magharibi.
Daima wanajivunia asili yao na utamaduni wa Kiafrika. Hawajatafunwa na utumwa wa akili. Wangali na fikra pevu.
Hushangaa kuona baadhi ya Watanzania hasa vijana wanakataa kucheza ngoma za asili na badala yake kukimbilia disko na kuiga utamaduni wa Kimagharibi.
Lakini kinachowasikitisha zaidi ni kwamba wananchi wengi hawana utamaduni wa kwenda kuangalia ngoma za asili.
“Hapa hakuna ari ya kupenda hizi ngoma, watu wanapenda muziki wa dansi au disko,” anasemaYusta ambaye ni kiongozi wa Zemkala.
“Hakuna kulala tutapigania haki zetu na utamaduni wa Mtanzania na bara la Afrika,” anasema Yusta.
Zemkala ni neno la Kiyao likiwa na maana ya maendeleo. Kwa namna hiyo vijana hawa hawana masihara katika kusaka ujira wao wa kila siku.
NAWAITA marafiki wa sanaa lakini wao hujiita Zemkala. Hili ni kundi la muziki asilia lenye maskani yake jijini Dar es Salaam.
Nimeshakutana nao mara nyingi katika matamasha mbalimbali. Pia wakati mwingine hujumuika nao kwenye mazoezi yao.
Ijumaa ya Aprili 6 mwaka huu nilikutana tena na wasanii hawa katika Ukumbi wa Hoteli ya Rombo Green View barabara ya Shekilango jijini Dar es Salaam. Walikuwa hapo kupendezesha hafla ya kuwatunuku waandishi bora wa habari za utamaduni na sanaa kwa mwaka uliopita.
Tofauti na nilivyowaona kiasi cha miezi miwili nyuma, Zemkala wamepaa. Wameongeza uwezo katika nyanja mbalimbali kama vile kutawala jukwaa na vyombo pia.
Moyo wangu ulifarijika kuona kuwa kile walichonieleza zaidi ya mwaka mmoja uliopita kuwa wameingia ulingoni kwa ajili ya kuhakikisha wanautangaza utamaduni wa Mtanzania.
Lakini mbali na hili walichonieleza siku ya kwanza kuonana nao ni kwamba wanalenga pia kujikwamua kimaisha na kuachana na mpango wa kukaa vijiweni kupiga soga.
Ni kundi linaloundwa na wasanii wanane ambao bado umri wao haujavuka miaka 30. Wangali na damu mbichi katika kueneza mila na utamaduni wa Mtanzania katika nchi mbalimbali duniani.
Wanaounda kundi hilo ni Yuster Nyakachara, Havintishi Baraza, Fadhili Mkenda, Yusuf Chambuso, Maulid Mastir, Kasembe Ungani, Shabaan Mugado na Fred Saganda.
Uzuri wa kundi hili ni kwamba karibu kila msaani ana uwezo wa kuimba, kupiga ala.
Kundi lilianza kupata uhai mwaka 2002, waanzilishi wakiwa Ungani na Mkenda. Hawa walijiengua kutoka Sisi Tambala.
Ni zaidi ya miaka minne sasa tangu liibuke na kwa hakika unapozungumza nao wanasema kila siku inaleta neema mpya.
Hilo lina ukweli kwani wameshasafiri katika nchi mbalimbali kuitangaza Tanzania kupitia ngoma na sauti zao za kuvutia.
Wameshafanya maonyesho Sweden, Msumbiji, Kenya na Zanzibar na katika ziara zote hizo wameacha gumzo kwa mashabiki wao.
Wanachosema Zemkala ni kwamba ifike siku Tanzania ijulikane kupitia ngoma zake kama walivyofanikiwa Wakongo au mataifa ya Afrika Magharibi.
Daima wanajivunia asili yao na utamaduni wa Kiafrika. Hawajatafunwa na utumwa wa akili. Wangali na fikra pevu.
Hushangaa kuona baadhi ya Watanzania hasa vijana wanakataa kucheza ngoma za asili na badala yake kukimbilia disko na kuiga utamaduni wa Kimagharibi.
Lakini kinachowasikitisha zaidi ni kwamba wananchi wengi hawana utamaduni wa kwenda kuangalia ngoma za asili.
“Hapa hakuna ari ya kupenda hizi ngoma, watu wanapenda muziki wa dansi au disko,” anasemaYusta ambaye ni kiongozi wa Zemkala.
“Hakuna kulala tutapigania haki zetu na utamaduni wa Mtanzania na bara la Afrika,” anasema Yusta.
Zemkala ni neno la Kiyao likiwa na maana ya maendeleo. Kwa namna hiyo vijana hawa hawana masihara katika kusaka ujira wao wa kila siku.
Wazo la BASATA kufufua taarabu asilia liungwe mkono
na innocent munyuku
MAPEMA wiki hii nilikuwa mmoja wanahabari walioalikwa kuhudhuria kikao cha 17 cha Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) jijini Dar es Salaam.
Katika hotuba yake fupi kwa wajumbe wa Baraza, Mwenyekiti wa BASATA, Dk. Frowin Nyoni alizungumzia umuhimu wa wajumbe kuchangia ajenda zilizopo ili kuwa na maamuzi yenye kujenga sanaa nchini.
Mengi yalisemwa na wajumbe kuchangia ajenda hizo ambazo nyingi zilielekeza katika ukuzaji wa sanaa na kuinua hali za maisha ya wasanii Tanzania ambao wengi wao wanaishi kwa taabu.
Lakini moja ya hoja iliyonivutia katika kikao hicho ni azma ya BASATA ya kuifufua taarabu asilia hapa nchini.
Dk. Nyoni alitamka kuwa kwa miaka ya hivi karibuni wamebaini muziki wa taarabu asilia unapotea na wenye uwezo wa kuanzisha vikundi vya taarabu wamebadili ladha ya muziki huyo kwa kile kilichopewa jina la modern taarabu.
ÒTaarabu asilia imekosa mashabiki lakini bado ipo nafasi ya kuwahamasisha wananchi kuipenda taarabu,Ó alisema Dk. Nyoni.
Hata hivyo, Dk. Nyoni aliongeza kuwa kuna vikwazo vya muziki huo kusonga mbele na anavitaja kuwa ni pamoja na ukosefu wa ala halisi kwa ajili ya taarabu muziki.
ÒHatuna maduka ya vyombo vya asiliaÉkwa hiyo mtu mwenye kikundi chake atakimbilia Kariakoo kununua gitaa lake na kinanda, jioni anafanya onyesho.
ÒHakuna duka linauza vifaa kama vile violin au akodiani,Ó alieleza Dk. Nyoni.
Kauli ya Dk. Nyoni kuhusu kufufua muziki wa taarabu ikanikumbusha maneno ya rafiki yangu marehemu Issa Matona kwamba taarabu ilishapoteza mwelekeo.
Matona alipozungumza nami zaidi ya zaidi ya miaka mitano iliyopita alisema anapata uchungu mkubwa kwa kuona muziki wa taarabu unaharibiwa kwa kuleta kile kinachoitwa modern taarabu.
Nakumbuka Matona alisema ÒMuziki wa taarabu una miiko yake, taarabu haichezwi kwa kukata mauno kama ndomboloÉmashairi pia wameyaharibu. Siku hizi wanaimba matusi ya wazi wazi.Ó
Matona ambaye atakumbukwa kuwa mwanamuziki aliyebobea katika taarabu na mkali wa mashairi alikuwa akijaribu kuwahimiza wanamuziki kwenye reli hiyo waache kuuharibu.
Kwa upande wa BASATA, ukuzaji wa muziki huo umewekewa programu ya miaka minne (2006-2010). Mpango huo utagharimu shilingi bilioni 1.6.
Katika hilo, wasanii mbalimbali watahamasishwa ili kutimiza lengo la kuupa hadhi yake muziki wa taarabu asilia.
Kwa mujibu wa historia, muziki huo uliletwa Zanzibar na Waarabu wa Oman katika karne ya 19 wakileta vifaa, tungo na hata lugha iliyotumika ilikuwa ni Kiarabu.
Lakini pia miiko ya muziki huo ni kwamba si muziki wa kucheza kwa nguvu bali uliundwa ili usikilizwe.
Baadaye watunzi wa Kizanzibari nao walianza kutunga mashairi wakitumia Kiswahili kwa kutumia melodia za Kimisri na Kihindi na inaaminika kuwa mwaka 1930 muziki huo ukaingia Tanganyika na kujikita katika miji ya Morogoro, Dodoma, Tabora, Mwanza na Kigoma.
Tangu wakati huo, muziki huo ulianza kukua na kuenea sehemu nyingi za Tanzania lakini kwa bahati mbaya uasili wake ukaanza kupotea siku hadi siku.
Kumekuwa na matatizo yaliyochangia muziki huo ukafa kama ilivyodokezwa awali lakini vikwazo vingine ni ukosefu wa wawekezaji na udhaifu katika uongozi na utawala.
Pamoja na matatizo hayo, BASATA imeweka mkakati maalumu wa kuboresha ufahamu na taaluma na kuhakikisha kuwa upatikanaji wa vifaa vya muziki huo hauwi kikwazo tena.
Lakini pia imepangwa kufanya uwekezaji na kutenga mfuko maalumu wa kusaidia ukuaji wa muziki wa taarabu asilia.
MAPEMA wiki hii nilikuwa mmoja wanahabari walioalikwa kuhudhuria kikao cha 17 cha Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) jijini Dar es Salaam.
Katika hotuba yake fupi kwa wajumbe wa Baraza, Mwenyekiti wa BASATA, Dk. Frowin Nyoni alizungumzia umuhimu wa wajumbe kuchangia ajenda zilizopo ili kuwa na maamuzi yenye kujenga sanaa nchini.
Mengi yalisemwa na wajumbe kuchangia ajenda hizo ambazo nyingi zilielekeza katika ukuzaji wa sanaa na kuinua hali za maisha ya wasanii Tanzania ambao wengi wao wanaishi kwa taabu.
Lakini moja ya hoja iliyonivutia katika kikao hicho ni azma ya BASATA ya kuifufua taarabu asilia hapa nchini.
Dk. Nyoni alitamka kuwa kwa miaka ya hivi karibuni wamebaini muziki wa taarabu asilia unapotea na wenye uwezo wa kuanzisha vikundi vya taarabu wamebadili ladha ya muziki huyo kwa kile kilichopewa jina la modern taarabu.
ÒTaarabu asilia imekosa mashabiki lakini bado ipo nafasi ya kuwahamasisha wananchi kuipenda taarabu,Ó alisema Dk. Nyoni.
Hata hivyo, Dk. Nyoni aliongeza kuwa kuna vikwazo vya muziki huo kusonga mbele na anavitaja kuwa ni pamoja na ukosefu wa ala halisi kwa ajili ya taarabu muziki.
ÒHatuna maduka ya vyombo vya asiliaÉkwa hiyo mtu mwenye kikundi chake atakimbilia Kariakoo kununua gitaa lake na kinanda, jioni anafanya onyesho.
ÒHakuna duka linauza vifaa kama vile violin au akodiani,Ó alieleza Dk. Nyoni.
Kauli ya Dk. Nyoni kuhusu kufufua muziki wa taarabu ikanikumbusha maneno ya rafiki yangu marehemu Issa Matona kwamba taarabu ilishapoteza mwelekeo.
Matona alipozungumza nami zaidi ya zaidi ya miaka mitano iliyopita alisema anapata uchungu mkubwa kwa kuona muziki wa taarabu unaharibiwa kwa kuleta kile kinachoitwa modern taarabu.
Nakumbuka Matona alisema ÒMuziki wa taarabu una miiko yake, taarabu haichezwi kwa kukata mauno kama ndomboloÉmashairi pia wameyaharibu. Siku hizi wanaimba matusi ya wazi wazi.Ó
Matona ambaye atakumbukwa kuwa mwanamuziki aliyebobea katika taarabu na mkali wa mashairi alikuwa akijaribu kuwahimiza wanamuziki kwenye reli hiyo waache kuuharibu.
Kwa upande wa BASATA, ukuzaji wa muziki huo umewekewa programu ya miaka minne (2006-2010). Mpango huo utagharimu shilingi bilioni 1.6.
Katika hilo, wasanii mbalimbali watahamasishwa ili kutimiza lengo la kuupa hadhi yake muziki wa taarabu asilia.
Kwa mujibu wa historia, muziki huo uliletwa Zanzibar na Waarabu wa Oman katika karne ya 19 wakileta vifaa, tungo na hata lugha iliyotumika ilikuwa ni Kiarabu.
Lakini pia miiko ya muziki huo ni kwamba si muziki wa kucheza kwa nguvu bali uliundwa ili usikilizwe.
Baadaye watunzi wa Kizanzibari nao walianza kutunga mashairi wakitumia Kiswahili kwa kutumia melodia za Kimisri na Kihindi na inaaminika kuwa mwaka 1930 muziki huo ukaingia Tanganyika na kujikita katika miji ya Morogoro, Dodoma, Tabora, Mwanza na Kigoma.
Tangu wakati huo, muziki huo ulianza kukua na kuenea sehemu nyingi za Tanzania lakini kwa bahati mbaya uasili wake ukaanza kupotea siku hadi siku.
Kumekuwa na matatizo yaliyochangia muziki huo ukafa kama ilivyodokezwa awali lakini vikwazo vingine ni ukosefu wa wawekezaji na udhaifu katika uongozi na utawala.
Pamoja na matatizo hayo, BASATA imeweka mkakati maalumu wa kuboresha ufahamu na taaluma na kuhakikisha kuwa upatikanaji wa vifaa vya muziki huo hauwi kikwazo tena.
Lakini pia imepangwa kufanya uwekezaji na kutenga mfuko maalumu wa kusaidia ukuaji wa muziki wa taarabu asilia.
Abiud Sikapizye: Mtoto wa mchungaji 'aliyeasi' kanisa
Na Innocent Munyuku
WAHENGA walipata kusema kuwa penye nia pana njia. Hivyo ndivyo ilivyo kwa mwanamuziki wa kujitegemea Abiud Sikapizye wa jijini Arusha.
Gitaa lake aina ya galatoni na uwezo wake wa kuimba nyimbo za wasanii wengine duniani ndiyo silaha yake katika vita ya kuelekea maskani ya mafanikio.
Kazi zake anafanyia katika baa mbalimbali jijini Arusha na kwa hakika ni maarufu kwa wakazi wengi wa jijini humo. Ni hodari katika kuimba nyimbo zilizowahi kuvuma zamani na hata zinazoendelea kufyatuliwa miaka hii.
Omba wimbo wa Daudi Kabaka, Bob Marley, Simba wa Nyika, Lionel Richie au Moro Jazz hatasita kukupa burudani kwa gharama ya Sh 500 kwa kila wimbo.
Nilipokutana naye jijini Arusha siku chache zilizopita niliduwazwa na uwezo wa mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 32.
Lakini cha kufurahisha ni kwamba mwanamuziki huyo aliamua kuachana na matakwa ya babaye ya kulitumikia kanisa. Baba wa Abiud wakati huo alikuwa Mchungaji wa Kanisa la Moravian Jimbo la Mbeya.
“Nilianza muziki nikiwa darasa la nne. Baadaye nikaanza kupiga ngoma kanisani na kujaribu kupita gitaa pia,” anasema Abiud.
Anapozungumzia kilichomtumbukiza kwenye muziki ni kitu gani, anaeleza kuwa alivutiwa na uimbaji wa Dk. Remmy Ongala.
Mara baada ya kumaliza elimu ya sekondari kidato cha nne Mbozi mwaka 1991, msanii huyo alitimkia mjini Morogoro kwa ajili ya kusaka maisha bora.
“Niliondoka nyumbani kwani niliona kama nina nafasi ya kujitafutia maisha sehemu nyingine. Hivyo nikaenda Morogoro nikafikia kwa mama mdogo.
“Huko ndoto yangu ya muziki ikawa bado ipo lakini hakuna wa kuniongoza na sikuwa na fedha za kuanzisha bendi.
“Nilichofanya ni kuuza chips na wakati mwingine kuuza machungwa mitaani,” anasema.
Anaeleza kuwa matarajio yake yakaanza kufifia na hivyo kuchukua uamuzi wa kubadili makazi. Safari hii akapanda basi hadi jijini Arusha Mei mwaka 1995.
Mwaka mmoja baadaye akapata bahati ya kuimba kwaya katika Kanisa la Moravian na kwamba huo ukawa mwanzo wake wa kufufua ndoto zake.
Mwaka huo akakutana na mtu anayemtaja kwa jina moja la Fadhil aliyemwongezea mwanga katika fani ya muziki.
Lakini vile Mbeya alitoroka, babaye mzazi akamlazimisha arejee huko. Akatii amri ya baba lakini kichwani mwake akiwa na nia ya kutokaa huko kwa muda mrefu. Hakukaa sana Mbeya na badala yake akaelekea jijini Dar es Salaam.
“Nilichonga gitaa langu nikaelekea Dar es Salaam lakini kwa bahati mbaya pesa niliyokuwa nayo ikaishia kulipa malazi kwenye nyumba ya kulala wageni.
“Nikaona hali inakuwa ngumu, sikukata tamaa nikawa napiga baa mbalimbali na kwa vile sikuwa na pesa nilikuwa nalala Kwa Macheni…nakesha hapo kwa sababu nilishatimuliwa kwenye chumba.
“Mwaka 1997 nikalazimika kurudi Mbeya, huko nikakuta shinikizo kwamba lazima nioe. Nikakubaliana na wazazi na Novemba 27 mwaka huo huo nikafunga ndoa kanisani na mke wangu Neema Silungwe.”
Anasema alipoona hali ya maisha ya kijijini ni ngumu akatamani kurudi Dar es Salaam. “Bahati nzuri kulikuwa na Mchungaji wa kanisa anahamishiwa Arusha, tukadandia gari lake nasi tukashuka Chalinze ili tuunganishe usafiri kwenda Dar es Salaam.”
Kwa vile alishaanza kuzoea mji akaamua kupanua maeneo ya upigaji gitaa. Akapiga maeneo ya Masaki, Coco Beach akiwa na msaidizi wake.
“Siku moja wakati nawajibika pale Rose Garden, mwanamke Mzungu raia wa Norway akathamini sana kazi yangu, akaniahidi kunipa gitaa la kisasa na akatimiza ahadi.
“Tenda zikawa nyingi, nikapiga Casanova, Shivers na kwa vile kazi ilikuwa inalipa, tukakodi vyombo ili kuweka vionjo vingine vya muziki.
“Lakini kwa bahati mwenzangu akarubuniwa na watu akajiondoa na kunidhulumu gitaa langu. Nikaamua kuja Arusha ambako Mungu alinishika mkono nikapata mkataba wa kupiga Hotel 77,” anasema.
Baadaye mkataba huo ulikoma na alichofanya ni kurejea mtaani kupiga sehemu mbalimbali.
Ameshaandaa nyimbo kwa ajili ya kutoa albamu yake ya kwanza lakini tatizo ni mtaji wa kumwezesha kuingia studio.
WAHENGA walipata kusema kuwa penye nia pana njia. Hivyo ndivyo ilivyo kwa mwanamuziki wa kujitegemea Abiud Sikapizye wa jijini Arusha.
Gitaa lake aina ya galatoni na uwezo wake wa kuimba nyimbo za wasanii wengine duniani ndiyo silaha yake katika vita ya kuelekea maskani ya mafanikio.
Kazi zake anafanyia katika baa mbalimbali jijini Arusha na kwa hakika ni maarufu kwa wakazi wengi wa jijini humo. Ni hodari katika kuimba nyimbo zilizowahi kuvuma zamani na hata zinazoendelea kufyatuliwa miaka hii.
Omba wimbo wa Daudi Kabaka, Bob Marley, Simba wa Nyika, Lionel Richie au Moro Jazz hatasita kukupa burudani kwa gharama ya Sh 500 kwa kila wimbo.
Nilipokutana naye jijini Arusha siku chache zilizopita niliduwazwa na uwezo wa mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 32.
Lakini cha kufurahisha ni kwamba mwanamuziki huyo aliamua kuachana na matakwa ya babaye ya kulitumikia kanisa. Baba wa Abiud wakati huo alikuwa Mchungaji wa Kanisa la Moravian Jimbo la Mbeya.
“Nilianza muziki nikiwa darasa la nne. Baadaye nikaanza kupiga ngoma kanisani na kujaribu kupita gitaa pia,” anasema Abiud.
Anapozungumzia kilichomtumbukiza kwenye muziki ni kitu gani, anaeleza kuwa alivutiwa na uimbaji wa Dk. Remmy Ongala.
Mara baada ya kumaliza elimu ya sekondari kidato cha nne Mbozi mwaka 1991, msanii huyo alitimkia mjini Morogoro kwa ajili ya kusaka maisha bora.
“Niliondoka nyumbani kwani niliona kama nina nafasi ya kujitafutia maisha sehemu nyingine. Hivyo nikaenda Morogoro nikafikia kwa mama mdogo.
“Huko ndoto yangu ya muziki ikawa bado ipo lakini hakuna wa kuniongoza na sikuwa na fedha za kuanzisha bendi.
“Nilichofanya ni kuuza chips na wakati mwingine kuuza machungwa mitaani,” anasema.
Anaeleza kuwa matarajio yake yakaanza kufifia na hivyo kuchukua uamuzi wa kubadili makazi. Safari hii akapanda basi hadi jijini Arusha Mei mwaka 1995.
Mwaka mmoja baadaye akapata bahati ya kuimba kwaya katika Kanisa la Moravian na kwamba huo ukawa mwanzo wake wa kufufua ndoto zake.
Mwaka huo akakutana na mtu anayemtaja kwa jina moja la Fadhil aliyemwongezea mwanga katika fani ya muziki.
Lakini vile Mbeya alitoroka, babaye mzazi akamlazimisha arejee huko. Akatii amri ya baba lakini kichwani mwake akiwa na nia ya kutokaa huko kwa muda mrefu. Hakukaa sana Mbeya na badala yake akaelekea jijini Dar es Salaam.
“Nilichonga gitaa langu nikaelekea Dar es Salaam lakini kwa bahati mbaya pesa niliyokuwa nayo ikaishia kulipa malazi kwenye nyumba ya kulala wageni.
“Nikaona hali inakuwa ngumu, sikukata tamaa nikawa napiga baa mbalimbali na kwa vile sikuwa na pesa nilikuwa nalala Kwa Macheni…nakesha hapo kwa sababu nilishatimuliwa kwenye chumba.
“Mwaka 1997 nikalazimika kurudi Mbeya, huko nikakuta shinikizo kwamba lazima nioe. Nikakubaliana na wazazi na Novemba 27 mwaka huo huo nikafunga ndoa kanisani na mke wangu Neema Silungwe.”
Anasema alipoona hali ya maisha ya kijijini ni ngumu akatamani kurudi Dar es Salaam. “Bahati nzuri kulikuwa na Mchungaji wa kanisa anahamishiwa Arusha, tukadandia gari lake nasi tukashuka Chalinze ili tuunganishe usafiri kwenda Dar es Salaam.”
Kwa vile alishaanza kuzoea mji akaamua kupanua maeneo ya upigaji gitaa. Akapiga maeneo ya Masaki, Coco Beach akiwa na msaidizi wake.
“Siku moja wakati nawajibika pale Rose Garden, mwanamke Mzungu raia wa Norway akathamini sana kazi yangu, akaniahidi kunipa gitaa la kisasa na akatimiza ahadi.
“Tenda zikawa nyingi, nikapiga Casanova, Shivers na kwa vile kazi ilikuwa inalipa, tukakodi vyombo ili kuweka vionjo vingine vya muziki.
“Lakini kwa bahati mwenzangu akarubuniwa na watu akajiondoa na kunidhulumu gitaa langu. Nikaamua kuja Arusha ambako Mungu alinishika mkono nikapata mkataba wa kupiga Hotel 77,” anasema.
Baadaye mkataba huo ulikoma na alichofanya ni kurejea mtaani kupiga sehemu mbalimbali.
Ameshaandaa nyimbo kwa ajili ya kutoa albamu yake ya kwanza lakini tatizo ni mtaji wa kumwezesha kuingia studio.
Usu Mallya: Jembe jipya makini TGNP
Na Innocent Munyuku
KAMA kuna masuala ambayo yamekuwa yakipigiwa zumari katika sehemu nyingi duniani, usawa katika jamii na maisha bora huwezi kuviweka kando.
Zipo asasi nyingi nchini zilizoweka mikakati ya kutatua mambo kama hayo na moja ya asasi hizo ni Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) iliyoanzishwa mwaka 1993.
TGNP ni asasi isiyo ya kiserikali na kuundwa kwake kulilenga zaidi kuleta usawa wa jinsia katika jamii, kuwawezesha wanawake, mafunzo, utafiti na kusambaza taarifa muhimu zinazolenga ustawi wa jamii.
Hivi karibuni TGNP ilipata Mkurugenzi Mtendaji, Usu Mallya anayechukua nafasi ya Mary Rusimbi aliyemaliza muda wake.
Je, mkurugenzi huyo mpya ana mkakati gani baada ya kukalia usukani wa kuipeleka asasi hiyo mbele kimafanikio?
Katika mahojiano maalumu na MTANZANIA Jumapili juzi, Usu anasema mbali na kuwa na jukumu la usimamizi wa asasi hiyo, mfumo wa TGNP unamweka katika mazingira ya kufurahia kazi yake.
“TGNP imejengwa kwa namna kwamba kila jambo linafanywa kwa ushirikiano, hakuna maamuzi ya mtu mmoja.
“Lakini pia niko hapa tangu mwaka 1998 kwa hiyo nimejifunza mengi hapa hasa katika mkakati wa kujenga nguvu za pamoja,” anasema Usu na kisha kuongeza:
“Mtandao wetu umejengwa katika mhimili wa pamoja katika dhamira na dira.”
Pamoja na ukweli kwamba manyanyaso au ubaguzi wa kijinsia upo duniani kwa miaka mingi, nchi nyingi za Afrika ikiwemo Tanzania zilipata mwamko baada ya Mkutano wa Beijing Septemba mwaka 1995.
Katika mkutano huo wa wanawake uliazimia mambo mbalimbali ikiwemo kubadili mtazamo wa jamii katika kutendeana haki pasipo kubaguana.
Pia kujali utu na kumpa mwanamke sauti na kwamba wanaume kwa miaka mingi wamekuwa kikwazo katika maendeleo binafsi ya mwanamke.
Lakini je, baada ya miaka 12 kupita, TGNP inatathimini vipi mafanikio ya azimio la Beijing?
“Zipo fursa nyingi kwa wanawake lakini bado Serikali ina changamoto nyingi kufikia maendeleo.
“Katika elimu kumekuwa na jitihada lakini uwiano ni mdogo katika ngazi ya elimu ya juu. Kwa mfano wasichana wanaovuka kwenda kidato cha tano, sita hadi chuo kikuu inashuka,” anasema Usu.
Anaeleza kuwa kushuka kwa kiwango hicho kunatokana na mazingira au mfumo uliopo katika sheria za nchi.
“Sheria ya ndoa kwa mfano inaweka wazi kuwa mtoto wa kike anaweza kuolewa afikishapo umri wa miaka 14 au 15…sasa huu ndio muda wa mtoto kuwa shule. Akishaolewa safari yake inakuwa imeishia hapo.
“Lakini pia sheria kwamba mtoto wa kike akipata ujauzito abaki nyumbani nayo imechangia kwa kiasi kikubwa kuongeza idadi ya wasichana wenye elimu ya chini katika jamii.”
Hata hivyo, anasema maazimio mengine ya Beijing yanakwamishwa na sera za ubinafsishaji nchini.
Kwamba uchumi sasa ni wa utandawazi unaoongozwa na makampuni kutoka nchi tajiri duniani.
“Mikataba mingi katika eneo hilo ni ya kuwakandamiza wananchi, hii mikataba haijengi nchi changa.
“Nitoe mfano wa hapa kwetu, mkataba wa Bi-water umeshatuumiza, angalia suala la Richmond na umeme wetu au madini.
“Haya mambo yote yametuathiri kwa sababu ya utandawazi, angalia nchi kama Afrika Kusini, imeendelea kwa kiwango kikubwa kwa vile wametumia madini yao kujinufaisha. Hali ni tofauti na Tanzania,” anasema.
Anasema kutokana na mazingira kama hayo, hata jitihada za kuwakomboa Watanzania kutoka katika umasikini zinakuwa ngumu.
“Wanawake kwa mfano wako kwenye uchumi mdogo mdogo. Ninachosema hapa ni kwamba kama Serikali imeshindwa kuhodhi rasilimali basi hata hawa wa chini wataendelea kuumia,” anasema Usu.
Anazungumzia pia sekta ya utalii ambayo kwa mtazamo wake haijampa fursa Mtanzania kunufaika nayo.
“Nani anafaidi matunda ya utalii? Bila shaka ni watu wachache sana,” anasema.
Mbali na uchumi kuwa suala gumu katika kuwaendeleza Watanzania, kuna kikwazo katika sekta ya afya.
“Eneo hili ni changamoto kubwa kwa Serikali kwani linatakiwa kuwezeshwa na anayeumia sana ni mwanamke.
“Vifaa au huduma katika sekta hii bado haijamhakikishia mwanamke hatima njema hasa katika uzazi. Kuna takwimu zinazoonyesha kuwa katika wanawake 560 kati ya 100,000 hufariki dunia kila mwaka kutokana na uzazi usio salama.
“Hii ni dalili au ishara kwamba Serikali inakabiliwa na changamoto kubwa katika sekta ya afya hasa kwa afya ya mwanamke.”
Analalamikia uonevu ambao unachukua sura tofauti kila siku dhidi ya mwanamke.
“Kuna manyanyaso kwa wanawake, wengi wana uwezo mdogo wa kufanya maamuzi kuhusu ngono au idadi ya watoto.
“Ni jambo linalofanywa kuwa ni kawaida kwa mjamzito kufanya kazi za nyumbani huku akiwa na lishe duni hii si ajabu ikachangia vifo wakati mwingine.”
Vipi kuhusu nafasi ya mwanamke katika uongozi?
Usu anasema pamoja kuwa na wabunge wanawake kwa asilimia 30, bado kiwango hicho hakitoshi.
“Wapewe sauti au nafasi pia kuanzia kwenye udiwani…lakini pia naweza kusema kuwa wanawake wanahitaji nafasi pia katika sekta binafsi.
“Hata serikalini ipo haja kwa wanawake kupewa nafasi za juu kama vile ukuu wa mikoa, ukatibu mkuu, ubalozi nje ya nchi, ukurugenzi wa bodi au ujaji,” anasema Usu.
Pamoja na hilo, Usu anasema kuna mambo ambayo lazima yasemwe kwa uwazi au kujadiliwa kitaifa kuhusu utamaduni wa Mtanzania kutokana na ukweli kwamba mengi yanatokana na upotoshwaji wa mila.
Anasema jamii mara nyingi inamwona mwanamke kama chombo cha starehe na hata watoto wanapokua, mtoto wa kike tayari ameshajenga dhana ya kuwa wa chini.
“Hili ni suala nyeti linalopaswa kujadiliwa kitaifa, ni kama ilivyo rushwa lazima lijadiliwe. Hili jambo si la TGNP pekee bali Serikali nayo ihusike.”
Tangu kuanzishwa kwake, TGNP imefanikiwa katika kufikisha ujumbe kwa jamii kwa njia ya semina mbalimbali na kushirikiana na wanaharakati katika ngazi mbalimbali.
Mara nyingi imeshirikiana na FemAct katika kuilemisha jamii na ushirikiano huo upo kwa wanaharakati katika wilaya mbalimbali nchini.
“Tunatambua kazi za wanaharakati katika ngazi husika kwa kufanya semina na nafasi ya elimu kwa watu wa rika mbalimbali,” anasema Usu.
Mbali na semina, kila baada ya miaka miwili, TGNP hufanya tamasha la kijinsia ambalo huwapa fursa washiriki kufanya tathimini.
“Watu mbalimbali hualikwa na kinachofanyika ni kuibua mijadala na kushinikiza mabadiliko.
“Kuna sera kama mgawanyo mbovu wa mali katika familia kama vile ardhi au ukatili nazo hujadiliwa.
“Tumeanza kuishinikiza Serikali ibadili pia Katiba ya nchi kwani haimtendei haki mwanamke linapokuja suala la ndoa.
“Kuna mapungufu kwa mfano Katiba inaruhusu sheria za jadi kutambuliwa, sasa katika hali kama hiyo ni wazi kuwa mwanamke anapewa haki na wakati huo huo kumnyang’anya.
“Unaporuhusu kutumika kwa sheria ya jadi maana yake ni kuruhusu unyanyasaji kwani sheria nyingi za jadi zinamkandamiza mwanamke,” anasema.
TGNP imeshatoa mabango ya aina mbalimbali yanayolenga kuielimisha jamii.
Katika Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge mwaka 2005 walitoa bango la ‘Wakati umefika! Uwezo wa kuongoza tunao! Wanawake tujitokeze’.
Yapo mabango mengine kama la mwaka 2001 linalosomeka ‘Jinsia, demokrasia na maendeleo mbinu mbadala za kukabiliana na kufukarishwa’.
Lipo jingine la mwaka 2004 ‘Tatizo la dunia ya leo si umasikini ni mgawanyiko wa rasilimali wa kinyonyaji’.
Mwaka jana walikemea ubinafsishaji holela wa sekta ya maji.
Na mwaka huu TGNP imekuja na bango la ‘Sema hapana kwa ukatili wa kijinsia’.
Mbali na hayo wamekuwa na machapichopendwa kwa njia ya vitabu kama vile, Kwangu Wapi, Vijana Taifa la Leo, Kondomu Yazua Kasheshe, Utandawazi na Wewe na Ahadi za Uongo.
Pia TGNP imekuwa ikitoa vitabu vya kitaaluma kwa watafiti na wanafunzi. Baadhi ni Gender Profile of Tanzania: Enhancing Gender Family, Activists Voices, Against Neo Liberalism na Gender Budget Analysis in Tanzania 1997-2000.
Kuna maktaba ya kisasa na duka la vitabu katika ofisi hizo zilizopo eneo la Mabibo jijini Dar es Salaam na kila Jumatano huendeshwa semina kwa watu wote katika ofisi hizo kuanzia saa tisa mchana hadi 11 jioni.
Usu Mallya alitokea wapi? Alizaliwa mkoani Shinyanga mwaka 1961 na elimu yake ya msingi aliipata Marangu Sembeti Wilaya ya Moshi Vijijini mkoani Kilimanjaro. Hii ilikuwa kati ya mwaka 1968-74.
Kati ya mwaka 1975-78 alikuwa Shule ya Sekondari ya Kibosho alikohitimu kidato cha nne. Elimu ya juu ya sekondari aliipata Korogwe mkoani Tanga.
Baadaye alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam alikopata shahada ya kwanza ya uongozi wa taasisi za umma, sayansi ya jamii na Kifaransa. Alihitimu mwaka 1985.
Aliwahi kufanya kazi chuoni hapo katika Idara ya Sayansi ya Jamii kati ya mwaka 1990-95.
Alirejea darasani kusomea shahada ya uzamili chuoni hapo akichukua masomo ya sayansi ya jamii. Alihitimu mwaka 1997.
Mwaka mmoja baadaye akajiunga na TGNP.
KAMA kuna masuala ambayo yamekuwa yakipigiwa zumari katika sehemu nyingi duniani, usawa katika jamii na maisha bora huwezi kuviweka kando.
Zipo asasi nyingi nchini zilizoweka mikakati ya kutatua mambo kama hayo na moja ya asasi hizo ni Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) iliyoanzishwa mwaka 1993.
TGNP ni asasi isiyo ya kiserikali na kuundwa kwake kulilenga zaidi kuleta usawa wa jinsia katika jamii, kuwawezesha wanawake, mafunzo, utafiti na kusambaza taarifa muhimu zinazolenga ustawi wa jamii.
Hivi karibuni TGNP ilipata Mkurugenzi Mtendaji, Usu Mallya anayechukua nafasi ya Mary Rusimbi aliyemaliza muda wake.
Je, mkurugenzi huyo mpya ana mkakati gani baada ya kukalia usukani wa kuipeleka asasi hiyo mbele kimafanikio?
Katika mahojiano maalumu na MTANZANIA Jumapili juzi, Usu anasema mbali na kuwa na jukumu la usimamizi wa asasi hiyo, mfumo wa TGNP unamweka katika mazingira ya kufurahia kazi yake.
“TGNP imejengwa kwa namna kwamba kila jambo linafanywa kwa ushirikiano, hakuna maamuzi ya mtu mmoja.
“Lakini pia niko hapa tangu mwaka 1998 kwa hiyo nimejifunza mengi hapa hasa katika mkakati wa kujenga nguvu za pamoja,” anasema Usu na kisha kuongeza:
“Mtandao wetu umejengwa katika mhimili wa pamoja katika dhamira na dira.”
Pamoja na ukweli kwamba manyanyaso au ubaguzi wa kijinsia upo duniani kwa miaka mingi, nchi nyingi za Afrika ikiwemo Tanzania zilipata mwamko baada ya Mkutano wa Beijing Septemba mwaka 1995.
Katika mkutano huo wa wanawake uliazimia mambo mbalimbali ikiwemo kubadili mtazamo wa jamii katika kutendeana haki pasipo kubaguana.
Pia kujali utu na kumpa mwanamke sauti na kwamba wanaume kwa miaka mingi wamekuwa kikwazo katika maendeleo binafsi ya mwanamke.
Lakini je, baada ya miaka 12 kupita, TGNP inatathimini vipi mafanikio ya azimio la Beijing?
“Zipo fursa nyingi kwa wanawake lakini bado Serikali ina changamoto nyingi kufikia maendeleo.
“Katika elimu kumekuwa na jitihada lakini uwiano ni mdogo katika ngazi ya elimu ya juu. Kwa mfano wasichana wanaovuka kwenda kidato cha tano, sita hadi chuo kikuu inashuka,” anasema Usu.
Anaeleza kuwa kushuka kwa kiwango hicho kunatokana na mazingira au mfumo uliopo katika sheria za nchi.
“Sheria ya ndoa kwa mfano inaweka wazi kuwa mtoto wa kike anaweza kuolewa afikishapo umri wa miaka 14 au 15…sasa huu ndio muda wa mtoto kuwa shule. Akishaolewa safari yake inakuwa imeishia hapo.
“Lakini pia sheria kwamba mtoto wa kike akipata ujauzito abaki nyumbani nayo imechangia kwa kiasi kikubwa kuongeza idadi ya wasichana wenye elimu ya chini katika jamii.”
Hata hivyo, anasema maazimio mengine ya Beijing yanakwamishwa na sera za ubinafsishaji nchini.
Kwamba uchumi sasa ni wa utandawazi unaoongozwa na makampuni kutoka nchi tajiri duniani.
“Mikataba mingi katika eneo hilo ni ya kuwakandamiza wananchi, hii mikataba haijengi nchi changa.
“Nitoe mfano wa hapa kwetu, mkataba wa Bi-water umeshatuumiza, angalia suala la Richmond na umeme wetu au madini.
“Haya mambo yote yametuathiri kwa sababu ya utandawazi, angalia nchi kama Afrika Kusini, imeendelea kwa kiwango kikubwa kwa vile wametumia madini yao kujinufaisha. Hali ni tofauti na Tanzania,” anasema.
Anasema kutokana na mazingira kama hayo, hata jitihada za kuwakomboa Watanzania kutoka katika umasikini zinakuwa ngumu.
“Wanawake kwa mfano wako kwenye uchumi mdogo mdogo. Ninachosema hapa ni kwamba kama Serikali imeshindwa kuhodhi rasilimali basi hata hawa wa chini wataendelea kuumia,” anasema Usu.
Anazungumzia pia sekta ya utalii ambayo kwa mtazamo wake haijampa fursa Mtanzania kunufaika nayo.
“Nani anafaidi matunda ya utalii? Bila shaka ni watu wachache sana,” anasema.
Mbali na uchumi kuwa suala gumu katika kuwaendeleza Watanzania, kuna kikwazo katika sekta ya afya.
“Eneo hili ni changamoto kubwa kwa Serikali kwani linatakiwa kuwezeshwa na anayeumia sana ni mwanamke.
“Vifaa au huduma katika sekta hii bado haijamhakikishia mwanamke hatima njema hasa katika uzazi. Kuna takwimu zinazoonyesha kuwa katika wanawake 560 kati ya 100,000 hufariki dunia kila mwaka kutokana na uzazi usio salama.
“Hii ni dalili au ishara kwamba Serikali inakabiliwa na changamoto kubwa katika sekta ya afya hasa kwa afya ya mwanamke.”
Analalamikia uonevu ambao unachukua sura tofauti kila siku dhidi ya mwanamke.
“Kuna manyanyaso kwa wanawake, wengi wana uwezo mdogo wa kufanya maamuzi kuhusu ngono au idadi ya watoto.
“Ni jambo linalofanywa kuwa ni kawaida kwa mjamzito kufanya kazi za nyumbani huku akiwa na lishe duni hii si ajabu ikachangia vifo wakati mwingine.”
Vipi kuhusu nafasi ya mwanamke katika uongozi?
Usu anasema pamoja kuwa na wabunge wanawake kwa asilimia 30, bado kiwango hicho hakitoshi.
“Wapewe sauti au nafasi pia kuanzia kwenye udiwani…lakini pia naweza kusema kuwa wanawake wanahitaji nafasi pia katika sekta binafsi.
“Hata serikalini ipo haja kwa wanawake kupewa nafasi za juu kama vile ukuu wa mikoa, ukatibu mkuu, ubalozi nje ya nchi, ukurugenzi wa bodi au ujaji,” anasema Usu.
Pamoja na hilo, Usu anasema kuna mambo ambayo lazima yasemwe kwa uwazi au kujadiliwa kitaifa kuhusu utamaduni wa Mtanzania kutokana na ukweli kwamba mengi yanatokana na upotoshwaji wa mila.
Anasema jamii mara nyingi inamwona mwanamke kama chombo cha starehe na hata watoto wanapokua, mtoto wa kike tayari ameshajenga dhana ya kuwa wa chini.
“Hili ni suala nyeti linalopaswa kujadiliwa kitaifa, ni kama ilivyo rushwa lazima lijadiliwe. Hili jambo si la TGNP pekee bali Serikali nayo ihusike.”
Tangu kuanzishwa kwake, TGNP imefanikiwa katika kufikisha ujumbe kwa jamii kwa njia ya semina mbalimbali na kushirikiana na wanaharakati katika ngazi mbalimbali.
Mara nyingi imeshirikiana na FemAct katika kuilemisha jamii na ushirikiano huo upo kwa wanaharakati katika wilaya mbalimbali nchini.
“Tunatambua kazi za wanaharakati katika ngazi husika kwa kufanya semina na nafasi ya elimu kwa watu wa rika mbalimbali,” anasema Usu.
Mbali na semina, kila baada ya miaka miwili, TGNP hufanya tamasha la kijinsia ambalo huwapa fursa washiriki kufanya tathimini.
“Watu mbalimbali hualikwa na kinachofanyika ni kuibua mijadala na kushinikiza mabadiliko.
“Kuna sera kama mgawanyo mbovu wa mali katika familia kama vile ardhi au ukatili nazo hujadiliwa.
“Tumeanza kuishinikiza Serikali ibadili pia Katiba ya nchi kwani haimtendei haki mwanamke linapokuja suala la ndoa.
“Kuna mapungufu kwa mfano Katiba inaruhusu sheria za jadi kutambuliwa, sasa katika hali kama hiyo ni wazi kuwa mwanamke anapewa haki na wakati huo huo kumnyang’anya.
“Unaporuhusu kutumika kwa sheria ya jadi maana yake ni kuruhusu unyanyasaji kwani sheria nyingi za jadi zinamkandamiza mwanamke,” anasema.
TGNP imeshatoa mabango ya aina mbalimbali yanayolenga kuielimisha jamii.
Katika Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge mwaka 2005 walitoa bango la ‘Wakati umefika! Uwezo wa kuongoza tunao! Wanawake tujitokeze’.
Yapo mabango mengine kama la mwaka 2001 linalosomeka ‘Jinsia, demokrasia na maendeleo mbinu mbadala za kukabiliana na kufukarishwa’.
Lipo jingine la mwaka 2004 ‘Tatizo la dunia ya leo si umasikini ni mgawanyiko wa rasilimali wa kinyonyaji’.
Mwaka jana walikemea ubinafsishaji holela wa sekta ya maji.
Na mwaka huu TGNP imekuja na bango la ‘Sema hapana kwa ukatili wa kijinsia’.
Mbali na hayo wamekuwa na machapichopendwa kwa njia ya vitabu kama vile, Kwangu Wapi, Vijana Taifa la Leo, Kondomu Yazua Kasheshe, Utandawazi na Wewe na Ahadi za Uongo.
Pia TGNP imekuwa ikitoa vitabu vya kitaaluma kwa watafiti na wanafunzi. Baadhi ni Gender Profile of Tanzania: Enhancing Gender Family, Activists Voices, Against Neo Liberalism na Gender Budget Analysis in Tanzania 1997-2000.
Kuna maktaba ya kisasa na duka la vitabu katika ofisi hizo zilizopo eneo la Mabibo jijini Dar es Salaam na kila Jumatano huendeshwa semina kwa watu wote katika ofisi hizo kuanzia saa tisa mchana hadi 11 jioni.
Usu Mallya alitokea wapi? Alizaliwa mkoani Shinyanga mwaka 1961 na elimu yake ya msingi aliipata Marangu Sembeti Wilaya ya Moshi Vijijini mkoani Kilimanjaro. Hii ilikuwa kati ya mwaka 1968-74.
Kati ya mwaka 1975-78 alikuwa Shule ya Sekondari ya Kibosho alikohitimu kidato cha nne. Elimu ya juu ya sekondari aliipata Korogwe mkoani Tanga.
Baadaye alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam alikopata shahada ya kwanza ya uongozi wa taasisi za umma, sayansi ya jamii na Kifaransa. Alihitimu mwaka 1985.
Aliwahi kufanya kazi chuoni hapo katika Idara ya Sayansi ya Jamii kati ya mwaka 1990-95.
Alirejea darasani kusomea shahada ya uzamili chuoni hapo akichukua masomo ya sayansi ya jamii. Alihitimu mwaka 1997.
Mwaka mmoja baadaye akajiunga na TGNP.
Makali ya Mikumi Sound yaenda Dar
Na Innocent Munyuku
KATIKA maisha ni jambo la kawaida kwa mwanadamu kupenda mabadiliko chanya. Pengine hili liko kwa viumbe hai wengine.
Kutokana na hali hiyo bila shaka ndio maana bendi ya muziki wa dansi ya Mikumi Sound imeamua kuyaacha maskani yake mjini Morogoro na kuhamia jijini Dar es Salaam.
Katika taarifa yake juzi Meneja wa bendi hiyo, Yona Vegula alisema wameamua kuihamishia bendi hiyo jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujipanua.
“Kusudio au lengo hasa ni kupata changamoto, huwezi kujiita mahiri sehemu ambayo haina ushindani mkubwa katika masuala ya muziki wa dansi, kwa hiyo kuhama kwetu kunajengwa na msingi wa kusaka upinzani wa kweli,” alisema Vegula.
Kwa mujibu wa Vegula, Mikumi Sound itatua jijini Dar es Salaam baada ya kumalizika kwa Pasaka.
Baadhi ya wanamuziki wanaounda bendi hiyo ni Sadiq Jakaya anayepiga gitaa la solo, Balely Mohamed anayevuma na gitaa la bass, Toto Site (kinanda), Abeid Said anayepiga drums huku Jose Kigenda ambaye ni rais wa bendi hiyo akiwa mtunzi.
Hadi sasa wanazo albamu tatu ambazo ni Cheo ni Dhamana ya mwaka 2004, Mama Mkwe (2005) na Pesa Makaratasi ya mwaka huu.
Kuibuka kwa bendi hiyo kulikuwa faraja kubwa kwa wakazi wa Morogoro hasa kutokana na ukweli kwamba baada ya kufifia kwa bendi maarufu mkoani Morogoro kama Moro Jazz iliyotamba na marehemu Mbaraka Mwinshehe, mkoa huo ulibaki kama yatima katika masuala ya muziki.
Sababu kubwa ni kwamba wadau wa muziki walikosa ari au uwezo wa kumiliki bendi za muziki wa dansi. Matokeo yake, burudani ya aina hiyo ikazidi kushamiri katika jiji la Dar es Salaam.
Umahiri wao jukwaani huwezi kuamiani kuwa bendi hii inaundwa na wanamuziki wenye usongo wa kujitangaza kimataifa.
Kinachofurahisha ni kwamba hawataki kuiga muziki wa Kongo na badala yake wanabuni vionjo vinavyokwenda na utamaduni wa Mtanzania.
Rais wa bendi hiyo, Jose Kigenda katika mahojiamo maalumu anasema kuwa wanamuziki wake wamekuwa wabunifu kutokana na maelewano baina yao.
Kwamba Mikumi Sound si ya wababaishaji na amewaomba mashabiki wa muziki wa dansi jijini Dar es Salaam kuwapa ushirikiano.
“Ndio maana kila siku nawaambia kuwa wanaodhani wamesimama kimuziki wakae chonjo, mwendo wetu ni wa taratibu lakini tuko makini sana,” anasema.
Ili kuhakikisha kuwa inabeba mashabiki wengi zaidi, bendi hiyo imeshazuru mikoa mbalimbali nchini kujitangaza. Moja ya ziara iliyofana ni ile ya kuitangaza albamu yake Mama Mkwe.
Hayo yote yasingewezekana kama si ubavu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Mikumi Sound, Rena Vegula. Huyu kwa watu wengine wanaweza kumwita mwanamke wa shoka kutokana na kutokuwa na woga katika uendeshaji wa masuala ya maendeleo.
Wazo la bendi lilianzia mjini Arusha mwaka 2003 na lengo hasa lilikuwa kuitangaza Mikumi kama mbuga nzuri Tanzania.
Bendi ilianza baada ya baadhi ya wanamuziki waliopo kushawishika na bendi ya Olduvai iliyokuwa ikipiga kwenye Ukumbi wa Ricks mjini Arusha. Baada ya bendi hiyo kufifia Rena akapata wazo na kuanzisha bendi yake ambayo ni Mikumi Sound.
“Baadhi ya wanamuziki wetu wakawa wanaonyesha moyo wa kuendeleza muziki lakini vifaa hatukuwa navyo, ndipo tukaamua kununua vifaa vyetu.”
KATIKA maisha ni jambo la kawaida kwa mwanadamu kupenda mabadiliko chanya. Pengine hili liko kwa viumbe hai wengine.
Kutokana na hali hiyo bila shaka ndio maana bendi ya muziki wa dansi ya Mikumi Sound imeamua kuyaacha maskani yake mjini Morogoro na kuhamia jijini Dar es Salaam.
Katika taarifa yake juzi Meneja wa bendi hiyo, Yona Vegula alisema wameamua kuihamishia bendi hiyo jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujipanua.
“Kusudio au lengo hasa ni kupata changamoto, huwezi kujiita mahiri sehemu ambayo haina ushindani mkubwa katika masuala ya muziki wa dansi, kwa hiyo kuhama kwetu kunajengwa na msingi wa kusaka upinzani wa kweli,” alisema Vegula.
Kwa mujibu wa Vegula, Mikumi Sound itatua jijini Dar es Salaam baada ya kumalizika kwa Pasaka.
Baadhi ya wanamuziki wanaounda bendi hiyo ni Sadiq Jakaya anayepiga gitaa la solo, Balely Mohamed anayevuma na gitaa la bass, Toto Site (kinanda), Abeid Said anayepiga drums huku Jose Kigenda ambaye ni rais wa bendi hiyo akiwa mtunzi.
Hadi sasa wanazo albamu tatu ambazo ni Cheo ni Dhamana ya mwaka 2004, Mama Mkwe (2005) na Pesa Makaratasi ya mwaka huu.
Kuibuka kwa bendi hiyo kulikuwa faraja kubwa kwa wakazi wa Morogoro hasa kutokana na ukweli kwamba baada ya kufifia kwa bendi maarufu mkoani Morogoro kama Moro Jazz iliyotamba na marehemu Mbaraka Mwinshehe, mkoa huo ulibaki kama yatima katika masuala ya muziki.
Sababu kubwa ni kwamba wadau wa muziki walikosa ari au uwezo wa kumiliki bendi za muziki wa dansi. Matokeo yake, burudani ya aina hiyo ikazidi kushamiri katika jiji la Dar es Salaam.
Umahiri wao jukwaani huwezi kuamiani kuwa bendi hii inaundwa na wanamuziki wenye usongo wa kujitangaza kimataifa.
Kinachofurahisha ni kwamba hawataki kuiga muziki wa Kongo na badala yake wanabuni vionjo vinavyokwenda na utamaduni wa Mtanzania.
Rais wa bendi hiyo, Jose Kigenda katika mahojiamo maalumu anasema kuwa wanamuziki wake wamekuwa wabunifu kutokana na maelewano baina yao.
Kwamba Mikumi Sound si ya wababaishaji na amewaomba mashabiki wa muziki wa dansi jijini Dar es Salaam kuwapa ushirikiano.
“Ndio maana kila siku nawaambia kuwa wanaodhani wamesimama kimuziki wakae chonjo, mwendo wetu ni wa taratibu lakini tuko makini sana,” anasema.
Ili kuhakikisha kuwa inabeba mashabiki wengi zaidi, bendi hiyo imeshazuru mikoa mbalimbali nchini kujitangaza. Moja ya ziara iliyofana ni ile ya kuitangaza albamu yake Mama Mkwe.
Hayo yote yasingewezekana kama si ubavu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Mikumi Sound, Rena Vegula. Huyu kwa watu wengine wanaweza kumwita mwanamke wa shoka kutokana na kutokuwa na woga katika uendeshaji wa masuala ya maendeleo.
Wazo la bendi lilianzia mjini Arusha mwaka 2003 na lengo hasa lilikuwa kuitangaza Mikumi kama mbuga nzuri Tanzania.
Bendi ilianza baada ya baadhi ya wanamuziki waliopo kushawishika na bendi ya Olduvai iliyokuwa ikipiga kwenye Ukumbi wa Ricks mjini Arusha. Baada ya bendi hiyo kufifia Rena akapata wazo na kuanzisha bendi yake ambayo ni Mikumi Sound.
“Baadhi ya wanamuziki wetu wakawa wanaonyesha moyo wa kuendeleza muziki lakini vifaa hatukuwa navyo, ndipo tukaamua kununua vifaa vyetu.”
Alice Lakwena…
KAMA kuna mambo ambayo Rais Yoweri Museveni wa Uganga yanamwumiza kichwa basi uwepo wa waasi wa LRA ni mojawapo.
Lakini ukiachana na jambo hilo, hakuna shaka kwamba katika utawala wake wa zaidi ya miaka 20, Rais Museveni hatasahau namna mwanamke mmoja alivyoichachafya Serikali yake mwanzoni kabisa mwa utawala wake.
Huyu ni Alice Auma ambaye baadaye alijipachika jina la Alice Lakwena. Lakwena likiwa na maana ya mjumbe maalumu.
Kwa nguvu ya Museveni na namna alivyokuwa ameanza kujijengea ngome kuu katika utawala wake, haikuwa rahisi kuamini kuwa angetokea mwanamke kuupinga utawala wake nchini Uganda.
Alice aliyezaliwa mwaka 1956 kutoka kabila la Acholi aliendesha mambo yake kwa staili ya imani za mizimu na katika hilo aliungwa mkono na wengi.
Hata alipoanzisha chama chake cha Holy Spirit Movement (HSM), haikuwa kazi ngumu kupata wafuasi kwani walio wengi waliamini kuwa Alice ana maono ya hali ya juu.
Kutokana na imani hiyo, akaingia mwituni kuupinga utawala wa Museveni kati ya Agosti mwaka 1986 hadi Novemba 1987.
Katika uhai wake, hakuwahi kupata mtoto ingawa aliolewa mara mbili. Baadaye akaachana na imani za kijadi na kujiunga na Kanisa Katoliki.
Hata hivyo, Mei 25, mwaka 1985 akaingiwa na pepo na kuwa mwendawazimu. Uendawazimu huo ukamfanya akose uwezo wa kusikia na kuzungumza pia.
Babaye akalazimika kumkimbiza kwa waganga wa jadi wapatao 11 kwa ajili ya tiba lakini hakuna aliyeweza kutatua tatizo hilo.
Zipo simulizi kwamba baada ya wataalamu hao wa tiba za asili kushindwa kumtibu Alice, babaye mzazi alimpeleka katika Mbuga ya Paraa ambako inaelezwa kuwa alitoweka kwa siku 40 na aliporejea aliambatana na mzimu.
Akawa miongoni mwa watu wenye nguvu za mizimu walioaminika karibu na eneo la Gulu nchini Uganda. Alikuwa na uwezo wa kutibu magonjwa mbalimbali. Inasemwa kwamba mzimu aliorejea nao baada ya kutoweka kwa siku 40 ndio uliomwezesha kupona uendawazimu.
Kutokana na nguvu hiyo, Alice alipata sifa kubwa ndani na nje ya Uganda. Wakati wa mapigano makali baina ya waasi na majeshi ya Serikali inaelezwa kuwa mwanamama huyo alielekezwa na mizimu kuacha kazi za tiba na badala yake aanzishe chama cha kuwakomboa Waganda.
Amri hiyo ya mizimu inadaiwa kutolewa Agosti 6, mwaka 1986 na kwamba kazi iliyokuwa mbele yake ni kusitisha uovu uliokuwa ikiendelea nchini humo.
Kwamba hapakuwa na haja ya kuhubiri au kukaa pembeni wakati kuna damu za raia wasio na hatia zinamwagika.
Katika mpango wake wa awali, Alice alikusudia kuuteka Mji Mkuu Kampala ambao ungekuja kuwa paradiso ya Waganda na bila shaka watu wa kabila la Acholi wangenufaika zaidi.
Alice katika mpango wake huo aliwaeleza watu wake kwamba kila anachopanga kina makusudio mazuri. “Haina maana kuwa daktari na kumtibu mtu leo wakati mtu huyo huyo kesho anauawa.”
Dhamira yake hiyo ndiyo ikamfanya aachane na udaktari na kusimama msitari wa mbele kupinga utawala uliopo.
Alikuja kuwa na msimamo kama wa Joseph Kony ambaye ni kinara wa kundi la waasi la Lord’s Resistance Army. Kwamba lengo ni kumwona Museveni akiachia ngazi nchini Uganda.
Lakini baadaye Alice alionekana kushindwa kutimiza dhamira yake kwani watu wa kabila la Acholi waliendelea kuangamia na ndoto ya kuiteka Kampala ikaanza kutoweka.
Jamii ikaendelea kuingiwa na hofu katika mambo mbalimbali na mbaya zaidi ni kuwa vifo vingi vilihusishwa na uchawi.
Hata hivyo, Alice hakukata tamaa na nguvu yake ikaibuka upya kwani katika hali fulani alipata ushindi kadri alivyoelekea Kampala.
Kwamba licha ya watu wake kuangamia, bado aliendelea kuwa na nguvu ya ushawishi na nguvu hiyo iliwafanya watu wengi kumuunga mkono na safari hii akitangaza kuwa ameongezewa mizimu.
Alifanikiwa kuwashawishi Waganda kwamba Museveni hakuwa mtu sahihi na kwamba aliikalia Uganda kimabavu na anapaswa kuondoka madarakani.
Kwa bahati nzuri kwake, wengi aliowahubiria ni wale ambao waliathirika vibaya na utawala wa Museveni na hivyo kuwa jambo rahisi kwao kumuunga mkono Alice.
Wahenga waliwahi kusema kuwa ngoma ikivuma sana haikawii kupasuka. Ndivyo ilivyotokea kwa Alice na safari yake ya kumng’oa Museveni. Baadhi ya wafuasi wake walianza kumtangaza kuwa ni mchawi.
Kwamba mizimu yake ni ya kichawi inayolenga kuleta maangamizi. Msuguano huo ukaifanya HSM kuzidiwa nguvu na hasa baada ya moto uliowashukia wakiwa mwituni karibu kabisa na Kampala. Alice akaikimbia nchi.
Alikimbilia katika kambi ya wakimbizi ya Ifo karibu na Dadaab kaskazini mwa Kenya na akiwa huko alitangaza kuwa ametengwa na mizimu.
Novemba mwaka 2004 alituhumiwa kusafirisha watoto kutoka Gulu nchini Uganda na kuwapeleka kambini kwake. Hata hivyo, mkono wa sheria haukumshukia.
Miaka miwili baadaye Alice aliibuka na kudai kuwa amegundua tiba ya ukimwi. Hata hivyo, alishindwa kuishawishi dunia katika madai yake hayo. Amefariki dunia Januari 17 mwaka huu baada ya kuugua kwa wiki moja. Haijulikani kapoteza maisha kwa maradhi gani.
Kuna simulizi kwamba mwanamama huyo enzi za uhai wake alikuwa na tabia ya kusema na wanyama au maji juu ya kilichokuwa kikiendelea nchini mwake.
“Nyie wanyama, Mungu kanituma kwenu niwaulize kama mnahusika na mauaji ya Uganda.” Katika simulizi hizo, wanyama walimjibu kuwa hawahusiki na badala yake nao pia waliumia na vitendo hivyo. Ikasemwa kuwa nyati alimwonyesha jeraha mguuni huku kiboko akionyesha jeraha mkononi.
Inaelezwa pia kuwa aliwahi kuyauliza maji kuhusu vita nchini Uganda. “Maji, nimekuja kukuuliza juu ya dhambi na umwagaji damu katika hii dunia.”
Nayo maji yakamjibu kwamba binadamu wenye miguu miwili wana tabia ya kuua ndugu zao na kutupa miili yao majini.
Simulizi hizo zinapasha pia kuwa baada ya majibu hayo, mzimu ulimtuma Alice kuendelea na jitihada za kuleta amani nchini Uganda. Akomeshe dhambi na umwagaji damu.
Wakati fulani alipokwenda katika Mlima Kilak, Alice anadaiwa kupewa nguvu na mlima huo kwenda kuutokomeza udhalimu. Pia alikabidhiwa dawa maalumu ya kuponya wagonjwa.
Baadaye akaja kutangaza pia kuwa kuna ujumbe kutoka kwa Mungu kwamba lipo kabila nchini Uganda ambalo lina damu ya kunguni. Akalitaja kabila hilo kuwa ni la Acholi.
Mbali na jitihada zake hizo, marehemu Alice anafanana na Joseph Kony katika mambo mawili. Mosi wote wawili ni wapinzani wa Museveni na pili, wote wanachanganya dini na uovu.
Alice amewahi kuchanganya mizimu na neno la Mungu kama ilivyo kwa Kony ambaye wakati wa Mfungo wa Ramadhan hufunga ingawa hula nyama ya nguruwe ambayo kwa imani ya Kiislamu ni haramu.
Makala hii imeandaliwa na INNOCENT MUNYUKU kwa msaada wa vyanzo mbalimbali vya habari.
Lakini ukiachana na jambo hilo, hakuna shaka kwamba katika utawala wake wa zaidi ya miaka 20, Rais Museveni hatasahau namna mwanamke mmoja alivyoichachafya Serikali yake mwanzoni kabisa mwa utawala wake.
Huyu ni Alice Auma ambaye baadaye alijipachika jina la Alice Lakwena. Lakwena likiwa na maana ya mjumbe maalumu.
Kwa nguvu ya Museveni na namna alivyokuwa ameanza kujijengea ngome kuu katika utawala wake, haikuwa rahisi kuamini kuwa angetokea mwanamke kuupinga utawala wake nchini Uganda.
Alice aliyezaliwa mwaka 1956 kutoka kabila la Acholi aliendesha mambo yake kwa staili ya imani za mizimu na katika hilo aliungwa mkono na wengi.
Hata alipoanzisha chama chake cha Holy Spirit Movement (HSM), haikuwa kazi ngumu kupata wafuasi kwani walio wengi waliamini kuwa Alice ana maono ya hali ya juu.
Kutokana na imani hiyo, akaingia mwituni kuupinga utawala wa Museveni kati ya Agosti mwaka 1986 hadi Novemba 1987.
Katika uhai wake, hakuwahi kupata mtoto ingawa aliolewa mara mbili. Baadaye akaachana na imani za kijadi na kujiunga na Kanisa Katoliki.
Hata hivyo, Mei 25, mwaka 1985 akaingiwa na pepo na kuwa mwendawazimu. Uendawazimu huo ukamfanya akose uwezo wa kusikia na kuzungumza pia.
Babaye akalazimika kumkimbiza kwa waganga wa jadi wapatao 11 kwa ajili ya tiba lakini hakuna aliyeweza kutatua tatizo hilo.
Zipo simulizi kwamba baada ya wataalamu hao wa tiba za asili kushindwa kumtibu Alice, babaye mzazi alimpeleka katika Mbuga ya Paraa ambako inaelezwa kuwa alitoweka kwa siku 40 na aliporejea aliambatana na mzimu.
Akawa miongoni mwa watu wenye nguvu za mizimu walioaminika karibu na eneo la Gulu nchini Uganda. Alikuwa na uwezo wa kutibu magonjwa mbalimbali. Inasemwa kwamba mzimu aliorejea nao baada ya kutoweka kwa siku 40 ndio uliomwezesha kupona uendawazimu.
Kutokana na nguvu hiyo, Alice alipata sifa kubwa ndani na nje ya Uganda. Wakati wa mapigano makali baina ya waasi na majeshi ya Serikali inaelezwa kuwa mwanamama huyo alielekezwa na mizimu kuacha kazi za tiba na badala yake aanzishe chama cha kuwakomboa Waganda.
Amri hiyo ya mizimu inadaiwa kutolewa Agosti 6, mwaka 1986 na kwamba kazi iliyokuwa mbele yake ni kusitisha uovu uliokuwa ikiendelea nchini humo.
Kwamba hapakuwa na haja ya kuhubiri au kukaa pembeni wakati kuna damu za raia wasio na hatia zinamwagika.
Katika mpango wake wa awali, Alice alikusudia kuuteka Mji Mkuu Kampala ambao ungekuja kuwa paradiso ya Waganda na bila shaka watu wa kabila la Acholi wangenufaika zaidi.
Alice katika mpango wake huo aliwaeleza watu wake kwamba kila anachopanga kina makusudio mazuri. “Haina maana kuwa daktari na kumtibu mtu leo wakati mtu huyo huyo kesho anauawa.”
Dhamira yake hiyo ndiyo ikamfanya aachane na udaktari na kusimama msitari wa mbele kupinga utawala uliopo.
Alikuja kuwa na msimamo kama wa Joseph Kony ambaye ni kinara wa kundi la waasi la Lord’s Resistance Army. Kwamba lengo ni kumwona Museveni akiachia ngazi nchini Uganda.
Lakini baadaye Alice alionekana kushindwa kutimiza dhamira yake kwani watu wa kabila la Acholi waliendelea kuangamia na ndoto ya kuiteka Kampala ikaanza kutoweka.
Jamii ikaendelea kuingiwa na hofu katika mambo mbalimbali na mbaya zaidi ni kuwa vifo vingi vilihusishwa na uchawi.
Hata hivyo, Alice hakukata tamaa na nguvu yake ikaibuka upya kwani katika hali fulani alipata ushindi kadri alivyoelekea Kampala.
Kwamba licha ya watu wake kuangamia, bado aliendelea kuwa na nguvu ya ushawishi na nguvu hiyo iliwafanya watu wengi kumuunga mkono na safari hii akitangaza kuwa ameongezewa mizimu.
Alifanikiwa kuwashawishi Waganda kwamba Museveni hakuwa mtu sahihi na kwamba aliikalia Uganda kimabavu na anapaswa kuondoka madarakani.
Kwa bahati nzuri kwake, wengi aliowahubiria ni wale ambao waliathirika vibaya na utawala wa Museveni na hivyo kuwa jambo rahisi kwao kumuunga mkono Alice.
Wahenga waliwahi kusema kuwa ngoma ikivuma sana haikawii kupasuka. Ndivyo ilivyotokea kwa Alice na safari yake ya kumng’oa Museveni. Baadhi ya wafuasi wake walianza kumtangaza kuwa ni mchawi.
Kwamba mizimu yake ni ya kichawi inayolenga kuleta maangamizi. Msuguano huo ukaifanya HSM kuzidiwa nguvu na hasa baada ya moto uliowashukia wakiwa mwituni karibu kabisa na Kampala. Alice akaikimbia nchi.
Alikimbilia katika kambi ya wakimbizi ya Ifo karibu na Dadaab kaskazini mwa Kenya na akiwa huko alitangaza kuwa ametengwa na mizimu.
Novemba mwaka 2004 alituhumiwa kusafirisha watoto kutoka Gulu nchini Uganda na kuwapeleka kambini kwake. Hata hivyo, mkono wa sheria haukumshukia.
Miaka miwili baadaye Alice aliibuka na kudai kuwa amegundua tiba ya ukimwi. Hata hivyo, alishindwa kuishawishi dunia katika madai yake hayo. Amefariki dunia Januari 17 mwaka huu baada ya kuugua kwa wiki moja. Haijulikani kapoteza maisha kwa maradhi gani.
Kuna simulizi kwamba mwanamama huyo enzi za uhai wake alikuwa na tabia ya kusema na wanyama au maji juu ya kilichokuwa kikiendelea nchini mwake.
“Nyie wanyama, Mungu kanituma kwenu niwaulize kama mnahusika na mauaji ya Uganda.” Katika simulizi hizo, wanyama walimjibu kuwa hawahusiki na badala yake nao pia waliumia na vitendo hivyo. Ikasemwa kuwa nyati alimwonyesha jeraha mguuni huku kiboko akionyesha jeraha mkononi.
Inaelezwa pia kuwa aliwahi kuyauliza maji kuhusu vita nchini Uganda. “Maji, nimekuja kukuuliza juu ya dhambi na umwagaji damu katika hii dunia.”
Nayo maji yakamjibu kwamba binadamu wenye miguu miwili wana tabia ya kuua ndugu zao na kutupa miili yao majini.
Simulizi hizo zinapasha pia kuwa baada ya majibu hayo, mzimu ulimtuma Alice kuendelea na jitihada za kuleta amani nchini Uganda. Akomeshe dhambi na umwagaji damu.
Wakati fulani alipokwenda katika Mlima Kilak, Alice anadaiwa kupewa nguvu na mlima huo kwenda kuutokomeza udhalimu. Pia alikabidhiwa dawa maalumu ya kuponya wagonjwa.
Baadaye akaja kutangaza pia kuwa kuna ujumbe kutoka kwa Mungu kwamba lipo kabila nchini Uganda ambalo lina damu ya kunguni. Akalitaja kabila hilo kuwa ni la Acholi.
Mbali na jitihada zake hizo, marehemu Alice anafanana na Joseph Kony katika mambo mawili. Mosi wote wawili ni wapinzani wa Museveni na pili, wote wanachanganya dini na uovu.
Alice amewahi kuchanganya mizimu na neno la Mungu kama ilivyo kwa Kony ambaye wakati wa Mfungo wa Ramadhan hufunga ingawa hula nyama ya nguruwe ambayo kwa imani ya Kiislamu ni haramu.
Makala hii imeandaliwa na INNOCENT MUNYUKU kwa msaada wa vyanzo mbalimbali vya habari.
Pepo la makocha Simba halipungwi kwa ungo
Na Innocent Munyuku
Kwa jina la mweza wa yote nakupa salamu za heri mdau wa Busati la Burudani. Mwenye Busati hana shaka wala dhiki kwani mambo yanakwenda kwa neema.
Hata hivyo, Mzee wa Busati ameona ni jambo la heri akiri kwamba kwa juma hili atakuwa adimu kwenye viunga vya kawaida. Hakika atakwenda mafichoni kwa ajili ya kupumzisha ubavu wake baada ya siku tele za kuwania nafasi kwenye daladala.
Lililo moyoni mwaka juma hili ni hili la Wekundu wa Msimbazi ambao kila kukicha wanasaka kocha na kumtimua. Kina Tupasyege wameandika juu ya hilo lakini Mzee wa Busati ana mtazamo tofauti.
Hataandika kuhusu ubovu wa uongozi na wala hatasema habari ya viongozi kuwa na uelewa mdogo katika masuala ya soka. Hilo anawaachia wenye ubavu wa kutema cheche. Mzee wa Busati hajazoea tafrani.
Mwataka aseme eti vinara wa Simba ni wabovu? La hasha! Au mwaridhia Mwenye Busati aseme kwamba kuna uvundo katika uongozi mzima wa Simba? Hapana. Hilo msitarajie hadi kiama kije.
Kama kuna wanaodhani kwamba Mwandika Busati atasimama kidete kusema ya kuwa ndani ya Simba kuna uzembe, hao wamenoa kwani siku kama hiyo haitafika.
Kwanini asimame atete juu ya maovu ya Simba wakati kuna Simba wa Yuda? Huyu aliyesifika kwa makali yake wakati alipokalia kiti cha Katibu Mkuu wa chama cha soka. Mwacheni aendelee kuwamo humo.
Lakini Mzee wa Busati angali na dukuduku juu ya hawa ndugu zake wenye maskani yao Mtaa wa Msimbazi jijini Darisalama. Wana mkosi gani hawa? Mbona makocha hawakai kwa muda mrefu kabla ya kutimka?
Je, ni kweli kwamba hao makocha wanaotua Msimbazi hawajui wanachokwenda kukifanya ndani ya Simba? Au mwataka tuamini kuwa huko wanakosaini mikataba kumejaa uvundo?
Yu wapi Trot Moloto? Neider dos Santos, mzee mzima wa Zambia Patrick Phiri nao walijaribu bahati yao na leo hawapo. Wameondoka na hivi karibuni katoweka Nielsen Elias aliyeamua kurejea kwao nchini Brazil.
Mara baada ya kuondoka ikaelezwa kuwa Elias ameshindwa kuendelea kukaa nchini kutokana na madai kuwa viongozi wa klabu hiyo wameshindwa kutekeleza majukumu yao na kusababisha kufanya kazi yake katika hali ngumu.
Mbrazili huyo ameondoka wakati Simba inashiriki Ligi Ndogo Tanzania Bara na hakufanya mkutano na uongozi wa timu kabla ya kuondoka kwake.
Hilo hawezi kulaumiwa kwani yasemwa kwamba wakati mwingine ni heri kuiga ujinga kuliko kuendeleza ustaarabu mbele ya mazuzu.
Mwaka juzi, Mzee wa Busati alikuwa nchini Zambia wakati huo Simba ilikuwa ikicheza na Zanaco kuwania fainali za Klabu Bingwa Afrika huku Phiri akiwa kocha wa Simba. Kulikuwa na mjadala mrefu juu ya majaliwa ya Simba katika mechi hiyo ambayo ilimalizika kwa wenyeji kushinda kwa mabao 3-1.
Katika mazungumzo mafupi kwenye Hoteli ya St. Andrew’s jijini Lusaka, Phiri alionyesha wasiwasi wake juu ya hatima yake ndani ya Simba. Alikuwa akilalama juu ya maisha halisi kama kocha nchini Tanzania.
Akaweka wazi kwamba ahadi nyingi zilizotolewa na uongozi wa Simba hazijatekelezwa na kulikuwa na kila dalili ya kutotekelezwa. Akarejea Darisalama na baada ya muda mfupi akachomoka akiiacha Simba chini ya Jamhuri Kihwelo.
Tatizo kama hilo ndilo lililowakuta kina Santos na Nielsen. Ahadi za Simba hazitekelezeki, kuna ubabaishaji mwingi ndani ya klabu hiyo. Kutekeleza ahadi limekuwa jambo gumu kama vile kuzikutanisha mbingu na ardhi.
Basi kama mmeshindwa kuwa na makocha kutoka ughaibuni ni heri mchukue nafasi hii kuwaajiri wenyeji waliozoea longolongo zenu. Kinachoonekana hapa ni kwamba pepo la makocha Simba haliwezi kupungwa hata kwa ungo.
Msilete aibu kwa taifa letu kwani matokeo yake huko mbele ya safari ni mabaya kuliko mnavyodhani. Tekelezeni ahadi zenu na kamwe msimwige tembo maliwatoni.
Kama mna senti 10 semeni uwezo wenu ni huo na msije mkajidanganya kwamba mna ubavu wa kutoa senti 20 mtapasuka msamba.
Vinginevyo Mwenye Busati anafikia mwisho wiki hii ya neema. Wiki ya kumwaga maharagwe na kupisha vipapatio vya kuku vifanye kazi yake tumboni.
Nyama ya ng’ombe, mbuzi haziliki kwani RVF imetawala. Hata panya buku wa Pachoto nao hawaliki. Basi imekuwa balaa.
Wasalaam,
Kwa jina la mweza wa yote nakupa salamu za heri mdau wa Busati la Burudani. Mwenye Busati hana shaka wala dhiki kwani mambo yanakwenda kwa neema.
Hata hivyo, Mzee wa Busati ameona ni jambo la heri akiri kwamba kwa juma hili atakuwa adimu kwenye viunga vya kawaida. Hakika atakwenda mafichoni kwa ajili ya kupumzisha ubavu wake baada ya siku tele za kuwania nafasi kwenye daladala.
Lililo moyoni mwaka juma hili ni hili la Wekundu wa Msimbazi ambao kila kukicha wanasaka kocha na kumtimua. Kina Tupasyege wameandika juu ya hilo lakini Mzee wa Busati ana mtazamo tofauti.
Hataandika kuhusu ubovu wa uongozi na wala hatasema habari ya viongozi kuwa na uelewa mdogo katika masuala ya soka. Hilo anawaachia wenye ubavu wa kutema cheche. Mzee wa Busati hajazoea tafrani.
Mwataka aseme eti vinara wa Simba ni wabovu? La hasha! Au mwaridhia Mwenye Busati aseme kwamba kuna uvundo katika uongozi mzima wa Simba? Hapana. Hilo msitarajie hadi kiama kije.
Kama kuna wanaodhani kwamba Mwandika Busati atasimama kidete kusema ya kuwa ndani ya Simba kuna uzembe, hao wamenoa kwani siku kama hiyo haitafika.
Kwanini asimame atete juu ya maovu ya Simba wakati kuna Simba wa Yuda? Huyu aliyesifika kwa makali yake wakati alipokalia kiti cha Katibu Mkuu wa chama cha soka. Mwacheni aendelee kuwamo humo.
Lakini Mzee wa Busati angali na dukuduku juu ya hawa ndugu zake wenye maskani yao Mtaa wa Msimbazi jijini Darisalama. Wana mkosi gani hawa? Mbona makocha hawakai kwa muda mrefu kabla ya kutimka?
Je, ni kweli kwamba hao makocha wanaotua Msimbazi hawajui wanachokwenda kukifanya ndani ya Simba? Au mwataka tuamini kuwa huko wanakosaini mikataba kumejaa uvundo?
Yu wapi Trot Moloto? Neider dos Santos, mzee mzima wa Zambia Patrick Phiri nao walijaribu bahati yao na leo hawapo. Wameondoka na hivi karibuni katoweka Nielsen Elias aliyeamua kurejea kwao nchini Brazil.
Mara baada ya kuondoka ikaelezwa kuwa Elias ameshindwa kuendelea kukaa nchini kutokana na madai kuwa viongozi wa klabu hiyo wameshindwa kutekeleza majukumu yao na kusababisha kufanya kazi yake katika hali ngumu.
Mbrazili huyo ameondoka wakati Simba inashiriki Ligi Ndogo Tanzania Bara na hakufanya mkutano na uongozi wa timu kabla ya kuondoka kwake.
Hilo hawezi kulaumiwa kwani yasemwa kwamba wakati mwingine ni heri kuiga ujinga kuliko kuendeleza ustaarabu mbele ya mazuzu.
Mwaka juzi, Mzee wa Busati alikuwa nchini Zambia wakati huo Simba ilikuwa ikicheza na Zanaco kuwania fainali za Klabu Bingwa Afrika huku Phiri akiwa kocha wa Simba. Kulikuwa na mjadala mrefu juu ya majaliwa ya Simba katika mechi hiyo ambayo ilimalizika kwa wenyeji kushinda kwa mabao 3-1.
Katika mazungumzo mafupi kwenye Hoteli ya St. Andrew’s jijini Lusaka, Phiri alionyesha wasiwasi wake juu ya hatima yake ndani ya Simba. Alikuwa akilalama juu ya maisha halisi kama kocha nchini Tanzania.
Akaweka wazi kwamba ahadi nyingi zilizotolewa na uongozi wa Simba hazijatekelezwa na kulikuwa na kila dalili ya kutotekelezwa. Akarejea Darisalama na baada ya muda mfupi akachomoka akiiacha Simba chini ya Jamhuri Kihwelo.
Tatizo kama hilo ndilo lililowakuta kina Santos na Nielsen. Ahadi za Simba hazitekelezeki, kuna ubabaishaji mwingi ndani ya klabu hiyo. Kutekeleza ahadi limekuwa jambo gumu kama vile kuzikutanisha mbingu na ardhi.
Basi kama mmeshindwa kuwa na makocha kutoka ughaibuni ni heri mchukue nafasi hii kuwaajiri wenyeji waliozoea longolongo zenu. Kinachoonekana hapa ni kwamba pepo la makocha Simba haliwezi kupungwa hata kwa ungo.
Msilete aibu kwa taifa letu kwani matokeo yake huko mbele ya safari ni mabaya kuliko mnavyodhani. Tekelezeni ahadi zenu na kamwe msimwige tembo maliwatoni.
Kama mna senti 10 semeni uwezo wenu ni huo na msije mkajidanganya kwamba mna ubavu wa kutoa senti 20 mtapasuka msamba.
Vinginevyo Mwenye Busati anafikia mwisho wiki hii ya neema. Wiki ya kumwaga maharagwe na kupisha vipapatio vya kuku vifanye kazi yake tumboni.
Nyama ya ng’ombe, mbuzi haziliki kwani RVF imetawala. Hata panya buku wa Pachoto nao hawaliki. Basi imekuwa balaa.
Wasalaam,
Ya Tunis na CCM Kirumba Mwanza
na innocent munyuku
ALITOKOMEA kusikojulikana na mbaya zaidi ni kwamba hakuwahi kuaga wala kusema kipi kilimsibu hadi akaingia mitini. Mzee wa Busati kaibuka na sijui aanze kujitetea kimtindo gani.
Pengine awe mtii kama ngamia kwa kusema kuwa alitenda kosa kuacha kuteta na wadau wake kama ilivyokuwa miaka ya ile ya neema. Miaka ambayo nchi ilifurika maziwa na asali ya mwitu.
Mzee wa Busati ameshaweka wazi kwamba yu radhi kwa adhabu lakini adhabu hiyo isiwe ya kumlaza njaa au kuutokomeza uhai wake kama alivyofanyiwa sahiba Saddam Hussein.
Huu ni mwanzo wa makazi yake mapya na kwa uweza wa Allah, Mwenye Busati atakuwa akinguruma hapa kila Jumatatu ambayo wengi wameipachika kuwa ‘Blue Monday’.
Juma hili analianza kwa kuwapa pole na pia kuwapa moyo Wana wa Jangwani ambao juzi walipigwa mweleka katika kuwania taji la Klabu Bingwa Afrika. Wameshindwa kufurukuta mbele ya Waarabu wa Esperance ya Tunisia.
Katika kipute chao mara ya kwanza mjini Tunis, Yanga ililala kwa mabao 3-0 na hapo shughuli ilipoanza kuwa ngumu. Kwani sasa kibarua cha Yanga kikawa lazima wawaadabishe Esperance kwa mabao 4-0 ili wasonge mbele.
Zikaja soga za kijiweni kwamba kipigo hicho cha Yanga kilitokana na mchezaji wake Hamis Yusuf kutolewa nje kwa kadi nyekundu.
Wenye akili zao walishangaa na kuguna. Kwamba hivi kweli kuondolewa kwa mchezaji huyo kuliwachanganya Yanga kiasi cha kushindwa kulinga lango lake? Hivi ni visingizio ambavyo havina maana kwa wanaojua soka.
Juzi Wana wa Jangwani wameumbuka kwa kauli hiyo ya visingizio kwani katika mechi yao ya marudiano kwenye Uwanja wa Kirumba jijini Mwanza, Esperance ikakumbwa na dhahama baada ya wachezaji wawili kulimwa kadi nyekundu.
Kwa bahati mbaya sana Mzee wa Busati hakuwapo uwanjani lakini alikuwa akifuatilia kipute hicho kwa njia ya redio na njia nyingine za mawasiliano na kwa hakika aliposikia kuwa wachezaji wawili wa Esperance wako nje kwa kadi nyekundu akaamini sasa neema kwa Yanga imetimia.
Hakika Mwandika Busati aliamini hivyo kwa kigezo cha Tunis kwamba kwa vile Yanga ilifungwa baada ya kuwa na wachezaji 10 dimbani basi kwa vyovyote mwisho wa Esperance ulishawadia kwani wako tisa dimbani. Dakika zikayoyoma na hakuna bao lililopatikana.
Mzee wa Busati hapendi unafiki. Kwanini mwaleta visingizio visivyo na kichwa wala miguu? Najua wenye kuipenda Yanga watafura kwa hasira lakini ukweli lazima usemwe ili kuepuka aibu kama hii ya juzi.
Mliporejea mlisema waamuzi waliwabeba Waarabu na je, vipi ya Kirumba mwasemaje? Mambo yanapoenda upogo ni heri mkakiri kwamba maji yamezidi unga. Semeni kwa uwazi ili hata wasojua soka wakaja kuwakebehi kwa vijembe vya kuchoma mitima yenu.
Waraka huu hauna lengo la kuwaumiza washirika wa Jangwani bali walenga kutoa changamoto ya moto ili siku zijazo msije mkaleta visingizio ambavyo mwisho wa siku vinawaletea aibu. Naam badilikeni kwani husemwa kwamba johari za mtu ni mbili, akili na haya.
Baada ya kuangukia pua katika Klabu Bingwa Afrika, Yanga sasa ina nafasi nyingine kuwania Kombe la Shirikisho. Huu ni muda wa kujipanga upya ili kufuta aibu iliyotokea.
Neno la Mzee wa Busati kwenu ni kuwa badala ya kuanza kusaka wachawi, Yanga ijipange upya kwa umakini wa hali ya juu. Huu usiwe muda wa kulala makaburini, sikilizeni na kutekeleza mafunzo ya makocha ili msije mkachacha.
Vinginevyo Mwenye Busati anakaribia kufika mwisho kwa leo hii akitafakari namna ya kuumalizia mwezi huu uliombatana na maumivu. Pasaka imefuja mifuko ya wengi, ngwenje zimeyeyuka na wanaokula mkate mchana si kama wamependa bali ni hali ngumu za maisha.
Mshirika mmoja kule Tabata Relini sasa amekuwa mpole kama aliyenyeshewa mvua. Kazizima na moyo wake huyo ajiitaye ‘mzee wa kutibua’ unatweta kwa hofu kama atafanikiwa kufika mwisho wa mwezi. Miayo imezidi na madeni yanazidi kipimo. Pole mwanakwetu kaza buti.
Wasaalam,
ALITOKOMEA kusikojulikana na mbaya zaidi ni kwamba hakuwahi kuaga wala kusema kipi kilimsibu hadi akaingia mitini. Mzee wa Busati kaibuka na sijui aanze kujitetea kimtindo gani.
Pengine awe mtii kama ngamia kwa kusema kuwa alitenda kosa kuacha kuteta na wadau wake kama ilivyokuwa miaka ya ile ya neema. Miaka ambayo nchi ilifurika maziwa na asali ya mwitu.
Mzee wa Busati ameshaweka wazi kwamba yu radhi kwa adhabu lakini adhabu hiyo isiwe ya kumlaza njaa au kuutokomeza uhai wake kama alivyofanyiwa sahiba Saddam Hussein.
Huu ni mwanzo wa makazi yake mapya na kwa uweza wa Allah, Mwenye Busati atakuwa akinguruma hapa kila Jumatatu ambayo wengi wameipachika kuwa ‘Blue Monday’.
Juma hili analianza kwa kuwapa pole na pia kuwapa moyo Wana wa Jangwani ambao juzi walipigwa mweleka katika kuwania taji la Klabu Bingwa Afrika. Wameshindwa kufurukuta mbele ya Waarabu wa Esperance ya Tunisia.
Katika kipute chao mara ya kwanza mjini Tunis, Yanga ililala kwa mabao 3-0 na hapo shughuli ilipoanza kuwa ngumu. Kwani sasa kibarua cha Yanga kikawa lazima wawaadabishe Esperance kwa mabao 4-0 ili wasonge mbele.
Zikaja soga za kijiweni kwamba kipigo hicho cha Yanga kilitokana na mchezaji wake Hamis Yusuf kutolewa nje kwa kadi nyekundu.
Wenye akili zao walishangaa na kuguna. Kwamba hivi kweli kuondolewa kwa mchezaji huyo kuliwachanganya Yanga kiasi cha kushindwa kulinga lango lake? Hivi ni visingizio ambavyo havina maana kwa wanaojua soka.
Juzi Wana wa Jangwani wameumbuka kwa kauli hiyo ya visingizio kwani katika mechi yao ya marudiano kwenye Uwanja wa Kirumba jijini Mwanza, Esperance ikakumbwa na dhahama baada ya wachezaji wawili kulimwa kadi nyekundu.
Kwa bahati mbaya sana Mzee wa Busati hakuwapo uwanjani lakini alikuwa akifuatilia kipute hicho kwa njia ya redio na njia nyingine za mawasiliano na kwa hakika aliposikia kuwa wachezaji wawili wa Esperance wako nje kwa kadi nyekundu akaamini sasa neema kwa Yanga imetimia.
Hakika Mwandika Busati aliamini hivyo kwa kigezo cha Tunis kwamba kwa vile Yanga ilifungwa baada ya kuwa na wachezaji 10 dimbani basi kwa vyovyote mwisho wa Esperance ulishawadia kwani wako tisa dimbani. Dakika zikayoyoma na hakuna bao lililopatikana.
Mzee wa Busati hapendi unafiki. Kwanini mwaleta visingizio visivyo na kichwa wala miguu? Najua wenye kuipenda Yanga watafura kwa hasira lakini ukweli lazima usemwe ili kuepuka aibu kama hii ya juzi.
Mliporejea mlisema waamuzi waliwabeba Waarabu na je, vipi ya Kirumba mwasemaje? Mambo yanapoenda upogo ni heri mkakiri kwamba maji yamezidi unga. Semeni kwa uwazi ili hata wasojua soka wakaja kuwakebehi kwa vijembe vya kuchoma mitima yenu.
Waraka huu hauna lengo la kuwaumiza washirika wa Jangwani bali walenga kutoa changamoto ya moto ili siku zijazo msije mkaleta visingizio ambavyo mwisho wa siku vinawaletea aibu. Naam badilikeni kwani husemwa kwamba johari za mtu ni mbili, akili na haya.
Baada ya kuangukia pua katika Klabu Bingwa Afrika, Yanga sasa ina nafasi nyingine kuwania Kombe la Shirikisho. Huu ni muda wa kujipanga upya ili kufuta aibu iliyotokea.
Neno la Mzee wa Busati kwenu ni kuwa badala ya kuanza kusaka wachawi, Yanga ijipange upya kwa umakini wa hali ya juu. Huu usiwe muda wa kulala makaburini, sikilizeni na kutekeleza mafunzo ya makocha ili msije mkachacha.
Vinginevyo Mwenye Busati anakaribia kufika mwisho kwa leo hii akitafakari namna ya kuumalizia mwezi huu uliombatana na maumivu. Pasaka imefuja mifuko ya wengi, ngwenje zimeyeyuka na wanaokula mkate mchana si kama wamependa bali ni hali ngumu za maisha.
Mshirika mmoja kule Tabata Relini sasa amekuwa mpole kama aliyenyeshewa mvua. Kazizima na moyo wake huyo ajiitaye ‘mzee wa kutibua’ unatweta kwa hofu kama atafanikiwa kufika mwisho wa mwezi. Miayo imezidi na madeni yanazidi kipimo. Pole mwanakwetu kaza buti.
Wasaalam,
Subscribe to:
Posts (Atom)