na innocent munyuku
SIKU zinazidi kukatika hii maana yake ni kwamba mwaka nao unayoyoma. Mambo nayo yanasogea huku ndoto za mwaka mpya kwamba masuala mengi yatakuwa poa zikiendelea kunasa kwenye bongo.
Lakini ukweli ni kwamba hakuna jipya katika maisha zaidi ya kuendelea kusuguana na makali ya bajeti. Mlo wa mmoja kwa siku haiwezi tena kuwa habari mpya.
Kupanda hata daladala iliyofurika hadi kutapita limekuwa jambo la anasa. Wabongo walio wengi sasa hasa waishio katika miji ya kuhitaji mabasi kwenda katika majukumu wamepungua miili.
Wanapungua miili kwani kila uchao wanasaga mguu kwenda katika majukumu yao. Hili ni jambo jema kwa afya ya mwili kwani vitambi vinapungua.
Nani atathubutu kupanda mabasi manne kila siku na nauli yenyewe iko juu? Kwa hiyo wakati mwingine unapunguza bajeti kwa kutembea kwa miguu ili nyumbani nako wauone mlango wa maliwato.
Huo ulikuwa utangulizi wa Mzee wa Busati Jumanne hii ambayo kwake ingali ikimpa hamu ya kuendelea kuwamo katika safina hii ya mwaka 2008.
Si lengo lake kujadili hali ya uchumi kwa Wadanganyika kwani kufanya hivyo kutazidi kumwongezea machungu ya maisha. Hana mbadala. Kujadili pasipo suluhisho ni dhambi.
Leo hii Mzee wa Busati ameona ni vema atete na wadau wa muziki nchini ambao bila shaka mambo mengine yamenasa katika vichwa vyao pasipo kujua kwamba wanapotoka.
Mwandika Busati ni msemakweli pia. Wala hajifichi na wala hawezi kukana kwamba anatumia yale maji yenye rangi ya mende kutoka Ilala.
Huwa anakaa kwenye mikusanyiko ya aina hiyo mara kwamba mara kwa kile kinachoitwa mkao wa majadiliano na wakati mwingine kupoteza mawazo.
Awapo huko mara nyingi huona wanamuziki wakipamba ukumbi kwa maikrofoni zao. Wanaimba kwa mbwembwe kuwapa burudani wateja katika baa husika.
Hakika wanatia faraja kwa nyimbo wanazoibuka nazo kwa siku. Wateja watahamasika na wengine pombe zikifika pahala pake huacha viti vyao na kwenda kuserebuka. Hiyo ni faraja ya moyo.
Lakini kinachomshangaza Mwandika Busati ni kwamba hao wanaoalikwa kutumbuiza wamekuwa kama ndege aitwaye kasuku.
Kama hujui sifa ya kasuku basi ni kwamba huyu ndege ana tabia ya kuiga kusema kama binadamu na mara nyingi hufugwa katika nyumba.
Atajitahidi kuiga kila kisemwacho. Hii ndiyo sifa kuu ya kasuku, ndege mwenye rangi nyingi ambaye ni kipenzi cha binadamu katika makazi yake.
Anachosema Mzee wa Busati kuhusu hizo bendi za muziki zinazotumbuiza katika flani flani ni kwamba wamezidi kuiga nyimbo za wasanii wengine.
Lakini wanatamba wakijiita wao ni wasanii mahiri. Watajiita wanamuziki waliobobea. Huku ni kupotosha ukweli wa mambo. Pengine lugha iko gongana na hivyo kutojua maana halisi ya msanii.
Ajuavyo Mzee wa Busati ni kwamba msanii ni kwamba ni mtu mwenye ustadi wa kuchora, kuchonga au kutia nakshi. Husemwa pia kuwa msanii ni mwenye ufundi wa kutunga na kutoa mawazo yake kama vile kwa ushairi, hadithi au tamthiliya.
Haijasemwa kwamba msanii ni mtu mwenye uwezo wa kuiga iga kama kasuku. Huo si usanii bali ubabaishaji.
Kama kweli mmeamua kuimba si mtunge nyimbo zenu? Ya nini kuendelea kuimba nyimbo za kale? Za kwenu zitasikizwa lini?
Mmebaki na nyimbo za Juma Kilaza na David Kabaka kila siku. Af mkitoka hapo mmeutwika kwa pombe za bure mnatembea kwa matao mkisema kwamba nyie ni wasanii.
Kama kweli mmeamua kushika vipaza sauti kwa jina la muziki basi leteni tungo zenu zisikike ili siku moja nanyi mtambe kwamba mlipata kufyatua albamu iliyovuma.
Si dhambi kuiga nyimbo za kale lakini isiwe kuwahadaa mashabiki kwa onyesho zima. Imbeni nyimbo zenu ili hata mkijisifu muwe na pa kuegemea.
Hivi leo hii Mwandika Busati anawezaje kujiita mwimbaji mahiri eti kwa vile tu kapaza sauti kanisani wakati wa kuimba tenzi za rohoni. Haikubaliki!
Nyimbo za kina Mbaraka Mwishehe zingali zinapendwa hadi kesho. Wengi wanapenda kuzikiza lakini ukweli wa mambo ni kwamba kubaki kuziiga pasipo kutunga mpya ni kupoteza wakati.
Mwandika Busati amefikia kikomo kwa wiki hii. Ataendelea na mengine juma lijalo kwa kasi ile ile pasipo kuogopa tindikali wala mtutu wa bunduki. Panapo ukweli tutaambizana.
Wasalaam,
Monday, January 14, 2008
Sunday, January 6, 2008
Kenya ilikuwa vipande mwaka mmoja kabla ya uchaguzi
MWAKA mmoja kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu nchini Kenya, wanasiasa waliotaka kuwania urais tayari walikuwa wanapigana vikumbo na kuwasha moto mkali wa kisiasa nchini humo. Rais wa sasa, Mwai Kibaki, anayedaiwa kuwa 'amebaka' demokrasia na kulazimisha kubakia Ikulu baada ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika Desemba 27 mwaka 2007, alikuwa akilalamikiwa sana wakati huo kwa kushindwa kudhibiti nafasi yake ya urais, na alikuwa anapewa nafasi ndogo ya kushinda.
KILA Mkenya alikuwa anaushangaa utitiri wa watu waliokuwa `wamejitokeza mapema sana kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu ambao ulifanyika Desemba 27 mwaka huu.
Rais Mstaafu wa Kenya, Daniel arap Moi, alikuwa miongoni mwao. "Wanasiasa wanahusika kwa kuigawa nchi ya Kenya vipande vipande kwa kuhubiri ukabila. Wanazungukazunguka huku na kule wakijidai kuwa hiyo ndiyo demokrasia, kumbe wao wanawinda maslahi yao ambayo hayataisaidia nchi.
"Katika chama cha KANU, Mwenyekiti wake Uhuru Kenyatta anapata upinzani kutoka kwa Katibu Mkuu wa chama hicho, William Ruto, ambaye naye pia anataka kugombea urais.
"Chama kilichoiasi KANU, Liberal Demoratic Party (LDP) ambacho kinaongozwa na Raila Odinga kina wawaniaji urais wengi, akiwamo Raila mwenyewe, Kalonzyo Musyoka, Najib Balala na Musalia Mudavadi.
"Rais Mwai Kibaki atagombea kupitia chama cha Narc - Kenya baada ya Umoja uliounda Narc na kuiondoa KANU madarakani kusambaratika.
"Mwenyekiti wa Ford Kenya, Musikari Kombo, ingawa bado yumo ndani ya umoja wa Narc, ambao ndio unatawala nchi, naye ameamua kuwania urais," alisema Moi kwa masikitiko makubwa mwaka mmoja uliopita, na kuongeza:
"Hali hii haitaisaidia Kenya, na hasa ikizingatiwa kwamba wote hawa kila mmoja ana ajenda binafsi iliyojikita katika ukabila ili kufikia malengo yake binafsi. Hali hii itaivunja nchi na kuiacha vipande vipande."
Haya yalikuwa matamshi ya kwanza ya Mzee Moi kuhusu hali ya siasa ya Kenya na mwelekeo wake tangu chama chake cha KANU kilipoondolewa madarakani na Umoja wa Narc uliomweka madarakani Rais Kibaki mwaka 2002.
Moi alikuwa akikwepa sana kutoa mtamshi yoyote kuhusu Serikali ya Kibaki kwa madai kuwa 'Kibaki alikuwa anahitaji muda kuweka misingi mizuri ya utawala.'
Moi hakuwa peke yake katika kuonyesha wasiwasi wa utiriri wa wawaniaji urais. Mwandishi Mashuhuri nchini Kenya, Mutuma Mathiu, katika kuonyesha wasiwasi wake kuhusu hali ya kisiasa alisema:
"Jinsi mambo yanavyokwenda nchini Kenya, kila kiumbe kinachovuta hewa, na hasa wanasiasa, kitaingia katika kinyang'anyiro cha kuwania urais ifikapo Desemba mwaka huu.
"Musikari Kombo, Najib Balala, Raila Odinga, William Ruto na mkururo wa wanasiasa wengine tayari wamekwisha kutamka kuingia kwenye kinyang'anyiro cha kuwania urais.
"Haitashangaza kuwa ifikapo Desemba mwaka 2007, hata wale ambao tayari wamekufa watafufuka kwa kuogopa kuachwa nyuma kwenye kinyang'anyiro hiki.
"Sasa itakapofika hasa wakati wenyewe ndipo kitakuwa kivumbi. Pengine itakuwa zamu ya mbuzi, ng'ombe, mbwa na paka ambao nao wataonyesha nia ya kuchukua nafasi aliyoikalia Rais Kibaki," alisema Mathiu kwa kejeli, na kuongeza:
"Kwa maoni yangu, uwaniaji huu wa urais mwaka mmoja kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu ni dalili za wazi kuwa viongozi wetu ni wabinafsi na wapenda madaraka. Hawawajali wananchi na maendeleo ya Kenya kwa ujumla wake, bali ni waroho, wanaojiangalia wao wenyewe tu. Siasa za Kenya sasa ni pori la vurugu na mkanganyiko wa uongo wa kisiasa."
Ni kweli Kenya ilikuwa tayari imemeguka vipande vipande, vyote vikijikita katika misingi ya ubinafsi na ukabila. Waluo wa Nyanza walikuwa hawasikii chochote, walikuwa wanataka kumsikia Raila Odinga tu, basi. Waluhya magharibi mwa Kenya walikuwa wanamwangalia mtu wao Musalia Mudavadi, japo kulikuwa na Mluhya mwingine, Musikari Kombo, wa chama cha Ford Kenya. Wakikuyu, kabila kubwa kabisa anakotoka Rais Kibaki, hao ndio kabisa damu yao inanuka Ukikuyu tu, na hii inajionyesha wazi wazi; na kabila hili linaamini kuwa ndilo lenye haki ya kuitawala Kenya kisiasa na kiuchumi.
Waluo na Waluhya ni majirani, na hawajawahi kuungana kwa nia ya kupeleka urais magharibi mwa Kenya. Kwa zaidi ya miaka 44 iliyopita, Waluo na Waluhya wamekuwa na sauti kubwa katika kuamua nani awe mpangaji wa Ikulu - ama kwa uamuzi wa moja kwa mja au wa chini chini.
Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2002, Waluo na Waluhya waliupigia umoja wa Narc kura na kumwezesha Kibaki kunyakua madaraka. Baada ya kuingia madarakani, Kibaki alimteua Mluhya, Kijana Wamalwa (sasa ni marehemu), kuwa Makamu wa Rais, na kumwacha pembeni Raila Odinga. Hii ilikuwa kinyume cha makubaliano ya awali kati yake (Kibaki) na Raila kwamba nafasi hiyo ingekuwa ya Raila hasa baada ya kumsaidia sana Kibaki kuukwaa urais.
Baada ya kifo cha Wamalwa, Kibaki alimteua Mluhya tena, Moody Awori, kushika nafasi ya Makamu wa Rais, hatua ambayo iliendelea kumuudhi sana Raila.
Kuna uvumi kuwa Mudavadi na Raila walijaribu kutafuta fomula ya kuunganisha makabila haya mawili (Waluo na Waluhya) ili kujihakikishia kura nyingi katika Uchaguzi Mkuu uliomalizika wiki iliyopita.
Hatua hii ilikuwa na nia ya kufifisha nguvu za kabila kubwa la Wakikuyu linalokaa katikati mwa Kenya, na watu wa Bonde la Ufa (Rift Valley) ambako Mzee Moi alikuwa anadaiwa kuwa na ushawishi mkubwa.
Raila, Mudavadi na Musyoka anayetoka katika kabila la Wakamba, wakiungwa mkono na watu wa pwani mwa Kenya ambako anatoka Balala walimshinda Rais Kibaki Novemba 21, 2005 kwa kutumia mwavuli wa Orange Democratic Movement (ODM) wakati wa kura za maoni ambako Rais Kibaki alitaka kubadili Katiba. Huu ulikuwa mchuano kati ya Chungwa na Ndizi ambao ulimwacha Rais Kibaki njia panda kisiasa.
Kwa upande mwingine, Rais Mstaafu Moi alikuwa anapenda safari hii Uhuru Kenyatta ashinde urais baada ya juhudi zake kupitia kilichoitwa Mradi wa Uhuru (Uhuru Project) kushindwa vibaya mwaka 2002, na kuufanya Umoja wa Narc kunyakua madaraka, hali iliyosababisha chama chake cha KANU kuwa chama cha upinzani kwa mara ya kwanza tangu Kenya ipate Uhuru Desemba mwaka 1963.
Lakini kwa hali ya kisiasa ilivyokuwa, hii isingewezekana. Maji yalikuwa marefu sana kwa Mzee Moi. Ni kweli wakati huo alikuwa na ushawishi mkubwa kisiasa nyumbani kwake katika Bonde la Ufa ambao sasa unafifia kwa kasi. Hivyo asingeweza kumuuza Uhuru Kenyatta kwa Waluhya, Waluo, Wakamba (anakotoka Musyoka) na sehemu za pwani mwa Kenya.
Uhuru ni Mkikuyu, na makabila mengine nchini Kenya hayawaamini kabisa Wakikuyu kwa sababu ya kuhodhi siasa na biashara za nchi hiyo kupitia migongo ya makabila mengine. Watu wa pwani wanakwenda mbali zaidi kwa kusema kuwa "heri kula na Mluo kuliko kula au kuwa karibu na Mkikuyu".
Tetesi zilizokuwa zinavuma wakati huo mingoni mwa makabila yanayoishi katika majimbo ya uchaguzi pwani mwa Kenya zilikuwa zinasema kuwa miongoni mwa watu waliojitokeza kugombea urais, Musyoka ndiye wangependa awe Rais, na Raila awe Waziri Mkuu baada ya Katiba kubadilishwa.
Watu wa pwani hawakuwa peke yao kwa hili. Walikuwapo baadhi ya Wakenya sehemu nyingine za nchi ambao walipenda kuona hali inakuwa hivyo baada ya Uchaguzi Mkuu ili kumfanya Raila asiendelee kutingisha nchi kisiasa.
Katika makubaliano na Kibaki kabla Raila hajajiunga na Umoja wa Narc, kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2002, Raila alipaswa awe Waziri Mkuu kama ilivyodokezwa hapo juu.
Baada ya Rais Kibaki kuingia Ikulu, alimpiga teke Raila baada ya washauri wa karibu sana wa Kibaki, hasa kutoka katika kabila lake, kufanikiwa kumshawishi kufanya hivyo. Inasemekana kuwa ni watu hawa hawa waliomshawishi na kumshinikiza agombee tena urais safari hii kwa madai kuwa 'nchi haiwezi kuchukuliwa na Mluo.'
Tangu Rais Kibaki amweke pembeni, Raila ameupa taabu sana uongozi wake hadi majuzi Uchaguzi Mkuu ulipofanyika. Amekuwa mwiba mkali kwake, na ni mtu anayeogopwa sana na Kibaki mwenyewe na wengi wa mawaziri wake.
Kwa bahati mbaya sana kitu kimoja ni dhahiri nchini Kenya, nacho ni kwamba siasa zimejikita kwenye ukabila kwa kiwango cha kutisha. Wanasiasa wengi wanahubiri demokrasia na nia ya kuwakwamua wanyonge wa Kenya kutokana na lindi la umasikini, lakini moyoni wamesheheni ukabila na ajenda binafsi za kuwanufaisha wao na watu wa karibu yao.
Mbali na ukabila, jambo ambalo Wakenya wengi linawakera ni jinsi Rais Kibaki alivyoshindwa kudhibiti nafasi yake ya urais kabla ya Uchaguzi Mkuu wa juzi, kushindwa kuwadhibiti mawaziri na maofisa wake waandamizi kiasi kwamba wanafanya mambo jinsi wanavyoona, ukiwamo ufisadi; na mke wake, Lucy Kibaki, kuingilia masuala ya Serikali wakati yeye si sehemu ya Baraza la Mawaziri.
Wakenya wengi hawawaamini wanasiasa wakati huu ambako ufisadi unaongezeka, na Serikali kuonyesha kushindwa kufanya chochote cha maana kuzuia baa hili.
Wananchi wengi jijini Nairobi na mjini Kisumu mwaka mmoja uliopita walikuwa wanasema wazi kuwa Rais Kibaki akiamua kusimama kugombea tena urais atajiaibisha mwenyewe, na hasa baada ya 'kuvurunda' sana tangu achaguliwe kuwa Rais, na kwamba ishara za nyakati hazipo upande wake, yaani tayari zimekwisha kumpa kisogo.
Walisema kuwa hii itakuwa mbaya zaidi kama atasimama kupambana na Raila Odinga ambaye ana nguvu na ushawishi mkubwa kisiasa. Walisema kuwa ikiwa itatokea hivyo, mambo mawili yangetokea; ama Kibaki angelazimika kukubali kushindwa na kuondoka Ikulu au kutumia vyombo vya dola kuiba kura ili aonekane ameshinda, kitu ambacho kingeitikisa nchi.
Na kweli imetokea hivyo. Nchi si tu imetikisika, bali pia imewaka moto. Ni kama moto wa nyika wakati wa kiangazi. Masikini Kenya!
KILA Mkenya alikuwa anaushangaa utitiri wa watu waliokuwa `wamejitokeza mapema sana kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu ambao ulifanyika Desemba 27 mwaka huu.
Rais Mstaafu wa Kenya, Daniel arap Moi, alikuwa miongoni mwao. "Wanasiasa wanahusika kwa kuigawa nchi ya Kenya vipande vipande kwa kuhubiri ukabila. Wanazungukazunguka huku na kule wakijidai kuwa hiyo ndiyo demokrasia, kumbe wao wanawinda maslahi yao ambayo hayataisaidia nchi.
"Katika chama cha KANU, Mwenyekiti wake Uhuru Kenyatta anapata upinzani kutoka kwa Katibu Mkuu wa chama hicho, William Ruto, ambaye naye pia anataka kugombea urais.
"Chama kilichoiasi KANU, Liberal Demoratic Party (LDP) ambacho kinaongozwa na Raila Odinga kina wawaniaji urais wengi, akiwamo Raila mwenyewe, Kalonzyo Musyoka, Najib Balala na Musalia Mudavadi.
"Rais Mwai Kibaki atagombea kupitia chama cha Narc - Kenya baada ya Umoja uliounda Narc na kuiondoa KANU madarakani kusambaratika.
"Mwenyekiti wa Ford Kenya, Musikari Kombo, ingawa bado yumo ndani ya umoja wa Narc, ambao ndio unatawala nchi, naye ameamua kuwania urais," alisema Moi kwa masikitiko makubwa mwaka mmoja uliopita, na kuongeza:
"Hali hii haitaisaidia Kenya, na hasa ikizingatiwa kwamba wote hawa kila mmoja ana ajenda binafsi iliyojikita katika ukabila ili kufikia malengo yake binafsi. Hali hii itaivunja nchi na kuiacha vipande vipande."
Haya yalikuwa matamshi ya kwanza ya Mzee Moi kuhusu hali ya siasa ya Kenya na mwelekeo wake tangu chama chake cha KANU kilipoondolewa madarakani na Umoja wa Narc uliomweka madarakani Rais Kibaki mwaka 2002.
Moi alikuwa akikwepa sana kutoa mtamshi yoyote kuhusu Serikali ya Kibaki kwa madai kuwa 'Kibaki alikuwa anahitaji muda kuweka misingi mizuri ya utawala.'
Moi hakuwa peke yake katika kuonyesha wasiwasi wa utiriri wa wawaniaji urais. Mwandishi Mashuhuri nchini Kenya, Mutuma Mathiu, katika kuonyesha wasiwasi wake kuhusu hali ya kisiasa alisema:
"Jinsi mambo yanavyokwenda nchini Kenya, kila kiumbe kinachovuta hewa, na hasa wanasiasa, kitaingia katika kinyang'anyiro cha kuwania urais ifikapo Desemba mwaka huu.
"Musikari Kombo, Najib Balala, Raila Odinga, William Ruto na mkururo wa wanasiasa wengine tayari wamekwisha kutamka kuingia kwenye kinyang'anyiro cha kuwania urais.
"Haitashangaza kuwa ifikapo Desemba mwaka 2007, hata wale ambao tayari wamekufa watafufuka kwa kuogopa kuachwa nyuma kwenye kinyang'anyiro hiki.
"Sasa itakapofika hasa wakati wenyewe ndipo kitakuwa kivumbi. Pengine itakuwa zamu ya mbuzi, ng'ombe, mbwa na paka ambao nao wataonyesha nia ya kuchukua nafasi aliyoikalia Rais Kibaki," alisema Mathiu kwa kejeli, na kuongeza:
"Kwa maoni yangu, uwaniaji huu wa urais mwaka mmoja kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu ni dalili za wazi kuwa viongozi wetu ni wabinafsi na wapenda madaraka. Hawawajali wananchi na maendeleo ya Kenya kwa ujumla wake, bali ni waroho, wanaojiangalia wao wenyewe tu. Siasa za Kenya sasa ni pori la vurugu na mkanganyiko wa uongo wa kisiasa."
Ni kweli Kenya ilikuwa tayari imemeguka vipande vipande, vyote vikijikita katika misingi ya ubinafsi na ukabila. Waluo wa Nyanza walikuwa hawasikii chochote, walikuwa wanataka kumsikia Raila Odinga tu, basi. Waluhya magharibi mwa Kenya walikuwa wanamwangalia mtu wao Musalia Mudavadi, japo kulikuwa na Mluhya mwingine, Musikari Kombo, wa chama cha Ford Kenya. Wakikuyu, kabila kubwa kabisa anakotoka Rais Kibaki, hao ndio kabisa damu yao inanuka Ukikuyu tu, na hii inajionyesha wazi wazi; na kabila hili linaamini kuwa ndilo lenye haki ya kuitawala Kenya kisiasa na kiuchumi.
Waluo na Waluhya ni majirani, na hawajawahi kuungana kwa nia ya kupeleka urais magharibi mwa Kenya. Kwa zaidi ya miaka 44 iliyopita, Waluo na Waluhya wamekuwa na sauti kubwa katika kuamua nani awe mpangaji wa Ikulu - ama kwa uamuzi wa moja kwa mja au wa chini chini.
Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2002, Waluo na Waluhya waliupigia umoja wa Narc kura na kumwezesha Kibaki kunyakua madaraka. Baada ya kuingia madarakani, Kibaki alimteua Mluhya, Kijana Wamalwa (sasa ni marehemu), kuwa Makamu wa Rais, na kumwacha pembeni Raila Odinga. Hii ilikuwa kinyume cha makubaliano ya awali kati yake (Kibaki) na Raila kwamba nafasi hiyo ingekuwa ya Raila hasa baada ya kumsaidia sana Kibaki kuukwaa urais.
Baada ya kifo cha Wamalwa, Kibaki alimteua Mluhya tena, Moody Awori, kushika nafasi ya Makamu wa Rais, hatua ambayo iliendelea kumuudhi sana Raila.
Kuna uvumi kuwa Mudavadi na Raila walijaribu kutafuta fomula ya kuunganisha makabila haya mawili (Waluo na Waluhya) ili kujihakikishia kura nyingi katika Uchaguzi Mkuu uliomalizika wiki iliyopita.
Hatua hii ilikuwa na nia ya kufifisha nguvu za kabila kubwa la Wakikuyu linalokaa katikati mwa Kenya, na watu wa Bonde la Ufa (Rift Valley) ambako Mzee Moi alikuwa anadaiwa kuwa na ushawishi mkubwa.
Raila, Mudavadi na Musyoka anayetoka katika kabila la Wakamba, wakiungwa mkono na watu wa pwani mwa Kenya ambako anatoka Balala walimshinda Rais Kibaki Novemba 21, 2005 kwa kutumia mwavuli wa Orange Democratic Movement (ODM) wakati wa kura za maoni ambako Rais Kibaki alitaka kubadili Katiba. Huu ulikuwa mchuano kati ya Chungwa na Ndizi ambao ulimwacha Rais Kibaki njia panda kisiasa.
Kwa upande mwingine, Rais Mstaafu Moi alikuwa anapenda safari hii Uhuru Kenyatta ashinde urais baada ya juhudi zake kupitia kilichoitwa Mradi wa Uhuru (Uhuru Project) kushindwa vibaya mwaka 2002, na kuufanya Umoja wa Narc kunyakua madaraka, hali iliyosababisha chama chake cha KANU kuwa chama cha upinzani kwa mara ya kwanza tangu Kenya ipate Uhuru Desemba mwaka 1963.
Lakini kwa hali ya kisiasa ilivyokuwa, hii isingewezekana. Maji yalikuwa marefu sana kwa Mzee Moi. Ni kweli wakati huo alikuwa na ushawishi mkubwa kisiasa nyumbani kwake katika Bonde la Ufa ambao sasa unafifia kwa kasi. Hivyo asingeweza kumuuza Uhuru Kenyatta kwa Waluhya, Waluo, Wakamba (anakotoka Musyoka) na sehemu za pwani mwa Kenya.
Uhuru ni Mkikuyu, na makabila mengine nchini Kenya hayawaamini kabisa Wakikuyu kwa sababu ya kuhodhi siasa na biashara za nchi hiyo kupitia migongo ya makabila mengine. Watu wa pwani wanakwenda mbali zaidi kwa kusema kuwa "heri kula na Mluo kuliko kula au kuwa karibu na Mkikuyu".
Tetesi zilizokuwa zinavuma wakati huo mingoni mwa makabila yanayoishi katika majimbo ya uchaguzi pwani mwa Kenya zilikuwa zinasema kuwa miongoni mwa watu waliojitokeza kugombea urais, Musyoka ndiye wangependa awe Rais, na Raila awe Waziri Mkuu baada ya Katiba kubadilishwa.
Watu wa pwani hawakuwa peke yao kwa hili. Walikuwapo baadhi ya Wakenya sehemu nyingine za nchi ambao walipenda kuona hali inakuwa hivyo baada ya Uchaguzi Mkuu ili kumfanya Raila asiendelee kutingisha nchi kisiasa.
Katika makubaliano na Kibaki kabla Raila hajajiunga na Umoja wa Narc, kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2002, Raila alipaswa awe Waziri Mkuu kama ilivyodokezwa hapo juu.
Baada ya Rais Kibaki kuingia Ikulu, alimpiga teke Raila baada ya washauri wa karibu sana wa Kibaki, hasa kutoka katika kabila lake, kufanikiwa kumshawishi kufanya hivyo. Inasemekana kuwa ni watu hawa hawa waliomshawishi na kumshinikiza agombee tena urais safari hii kwa madai kuwa 'nchi haiwezi kuchukuliwa na Mluo.'
Tangu Rais Kibaki amweke pembeni, Raila ameupa taabu sana uongozi wake hadi majuzi Uchaguzi Mkuu ulipofanyika. Amekuwa mwiba mkali kwake, na ni mtu anayeogopwa sana na Kibaki mwenyewe na wengi wa mawaziri wake.
Kwa bahati mbaya sana kitu kimoja ni dhahiri nchini Kenya, nacho ni kwamba siasa zimejikita kwenye ukabila kwa kiwango cha kutisha. Wanasiasa wengi wanahubiri demokrasia na nia ya kuwakwamua wanyonge wa Kenya kutokana na lindi la umasikini, lakini moyoni wamesheheni ukabila na ajenda binafsi za kuwanufaisha wao na watu wa karibu yao.
Mbali na ukabila, jambo ambalo Wakenya wengi linawakera ni jinsi Rais Kibaki alivyoshindwa kudhibiti nafasi yake ya urais kabla ya Uchaguzi Mkuu wa juzi, kushindwa kuwadhibiti mawaziri na maofisa wake waandamizi kiasi kwamba wanafanya mambo jinsi wanavyoona, ukiwamo ufisadi; na mke wake, Lucy Kibaki, kuingilia masuala ya Serikali wakati yeye si sehemu ya Baraza la Mawaziri.
Wakenya wengi hawawaamini wanasiasa wakati huu ambako ufisadi unaongezeka, na Serikali kuonyesha kushindwa kufanya chochote cha maana kuzuia baa hili.
Wananchi wengi jijini Nairobi na mjini Kisumu mwaka mmoja uliopita walikuwa wanasema wazi kuwa Rais Kibaki akiamua kusimama kugombea tena urais atajiaibisha mwenyewe, na hasa baada ya 'kuvurunda' sana tangu achaguliwe kuwa Rais, na kwamba ishara za nyakati hazipo upande wake, yaani tayari zimekwisha kumpa kisogo.
Walisema kuwa hii itakuwa mbaya zaidi kama atasimama kupambana na Raila Odinga ambaye ana nguvu na ushawishi mkubwa kisiasa. Walisema kuwa ikiwa itatokea hivyo, mambo mawili yangetokea; ama Kibaki angelazimika kukubali kushindwa na kuondoka Ikulu au kutumia vyombo vya dola kuiba kura ili aonekane ameshinda, kitu ambacho kingeitikisa nchi.
Na kweli imetokea hivyo. Nchi si tu imetikisika, bali pia imewaka moto. Ni kama moto wa nyika wakati wa kiangazi. Masikini Kenya!
Twende wapi tukausikilize muziki wa Tanzania?
na innocent munyuku
JUMA moja limeshapita tangu mwaka mpya wa 2008 uanze. Salamu zingali zikimiminika kila mmoja kwa dua yake anaomba mema kwake na jirani yake. Ni dua mtindo mmoja.
Meseji zimejaa kwenye simu za viganjani. Maneno matamu yanapendezesha nafsi ingawa ukweli wa mambo ni kwamba si kila liombwalo huja kama atakavyo mwombaji.
Dunia ndivyo ilivyo. Nyakati kama hizi hata aliyekuwa akikusengenya atapumzika kwa muda kwani anayo furaha ya kuuona mwaka mpya.
Mzee wa Busati naye yu kundini akiwaza na kuwazua. Ameshatafakari mengi ya mwaka uliopita. Mwaka ulikuwa umejaa zege mgongoni. Mizigo ilikuwa mizito.
Utafanyaje katika hilo? Utakimbia familia? La hasha! Ni mapambano kwa kwenda mbele hata ikibidi kuwa mpambe wa mwenye ngwenje ni jambo jema.
Mbona kina Momburi ndivyo wanavyoishi? Wakiwa na haja ya bia za bure wanajua pa kukimbilia. Watapiga mguu hadi Mwana Mkude. Huko watakula matumbo na vichwa vya kuku wakishashibisha minyoo tumboni watashushia na safari lager mbili zilizoongezewa viroba vya konyagi.
Hapo mwanawane muziki unakuwa mkubwa kichwani. Watachanganya Kimombo na Kichaga juu. Basi utamu huo hauna maelezo ni kama vile wako peponi.
Enewei tuachane na hilo kwani alilojia Mzee wa Busati wiki hii ni hili la sanaa na utamaduni wa M-bongo. Ni ngumu kidogo kusema kwa uwazi kabisa kwamba ni wapi hasa utakumbana na sanaa ya Tanzania hasa katika muziki.
Pengine Mwandika Busati ataonekana mtata katika hili lakini ukweli ni kwamba leo hii ukisikia matamasha ya muziki basi usikae ukadhani kuwa huko utakuta mdumange au mganda.
Wala usisumbuke ukatoka mbio kuwahi tamasha hilo kwa ndoto ya kukuta Ingoma au Sindimba. Huko utakuta magoma kutoka ng’ambo. Vijana wakipishana kwa vikumbo kughani mashairi ya kina Tupac au Britney Spears.
Wataimba kama waimbavyo Waingereza na Wamarekani. Hakuna anayethubutu kufuata nyayo za Fela Kuti na Afrobeat zake. Wamesahau kabisa kuwaenzi wasanii wa bara la Afrika.
Hakuna tena ile shauku ya kuusambaza muziki wa Afrika. Kilichobaki sasa ni kujivunia mengine yanayovuma nchi za Kimagharibi. Watavaa kama Wamarekani na hata sema yao katika ndimi zao ni lafudhi za huko huko.
Huwezi tena kumtofautisha Ambwene na Cooper. Si rahisi tena kumtambua Achimwene na Smith. Ni ngumu pia kumtofautisha Shemakame na Erickson. Wote wanafanana kwa tabia, mavazi na mengineyo.
Ukiwaambia kuwa huko waendako siko wanakuja juu na kukuona u mjinga, mwingi wa tongotongo na usiyejua lolote katika dunia hii. Watakueleza kwa tambo pasipo hofu kwamba wao wanakwenda na wakati na huu ndio wakati.
Lakini je, hivi kweli huko ni kwenda na wakati au ni kukosa mkakati? Usingizi gani huu usiokuwa na tamati? Akili zimedumaa hata akawapiku nyati?
Hata simba mwituni wanazo kanuni hali kadhalika kunguni na nyuni. Iweje mwana wa adamu akose msimamo akashindwa kutambua kuwa kuendelea kukumbatia ya Magharibi ni hila kwa sanaa ya Afrika?
Mzee wa Busati kama hakosei huu ni mwaka wa nane tangu atambe na safu hii katika magazeti mbalimbali ya Kibongo na katika siku zote hizo amekuwa akipayuka juu ya uovu wa wasanii wengi nchini kuidharau sanaa ya Tanzania.
Walio wengi wanadhani kukaa na kujifunza kupiga ngoma ni ushamba na hapaswi kuitwa msanii. Wanadhani kuimba nyimbo za asili yao ni kujidhalilisha. Hawa wamezingirwa na utumwa wa akili.
Wamefugwa kwenye zizi la ujinga wa kujitakia. Hawaoni tena kama nyimbo za asili zina nguvu ya kuutambulisha utamaduni wa Mtanzania. Wamebaki kuchungulia runinga na kuiga wayaonayo kwenye vioo hivyo.
Bila shaka watasema huko ndiko liliko soko kubwa la muziki lakini je, kuna maana gani ya kuimba nyimbo zenye maisha kama karatasi ya chooni? Zitavuma leo, kesho kwisha habari.
Huo ni mtazamo tu wa Mwandika Busati. Mwenye kuwaza vinginevyo yu huru kuleta yake yapate kujadiliwa bila ncha ya upanga.
Ndoto ya Mzee wa Busati ni kwamba ifike siku M-bongo afike Ottawa kwa ziara ya kutambulisha nyimbo za Tanzania. Ifike siku Mtanganyika azuru New York au London akitangaza mema ya kwetu kupitia santuri zake.
Pamoja na ukweli kwamba wapo waliowahi kufanya hilo, bado kuna ufinyu wa wasanii kujitutumua na kufikia hatua hiyo. Walio wengi wanaimba ili wapate kula leo.
Kutokana na hilo ndiyo maana wamebaki kuiga badala ya kubuni. Amkeni msilale kama pono. Badilikeni ili wadau wapate pahala pa kuusikiliza muziki wa Tanzania.
Huu ni ukomo wa Mzee wa Busati wiki hii. Anatulia na kujipinda kwa ajili ya mambo mengine ya kujenga nchi. Lakini hajaacha kuomba mema kwa ajili ya Wakenya wanaopukutika sasa huku mzee mzima Kibaki akipunga upepo kwenye kasri lake jijini Nairobi ingawa wengine wanaliita jiji hilo kuwa ni New Robbery.
Wasalaam,
JUMA moja limeshapita tangu mwaka mpya wa 2008 uanze. Salamu zingali zikimiminika kila mmoja kwa dua yake anaomba mema kwake na jirani yake. Ni dua mtindo mmoja.
Meseji zimejaa kwenye simu za viganjani. Maneno matamu yanapendezesha nafsi ingawa ukweli wa mambo ni kwamba si kila liombwalo huja kama atakavyo mwombaji.
Dunia ndivyo ilivyo. Nyakati kama hizi hata aliyekuwa akikusengenya atapumzika kwa muda kwani anayo furaha ya kuuona mwaka mpya.
Mzee wa Busati naye yu kundini akiwaza na kuwazua. Ameshatafakari mengi ya mwaka uliopita. Mwaka ulikuwa umejaa zege mgongoni. Mizigo ilikuwa mizito.
Utafanyaje katika hilo? Utakimbia familia? La hasha! Ni mapambano kwa kwenda mbele hata ikibidi kuwa mpambe wa mwenye ngwenje ni jambo jema.
Mbona kina Momburi ndivyo wanavyoishi? Wakiwa na haja ya bia za bure wanajua pa kukimbilia. Watapiga mguu hadi Mwana Mkude. Huko watakula matumbo na vichwa vya kuku wakishashibisha minyoo tumboni watashushia na safari lager mbili zilizoongezewa viroba vya konyagi.
Hapo mwanawane muziki unakuwa mkubwa kichwani. Watachanganya Kimombo na Kichaga juu. Basi utamu huo hauna maelezo ni kama vile wako peponi.
Enewei tuachane na hilo kwani alilojia Mzee wa Busati wiki hii ni hili la sanaa na utamaduni wa M-bongo. Ni ngumu kidogo kusema kwa uwazi kabisa kwamba ni wapi hasa utakumbana na sanaa ya Tanzania hasa katika muziki.
Pengine Mwandika Busati ataonekana mtata katika hili lakini ukweli ni kwamba leo hii ukisikia matamasha ya muziki basi usikae ukadhani kuwa huko utakuta mdumange au mganda.
Wala usisumbuke ukatoka mbio kuwahi tamasha hilo kwa ndoto ya kukuta Ingoma au Sindimba. Huko utakuta magoma kutoka ng’ambo. Vijana wakipishana kwa vikumbo kughani mashairi ya kina Tupac au Britney Spears.
Wataimba kama waimbavyo Waingereza na Wamarekani. Hakuna anayethubutu kufuata nyayo za Fela Kuti na Afrobeat zake. Wamesahau kabisa kuwaenzi wasanii wa bara la Afrika.
Hakuna tena ile shauku ya kuusambaza muziki wa Afrika. Kilichobaki sasa ni kujivunia mengine yanayovuma nchi za Kimagharibi. Watavaa kama Wamarekani na hata sema yao katika ndimi zao ni lafudhi za huko huko.
Huwezi tena kumtofautisha Ambwene na Cooper. Si rahisi tena kumtambua Achimwene na Smith. Ni ngumu pia kumtofautisha Shemakame na Erickson. Wote wanafanana kwa tabia, mavazi na mengineyo.
Ukiwaambia kuwa huko waendako siko wanakuja juu na kukuona u mjinga, mwingi wa tongotongo na usiyejua lolote katika dunia hii. Watakueleza kwa tambo pasipo hofu kwamba wao wanakwenda na wakati na huu ndio wakati.
Lakini je, hivi kweli huko ni kwenda na wakati au ni kukosa mkakati? Usingizi gani huu usiokuwa na tamati? Akili zimedumaa hata akawapiku nyati?
Hata simba mwituni wanazo kanuni hali kadhalika kunguni na nyuni. Iweje mwana wa adamu akose msimamo akashindwa kutambua kuwa kuendelea kukumbatia ya Magharibi ni hila kwa sanaa ya Afrika?
Mzee wa Busati kama hakosei huu ni mwaka wa nane tangu atambe na safu hii katika magazeti mbalimbali ya Kibongo na katika siku zote hizo amekuwa akipayuka juu ya uovu wa wasanii wengi nchini kuidharau sanaa ya Tanzania.
Walio wengi wanadhani kukaa na kujifunza kupiga ngoma ni ushamba na hapaswi kuitwa msanii. Wanadhani kuimba nyimbo za asili yao ni kujidhalilisha. Hawa wamezingirwa na utumwa wa akili.
Wamefugwa kwenye zizi la ujinga wa kujitakia. Hawaoni tena kama nyimbo za asili zina nguvu ya kuutambulisha utamaduni wa Mtanzania. Wamebaki kuchungulia runinga na kuiga wayaonayo kwenye vioo hivyo.
Bila shaka watasema huko ndiko liliko soko kubwa la muziki lakini je, kuna maana gani ya kuimba nyimbo zenye maisha kama karatasi ya chooni? Zitavuma leo, kesho kwisha habari.
Huo ni mtazamo tu wa Mwandika Busati. Mwenye kuwaza vinginevyo yu huru kuleta yake yapate kujadiliwa bila ncha ya upanga.
Ndoto ya Mzee wa Busati ni kwamba ifike siku M-bongo afike Ottawa kwa ziara ya kutambulisha nyimbo za Tanzania. Ifike siku Mtanganyika azuru New York au London akitangaza mema ya kwetu kupitia santuri zake.
Pamoja na ukweli kwamba wapo waliowahi kufanya hilo, bado kuna ufinyu wa wasanii kujitutumua na kufikia hatua hiyo. Walio wengi wanaimba ili wapate kula leo.
Kutokana na hilo ndiyo maana wamebaki kuiga badala ya kubuni. Amkeni msilale kama pono. Badilikeni ili wadau wapate pahala pa kuusikiliza muziki wa Tanzania.
Huu ni ukomo wa Mzee wa Busati wiki hii. Anatulia na kujipinda kwa ajili ya mambo mengine ya kujenga nchi. Lakini hajaacha kuomba mema kwa ajili ya Wakenya wanaopukutika sasa huku mzee mzima Kibaki akipunga upepo kwenye kasri lake jijini Nairobi ingawa wengine wanaliita jiji hilo kuwa ni New Robbery.
Wasalaam,
Wednesday, January 2, 2008
Manabii wa soka mpeni pumzi Maximo
na innocent munyuku
HERI ya Krismasi na fanaka ya mwaka mpya wa 2008. Mzee wa Busati anaimba Haleluya akila vipapatio vya kuku kwa pumzi yenye rutuba ambayo Mola amemjalia.
Yamekuja mengi mabaya na mazuri lakini kwa sasa neema imefika mlangoni. Kaya yake inadunda kwa mema. Hakuna matata.
Wiki hii Mwandika Busati kama ilivyo ada anakuja na porojo zake lakini zilizojaa udadisi na changamoto kwenye bongo za Wadanganyika.
Wiki hii Mwandika Busati ameamua kuwa tofauti na fikra za Wabongo walio wengi hasa kwa wapenda soka nchini.
Linalosemwa na Mzee wa Busati ni hali ya timu ya taifa ya Tanzania Bara ambayo wiki msimu huu kwa mara nyingine imeshindwa kubeba Kombe la Chalenji.
Kocha Mkuu wa timu hiyo Marcio Maximo kwa sasa bila shaka hawezi kutembea mitaa ya Kariakoo kama ilivyokuwa miezi sita nyuma.
Hawezi kutembea kwa matao kwa sababu watu wamefura. Wanachosema ni kwamba Maximo hawezi tena kuwa kocha wa timu hiyo. Kisa? Timu yao imefanya vibaya kwenye michuano hiyo.
Walitamani kombe libaki nyumbani na bila shaka hiyo ingekuwa zawadi mwafaka kwa Noeli na Mwaka Mpya. Lakini ndoto hiyo imekuwa chungu.
Kinachosemwa kwenye vijiwe sasa ni kwamba Maximo kashindwa kazi na kilichobaki afungashe aende zake Brazil.
Lakini Mzee wa Busati angependa hoja ya kumbeza Maximo sasa iwekwe kando kwa sababu ukweli wa mambo ni kwamba bado Tanzania haijasukwa vema katika soka.
Wakati fulani Mwandika Busati alipata kusema kuwa wanaopiga kelele kwamba Maximo hafai bila shaka ni wendawazimu kutokana na historia ya soka nchini.
Maximo kutoka Brazil ambako wanavuma katika soka haina maana kwamba angeweza kuibadilisha soka ya bongo kwa siku moja. Angali anahitaji muda.
Leo hii mwapiga kelele kwamba hafai, waliokuwapo kabla ya Maximo walitenda nini jema katika soka ya Tanzania? Si waliishia kupiga soga na kulumbana kila kukicha?
Mwasema ati Maximo hashauriki. Nani aliwahi kumshauri naye akagoma kufuata kilichosemwa?
Mwanena pia kwamba ati mlijua Maximo hana lolote. Huu ni unabii ambao kimsingi hauna tija katika maslahi ya soka nchini. Aliwakuta wachezaji wameshakauka hata akijaribu kuwakunja wanameguka. Huo ndio ukweli wa mambo.
Mwacheni apange timu awezavyo. Kumrushia madongo ya lawama ni kutomtendea haki kwani wengi wenu bila shaka mwaelewa matatizo ya huko nyuma.
Mzee wa Busati kwa kawaida hafichi kuweka wazi misimamo yake. Hata kama anaona kufanya hivyo kunaweza kumtenga na masahiba zake hilo kwake halimpi shida.
Maximo si wa kulaumiwa. Jiulizeni tuliteleza wapi na Maximo anajaribu kufanya nini.
Kama Mwandika Busati haendi mbali na ukweli ni kwamba anachofanya Maximo kwa sasa ni kutengeneza pepo ya soka kwa miaka ijayo.
Mnaodhani leo hii mtabeba Kombe la Dunia ni kupoteza wakati kwani hilo kimsingi haliwezakani. Acheni porojo mwacheni Maximo na programu yake.
Vinginevyo Mzee wa Busati anawapa uhondo wa shairi ambalo katumiwa na sahiba yake anayekwenda kwa jina la Mwafrika Merinyo. Kila la heri!
Sikukuu ziwe na raha
Zisijewepo karaha
Sote tuombe furaha
Na ucheshi na mizaha
Tule tunywe kwa staha
Ituwakie ya jaha!
Tumuombe na Karima
Tujalie yalo mema
Mwaka uishe salama
Heri isije tuhama
Tuondolee zahama
Riziki zisije zama!
Tufanyiane mazuri
Ya baraka na ya heri
Tujiepushie shari
Na fahari na kiburi
Tuzisafishe saduri
Mabaya tusihiyari!
Upendo kita mizizi
Heshima ikaze uzi
Vita tupige uozi
Tusije lia machozi
Ukweli nao uwazi
Ziwe ndo zetu hirizi!
Sinza kwetu karibuni
Mwaka huu na mwakani
Mavazi furahieni
Myavae maungoni
Kwa maarufu washoni
Msisahau jamani!!!!!!!!!!!
Wasalaam,
HERI ya Krismasi na fanaka ya mwaka mpya wa 2008. Mzee wa Busati anaimba Haleluya akila vipapatio vya kuku kwa pumzi yenye rutuba ambayo Mola amemjalia.
Yamekuja mengi mabaya na mazuri lakini kwa sasa neema imefika mlangoni. Kaya yake inadunda kwa mema. Hakuna matata.
Wiki hii Mwandika Busati kama ilivyo ada anakuja na porojo zake lakini zilizojaa udadisi na changamoto kwenye bongo za Wadanganyika.
Wiki hii Mwandika Busati ameamua kuwa tofauti na fikra za Wabongo walio wengi hasa kwa wapenda soka nchini.
Linalosemwa na Mzee wa Busati ni hali ya timu ya taifa ya Tanzania Bara ambayo wiki msimu huu kwa mara nyingine imeshindwa kubeba Kombe la Chalenji.
Kocha Mkuu wa timu hiyo Marcio Maximo kwa sasa bila shaka hawezi kutembea mitaa ya Kariakoo kama ilivyokuwa miezi sita nyuma.
Hawezi kutembea kwa matao kwa sababu watu wamefura. Wanachosema ni kwamba Maximo hawezi tena kuwa kocha wa timu hiyo. Kisa? Timu yao imefanya vibaya kwenye michuano hiyo.
Walitamani kombe libaki nyumbani na bila shaka hiyo ingekuwa zawadi mwafaka kwa Noeli na Mwaka Mpya. Lakini ndoto hiyo imekuwa chungu.
Kinachosemwa kwenye vijiwe sasa ni kwamba Maximo kashindwa kazi na kilichobaki afungashe aende zake Brazil.
Lakini Mzee wa Busati angependa hoja ya kumbeza Maximo sasa iwekwe kando kwa sababu ukweli wa mambo ni kwamba bado Tanzania haijasukwa vema katika soka.
Wakati fulani Mwandika Busati alipata kusema kuwa wanaopiga kelele kwamba Maximo hafai bila shaka ni wendawazimu kutokana na historia ya soka nchini.
Maximo kutoka Brazil ambako wanavuma katika soka haina maana kwamba angeweza kuibadilisha soka ya bongo kwa siku moja. Angali anahitaji muda.
Leo hii mwapiga kelele kwamba hafai, waliokuwapo kabla ya Maximo walitenda nini jema katika soka ya Tanzania? Si waliishia kupiga soga na kulumbana kila kukicha?
Mwasema ati Maximo hashauriki. Nani aliwahi kumshauri naye akagoma kufuata kilichosemwa?
Mwanena pia kwamba ati mlijua Maximo hana lolote. Huu ni unabii ambao kimsingi hauna tija katika maslahi ya soka nchini. Aliwakuta wachezaji wameshakauka hata akijaribu kuwakunja wanameguka. Huo ndio ukweli wa mambo.
Mwacheni apange timu awezavyo. Kumrushia madongo ya lawama ni kutomtendea haki kwani wengi wenu bila shaka mwaelewa matatizo ya huko nyuma.
Mzee wa Busati kwa kawaida hafichi kuweka wazi misimamo yake. Hata kama anaona kufanya hivyo kunaweza kumtenga na masahiba zake hilo kwake halimpi shida.
Maximo si wa kulaumiwa. Jiulizeni tuliteleza wapi na Maximo anajaribu kufanya nini.
Kama Mwandika Busati haendi mbali na ukweli ni kwamba anachofanya Maximo kwa sasa ni kutengeneza pepo ya soka kwa miaka ijayo.
Mnaodhani leo hii mtabeba Kombe la Dunia ni kupoteza wakati kwani hilo kimsingi haliwezakani. Acheni porojo mwacheni Maximo na programu yake.
Vinginevyo Mzee wa Busati anawapa uhondo wa shairi ambalo katumiwa na sahiba yake anayekwenda kwa jina la Mwafrika Merinyo. Kila la heri!
Sikukuu ziwe na raha
Zisijewepo karaha
Sote tuombe furaha
Na ucheshi na mizaha
Tule tunywe kwa staha
Ituwakie ya jaha!
Tumuombe na Karima
Tujalie yalo mema
Mwaka uishe salama
Heri isije tuhama
Tuondolee zahama
Riziki zisije zama!
Tufanyiane mazuri
Ya baraka na ya heri
Tujiepushie shari
Na fahari na kiburi
Tuzisafishe saduri
Mabaya tusihiyari!
Upendo kita mizizi
Heshima ikaze uzi
Vita tupige uozi
Tusije lia machozi
Ukweli nao uwazi
Ziwe ndo zetu hirizi!
Sinza kwetu karibuni
Mwaka huu na mwakani
Mavazi furahieni
Myavae maungoni
Kwa maarufu washoni
Msisahau jamani!!!!!!!!!!!
Wasalaam,
Mwalilia paradiso pasipo mauti?
na innocent munyuku
HERI ya mwaka mpya! Mzee wa Busati anawasabahi kwa furaha ya kuuona mwaka huu wa 2008. Yalopita si ndwele tugange yajayo.
Yawezakana mwaka uliomalizika jana ulijaa maumivu kwa wadau lakini hilo lisiwavunje moyo. Kazeni buti ili mambo yanyooke msimu huu.
Wiki hii pamoja na kuwa na furaha ya kuuona mwaka mpya, Mzee wa Busati anakenua meno baada ya kubaini kuwa katika kaya kumejaa mabahau na malimbukeni.
Hao hawataki kuguswa. Wakiguswa basi hufura kama moto wa volcano. Watapaza sauti zao kwa hasira na maneno machafu yawatoke kama vile hawakunyonya maziwa ya mama zao.
Juma lililopita Mzee wa Busati alitua kwenye safu yake akielezea umuhimu wa kumwacha huru Kocha Mkuu wa Taifa Stars Marcio Maximo.
Alichonena Mwandika Busati ni kwamba Maximo ambaye pia ni kocha wa Kilimanjaro Stars asiadhibiwe au kutupiwe lawama kupita kiasi.
Leo hii Maximo kwa wengine anaonekana adui mkubwa wa soka Tanzania. hawataki kumsikia wala kumwona usoni. Wanasema anaua soka Bongo.
Kimsingi alichokuwa anasema Mzee wa Busati ni kwamba kumtupia lawama kocha huyo ni jambo jema kama watupa lawama watakuwa na hoja mbadala.
Kwa bahati mbaya, hao wanaojiita wadau wa soka wakarusha makombora mazito kwa Mzee wa Busati. Wakatukana walivyoweza. Hapa akageuzwa Simon wa Kirene aliyemsaidia Yesu kubeba msalaba.
Wakasema hawana haja ya kuwa na Maximo eti kwa sababu analipwa mamilioni na hakuna analolifanya. Ameshindwa kazi! Hiyo ikawa kauli yao ya uhitimisho.
Wakaongeza kuwa kuna makocha wazawa ambao wakilipwa kama Maximo basi mambo yatakwenda sawia dimbani.
Lakini ukweli wa mambo ni bado kuna mengi ya kufanywa zaidi ya kulipwa vizuri katika kibarua cha ukocha. Lililo kuu ni maandalizi.
Juzi Mzee wa Busati kasikia mpango wa kujenga taasisi ya kukuza vipaji kwa vijana wenye umri usiozidi miaka 17.
Hayo ndiyo mambo ambayo yalipaswa kufanywa kabla hata Maximo hajaja. Yangeanza miaka tele nyuma leo hii tusingekuwa tunalaumu makocha gizani pasipo mbadala.
Leo kungekuwa na furaha kila kona kwani wachezaji waliopikwa wangekuwa tele na vipaji vyao viking’ara kimataifa.
Kelele hizi kwamba Maximo hafai wakati mwingine ni ufinyu wa fikra. Hao wanaopayuka leo hii hawana tofauti na wale wanaotamani kufika paradiso huku wakikataa kuonja mauti.
Miaka tele soka ya bongo ilitegemea tunguli na misimamo mibovu ya viongozi wa klabu na mamlaka zingine za soka.
Bila watu kulala makaburini timu isingeingizwa uwanjani. Bila mbuzi kuchinjwa na damu kupakwa wachezaji hakuna kutinga dimbani. Haya mambo si siri yamefanyika sana.
Hebu tusemezane kwa hoja. Hao makocha wazawa waliokuwapo kabla ya Maximo wamefanya jipya gani zaidi ya kukumbatia malumbano?
Mambo ya ulozi yamekuwa yakionekana kwa uwazi kabisa na ndio maana hivi karibuni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Soka wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), Ashford Mamelodi alizitaka klabu kuachana na ndumba.
Mamelodi alitoa kauli hiyo wakati akifunga semina elekezi kwa timu za Ligi Kuu Tanzania Bara mjini Bagamoyo.
La maana linalopaswa kufanywa ni kuhakikisha kuwa kila anayejiita mdau na mkereketwa wa soka atambue majukumu ya kuendeleza soka kwa uongozi na ufundi.
Turejee kwa Maximo. Kocha huyo raia wa Brazil ametua nchini katika muda ambao Tanzania ilikuwa katika mlolongo wa migogoro katika klabu za soka.
Kwa bahati mbaya sana migogoro hiyo ingali ikiendelea kuzitafuna klabu. Klabu ambazo Maximo anastahili kubeba wachezaji kwa ajili ya timu ya taifa.
Hebu basi tuangalie mizizi ya soka yetu kabla ya kumtupia mawe Maximo. Bila shaka msimamo wake wafaa uheshimiwe, asipigiwe miluzi mingi. Huo ndio mtazamo wa Mzee wa Busati.
Vinginevyo Mwandika Busati anaomba mema yatue mwaka huu kwa wadau wake. Endeleeni kupanga yenye tija na kila mmoja awajibike kwa nafasi yake.
Wasalaam,
HERI ya mwaka mpya! Mzee wa Busati anawasabahi kwa furaha ya kuuona mwaka huu wa 2008. Yalopita si ndwele tugange yajayo.
Yawezakana mwaka uliomalizika jana ulijaa maumivu kwa wadau lakini hilo lisiwavunje moyo. Kazeni buti ili mambo yanyooke msimu huu.
Wiki hii pamoja na kuwa na furaha ya kuuona mwaka mpya, Mzee wa Busati anakenua meno baada ya kubaini kuwa katika kaya kumejaa mabahau na malimbukeni.
Hao hawataki kuguswa. Wakiguswa basi hufura kama moto wa volcano. Watapaza sauti zao kwa hasira na maneno machafu yawatoke kama vile hawakunyonya maziwa ya mama zao.
Juma lililopita Mzee wa Busati alitua kwenye safu yake akielezea umuhimu wa kumwacha huru Kocha Mkuu wa Taifa Stars Marcio Maximo.
Alichonena Mwandika Busati ni kwamba Maximo ambaye pia ni kocha wa Kilimanjaro Stars asiadhibiwe au kutupiwe lawama kupita kiasi.
Leo hii Maximo kwa wengine anaonekana adui mkubwa wa soka Tanzania. hawataki kumsikia wala kumwona usoni. Wanasema anaua soka Bongo.
Kimsingi alichokuwa anasema Mzee wa Busati ni kwamba kumtupia lawama kocha huyo ni jambo jema kama watupa lawama watakuwa na hoja mbadala.
Kwa bahati mbaya, hao wanaojiita wadau wa soka wakarusha makombora mazito kwa Mzee wa Busati. Wakatukana walivyoweza. Hapa akageuzwa Simon wa Kirene aliyemsaidia Yesu kubeba msalaba.
Wakasema hawana haja ya kuwa na Maximo eti kwa sababu analipwa mamilioni na hakuna analolifanya. Ameshindwa kazi! Hiyo ikawa kauli yao ya uhitimisho.
Wakaongeza kuwa kuna makocha wazawa ambao wakilipwa kama Maximo basi mambo yatakwenda sawia dimbani.
Lakini ukweli wa mambo ni bado kuna mengi ya kufanywa zaidi ya kulipwa vizuri katika kibarua cha ukocha. Lililo kuu ni maandalizi.
Juzi Mzee wa Busati kasikia mpango wa kujenga taasisi ya kukuza vipaji kwa vijana wenye umri usiozidi miaka 17.
Hayo ndiyo mambo ambayo yalipaswa kufanywa kabla hata Maximo hajaja. Yangeanza miaka tele nyuma leo hii tusingekuwa tunalaumu makocha gizani pasipo mbadala.
Leo kungekuwa na furaha kila kona kwani wachezaji waliopikwa wangekuwa tele na vipaji vyao viking’ara kimataifa.
Kelele hizi kwamba Maximo hafai wakati mwingine ni ufinyu wa fikra. Hao wanaopayuka leo hii hawana tofauti na wale wanaotamani kufika paradiso huku wakikataa kuonja mauti.
Miaka tele soka ya bongo ilitegemea tunguli na misimamo mibovu ya viongozi wa klabu na mamlaka zingine za soka.
Bila watu kulala makaburini timu isingeingizwa uwanjani. Bila mbuzi kuchinjwa na damu kupakwa wachezaji hakuna kutinga dimbani. Haya mambo si siri yamefanyika sana.
Hebu tusemezane kwa hoja. Hao makocha wazawa waliokuwapo kabla ya Maximo wamefanya jipya gani zaidi ya kukumbatia malumbano?
Mambo ya ulozi yamekuwa yakionekana kwa uwazi kabisa na ndio maana hivi karibuni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Soka wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), Ashford Mamelodi alizitaka klabu kuachana na ndumba.
Mamelodi alitoa kauli hiyo wakati akifunga semina elekezi kwa timu za Ligi Kuu Tanzania Bara mjini Bagamoyo.
La maana linalopaswa kufanywa ni kuhakikisha kuwa kila anayejiita mdau na mkereketwa wa soka atambue majukumu ya kuendeleza soka kwa uongozi na ufundi.
Turejee kwa Maximo. Kocha huyo raia wa Brazil ametua nchini katika muda ambao Tanzania ilikuwa katika mlolongo wa migogoro katika klabu za soka.
Kwa bahati mbaya sana migogoro hiyo ingali ikiendelea kuzitafuna klabu. Klabu ambazo Maximo anastahili kubeba wachezaji kwa ajili ya timu ya taifa.
Hebu basi tuangalie mizizi ya soka yetu kabla ya kumtupia mawe Maximo. Bila shaka msimamo wake wafaa uheshimiwe, asipigiwe miluzi mingi. Huo ndio mtazamo wa Mzee wa Busati.
Vinginevyo Mwandika Busati anaomba mema yatue mwaka huu kwa wadau wake. Endeleeni kupanga yenye tija na kila mmoja awajibike kwa nafasi yake.
Wasalaam,
Subscribe to:
Posts (Atom)